Thursday 1 October 2020

KISHINDO CHA MGOMBEA URAIS CCM DKT. JOHN POMBE MAGUFULI MJI WA VWAWA SONGWE LEO


Mambo mbalimbali yaliyojiri na aliyoyazungumza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dkt John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wake mkubwa wa Kampeni za Kuomba Kura kwenye Mji wa Vwawa Uliopo Mkoani Songwe leo Oktoba 1,2020. Kila anakopita Watu wanafurika. Nchi inamtaka Magufuli, Watu Wanaitaka CCM.#T2020JPM #MITANOTENA
Share:

Head of Business Performance & Analytics (BP&A) at Absa Bank

Bring your possibility to life! Define your career with us   With over 100 years of rich history and strongly positioned as a local bank with regional and international expertise, a career with our family offers the opportunity to be part of this exciting growth journey, to reset our future and shape our destiny as […]

The post Head of Business Performance & Analytics (BP&A) at Absa Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Veterinary Officer at Washington State University – Global Animal Health Tanzania

POSITION ANNOUNCEMENTS Washington State University – Global Animal Health Tanzania Global Animal Health Tanzania (GAHT), a legally registered NGO that is supported by Washington State University and collaborating partners in Tanzania, serves to manage a broad range of public and animal health research projects in Tanzania. GAHT has the following openings: Position: Veterinary Officer (1 […]

The post Veterinary Officer at Washington State University – Global Animal Health Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Field Officer at Washington State University – Global Animal Health Tanzania

POSITION ANNOUNCEMENTS Washington State University – Global Animal Health Tanzania Global Animal Health Tanzania (GAHT), a legally registered NGO that is supported by Washington State University and collaborating partners in Tanzania, serves to manage a broad range of public and animal health research projects in Tanzania. GAHT has the following openings: Position: Field Officer Contract […]

The post Field Officer at Washington State University – Global Animal Health Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

ToR Partnerships Advisor at D-tree International

We are seeking a Partnerships Advisor, based in Dar es Salaam, Tanzania, to lead D-tree’s partnerships efforts with the government, NGO partners and funders in Mainland Tanzania. Job Description Who we are D-tree International is a digital health organization with 15 years of experience using innovations in technology to strengthen the quality of health systems in […]

The post ToR Partnerships Advisor at D-tree International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Study Coordinator at MUHAS September

Job Title: Study Coordinator Reports to: Principal Investigator Location: Muhimbili University of health and Allied Sciences/  Tanzania Job Summary The E-MOTIVE research programme is seeking to deliver a reduction in morbidity and mortality from postpartum haemorrhage (PPH). The research is conducted in a coordinated fashion by the central coordinating hub in Birmingham (Birmingham Clinical Trials […]

The post Study Coordinator at MUHAS September appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Data Manager – E-MOTIVE trial at MUHAS

Job Title: Data Manager – E-MOTIVE trial Reports to: Study Coordinator Location: Muhimbili University of Health and Allied Sciences/ Tanzania Job Summary The E-MOTIVE research programme is seeking to deliver a reduction in morbidity and mortality from postpartum haemorrhage (PPH). The position is within the Tanzania central management team (Hub), and the Data Manager will […]

The post Data Manager – E-MOTIVE trial at MUHAS appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Research Nurse 20 posts at MUHAS

Job Title: Research Nurse Reports to: Study Coordinator Location: Mwanza, Simiyu, Geita and Pwani Regions Job Summary The E-MOTIVE research programme is seeking to deliver a reduction in morbidity and mortality from postpartum haemorrhage (PPH). The E-MOTIVE research programme is seeking to hire the services of 20 Research Nurse/Midwives to be based within study regions […]

The post Research Nurse 20 posts at MUHAS appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Picha : KAMPUNI YA AKO GROUP LTD YATOA MSAADA WA MIFUKO 200 YA SARUJI KUSAIDIA UJENZI MADARASA SHULE YA BUGARAMA

Kushoto ni Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi akimkabidhi mifuko ya saruji Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi kwa ajili ya ujenzi wa madaras katika shule ya Msingi Bugarama.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kampuni ya Ako Group Limited inayotoa huduma ya chakula na usafi wa mazingira katika Mgodi wa Bulyanhulu imetoa msaada wa mifuko 200 ya saruji yenye thamani ya shilingi milioni 4.2 ili kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga.



Mifuko hiyo ya saruji imekabidhiwa Jumatano Septemba 30,2020 na Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ambayo imefanyika katika shule ya Msingi Bugarama.



Akizungumza katika hafla hiyo iliyohudhuriwa pia na wafanyabiashara wanaoshirikiana na Kampuni ya Ako Group Limited Kahigi alisema wao kama wafanyabiashara wanaofanya kazi na Mgodi wa Bulyanhulu ni sehemu ya jamii hivyo wanao wajibu kusaidia jamii inayozunguka mgodi huo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria Mpya ya Madini.

“Tulitembelea shule hii ya Bugarama na kujionea jinsi wanafunzi wanavyosoma katika mazingira yasiyo rafiki kutokana upungufu wa madarasa na wingi wa wanafunzi nasi Ako Group Ltd tukaahidi kuchangia mifuko ya saruji 200 yenye thamani ya shilingi milioni 4.2 na leo tumekuja kuikabidhi ili ujenzi wa madarasa”,alisema Kahigi.

Aidha aliwashukuru wafanyabiashara wanaoshirikiana na Ako Group Limited kuchangia vifaa vya ujenzi na fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo huku akiwataka wajiandae kuzalisha zaidi kwani mgodi utaanza rasmi kufanya shughuli za uzalishaji rasmi hivi karibuni.

Katika hatua nyingine Ako Group Ltd inaendelea kusaidia jamii kwa kufanya shughuli mbalimbali kama vile kujenga chumba cha darasa katika shule ya sekondari Bulyanhulu pamoja na kutoa ajira katika mgodi wa Bulyanhulu ambapo wameajiri wafanyakazi 69 katika shughuli za upishi,usafi wa vyumba,ofisi na udhibiti wa taka kati yao wanawake ni 30,wanaume 39 kutoka vijiji 14 jirani na mgodi.

"Katika kutekeleza sheria Mpya ya Madini kupitia kitengo cha huduma za jamii inayozunguka eneo la Mgodi wa Bulyanhulu, Ako Group Ltd imeajiri mtu mwenye ulemavu wa ngozi 'mtu mwenye ualbino' Gaspal William kutoka kijiji cha Ilogi katika kitengo cha usafi wa ofisi na tayari kikundi kipya cha wanawake cha Mkombozi kutoka Igudija tumekipa utaratibu wa usambazaji matunda safi na mbogamboga kutoka kwenye mashamba yao",aliongeza Kahigi.

Akipokea mifuko hiyo ya saruji, Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala, Cosmas Magigi ambaye ni Afisa Elimu Shule za Msingi halmashauri hiyo,aliipongeza Kampeni ya Ako Group Limited ambao ni wakandarasi wazawa kusaidia sekta ya elimu ambapo baada ya ujenzi wa madarasa kukamilika watoto watasoma katika mazingira mazuri.

“Tunawashukuru sana Ako Group Ltd na wadau wengine waliojitokeza kuchangia vifaa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa hali ambayo itapunguza msongamano wa wanafunzi darasani. Tunaomba wadau wengine waendelee kutusaidia ili elimu iweze kupanda katika halmashauri yetu”,alisema Magigi.

Kwa Mujibu wa Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Bugarama Kubebeka Leonard alisema shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 2324, walimu waliopo ni 23,kuna upungufu wa walimu 27, madarasa yaliyopo ni 18 na kuna upungufu wa madarasa 32.

Naye Katibu wa Chama cha Ushirika Igaka, Emmanuel Kasala ambao ni miongoni mwa wadau wanaofanya biashara na Kampuni ya Ako Group Ltd waliochangia mifuko mitano ya saruji wamesema wataendelea kushirikiana na jamii kutatua changamoto zilizopo.

Katika hafla hiyo, Kampuni ya Ako Group Ltd imetoa zawadi ya ya vyeti kwa wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni hiyo ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao,ambao ni Afrimar, Alpher Choice, Igaka, Nyakabale, Mamuu Chicken, Bufaso,Mkombozi na Juago Food Products ambapo pia walichangia vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama kuunga mkono juhudi za Kampuni ya Ako Group Ltd.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kushoto ni Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi akimkabidhi mifuko ya saruji Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama Septemba 30,2020. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi ,Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi na viongozi wa shule na kijiji cha Bugarama wakipiga picha ya pamoja wakati wa makabidhiano ya mifuko ya saruji.
Muonekano wa sehemu ya mifuko 200 ya saruji iliyotolewa na Kampuni ya Ako Group Limited
Trekta la Ako Group Limited likiwa limebeba mifuko ya saruji.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi (kushoto) akipokea mifuko mitano ya saruji kutoka kwa viongozi wa Chama Cha Ushirika Igaka wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited.
Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi akielezea kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Kampuni hiyo katika Mgodi wa Bulyanhulu ikiwa ni pamoja na kusaidia jamii inayozunguka mgodi huo. Alisema wamekabidhi mifuko 200 ya saruji ili kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama. Kushoto ni Mwalimu Mkuu shule ya msingi Bugarama, Kubebeka Leonard. Wa kwanza kulia ni Meneja Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu, Dk. Zumbi Musiba.
Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi akizungumza wakati wa kukabidhi mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akiishukuru Kampuni ya Ako Group Limited kuchangia mifuko ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Mwalimu Mkuu shule ya Msingi Bugarama akiishukuru Kampuni ya Ako Group Limited na wadau wengine kuchangia vifaa vya ujenzi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Meneja Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu, Dk. Zumbi Musiba akizungumza wakati Kampuni ya Ako Group Limited inayojishughulisha na uuzaji wa vyakula na usafi wa mazingira katika mgodi wa Bulyanhulu ikitoa msaada wa mifuko ya saruji kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama iliyopo katika Halmashauri ya wilaya ya Msalala.
Afisa Mtendaji kata ya Bugarama Prisca Joseph akizungumza wakati Kampuni ya Ako Group Limited ikitoa msaada wa mifuko ya saruji kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama iliyopo katika Halmashauri ya wilaya ya Msalala.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Bugarama Emmanuel Masanja Mhoja akizungumza wakati Kampuni ya Ako Group Limited ikitoa msaada wa mifuko ya saruji kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama iliyopo katika Halmashauri ya wilaya ya Msalala.
Wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited wakiwa kwenye hafla ya kukabidhi vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited wakiwa kwenye hafla ya kukabidhi vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited wakiwa kwenye hafla ya kukabidhi vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Kulia ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa mfanyabiashara anayefanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa mfanyabiashara anayefanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa mfanyabiashara anayefanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa mfanyabiashara anayefanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog



Share:

Picha : MAGUFULI AKIWAHUTUBIA WANANCHI WA MBALIZI MBEYA LEO ASUBUHI


Baadhi ya Wananchi wakimsikiliza Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia wakazi wa eneo hilo la Mbalizi mkoani Mbeya wakati akielekea Tundumba kwa ajili ya Mikutano ya Kampeni za Urais kwa upande wa CCM leo tarehe 01 Oktoba 2020. 
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Mbalizi mkoani Mbeya wakati akielekea Tundumba kwa ajili ya Mikutano ya Kampeni za Urais kwa upande wa CCM leo Oktoba 01,2020. 

Share:

MWENYEKITI WA MTAA ASIMULIA JINSI MJUKUU WAKE WA MIAKA 7 ALIVYOCHINJWA NA MAMA YAKE

Picha haihusiani na habari hapa chini

Na Doreen Aloyce,TimesMajira, Online Dodoma

Mtoto wa miaka saba aitwaye Willy Wiliam mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Msingi Ihumwa ameuawa kwa kuchinjwa shingo na mtu anayedaiwa kuwa ni mama yake mzazi, Grace William (45) kisha kutokomea kusikojulikana.

Tukio hilo limetokea usiku wa manane kuamkia Septemba 30,2020 katika Mtaa wa Ihumwa, nje kidogo ya Jiji la Dodoma ambako mtoto alikuwa akiishi na mama huyo.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Ihumwa ambaye pia ni baba mzazi wa Grace, William Ngilimunji, amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kwamba aliyekufa ni mjukuu wake. Alidai wakati mauaji hayo yanafanyika mtoto alikuwa amelala.

Amedai kwamba aliyehusika na mauaji hayo ni mama wa mtoto huyo ambaye ana matatizo ya akili na kwamba alikuwa akihudhuria kliniki Hospitali ya Wagonjwa wa Akili Mirembe, mkoani hapa.

Ngilimunji amesema mtoto wake huyo (mama wa marehemu) hana mume na amekuwa akiishi Ihumwa. 

Via TimesMajira
Share:

Financial Management Analyst – OSC at U.S. Embassy Dar es Salaam

U.S. MISSION DAR ES SALAAM VACANCY ANNOUNCEMENT The U.S. Mission in Dar es Salaam is seeking eligible and qualified applicants for the position below. Position Title: Financial Management Analyst – OSC Vacancy Number: DaresSalaam-2020-029 Duties Budget Analyst 60% Serves as the Budget Analyst for the Office of Security Cooperation (OSC), with the responsibility of performing […]

The post Financial Management Analyst – OSC at U.S. Embassy Dar es Salaam appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Nyasa District Council Jobs September, 2020. Nyasa District is a district of the Ruvuma Region of Tanzania.

The deadline for submitting the application is October 13, 2020

The post Nyasa District Council Jobs September, 2020. Nyasa District is a district of the Ruvuma Region of Tanzania. appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MAASKOFU NA WACHUNGAJI WAZINDUA KITABU CHA UONGOZI ULIOTUKUKA WA RAIS JOHN MAGUFULI


Askofu Mkuu wa Makanisa ya Naioth Gospel Assemblies of God ambaye pia ni Katibu Mkuu mstaafu wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania, Dkt. David Mwasota.(kushot) akiwaongoza Maaskofu na Wachungaji kwenye maombi ya kukiombea Kitabu cha Uongozi Uliotukuka wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwanzoni mwa wiki.
Maombi ya kukiombea kitabu hicho yakiendelea kufanyika.
Askofu Mkuu wa Makanisa ya Naioth Gospel Assemblies of God ambaye pia ni Katibu Mkuu mstaafu wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania, Dkt. David Mwasota., akizungumza na Maaskofu na Wachungaji kwenye maombi ya kukiombea Kitabu cha Uongozi Uliotukuka wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwanzoni mwa wiki.
Muonekano wa kitabu hicho.
Askofu Sedrick Ndonde wa Kanisa la Restroration Bible ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kanisa hilo walioandika kitabu hicho.
Uzinduzi wa kitabu hicho ukifanyika.

Na Dotto Mwaibale

MUUNGANO wa Maaskofu zaidi ya 15 na Wachungaji 100 mwanzoni mwa juma walizindua kitabu kinachoelezea uongozi uliotukuka wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Kitabu hicho kimeandikwa na Mtendakazi katika shamba la Bwana, Restoration Bible Church Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi wa kitabu hicho kiitwacho Uongozi Uliotukuka, JPM ni Kiongozi wa Kisiasa na Kiroho, uliofanyika jijini Dar es Salaam uliongozwa na Askofu Mkuu wa Makanisa ya Naioth Gospel Assemblies of God ambaye pia ni katibu Mkuu mstaafu wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania, Dkt. David Mwasota.

Mwasota alisema lengo la kuandikwa kitabu hicho ni kutazama uongozi wa Rais Magufuli kwa pande za kisiasa na kiroho.

Askofu huyo alisema katika utendaji kazi wake, Magufuli anamtegemea Mungu hivyo kumfanya aonekane anaiongoza nchi kwa upande wa kiroho.

“Imani ya Mheshimiwa Magufuli katika kushughulikia janga la Corona kiroho limefanya kuinua imani ya watu wengi kwa kulisaidia kanisa ambalo ndiyo kazi yake kubwa kuwajenga watu kiimani,” alisema askofu huyo.

Mwasota aliwaomba maaskofu, wachungaji na waumini wote kuendelea kumuombea Rais Magufuli kwani ndiyo yalikuwa maombi yao kwa miaka mingi kwa Mungu atuletee kiongozi kama yeye.

“Tunamshukuru Mungu aliyejibu maombi yetu kwa kutuletea kiongozi tuliyemuomba miaka mingi ambaye ni Magufuli anayeliongoza taifa letu kisiasa na kiroho,” alisema Mwasota.

Askofu huyo aliongeza kuwa katika nchi yetu hatukuwahi kumpata kiongozi wa juu anayemtaja Mungu wakati wote na kuwaagiza watendaji wake kila anapowaapisha wamtangulize na kumtegemea Mungu.

Naye Bishop Sedrick Ndonde wa Kanisa la Restroration Bible ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kanisa hilo walioandika kitabu hicho, alisema lengo la kitabu hicho ni kuelezea ukweli kuhusu Rais Dkt. John Magufuli ili kufahamu zaidi nini alichobeba mbali ya wadhifa wa urais alionao na kulikumbusha kanisa na watumishi wa Mungu kuutafakari uongozi wake.

“Umuhimu wa kitabu hiki ni kuwakumbusha watumishi wa Mungu kuwa na muda wa kutafakari uongozi wa JPM kwa yote aliyoyafanya kwa upande wa kiroho,” alisema Askofu Ndonde.

Aliongeza kwa kumtegemea Mungu amefanya mambo makubwa kama kujenga miundombinu ya barabara, umeme, maji, shule, hospitali na kuwawezesha watanzania kunufaika na madini, mbuga za wanyama ambapo awali waliokuwa wakinufaika walikuwa watu kutoka nje.

 “Magufuli ni mfalme anayekiri ufalme wa Mungu kutawala taifa letu,” alisema Ndonde.

Ndonde aliongeza kuwa kuna umuhimu wa kukisambaza kitabu hicho kwa waumini wao na wananchi wengine kwa ujumla  bila kujali dini wala madhehebu wanayotoka ili waweze kuwa na mtazamo chanya. 




Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi October 1
















Share:

Wednesday 30 September 2020

Individual National consultancy at UNICEF

The aim is to assess whether the Parenting Education Programme has been implemented effectively and whether it has brought about positive change in the knowledge and behaviour of parents and caregivers in how to protect their children from violence. UNICEF works in some of the world’s toughest places, to reach the world’s most disadvantaged in […]

The post Individual National consultancy at UNICEF appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

HESLB Yatoa Siku Tano (05) Kwa Wahitimu Mafunzo Jkt Kuomba Mikopo


Na Mwandishi Wetu, HESLB
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa muda wa siku 5 kuanzia Oktoba mosi hadi 5 mwaka huu ili kuwawezesha wanafunzi waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) hivi karibuni kuingia katika mfumo wa kuomba mkopo kwa njia ya mtandao na kukamilisha maombi yao.

Katika taarifa yake aliyotoa kwa vyombo vya habari leo Jumatano (Septemba 30, 2020) Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru alisema uamuzi huo unatokana na maombi ya wanafunzi, wazazi na walezi ambao hawakuweza kuomba au kukamilisha maombi yao kutokana na sababu ya kujiunga na mafunzo hayo.

Kwa mujibu wa Badru alisema katika muda huo wa siku tano, mfumo pia utakuwa wazi ili kuwawezesha waombaji ambao maombi yao yana upungufu kurekebisha kwa kuweka nyaraka sahihi ili kuiwezesha HESLB kuendelea na hatua nyingine.

“Kwa wanaorekebisha taarifa, wanapaswa kuingia katika akaunti zao walizofungua kuombea mkopo na watapata ujumbe kuhusu maeneo ya kurekebisha. Tunawasihi watumie muda huu wa siku tano kurekebisha na kukamilisha maombi yao’’ alisema Badru.

Katika mwaka wa masomo 2020/2021, Serikali imetenga TZS Bilioni 464 zitakazowanufaisha jumla ya wanafunzi 145,000. Kati yao, wanafunzi 54,000 watakuwa wa mwaka wa kwanza na wengine 91,000 ni wanafunzi wanufaika wanaoendelea na masomo. Mwaka 2019/2020 jumla ya TZS 450 bilioni zilitengwa na zimewanufaisha jumla ya wanafunzi 132,119.

MWISHO


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger