Thursday 26 November 2020

MAMA AKATA SEHEMU ZA SIRI ZA MTOTO WAKE NA KUZITUPA CHOONI

Mwanamke mmoja kaunti ya Kiambu nchini Kenya ameripotiwa kumkata mwanawe wa umri wa mwaka mmoja na miezi 8 sehemu nyeti kisha kuzitupa chooni. 

Haijabainika ni kwa nini mama huyo alitekeleza kitendo hicho ila maafisa wa polisi wameanza kufanya uchunguzi kufuatia kisa hicho.

Babake mtoto huyo aliripoti katika kituo cha polisi cha Tigoni akidai kuwa Winnie Mutheu ambaye alikuwa mkewe alitoroka baada ya kutekeleza kitendo hicho. 

Kulingana na jirani, mwanamke huyo alitupa sehemu za siri za mwanawe kwenye choo kabla ya kutorokea mafichoni.

Akithibitisha kisa hicho, OCPD wa Tigoni Mwaniki Irei alisema mtoto huyo amelazwa katika hospitali ya Kijabe akiwa hali mahututi.

Afisa anayeshughulika maslahi ya watoto eneo la Tigoni George Ngugi amesema watashikiriana na maafisa wa polisi kuhakikisha mshukiwa anakamatwa na kukabiliwa vilivyo kisheria. 

Visa vya aina hii vimekithiri nchini, mapema wiki jana mama mmoja kaunti ya Nakuru alimuua mtoto wake wa miaka mitatu baada ya kugombana na mumewe. 

Kulingana na taarifa ya polisi, mshukiwa Faith Chepkemoi Maritim alitekeleza kitendo hicho kufuatia mzozo wa kinyumbani wa mara kwa mara kati ya na mumewe Benard Maritim.

Chepkemoi aliambia polisi kwamba alikuwa amechoshwa na ndoa hiyo na ndiyo sababu aliamua kujinyakulia mpenzi mpya ambaye tayari alikuwa ameahidi kumuoa.

Via>>Tuko News

Share:

Mama Samia kumwakilisha JPM Mkutano wa SADC Organ Troika


Na Nelson Kessy, Gaborone-Botswana
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajia kumwakilisha Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwenye Mkutano wa dharura wa pamoja baina ya SADC Organ Troika (Botswana, Malawi na Zimbabwe), na nchi zinazochangia Vikosi vya ulinzi na amani vya Umoja wa Mataifa, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwenye Kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini DRC utakaofanyika tarehe 28 Novemba 2020, mjini Gaborone, Botswana.

Akithibitisha kuhusu ushiriki wa Tanzania katika mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amesema kuwa ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo utaongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye atakuwa anamwakilisha Mhe. Rais.

Kwa mujibu wa Prof. Kabudi, mkutano huu utatanguliwa na mkutano wa Maafisa Waandamizi/Makatibu Wakuu wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama na kufuatiwa na mkutano wa Dharura wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama tarehe 26 Novemba 2020.

"Pamoja na Mambo mengine, mkutano huo utajadili hali ya siasa, ulinzi na usalama katika kanda ya SADC na kuweza kuona changamoto mbalimbali zilizojitokeza na kupata majibu ya kutatua changamoto hizo," Amesema Prof. Kabudi

Makamu wa Rais ataambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi Dkt. Faraji Mnyepe pamoja na Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda na Mratibu Kitaifa wa Masuala ya SADC, Bibi Agnes Kayola.

ASASI ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama (Troika) ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) inawajibika kukuza amani na usalama katika eneo la SADC na pia ina wajibu wa kuongoza na kuzipatia nchi Wanachama mwongozo kuhusu mambo ambayo yanatishia amani, ulinzi na usalama.



Share:

HII NDIYO HISTORIA FUPI YA DIEGO MARADONA

Mmoja wa wachezaji waliobarikiwa, Argentina ilijivunia kipaji cha kipekee, madoido ya ajabu akiwa uwanjani, maono na kasi vilivyovutia mashabiki wengi.

Lakini pia alisababisha hasira na goli lake alilolipa jina 'Hand of God' ambalo lilizua utata pamoja na kutumbukia katika utumiaji wa dawa za kulevya na mapungufu mengine yaliyojitokeza baada ya kustaafu soka.

Mfupi lakini imara - Nyota wa kandanda

Alizaliwa miaka 60 iliyopita huko Buenos Aires eneo la kitongoji duni, Diego Armando Maradona aliepuka umaskini wakati akiwa kijana kwa kuwa nyota wa mpira wa soka ambaye kuna wale wanaomchukulia kuwa bora zaidi akilinganishwa na mchezaji Pele wa Brazil.

Mchezaji huyo wa Argentina, aliyefunga magoli 259 katika mechi 491 alizoshiriki alimshinda mpinzani wake wa Marekani Kusini katika kura ya maoni ya kuamua mchezaji wa karne ya 20 kabla ya Fifa kubadilisha sheria za upigaji kura na wote wawili wakatunukiwa hadhi hiyo.

Maradona alionesha uwezo wa hali ya juu kutoka akiwa mtoto na kuwa chanzo cha timu ya vijana ya Los Cebollitas kuwa kidedea kwa kupata magoli 136 bila kufungwa na timu yoyote kando na kujitokeza kwake kama mchezaji wa kimataifa akiwa na umri wa miaka 16 pekee na siku 120.

Akiwa mfupi na imara, futi 5 na inchi 5 pekee, uchezaji wake haukuwa wa kawaida.

Lakini ujuzi wake, wepesi, maono, jinsi alivyodhibiti mpira, alivyopiga chenga na kupitisha mpira kwa wengine kwasababu ya kukosa kasi na wakati mwingine hata kuwa na matatizo ya uzito wa kupita kiasi.

Huenda alikuwa na kasi ya ajabu mno akiwa uwanjani karibu na mahasimu wake lakini alikuwa na wakati mgumu kukwepa changamoto.

Goli maarufu la 'Hand of God' na 'Goli la Karne'

Maradon alimfunga kipa wa England kwa kufunga na mkono na goli hilo lilikubalika mwaka 1986.

Maradona alifunga magoli 34 kwa kushiriki mechi 91 kama mchezaji wa Argentina na Yeye ndio chanzo cha nchi yake kuibuka na ushindi katika kombe la dunia mwaka 1986 nchini Mexico na kupata fursa kuingia fainali miaka minne baadaye.

Katika robo fainali ya mchezo wa awali kulijitokeza utata ambao kumbe baadaye ungekumba maisha yake.

Mechi dhidi ya England ilikuwa na mkwaruzano uliopitiliza kidogo huku vita vya Falklands kati nchi hizo mbili vikiwa ndio vimetokeo miaka minne tu nyuma. Na kumbe hilo lingesababisha hali uwanjani kuzua wasiwasi zaidi.

Dakika 51zikiwa zimekatika na hakuna timu iliyoona lango la mwingine, Maradona aliruka na mlinda lango wa timu pinzani Peter Shilton na kufunga kwa kupiga mpira hadi kwenye neti.

Baadaye alisema goli hilo lilitokana na "Maradona kuupiga mpira kwa kichwa kidogo na mkono wa Mungu".

Dakika nne baadaye, alifunga kile kimekuwa kikitambuliwa kama 'goli bora la karne' - baada ya kuchukua mpira mwenyewe na kuanza mbio kwa kasi ya ajabu ambako kuliacha wachezaji kadhaa wakimfuata nyuma kabla ya kumzunguka Shilton na kufunga bao.

Maradona alikuwa mchezaji nyota katika klabu ya Napoli ambapo alifunga magoli 81 katika mechi 188

"Lazima tu ungesema ulikuwa mchezo mzuri. Hakuna shaka yoyote na goli hilo. Kulikuwa tu na mchezaji nyota wa mpira wa soka," alisema mchambuzi wa BBC Barry Davies.

England ilikuwa nyuma kwa bao moja lakini Argentina ikafaulu na Maradona akasema "ilikuwa zaidi ya kushinda mechi, ilikuwa ni suala na kuwatoa nje Waingereza".

Shujaa kwa Napoli lakini akatumbukia katika matumizi ya dawa za kulevya.

Maradona alivunja rekodi ya uhamisho mara mbili - akiondoka timu ya vijana ya Boca Juniors mji wake wa nyumbani na kujiunga na timu ya Barcelona, Uhispani kwa kima cha pauni milioni 3 mwaka 1982 na kujiunga na klabu ya Italia ya Napoli miaka miwili baadaye kwa kima cha pauni milioni 5.

Waliomlaki walikuwa ni mashabiki zaidi ya mashabiki 80,000 waliomsubiri uwanja wa Stadio San Paolo alipowasili kwa helikopta. Shujaa mpya.

Alichezea klabu bora katika taaluma yake nchini Italia akishangiliwa na wafuasi wake wakati huo akiwa kichocheo cha kupata mataji ya kwanza ya Ligi mwaka 1987 na 1990 na pia katika kombe la Uefa mwaka 1989.

Sherehe ya kufurahia ushindi wa kwanza ilidumu kwa siku tano huku mamia ya maelfu ya watu wakijitokeza lakini Maradona alionekana kuchoshwa na sherehe hizo.

"Huu ni mji mzuri lakini napata shida, hata siwezi kupumua kwa amani. Nataka kuwa huru na kutembea. Mimi ni kijana kama mwingine yeyote yule," alisema.

Hata hivyo hakuwezi kujitenga na sakata ya uhalifu ya Camorra, akatumbukia katika utumiaji wa dawa za kulevya na kufunguliwa kesi mahakamani ya kutafuta atambuliwe rasmi kama baba.

Baada ya kushindwa bao 1-0 na Ujerumani mwaka wake wa mwisho Italia 90, alipatikana na kashfa ya utumiaji wa dawa zilizopigwa marufuku mwaka uliofuata na kupigwa marafuku kucheza soka kwa miezi 15.

Hata hivyo, alirejea tena kwenye ulimwengu wa soka katika Kombe la Dunia la mwaka 1994 nchni Marekani.
Diego Maradona

Lakini pia alifanya watazamaji kuwa na wasiwasi jinsi alivyosherehekea goli akiwa kama kichaa mbele ya kamera na kutolewa nje katikati ya mechi baada ya kubainika kuwa ametumia dawa iliyopigwa marufuku ya ephedrine.

Matukio ya Maradona

1977: Alijitokeza katika mchuano kati ya Argentina v Hungary
1982: Alijiunga na Napoli baada ya kuwa Barcelona kwa miaka miwili ya mafanikio makubwa
1986: Alishinda Kombe la Dunia akichezea Argentina
1990: Alikuwa mshindi wa pili wa Kombe la Dunia akichezea Argentina. Kombe la pili la Ligi Napoli
1991: Alipigwa marufuku ya miezi 15 baada ya kuthibitishwa kutumia dawa zilizopigwa marufuku
1994: Alicheza katika kombe la dunia kwa mara ya nne lakini akatolewa nje baada ya kuthibitishwa kutumia dawa zilizopigwa marufuku
1997: Alistaafu kucheza soka baada ya kuthibitishwa kutumia dawa zilizopigwa marufuku kwa mara ya tatu
2010: Alikamilisha miaka miwili ya kuwa kocha wa Argentina baada ya kutolewa katika robo fainali ya Kombe la Dunia

Maisha baada ya kustaafu

Baada ya kupatikana tena ametumia dawa zilizopigwa marufuku, miaka mitatu baadaye alistaafu kucheza soka akiwa na umri wa miaka 37 lakini akaendelea kuandamwa na matatizo.

Maradona alihukumiwa kifungo cha miaka miwili na miezi 10 kilichocheleweshwa kwasababu ya kufyatulia risasi wanahabari hewani.

Tabia yake ya kutumia dawa za kulevya na pombe ilimsababishia matatizo mengi ya kiafya. Aliongeza uzito na kuna wakati fulani alikuwa na kilogramu 128. Mwaka 2004 akapata mshtuko wa moyo uliosababisha apelekwe katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Pia alifanyiwa upasuaji wa kupunguza tumbo lake kumsadia kukabiliana na tatizo la uzito wa kupindukia na kutafuta hifadhi Cuba wakati anakabiliana na utumiaji wa dawa za kulevya.
Share:

VIJIJI VYA LIWALE LINDI VYANEEMEKA NA UHIFADHI WA MISITU

 

Katibu Tawala wa Wilaya  ya Liwale mkoani Lindi, Rajabu Kambangwa  akizungumza na wandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini kuhusu mchango wa sekta ya misitu kwenye wilaya hiyo.
Afisa Sera na Majadiliano  wa Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA) Elida Fundi   akizungumza na waandishi wa habari walipokuwa kwenye ziara ya kuona namna Vijiji vya Darajani, Mihumo na Mtawatama zilivyofanikiwa katika jitihada za utunzaji shirikishi wa misitu.
Afisa Misitu wa Wilaya ya Liwale Nassoro Ali Mzui akizungumza na waandishi wa habari kuhusu jitihada wanazozifanya kwa kushirikiana na Serikali za vijiji na wadau wengine wa misitu kwenye ulizi shirikishi wa misitu.
Afisa Sera na Majadiliano  wa Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA) Elida Fundi akiwa kwenye picha ya pamoja na kamati ya maliasili ya kijiji cha Mtawatawa Wilayani Liwale.
 

Na Calvin  Gwabara, Liwale.

ZAIDI ya shilingi milioni 957 zimepatikana kwenye vijiji kutokana sekta ya misitu katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale mkoani Lindi na hivyo kuchangia katika kusaidia shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo elimu, afya na maji.

Hayo yamebainishwa na KatibuTawala wa Wilaya  hiyo,  Rajabu Kambangwa wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mchango wa sekta ya misitu na ushiriki wa wilaya hiyo kwenye uhifadhi shirikishi wa misitu ya vijiji.

Alisema kuwa wilaya ya Liwale misitu ni chanzo kikubwa cha mapato ya wilaya kwani katika mwaka wa fedha wa 2019/2020 iliingizia serikali kiasi cha shilingi bilioni 2.6 ikifuatiwa na sekta ya kilimo na hivyo kuifanya sekta ya misitu kuwa sekta muhimu kwauchumi.

” Sisi kama wilaya tunanufaika sana na uwepo wa rasilimali hizi kwa hiyo tunafarijika sana ujio wa miradi kama huu ya Uhifadhi shirikishi wa misitu kwani inasaidia kuwajengea uwezo wananchi kwenye vijiji vyetu kuona umuhimu wa misitu na uhifadhi wake kwa maendeleo endelevu lakini kubwa zaidi kuona misitusi ya serikali bali ni mali yao” alisema  Kambangwa.

Katibu Tawala huyo alisema kwenye Kijiji cha Likombola pekee kiliingiza kiasi cha shilingi milioni 253 huku Kijiji cha Mtawatawa wakiingiza kiasi cha shilingi milioni 122 ambazo zimetumika kufanya shunguli mbalimbali za maendeleo kwenye vijiji hivyo ikiwemo kujenga vyumba vya madarasa, Zahanati, Nyumba ya Mtendaji wa Kijiji Pamoja naTrekta la Kijiji ambalo linawasaidia kwenye kilimo kwa kukodishiana kwa gharama za chini na kwa wakati.

Alisema pamoja na mafanikio hayo makubwa lakini swala la uhifadhi bado linahitaji elimu kwa jamii maana Wananchi wasipoona faida za moja kwa moja kwenye vijiji vyao hawawezi kuitunza wala kuilinda na hivyo kusababisha misitu kupotea wakidhani ni mali ya Serikali.

Kwa upande wake Afisa Sera na Majadiliano wa Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA)Elida Fundi alisema kuwa vijiji vinafanyakazi kubwa na nzuri katika kuhifadhi misitu ya vijiji na hii inatokana na elimu na motisha wanayoipata kwenye vijiji vyao baada ya kuvuna misitu hiyo kwa uendelevu.

Alisema MJUMITA kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo na misitu wataendelea kushiriki kikamilifu kwenye kuzisaidia Halmashauri na vijiji katika awamu hii ya tatu ya mradi kuweka mipango bora yamatumizi ya ardhi na utengaji wa maeneo ya misitu ya hifadhi za vijiji ili itunzwe na kuvunwa kwa njia endelevu ambazo zitatunza misitu hiyo.

Kwa upande wake Afisa Misitu wa wilaya hiyo, Nassoro Ali Mzui alisema changamoto kubwa wanayokumbana nayo kwenye uhifadhi wa misitu hiyo ni vitendea kazi hasa vyombo vya usafiri kama pikipiki na zana zingine kwani misitu mingine inaukubwa wa zaidi ya hekta elfu 13 hivyo kuwawia vigumu kufanya doria na kuizunguka kwa miguu.

Alisema kwa kuwa vijiji vinachangia asilimia kumi ya mapato yatokanayo namisitu kwenda kwenye halmashauri wamekuwa wakifanya doria za pamoja na wanavijiji na kamati zao za maliasili za kijiji pamoja na maafisa wa maliasili na askari ili kusaidia kuongeza nguvu na kurahisha zoezi la ulinzi kwenye misitu hiyo.

Share:

AFISA VIJANA SINGIDA AWATAKA VIJANA KUTUMIA FURSA YA MSIMU HUU WA MVUA KWA KILIMO

 

Kaimu Afisa Vijana mkoa wa Singida, Frederick Ndahani 

Na Mwandishi Wetu, Singida
KAIMU Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani amehamasisha vijana mkoani hapa na kwingineko nchini kuhakikisha wanatumia fursa ya msimu huu wa mvua kujikita katika kilimo cha kibiashara ili kujiongezea kipato.

Akizungumza mkoani hapa jana, Ndahani alisema anaamini kijana yeyote atakayethubutu kujiingiza katika kilimo kamwe hatajutia kutokana na faida kubwa atakayoipata.

"Nawahamasisha vijana wenzangu tujitokeze tukalime, tusiiache mvua hii ikapita bure. Kwa wasio na mashamba wasisite kwenda kukodi...shamba la kukodisha gharama yake ni wastani wa kati ya shilingi elfu 25 na 30 kwa ekari moja," alisema.

Alisema wakati serikali ikipambana kuhamasisha mageuzi ya kilimo ni jukumu la vijana kuhakikisha wanaunga mkono juhudi hizo kwa kutambua kilimo ndio uti wa mgongo wa uchumi wa Taifa.

Ndahani alisema takribani asilimia 60 za malighafi ya viwanda vilivyopo nchini hutegemea kilimo hivyo ni jukumu la vijana kuhakikisha wanakwenda na kasi ya mheshimiwa Rais John Magufuli katika kulifanya taifa hili kuendelea kustawi kiuchumi.

"Niwaombe sana tusiwaachie wazee na wanawake peke yao bali vijana tuingie rasmi shambani tusiache mvua hizi zikapita hivi hivi,"alisema afisa huyo wa vijana.

Alisisitiza mathalani kwa vijana wa mkoa wa singida, wana kila sababu ya kuchangamkia fursa ya kilimo chenye tija kutokana na uwepo wa viwanda vingi vinavyohitaji malighafi, hususan zao la alizeti ambalo ndio zao kuu mkoani humo.

Pia aliwakumbusha vijana kuwa mbali ya alizeti tayari serikali imekwishafungua dirisha lingine kwa kilimo cha korosho kwenye mikoa yote ya Kanda ya Kati ikiwemo Singida, zao ambalo lina usalama zaidi na soko la uhakika ndani na nje ya nchi...na kwamba wasichelewe kuchangamkia fursa hiyo ili kuondokana na umasikini na kuinua kipato.

Ndahani ambaye ameshawahi kushiriki kwenye timu maalumu ya kukimbiza Mwenge wa Uhuru miaka ya hivi karibuni, alisema anaamini misingi bora ya taifa lolote lenye amani, utulivu na usalama hutokana na watu wake hususan vijana kujikita ipasavyo katika  uwajibikaji kwenye nyanja mbalimbali-ikiwemo shughuli za kilimo.


Share:

WANAUSHIRIKA KIGOMA WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA KILIMO CHA MICHIKICHI

 Naibu Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Charles Malunde, amewataka Viongozi wa Vyama vya Ushirika vinavyolima zao la Michikichi mkoani Kigoma kushirikiana kwa pamoja ili kuongeza nguvu ya kuzalisha na kukuza miche bora ya Chikichi kwenye vitalu ili wakulima wapate miche hiyo kwa wakati pale inapohitajika.

Bwana Malunde ametoa wito huo  Jumanne, Novemba 24, 2020 mjini Kigoma alipokutana na viongozi wa Vyama vya Ushirika vinavyolima zao la Michikichi ambapo amewataka kushirikiana Serikali katika kuongeza uzalishaji wa michikichi mkoani humo.

“Wanaushirika na Wanakigoma kwa ujumla itumieni fursa hii ya kilimo cha zao la Michikichi kwa kuwa ardhi mnayo na inayofaa kwa kilimo hiki, mkizembea msishangae watu kutoka maeneo mengine wakachangamkia fursa hii na kuanzisha mashamba makubwa nakumiliki soko,” amesema Naibu Mrajis.

Aidha, Bw. Malunde amesema kuwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika watakaoshindwa kuwahamasisha na kuwashirikisha wanaushirika na wakulima kwa ujumla kuzalisha na kukuza miche bora ya Chikichi, wajipime na kuona kama bado wanafaa kuchaguliwa kuendelea kuviongoza vyama hivyo.

“Kama kiongozi ameshindwa kuwahimiza wanachama wake kushiriki katika kazi za kujiletea maendeleo; ikiwemo kuongeza uzalishaji wa mazao yao, hatuoni sababu za yeye kuendelea kukiongoza chama cha ushirika,” amesema Naibu Mrajis.

Taarifa iliyotolewa na Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Kigoma, Robert Kitambo, wakati wa ziara ya Naibu Mrajis imeonesha kuwa eneo lililopandwa Michikichi mkoani Kigoma ni Hekta 19,656 na eneo linalofaa kwa ajili ya kupanua kilimo cha Chikichi ni Hekta 48,085.

“Jumla ya eneo linalofaa kwa kilimo cha Chikichi ni Hekta 67,880 ambapo eneo hilo kwa ujumla wake linahitaji miche 9,503,340 kuikidhi eneo lote linalofaa kwa kilimo cha michikichi. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupitia Sekretarieti ya Mkoa inaendelea kuhimiza na kusimamia ufufuaji wa zao la michikichi kupitia Taasisi za Serikali zilizopo mkoani Kigoma na Wadau mbalimbali kutoka Sekta Binafsi,” amesema Kitambo.

Mkoa wa Kigoma baada ya kutolewa kwa Agizo la Serikali la kufufua kilimo cha Chikichi mwaka 2018, vyama 13 vya ushirika vimeanzishwa na kusajiliwa: Luiche Basin AMCOS, Kasuku AMCOS, Simbo AMCOS, Mahembe AMCOS, Chakulu AMCOS, Bitale Mkongoro AMCOS, Nkungwe AMCOS, Mkuti Mchikichi AMCOS, Kagongo AMCOS, Mungonya AMCOS, Ngogomyi AMCOS, Wamiki AMCOS na Wami AMCOS.


 


Share:

WANAUSHIRIKA KIGOMA WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA KILIMO CHA MICHIKICHI

 Naibu Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Charles Malunde, amewataka Viongozi wa Vyama vya Ushirika vinavyolima zao la Michikichi mkoani Kigoma kushirikiana kwa pamoja ili kuongeza nguvu ya kuzalisha na kukuza miche bora ya Chikichi kwenye vitalu ili wakulima wapate miche hiyo kwa wakati pale inapohitajika.

Bwana Malunde ametoa wito huo  Jumanne, Novemba 24, 2020 mjini Kigoma alipokutana na viongozi wa Vyama vya Ushirika vinavyolima zao la Michikichi ambapo amewataka kushirikiana Serikali katika kuongeza uzalishaji wa michikichi mkoani humo.

“Wanaushirika na Wanakigoma kwa ujumla itumieni fursa hii ya kilimo cha zao la Michikichi kwa kuwa ardhi mnayo na inayofaa kwa kilimo hiki, mkizembea msishangae watu kutoka maeneo mengine wakachangamkia fursa hii na kuanzisha mashamba makubwa nakumiliki soko,” amesema Naibu Mrajis.

Aidha, Bw. Malunde amesema kuwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika watakaoshindwa kuwahamasisha na kuwashirikisha wanaushirika na wakulima kwa ujumla kuzalisha na kukuza miche bora ya Chikichi, wajipime na kuona kama bado wanafaa kuchaguliwa kuendelea kuviongoza vyama hivyo.

“Kama kiongozi ameshindwa kuwahimiza wanachama wake kushiriki katika kazi za kujiletea maendeleo; ikiwemo kuongeza uzalishaji wa mazao yao, hatuoni sababu za yeye kuendelea kukiongoza chama cha ushirika,” amesema Naibu Mrajis.

Taarifa iliyotolewa na Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Kigoma, Robert Kitambo, wakati wa ziara ya Naibu Mrajis imeonesha kuwa eneo lililopandwa Michikichi mkoani Kigoma ni Hekta 19,656 na eneo linalofaa kwa ajili ya kupanua kilimo cha Chikichi ni Hekta 48,085.

“Jumla ya eneo linalofaa kwa kilimo cha Chikichi ni Hekta 67,880 ambapo eneo hilo kwa ujumla wake linahitaji miche 9,503,340 kuikidhi eneo lote linalofaa kwa kilimo cha michikichi. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupitia Sekretarieti ya Mkoa inaendelea kuhimiza na kusimamia ufufuaji wa zao la michikichi kupitia Taasisi za Serikali zilizopo mkoani Kigoma na Wadau mbalimbali kutoka Sekta Binafsi,” amesema Kitambo.

Mkoa wa Kigoma baada ya kutolewa kwa Agizo la Serikali la kufufua kilimo cha Chikichi mwaka 2018, vyama 13 vya ushirika vimeanzishwa na kusajiliwa: Luiche Basin AMCOS, Kasuku AMCOS, Simbo AMCOS, Mahembe AMCOS, Chakulu AMCOS, Bitale Mkongoro AMCOS, Nkungwe AMCOS, Mkuti Mchikichi AMCOS, Kagongo AMCOS, Mungonya AMCOS, Ngogomyi AMCOS, Wamiki AMCOS na Wami AMCOS.


 


Share:

Senior Specialist; IT Infrastructure Capacity Management at CRDB Bank

Job Purpose To ensure that technology infrastructure, storage and compute capacity meet current and future business requirements. Responsible for the design, installation, maintenance, and administration of the server, storage, backup and virtualization Technologies. Key Responsibilities Responsible for monitoring storage and compute capacity needs and develop short- and long-term plan to meet current and future business […]

The post Senior Specialist; IT Infrastructure Capacity Management at CRDB Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Senior Specialist; Networks (UCS) at CRDB Bank

Job Purpose Oversee and support unified communication infrastructure (Data, Voice, Video & IM, audio and video Conference, presentation) to satisfy business and customer’s requirements (flexibility, availability, performance, security and continuous improvement). Key Responsibilities Manage multiple unified communications infrastructure projects and operational tasks. Responsible for design, staging, configuration, implementation, and support for VoIP & Contact center […]

The post Senior Specialist; Networks (UCS) at CRDB Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Senior Manager; Data Centers Infrastructure at CRDB Bank

Job Purpose Creates and maintains overall Data center plans to support the organization’s business strategy, agrees service level agreements with vendors and plans all aspects of the infrastructure necessary to ensure provision of Data center services to meet such agreements. Key Responsibilities 24x7x365 management of CRDB Bank Data Centers to ensure services are available to […]

The post Senior Manager; Data Centers Infrastructure at CRDB Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Grants and Budget Manager, Airbel Impact Lab at International Rescue Committee

Requisition ID: req11069 Job Title: Grants and Budget Manager, Airbel Impact Lab Sector: Research & Development Employment Category: Regular Employment Type: Full-Time Open to Expatriates: No Location: Amman, Jordan Job Description The IRC’s Airbel Impact Lab designs, tests, and scales life-changing, cost-effective solutions for people affected by conflict and disaster. By applying the IRC’s deep technical expertise and field experience with a […]

The post Grants and Budget Manager, Airbel Impact Lab at International Rescue Committee appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Swimming Coach at Braeburn International School Arusha

SWIMMING COACH VACANCY Braeburn International School Arusha requires an experienced Swimming Coach to lead in delivering and developing the school’s swimming programme from January 2021. Applicants must be prepared to run the early morning and after school training sessions, to take our swimmers onto the next level. Applicants must also be prepared to teach swimming […]

The post Swimming Coach at Braeburn International School Arusha appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Performance and Analytics Advisor at Global Health Supply Chain Program

Job Title: Performance and Analytics Advisor – Malaria Commodity Supply Chain Department/Unit: Performance and Analytics. Location: GHSC – TA – TZ office Dar es Salaam. Reports to: Performance and Analytics Team Lead. OVERVIEW: The Global Health Supply Chain Program Technical Assistance – Tanzania (GHSC-TA-TZ) project, supported by the United States Agency for International Development (USAID), […]

The post Performance and Analytics Advisor at Global Health Supply Chain Program appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Deputy Head KS Coordinator Y4 Teacher Y1 Teacher at Latham School

The Latham School is a private School, which offers a British international curriculum. We are an authorised Cambridge international School. Nursery and Reception Children follow the Early Years Foundation Stage programme. This is followed by the English National Curriculum up to IGCSE. All our pupils aged from 2 to 16 years are provided with a […]

The post Deputy Head KS Coordinator Y4 Teacher Y1 Teacher at Latham School appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Human Resource Manager at Mwananchi Communications Limited

About the job This role reports to the Managing Director MCL and is key in the design and implementation of the Country’s HR digital transformation initiatives. You will lead the delivery of the Country’s people agenda, ensuring the required HR strategies and services that support the Country’s performance and outcomes are met. As a member […]

The post Human Resource Manager at Mwananchi Communications Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Trial Attorney, P4 at UN/ IRMCT

Posting Title: Trial Attorney, P4 Job Code Title: LEGAL OFFICER Department/ Office: International Residual Mechanism for Criminal Tribunals Duty Station: ARUSHA Posting Period: 24 November 2020-23 December 2020 Job Opening number:20-LEG-RMT-144730-R-ARUSHA (R) Staffing Exercise ID:N/A United Nations Core Values: Integrity, Professionalism, Respect for Diversity Org. Setting and Reporting This position is located in the Office […]

The post Trial Attorney, P4 at UN/ IRMCT appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Senior Investigator, P4 at UN/ IRMCT

Posting Title: Senior Investigator, P4 Job Code Title: INVESTIGATOR Department/ Office: International Residual Mechanism for Criminal Tribunals Duty Station: ARUSHA Posting Period:24 November 2020-23 December 2020 Job Opening number:20-ING-RMT-144733-R-ARUSHA (R) Staffing Exercise ID:N/A Org. Setting and Reporting This position is located in the Office of the Prosecutor of the International Residual Mechanism for Criminal Tribunals, […]

The post Senior Investigator, P4 at UN/ IRMCT appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger