Thursday 28 May 2020

Riwaya Kali ya Kusisimua....SIN- Sehemu Ya Tano (05)

Mwandishi- EDDAZARIA G.MSULWA
Age-18+
Simu-0657072588(whatsapp) au 0768516188


ILIPOISHIA
“Kwa nini kaka?”
“Kuna watu wana wateka watu na wanavishwa jina.... Yaani nashindwa hata kuelewa, tunaelekea wapi?”
“Nani mwengine ametekwa?”
“Si yule nabii Sanga wa kanisa la Heaven light ministry”
Mapigo ya moyo wa Magreth, yakasimama kwa sekunde kadhaa, kisha yakaanza kumuenda kasi, mwili mzima ukaanza kumtetemeka na jasho likimtiririka usoni mwake, hadi muendesha bajaji akabaki akiwa ameshikwa na butwaa kwa nini hali ya abiria wake imebadilika gafla mara ya kusikia taarifa hiyo.


ENDELEA   
“Dada upo salama?”
Dereva wa bajaji aliuliza huku akimtazama Magreth kwa macho ya kuiba iba kwani anahitajika kuwa makini katika barabara hiyo yenye magari mengi sana.
“Dada”
“Beee”
“Upo salama?”
“Umesema wamemteka nani?”
“Nabii Sanga, “
“Wamemuaa?”
“Hapana, hakuna taarifa kama hiyo, ila polisi wana dai kwamba gari lake kwenye kioo cha mbele kilipigwa kwa risasi moja”
Magreth akazidi kutetemeka kwa woga huku hali ya kukata tamaa ikiendelea kumtawala. Akataka kupiga namba ya nabii Sanga na kujikuta nafsi yake ikiendelea kusita na kushindwa kabisa kufanya hivyo. Akafikishwa hospitalini, akamlipa muendesha bajaji kiasi cha pesa anacho kihitaji, kisha akashuka kwenye bajaji hiyo, huku mwili mzima ukiwa umeishiwa na nguvu. Akaanza kutembea kwa mwendo wa taratibu, huku akihisi kukata tamaa, ndoto zake zote ambazo kwa siku hiyo zilikuwa zinakwenda kutimia, zote zimepotea. Akaingia ndani ya chumba alicho lazwa Evans. Wakatazamana na Evans kwa sekunde kadhaa kisha akaanza kuangua kilio kizito, kilicho mfanya Evans kushangazwa.
“Hei Mage kwa nini unalia?”
“Mchungaji?”
“Mchungaji amefanya nini?”
“Ametekwa na watu wasio julikana”
Habari hii hakika haikuwa nzuri kwa Evans.
“Mchungaji gani lakini, au yule uliye kuja naye hapa jana usiku?”
“Huyo huyo, ohoo Mungu wangu. Ni kina nani wamemfanyia mambo hayo jamani”
Magreth alizungumza huku akiendelea kulia kwa uchungu sana, hadi ikamlazimu, Evans kuanza kumbembeleza.
                                                                                                                                ***
    Majira ya saa mbili asubuhi, watekaji wawili wakaingia kwenye chumba walicho muhifadhi nabii Sanga. Wakamfungua kamba walizo mfunga na kumkalisha kwenye kiti. Wakamfungua kitambaa usoni mwake. Nabii Sanga akakutana na wanaume hao ambao wameendelea kufunika sura zao. Mbele yake kuna meza iliyo wekwa kikombe cha chai ya maziwa pamoja na vipande vinne vya mkate ulio pakwa blueband vizuri.
“Pata kifungua kinywa”
Mtekaji mmoja alizungumza huku mkononi mwake akiwa na bastola.
“Vijana, ninaomba tuweze kuzungumza. Kama ni pesa ambayo mumelipwa kwa ajili ya kuniteka. Tafadhali, nipo tayari kuhakikisha kwamba nina walipa mara mbili ya pesa hiyo ambayo mume pangiwa kunilipa”
“Mzee acha siasa, unahitaji kula au unahitaji kufa?”
Mtekaji wa pili alizungumza kwa ukali sana, mwezake akamnyooshea mkono kwa ishara ya kumuomba aweze kutulia.
“Una weza kutupatia ofa gani?”
“Mkuu unakosea?”
“Hapa, tuna fanya kazi hii kwa pesa. Upo tayari kutupa ofa gani?”
Mtekaji huyo alizugumza huku akisimama mbele ya nabii Sanga.
“Semeni aliye wapa hii kazi amewalipa kiasi gani?”
“Milioni ishirini”
“Nipo tayari kuwapa milioni hamsini by cash”
“By cash, unazo hapo ili uweze kutupatia?”
“Mukikubali na mukiniamini basi nita hakikisha kwamba nina wapatia hicho kiasi. Ila kabla sijafanya hivyo, nina waomba muweze kunisaidia jambo moja”
“Jambo gani?”
“Ninahitaji kumfahamu mtu aliye weza kutoa kazi hii”
“Siku zote huwa tuna linda siri za wateja wetu. Hatuto weza kukuambia ni nani ambaye ametupatia kazi hiyo.”
“Milioni sabini nawapatia”
“Hatuwezi kutoa siri”
“Milioni themani”
“Mzee hatuto weza kukuambia siri kwa ajili ya pesa”
“Milioni mia moja cashe munazipata katika siku hii hii ya leo”
Watekaji hawa wakatazamana usoni. Hapakuwa na kazi kubwa walio ifanya kwenye maisha yao, ambayo walihi kulipwa milioni mia moja. Uchu wa pesa ukawajaa mioyoni mwao, wakavutana pembeni ya chumba hicho na kuanza kunong’onezana.
“Mkuu tukubali hiyo ofa, milioni mia moja ni kubwa sana”
“Kawaite wezako”
“Sawa”
Mtekaji huyo akatoka na baada ya dakika moja akarudi akiwa ameongozana na wezake ambao nao sura zao wamezifunika. Mkuu wao akawaeleza ofa iliyo wekwa mezani na nabii Sanga.
“Mkuu ni pesa nyingi, kama ana uhakika wa kutupatia hicho kiasi hakuna haja ya sisi kuendelea kumshikilia. Yaani hapo ni sawa una ambiwa uchague Vitz na Hammer”
Hapakuwa na mtekaji yoyote ambaye aliweza kukataa ofa hiyo.
“Natambua kwamba muna fanya kazi hii kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya maisha yenu, ikiwemo familia zenu. Nipo tayari kuwalipa kiasi hicho cha pesa na nyinyi mkawa ni watu wa mkono wangu wa kushoto”
Nabii Sanga aliendelea kuwashawishi watekaji hawa.
“Una maanisha nini kusema tuwe watu wa mkono wako wa kushoto?”
“Haya ni maisha, kesho na kesho kutwa nami nitakuwa na kazi ya kuwapatia, je mtashindwa kuifanya?”
Watekaji hawa wakatazamana huku sura zao wakiwa wamezifunika na kubakisha macho tu.
“Tutafanya”
“Basi kwa leo nipatieni hiyo nafasi ya kuwalipa na muweze kuniambia ni nani ambaye ameifanya kazi hiyo.”
Ushawishi wa nabii Sanga ukazidi kuwapagawisha watekaji hawa.
“Sawa tupo tayari ila kwa sharti moja”
“Niambieni”
“Pesa tuna ihitaji iweze kuletwa hapa”
“Ndio iletwe hapa, hatuwezi kurudi mjini. Polisi wapo makini kukutafuta nchi nzima. Changanua akili yako kisha hakikisha kwamba hiyo pesa ina letwa hapa na huyo atakaye ileta hapa awe ni mtu ambaye una muamini na asije akafanya kosa lolote la kipumbavu, kuwaeleza polisi. Akifanya hivyo nina apia kwa MUNGU. Nitakuchinja kama kuku”
Mkuu wa kikosi hicho cha watekaji alizungumza huku akimtazama nabii Sanga usoni mwake. Nabii Sanga akaanza kuchanganua akilini mwake ni nani ambaye ata muamini. Akili ikatua kwa mke wake, ila akajikuta akipata ukinzani mkubwa sana moyoni mwake.
‘Kwa nini nafsi yangu ina kataa kwa mke wangu. Kuna nini?’
Nabii Sanga alizungumza kimoo moyo huku akiendelea kutafuta ni nani ambaye anaweza kumuamini na kumkabidhi kazi hiyo. Akafikiria baadhi ya wachungaji wa kanisani kwake, ila hapo napo hakuweza kupata mtu wa uhakika wa kuwaamini.
“Mzee una dakika moja ya kutujulisha ni nani utakaye muamini”
Mtekaji huyo alizungumza na kumfanya nabii Sanga kuongeza umakini wa kuwachanganua watu wake wa karibu na kujua ni nani anaweza kuwaamini. Akili ikaangukia kwa Magreth, mwanamke aliye tokea kumpenda na kumjali kwa kipindi cha hivi karibuni. Moyo wake katika kumuamini Magreth haukuwa na wasiwasi hata kidogo.
“Nimempata”
“Nani?”
“Ahaa ni muumini wangu wa karibu ana itwa Magreth”
“Muumini, hato weza kutoboa siri kwa askari?”
“Hapana. Nina muamini sana.”
Watekaji hawa wakatazamana kisha mkuu wao akamsogelea nabii Sanga. Akamtazama machoni mwake kwa sekunde kadhaa kisha akatoa simu yake na kuiweka mezani.
“Endapo utafanya kosa lolote, nitakufumua ubongo wako. Mpigie na uweke loud speaker”
“Sawa sawa”
Nabii Sanga akaichukua simu hiyo, akafumba macho yake kwa sekunde kadhaa, huku akijaribu kuikumbuka namba ya Magreth na kwa bahati nzuri akafanikiwa kuikumbuka, akaiingiza katika simu hiyo kisha akaipiga na kwa bahati nzuri akakuta ina patikana hewani.
                                ***
    Mlio wa taratibu unao ita katika simu yake, ukamfanya Magreth kuitazama simu yake. Evans aliye lala pembeni yake, naye akamtazama Magreth kwa sekunde kadhaa anaye endelea kuitazama simu yake inayo ita.
“Mbona hupokei simu?”
“Hii namba yangu ni mpya na hakuna mtu yoyote anye ifahamu”
“Mmmm sasa inakuwaje watu wameifahamu?”
Evans aliuliza, taratibu Magreth akaipokea simu hiyo na kuiweka sikioni mwake.
“Haloo”
Magreth alizungumza kwa umakini sana huku akisubiria kusikilizia ni nani huyo aliye mpigia.
“Ni mimi Magreth, usijaribu kutaja jina langu wala kuonyesha dalili yoyote ya kuweza kunifahamu, kwa maana nina hisi upo na watu”
Sauti ya nabii Sanga ikamfanya Magreth macho kumtoka. Akasimama huku akiwa amejawa na tabasamu.
“Nisikilize kwa umakini mkubwa sana, kwanza upo wapi?”
“Hospitali”
“Simama sehemu ambayo hakuna mtu anaye weza kusikiliza mazungumzo yetu”
Magreth kwa haraka akatoka ndani humo pasipo hata kumuaga Evans. Akatafuta eneo lisilo na mtu na akasimama.
“Unaweza kuendelea”
“Nipo chini ya watekaji, wanahitaji kiasi cha milioni mia moja.”
“Mungu wangu!!”
“Nisikilize, wewe ndio mtu wa pekee ambaye ninakuamini na unaye weza kunisaidia mimi kutoka katika kifungo hichi”
Nabii Sanga alizungumza kwa msisitizo mkubwa sana.
“Ehee”
“Nenda pale kanisani, password ya mlango wa ofisini kwangu ni tisa, moja, moja tisa moja, sifuri. Fungua mlango wa ofisini kwangu, kuna shelf kubwa imo mule ofisini, fungua hiyo shelf kwa kutumia password hizo hizo nilizo kutajia. Kuna pesa za kimarekani. Chukua dola alfu sitini, weka kwenye begi, ukifanikisha kufanya hivyo hakikisha kwamba una piga namba hii, kwa ajili ya maelekezo zaidi. Ninakuomba Magreth usimuambie mtu wa aina yoyote. Ukifungua kinywa chako, basi tambua mimi huku nina kufa”
Magreth mwili mzima ukamtetemeka, akashusha pumzi huku akifikiria ni wapi anapo weza kuanzia.
“Baba mchungaji lakini upo salama”
“Ndio yupo salama na endapo utafungua kinywa chako kwa askari. Tutamuua na wewe tutakutafuta na kukuua”
Sauti hiyo nzito ya mwanaume, ikamstua sana Magreth. Mwili mzima ukazidi kutawaliwa kwa woga. Simu ikakatwa na kumfanya aishiwe hata nguvu za kusimama. Akakaa chini kwa sekunde kadhaa huku akitafakari ni wapi kwa kuanzia.
‘Lazima nimsaidie, ndio lazima nimsaidie’
Magreth alizungumza kimoyo moyo huku akinyanyuka eneo hilo. Wazo la kurudi chumbabini kwa Evans wala hakuweza kuwa nalo kabisa. Akakodisha pikipiki na akarudi nyumbani kwake, akatoa nguo zilizomo kwenye begi lake la mgongoni. Alipo hakikisha begi hilo halina nguo akalivaa na kutoka ndani humu. Akapanda pikipiki nyingine na kufikishwa kanisani. Kutokana mlinzi wa kanisa hilo wana fahamiana, hapakuwa na tatizo la yeye kufunguliwa geti.
“Mage una habari yoyote ya kupatikana kwa nabii?”
Mlinzi aliuliza huku akiwa amejawa na unyonge mkubwa sana.
“Hapana kaka. Nimekuja kumuomba MUNGU japo aweze kulete rehema yake”
“Sawa Mage ila huko hakuna mtu yoyote”
“Hakuna shaka”
Magreth akamuongopea mlinzi huyo. Akaingia kwa mlango wa mbele wa kanisa hilo, ili kumdanganya mlinzi asiweze kufahamu kwamba lengo na nia iliyo mleta hapo kanisani ni kuingia katika ofisi ya nabii Sanga. Magreth akatoke katika mlango mwingine wa kanisa hilo na kuelekea ilipo ofisi ya mchungaji. Akasimama mlangoni hapo na kuchunguza eneo hilo kwa umakini. Alipo hakikisha hakuna mtu wa aina yoyote akaingiza namba hizo za siri alizo tajiwa na mchungaji. Mlango ukafunguka na kuzama ndani na huku nyuma mlango ukajifunga.
Magreth akaanza kuangaza macho yake huku na huku na kufanikiwa kuona shelf kubwa iliyomo ofisini hapo, akaisogelea na akaingiza namba hizo za siri. Mlango mzito wa shelf hiyo ukafunguka. Magreth macho yakamtoka mara baada ya kukuta vibunda vya pesa za kimarekani(USD DOLLARS) vikiwa vimepangwa vizuri. Akaanza kuvihesabu kwa haraka haraka. Alipo hakikisha kwamba ni dola elfu stini, akaziingiza kwenye begi lake na kulivaa mgongoni. Akaanza kutembea kuelekea mlangoni, ila kabla hajaufungua mlango, akasikia hatua za miguu ya watu zikija katika mlango huo. Akatazama eneo hilo na kwa haraka akakimbilia kwenye moja ya sofa iliyomo ndani humo. Akajificha nyuma ya sofa ambapo sio rahisi kwa mtu kuweza kumuona.
“Yaani mpenzi wangu, nimewakimbia maaskari nyumbani kwa ajili yako. Nimeona tusikutanie kwako kwa maana una weza kufaatiliwa na ukakamatwa bure”
Sauti ya mama chungaji ikamstua sana Magreth aliye jibanza nyuma ya sofa hilo.
“Usijali mpenzi wangu, acha nikupe chap chap tuondoke kwa maana nina hamu na wewe sasa”
Sauti ya Tomas haikuwa ngeni kabisa masikoni mwa Magreth, kwani mtu huyo ni jana tu ametoka kuonana naye uso kwa uso.
“Ila vijana wako walio mteka huyo mpuuzi, una waamini au ni watu wa ajabu ajabu?”
Magreth akazidi kujawa na mshangao ulio sababisha mapigo yake ya moyo kuanza kumuenda kasi sana. Siri ya Mrs Sanga na Tomas, imevuja masikioni mwake.
“Nina waamini sana, tena hakuna ambaye ana weza kuenenda kinyume na mimi. Unacho paswa ni wewe kunipatia milioni arobaini za kuwalipa tu”
“Usijali pesa sio tatizo kwangu, jambo la msingi ni kuhakikisha kwamba wana mshikilia hadi wiki ijayo, na akiondoka kuelekea nchini Nigeria, yule kimada wake aliye panga kumnunulia nyumba na kumfungulia mgahawa nitamuua kwa mikono yangu mimi mwenyewe.”
Maneno hayo ya Mrs Sanga yakamfanya Magreth kuhisi haja ndogo ikianza kumtoka. Kama mwana mama huyo amefanya maamuzi ya kumteka mume wake bila ya huruma na yeye ndio anaye faatia kuuwawa, je itakuwaje endapo wata muona nyuma ya sofa hilo.
                                                                                                   ITAENDELEA
Haya sasa Magreth ametambua siri ambayo hakuna mtu mwingine ameweza kuifahamu huku akiwa na mzigo mkubwa sana wa kumsaidia nabii Sanga.Je ataweza kumsaidia nabii huyo?. Nini kitatokea? Endelea kufatilia kisa hiki cha kusisimua, usikose sehemu ya 06

 


Share:

Kenya Yaendelea Kurekodi Maambukizi Makubwa Zaidi Ya Wagonjwa Wa Corona

Idadi ya maambukizi ya corona nchini Kenya imefikia watu 1618, hii ni baada ya watu 147 zaidi kuthibitishwa kuwa na virusi hivyo katika muda wa saa 24 zilizopita baada ya sampuli 2831 kufanyiwa uchunguzi.

Waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema  kuwa miongoni mwa maambukizi hayo mapya 147, 90 ni jijini Nairobi na 41 ni huko Mombasa.

Vilevile idadi ya waliofariki imefikia 58 baada ya watu wengine watatu kufariki,wawili huko Mombasa na mmoja huko Kiambu.

Idadi ya waliopona imefikia 421 baada ya watu 13 zaidi kupona na kuondoka hospitalini.


Share:

Mpangaji Anayelipa Kodi Ya Zuio Anapaswa Kurejeshewa Na Mwenye Nyumba

Na. Peter Haule na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Serikali imesema kuwa Sheria ya Kodi ya Mapato inaruhusu mpangaji wa nyumba ya biashara kusajiliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania na kuwa Wakala wa ukusanyaji wa Kodi ya Zuio (Withholding Tax) hivyo kuwa sehemu ya mlipaji wa kodi ya pango.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Pauline Gekul, aliyetaka kujua lini Serikali itabadili utaratibu wa kumtoza mpangaji wa nyumba ya biashara Kodi ya Zuio ya asilimia 10 badala ya mpangishaji.

Dkt. Mpango alisema kuwa, Kodi ya Zuio siyo ya mpangaji, na kwa kuwa Sheria ya Kodi ya Mapato inamtambua mpangaji kama Wakala, kiasi cha kodi ya pango ambacho kimelipwa na mpangaji huhesabiwa kama sehemu ya fedha ambazo anapaswa kurejeshewa na mwenye nyumba.

“Kwa mujibu wa Sheria ya Kodi ya Mapato, mpangaji ambaye sio mfanyabiashara na hajasajiliwa na TRA kama mlipakodi hapaswi kukusanya kodi hii”, alieleza Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango alisema kuwa utaratibu wa ukusanyaji Kodi ya Zuio kupitia Wakala ambaye ni mpangaji umewekwa ili kurahisisha ukusanyaji wa kodi hiyo, kwa kuwa inarahisisha ukusanyaji wa kodi hasa ambapo mpangishaji hajasajiliwa na TRA kama mlipa kodi.

Sheria ya Kodi ya Mapato inamtaka mmiliki wa nyumba ya biashara mwenye mapato yanayozidi shilingi laki tano kulipa Kodi ya Zuio kutokana na mapato yanayotokana na upangishaji wa pango (rental tax) kwa kiwango cha asilimia 10 ya mapato ya kodi ya pango husika.

Mwisho.


Share:

Jakaya Kikwete: Hostel za Magufuli Ziko Salama na tayari kwa matumizi, Vijana Njooni Muendelee na Masomo

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jakaya Kikwete amesema hosteli za chuo hicho maarufu hostel za Magufuli ambazo zilibadilishwa matumizi na kuwa karantini kwa watu waliokuwa wakitoka nchi za nje ikiwa ni hatua ya kupambana na corona, ziko salama na tayari kwa matumizi. 

Kikwete ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Mei 28, alipotembelea hosteli hizo kwa ajili ya kukagua mazingira kabla ya wanafunzi kuanza kupokelewa kwa ajili ya kuendelea na masomo yao kuanzia Juni Mosi mwaka huu. 

"Tulitaka waliochukua ile hosteli watangaze rasmi kwamba wameshafanya yale yote waliyoahidi, ya kutayarisha hii hosteli kuwa salama kwa ajili ya kupokea wanafunzi wetu.  Kauli hiyo hatutakiwi kutoa sisi, wala DVC, tunataka watoe wenyewe waliochukuliwa hizo hosteli na waeleze walichokifanya kuhakikisha wanafunzi na jamii yetu kwamba hapa mahali pako salama, kwa hiyo Neema ( kwa niaba ya mganga mkuu wa mkoa Dar) nikushukuru kwa kauli uliyotoa, wamekusikia

"Niliposikia wanawaleta wasafiri kutoka nje na kukaa hapa kwa siku 14, shaka yangu kubwa ilikuwa, itakuwaje kama hao watu watakuwa na maradhi, je, wakiondoka hawataacha mbegu? Na vijana wetu wakija wakaja kupatia maradhi hapa?

"Lakini tukazungumza sana na uongozi wakanihakikisha kwamba serikali imechukua tahadhari zote kuhakikisha panakuwa  sterilized, disinfected kiasi cha kutosha ili wakija vijana pasiwe na shaka yoyote. Waliponieleza hivyo nilipata matumaini. Lakini nikawaeleza kuwa lazima tuhakikishe hilo limefanyika kwa sababu hatutaki hii kambi tukufu sana yenye jina la Rais… iwe ndio kitovu cha ugonjwa.

"Maana watu walikwenda makwao, isije ikatokea watakaporudi wakaugua wakasema si unaona serikali imewaleta na wametuachia mbegu za virusi. Hata tulipopata agizo la vyuo vifunguliwe mazungumzo yangu na DVC yslikues ni  kwamba tumejiandaaje. Akaniambia tumeshajiandaa vya kutosha ndipo siku ya pili yake ikatoka kwamba vyuo vifunguliwe Juni mosi

"Kwa maeleo yake ni kwamba hakuna hata mmoja miongoni mwa 426 waliogusana wale waliokutwa na maambukizi, 418 wametoka, kati ya hao hakuna hata mmoja aliyekutwa na virusi, kwa maana waliokuwepo hapa walikuwa salama ina maana kuwa hapa ni salama, ila makubaliano yetu ni lazima kufanya disinfection na wamefanya mwezi moja uliopita.

"Kwa hiyo tunaichukua kauli yenu kwamba pako salama, niwahakikishie vijana kwamba pako salama njooni, wale tuliowakabidhi wamefanya vile tulivyokubaliana, basi likitokea la kutokea tutawasiliana

"Lakini kwa upande wenu mmefanya tuliyoahidiana, kwa niaba ya uongozi wa chuo niwashukuru. Mmetimiza ahadi yenu, ndio uungwana. Ada ya mja hunena muungwana ni vitendo, mmenena lakini pia mmetenda." Amesema Kikwete


Share:

Taarifa Kwa Umma Kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete-JKCI Kuhusu Kutohusika Kwa Njia Moja au Nyingine na Mashindano ya Mbio za Heart Marathon 2020

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kuujulisha Umma kuwa haihusiki kwa njia moja au nyingine na mashindano ya mbio za Heart Marathon 2020 yaliyokuwa yafanyike  tarehe 19 Aprili mwaka huu jijini Dar es Salaam na Zanzibar na kuahirishwa kutokana na kuwepo kwa ugonjwa unaosababishwa na Virusi vya Corona (COVID – 19).

Mbio hizo za Heart Marathon ambazo zimepangwa kufanyika siku za mbeleni zimeandaliwa  na Asasi ya kiraia ya Tanzania Health Summit na siyo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Aidha Taasisi inatoa rai kwa wananchi watakaopenda kushiriki katika mashindano hayo kuwasiliana moja kwa moja na waandaaji  kama matangazo yao yanavyoonesha.

Hata hivyo kama unapenda kuchangia sehemu ya gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto wanaotoka katika familia zenye uwezo mdogo kiuchumi wanaotibiwa katika Taasisi yetu unakaribishwa. Unaweza kuchangia kiasi chochote cha fedha kupitia  namba ya malipo ya Serikali 994830000022.


Share:

Kutana na Mtabibu wa Nyota za Binadamu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo fanya mawasiliano kupitia wasaa Husika.

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasiliana nae sasa atatue tatizo lako.
.
Adam shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu. Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI
.
Nguvu za KIUME, Kesi .... Kwa mawasiliano piga simu namba(+255 )715971688 au (+255 )756914036
.+255 712921834
.

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE


Share:

Logistics Officer at Kibogate Company Limited

Position: LOGISTICS OFFICER (1 POSITION) EQUPOINT PROPERTIES LTD Job Summary Kibogate Tanzania Ltd is a main distributor of both road and building materials including granite aggregates, washed sand, Pit Sand, crushed stone , building blocks , iron steel, Pavel’s and others, The company is located in Dar es Salaam and now looking forward to extend its other branches in Coastal… Read More »

The post Logistics Officer at Kibogate Company Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job at Tanga Cement PLC, Dispatch Clerk II

Dispatch Clerk II Employment Opportunity Position: Dispatch Clerk II Reporting to: Weighbridge Supervisor Location: Tanga Key responsibilities: Responsible for Weighbridge administration ensuring compliance with procedures Principle Accountabilities: Accurate weighing and recording of truck weights Preparation of daily and monthly weighbridge reports Plan, coordinate and control plant operations Customer Care Ultimate responsible for safe working practices especially areas of… Read More »

The post Job at Tanga Cement PLC, Dispatch Clerk II appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Mwanamke Aua Mwanae Na Kisha Kumzika Baada Ya Kutelekezwa Na Mwanaume Aliyempa Mimba

Na salvatory Ntandu
Mkazi wa kijiji cha Seke Ididi wilayani Kishapu mkoani shinyanga Lucia Lukenya (42) kwa tuhuma ya kumuua na kisha kumzika mwanae mwenye jinsia ya kiume mwenye umri wa siku mbili.

Akizungumza na Waandishi wa habari Leo Mei 28 mwaka huu Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Aprili 19 Mwaka huu katika kitongoji cha Wizunza wilayani humo baada ya kujifungua.

Alisema kuwa Lucia alikamatwa na jeshi la polisi Mei 26 mwaka huu majira ya saa 12 baada ya wananchi wa kitongoji hicho kubaini hana mtoto aliyejifungua salama ndipo walipoamua kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi.

"Uchunguzi wa awali unaonesha kuwa Mtuhumiwa alijifungua mtoto huyo tarehe 17/4/2020 na kisha kumuua Tarehe 19/4/2020 na kuamua kumzika peke yake katika eneo la shule ya msingi Ididi majira ya saa 12 jioni wakati mvua ikiendelea kunyesha ili watu wasimuone,"alisema Magiligimba.

Kamanda Magiligimba alifafanua kuwa Mabaki ya mwili wa marehemu yalipatikana tarehe 26 mwaka huu katika kaburi alilozikwa na Mtuhumiwa huyo na kukabidhiwa kwa ndugu zake kwaajili ya taratibu za mazishi.

Ameongeza kuwa chanzo cha mauaji hayo ni ugumu wa maisha baada ya kutelekezwa na mwanaume aliyempa mimba na kutoa wito kwa wananchi mkoani humo hususani wanawake kuacha kukatisha uhai wa watoto kwa visingizio vya   kutelekezwa na badala yake wafike katika madawati ya jinsia yanayopatikana katika vituo vya polisi ili kupata ufumbuzi.

Amesema baada ya kukamilika kwa upelelezi mshitakiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Mwisho.


Share:

Mwongozo Wa Udhibiti Wa Maambukizi Ya Ugonjwa Wa Corona (Covid-19) Katika Shule, Vyuo Na Taasisi Za Elimu Nchini

Kufuatia Mlipuko wa Ugonjwa wa Homa kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19) uliripotiwa kwa mara ya kwanza hapa nchini tarehe 16 Machi, 2020, Serikali ilichukua hatua mbalimbali kwa ajili ya kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huu nchini. 


Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kufunga shule zote za Awali, Msingi, Sekondari, Vyuo na taasisi za elimu nchini. Kutokana na takwimu za mwenendo wa ugonjwa huu nchini kwa sasa kuonyesha kupungua kwa maambukizi ya Virusi vya Corona, mnamo tarehe 20 Mei 2020 Serikali kupitia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ilitangaza uamuzi wa kurejesha ratiba za masomo kwa shule (Kidato cha 6), Vyuo na Taasisi za Elimu kuanzia tarehe 01 Juni 2020.  
 
Katika kuendeleza jitihada za kudhibiti maambukizi mapya ya virusi vya Corona (COVID-19) nchini, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeandaa Mwongozo huu ambao unalenga kuweka mazingira wezeshi ya udhibiti wa maambukizi ya COVID-19 katika Taasisi za Elimu ikiwa ni pamoja na Vyuo, Shule za Sekondari na Shule za Msingi.  
 
Ili kufanikisha uwepo wa mazingira hayo, Mwongozo huu umezingatia maeneo makuu manne ambayo ni Maandalizi ya mazingira ya taasisi za elimu kabla ya kufunguliwa, Uchunguzi wa Afya, Usafiri wa kwenda na kurudi shuleni/Chuoni na Mazingira ya kujifunzia kama inavyoonekana hapo chini: - 

    i. Maandalizi ya Mazingira ya Taasisi za Elimu kabla ya kufunguliwa 
    a. Kutakasa (Decontamination) mazingira yote ya shule, Chuo au taasisi kwa kuzingatia miongozo ya utakasaji iliyotolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Hii inahusisha taasisi ambazo zilitumika kwa ajili ya kutunza washukiwa au wagonjwa wa Corona. Utakasajii huu ufanyike angalau masaa 72 kabla ya wanafunzi kuingia.  
 
    b. Siku ya kwanza ya kufunguliwa shule, chuo au taasisi ya Elimu ni muhimu itumike kutoa elimu kwa wanafunzi/wanachuo na wafanyakazi wote kuhusu ugonjwa wa COVID-19 pamoja na dalili zake na hatua za kuchukua ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huu.  
 
    c. Kuhakikisha uwepo wa vifaa vya kunawia mikono (sabuni na maji tiririka) kwa ajili ya usafi wa mikono katika kila eneo au maeneo ya madarasa, ofisi, kila geti/lango kuu, mabweni, maktaba, bwalo la chakula, vyoo na maeneo mengine muhimu. Wizara inasisitiza matumizi ya sabuni na maji tiririka ndiyo iwe njia kuu ya usafi wa mikono. Vilevile vifaa vya kunawa mikono vizingatie mahitaji ya wanafunzi/wanavyuo wenye ulemavu. Aidha, Vitakasa Mikono (Hand sanitizer) vinaweza kutumika kama mbadala wa maji tiririka na sabuni.  
 
    d. Uongozi wa Shule/Chuo uhakikishe vitakasa mikono (hand sanitizer) vinavyotumika vina ubora unaotakiwa (iliyotengenezwa kwa ethanol yenye asilimia zaidi ya 70) kwa wanafunzi na wanavyuo. Matumizi ya vitakasa mikono ni suala la hiari kwa mwanafunzi/mwanachuo kwa sababu Wizara tunasisitiza zaidi matumizi ya maji tiririka na sabuni.  
 
    e. Spirit (Methanol) isitumike kama kitakasa mikono katika maeneo yote ya shule, Chuo na taasisi. Wanafunzi wasiagizwe kwenda na spirit shuleni na Chuoni. Uongozi wa Shule/Chuo uhakikishe wanafunzi hawaingii na spirit katika maeneo/Taasisi zao.  
 
    f. Shule, Chuo au taasisi yenye vituo vya kutolea huduma za afya, watumishi wote wanaohusika wapewe elimu juu ya kuwahudumiwa wanafunzi, walimu na wafanyakazi wote watakaoshukiwa kuwa na COVID-19 ikiwemo kuwapatia msaada wa kisaikolojia na kuondoa unyanyapaa. Aidha, Shule/Chuo/Taasisi hizi zinapaswa kuwa na dawa na vifaa kwa ajili ya dharura.  
 
    g. Uongozi wa Shule, Chuo na taasisi za Elimu zinazotoa huduma za kulaza wanafunzi (bweni) uhakikishe kadri inavyowezekana kunakuwepo na nafasi ya kutosha kati ya kitanda kimoja hadi kingine na kudhibiti uchangiaji vifaa kwa wanafunzi kama vile taulo, mashuka, vyombo vya kuogea na vifaa vya usafi wa mwili.  
 
    h. Uongozi wa Shule, Chuo na taasisi za elimu zihamasishe wanafunzi, walimu na wafanyakazi wao kuvaa barakoa za vitambaa (Cloth masks) wakati wanaporudi shuleni au vyuoni. Aidha, wazazi/walezi wahimizwe kuwapatia watoto wao barakoa za vitambaa kabla ya kwenda shuleni/Vyuoni.  
 
    i. Uongozi wa Shule, Chuo na Taasisi za elimu ziweke utaratibu mzuri wa upatikanaji wa barakoa za vitambaa  (Cloth Masks) zinazotengenezwa nchini na ambazo vinaweza kufuliwa na kupigwa pasi kila siku katika maeneo yao kwa gharama nafuu. Barakoa za vitambaa vya pamba zenye safu mbili (two layers) ndizo zinazoshauriwa kuvaliwa kwa kuwa ni bora na salama kiafya.Wazazi wanaweza kuwapa au kuwanunulia watoto wao.  
 
    j. Uongozi wa Shule, Chuo na Taasisi ya Elimu unapaswa kuhakikisha uwepo wa vifaa vya kuhifadhia taka zitokanazo na barakoa zilizotumika na kuziteketeza kama taka nyingine hatarishi ili kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona. 

ii. Uchunguzi wa Afya;
 a. Wanafunzi watakaohisiwa kuwa na dalili za COVID-19 wafanyiwe vipimo kabla ya kurudi shuleni/chuoni. 
 b. Wanafunzi watakaobainika kuwa na maambukizi wabaki nyumbani hadi hapo hali zao za afya zitakapoimarika. 
 c. Kwa wanafunzi ambao watabainika kuwa na dalili za ugonjwa wa Corona wakiwa Shuleni/chuoni, Uongozi wa Shule au chuo utoe taarifa kwenye kituo cha huduma za afya kilicho karibu nao kwa ajili ya uchunguzi na matibabu zaidi.


    iii. Usafiri wa kwenda na kurudi shuleni/chuoni: 
a. Wamiliki wa magari ya Shule/Chuo (School bus) waweke vitakasa mikono kwenye magari yao kwa ajili ya wanafunzi wakati wa kupanda kuelekea shuleni/Chuoni, 
b. Wamiliki wa magari ya Shule/Chuo (School bus) wahakikishe kuwa abiria na wahudumu wote wanavaa barakoa za vitambaa na kutumia vitakasa mikono kabla ya kupanda gari husika.
   
    iv. Mazingira ya kujifunzia:  
a. Uongozi wa Shule au Chuo unapaswa kuhimiza wanafunzi/wanachuo, walimu na watumishi wao kuzingatia Kanuni za Usafi binafsi ikiwemo kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni kabla ya kuingia getini/lango kuu, darasani, bwenini, maktaba, bwalo la chakula, ofisini na maeneo mengine muhimu. Wizara inasisitiza matumizi ya sabuni na maji tiririka ndiyo iwe njia kuu ya usafi wa mikono. Aidha, Vitakasa Mikono (Hand sanitizer) vinaweza kutumika kama mbadala wa maji tiririka na sabuni. Inaelekezwa walimu wa madarasa wakisaidiana na viongozi wa wanafunzi/viranja wahakikishe haya yanasimamiwa ipasavyo.  
 
 b. Uongozi wa Shule au Chuo unapaswa kuhakikisha, kadri inavyowezekana, watumishi wote na wanafunzi/wanachuo wanakaa/kusimama kwa umbali utakaokuwa ni salama kati ya mtu mmoja na mwingine wawapo sehemu yoyote wakati wa mafunzo. 
 
    c. Uongozi wa Shule, Chuo na taasisi za elimu zihakikishe wanafunzi, walimu na wafanyakazi wao wanavaa barakoa za vitambaa (Cloth masks) wakati wote wawapo shuleni na vyuoni hususani wanapokuwa katika mikusanyiko ikiwa ni pamoja na darasani au katika vikundi vya majadiliano. Watoto wenye umri chini ya miaka mitano, wanafunzi/walimu/watumishi wenye magonjwa ya moyo, selimundu (sickle cell) na wenye magonjwa ya mfumo wa hewa kama vile pumu hawapaswi kuvaa barakoa.  
 
    d. Kwa shule na vyuo vyenye wanafunzi wenye mahitaji maalumu, walimu wanapaswa kuvaa barakoa maalum zitakazoruhusu mwanafunzi mwenye matatizo ya usikivu kuwasiliana na mwalimu.  
 
    e. Wataalam wa Afya wa Mkoa na Halmashauri husika washirikiane na Uongozi wa Shule au Chuo kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya barakoa, hatua sahihi za unawaji mikono kwa maji tiririka na sabuni na utumiaji sahihi wa vitakasa mikono kwa wanafunzi, walimu na wafanyakazi wa Shule/Chuo husika.  
 
    f. Pale ambapo Shule, Chuo au Taasisi ina watumishi wenye taaluma ya afya, inashauriwa watumishi hawa watumike ipasavyo kutoa elimu ya COVID-19 na kusimamia Utekekelezaji wa Mwongozo huu kwa kushirikiana na Watalaam wa afya wa Mkoa na Halmashauri zao. 
 
    g. Ziara za mafunzo nje ya shule zifanyike kwa kuzingatia tahadhari zote za kujikinga na maambukizi  ya COVID-19. 
 
    h. Uongozi wa Shule, Chuo au Taasisi ya Elimu zinahimizwa kuzingatia Matumizi ya TEHAMA katika kufundisha na kujifunzia ili kupunguza uwezekano wa maambukizi ya COVID-19. 
 
    i. Wataalamu wa Afya wa Mikoa na Halmashauri zote nchini wafanye ukaguzi wa mara kwa mara katika shule, vyuo na taasisi za elimu zilizoko katika maeneo yao ili kuhakikisha tahadhari zote za kujikinga na maambukizi ya COVID-19 zinazingatiwa kabla ya kufunguliwa Shule/Chuo na wakati wa masomo ikiwemo kutoa taarifa kwenye mamlaka husika. 
   
Mwongozo huu utaboreshwa mara kwa mara ili kukidhi mahitaji ya wakati husika. 


Ummy A. Mwalimu (Mb) 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, 
Jinsia, Wazee na Watoto 
27 Mei, 2020


Share:

Halima Mdee Akutwa Na Kesi Ya Kujibu Katika Kesi Ya Kutoa Maneno ya Kuudhi Dhidi ya Rais

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemkuta na kesi ya kujibu, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee,  katika kesi ya uchochezi ya kutoa maneno ya kuudhi dhidi ya Rais John Magufuli. 

Uamuzi huo umetolewa leo tarehe 28 Mei, 2020 na Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba.

Inadaiwa Julai 3, 2017 katika ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA zilizopo mtaa wa Ufipa Wilayani Kinondoni, Mdee alitamka maneno  ya kuudhi dhidi ya Rais Magufuli


Share:

Maandamano dhidi ya kifo cha Mmarekani mweusi Aliyeuawa Kikatili na Polisi Yaendelea Marekani

Waandamanaji mjini Minneapolis nchini Marekani wamepambana na polisi wa kutuliza ghasia kwa usiku wa pili mfululizo kufuatia hasira ya umma inayotokana na kifo cha kikatili cha mmarekani mweusi aliyekuwa chini ya mikono ya polisi. 

Hasira ya umma inatokana na video iliyorekodiwa na mpita njia siku ya Jumatatu ikionesha polisi mzungu akitumia goti kumkandamiza shingoni mwanaume mmoja mweusi aliyefungwa pingu huku akiomba msaada kutokana na kukosa pumzi. 

Siku ya pili ya maandamano iliyoambatana na visa vya wizi na uharibifu wa mali ilianza saa chache tangu meya wa mji huo alipotoa wito kwa waendesha mashtaka kufungua kesi ya jinai dhidi ya polisi huyo aliyesababisha kifo cha George Floyd. 

Mauaji ya kiholela ya Wamarekani wenye asili ya Afrika ambayo yanatekelezwa na polisi wazungu nchini Marekani yameongezeka sana katika miaka ya hivi karibuni nchini humo.


Share:

Bashe: Serikali Yaokoa Tani 556.5 Ya Mbegu Za Nafaka Kwa Kudhibiti Kwelea Kwelea

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe.Hussein Bashe amepokea ndege ya kunyunyizia  dawa aina ya beaver 5Y DLD kwaajili ya kudhibiti visumbufu vya mimea aina ya kweleakwelea ambao wana uwezo wa kuharibu gramu 10 za nafaka kwa ndege mmoja kila siku.

“Kwa kawaida mikoa 12 ya Tanzania bara hupatwa na milipuko ya kwelea kwelea kila mwaka kutokana na tabia ya kwelea kwelea kuwa na uwezo wa kuharibu gramu 10 za nafaka kwa ndege mmoja kila siku.,kundi dogo lenye idadi ya wastani wa ndege milioni moja lina uwezo wa kuharibu tani 10 kwa siku.” Alisema Bashe

Mhe.Bashe ameendelea kusema kwamba uvamizi wa kwelea kwelea katika mashamba husababisha wastani wa uharibifu wa asilimia 30 kwa mazao yetu kila mwaka, na pia visumbufu vya mimea hususan vya milipuko ni tishio kubwa la usalama wa chakula hapa nchini.

Hata hivyo Tanzania husumbuliwa kila mwaka na aina nne ya visumbufu , ambavyo ni ndege aina ya kwelea kwelea, Viwavijeshi,Nzige na Panya. Visumbufu hivi vina tabia ya kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine vikifuata chakula.Ili kuweza kufanya kazi kwa ukaribu zaidi na kudhibiti visumbufu hivyo  Mhe. Bashe amesema Wizara inatarajia kuanzisha Kitengo cha Kilimo anga ambacho kitafanya kazi hii.

Aidha, katika msimu 2019/2020  jumla ya ndege milioni 55.65 wameuwawa na kuweza kuokoa tani   556.5 za mbegu za nafaka kwa siku. Pia kwa ajili ya udhibiti wizara imetumia jumla ya lita 1,905 za kiuatilifu (FenthionULV 60%) na lita 5,716 za mafuta JET A-1.

 Kwa musimu wa 2019/2020 ndege hawa wamedhibitiwa katika Mikoa ya Mwanza; (wilaya ya Sengerema), Mkoa wa Shinyanga; (wilaya ya Kishapu na Shinyanga DC), Tabora; (wilaya ya Igunga, Uyui na Nzega), Mkoa wa Geita;  (wilaya ya Geita DC na Chato).

Mkoa wa Dodoma; (wilaya ya Dodoma jiji,  Bahi na Kondoa), Mkoa wa Singida; (wilaya ya Singida DC, Manyoni na Ikungi).

 Mkoa wa Iringa; (wilaya ya Iringa DC) na Mkoa wa Mbeya (wilaya ya Mbarali) na   Mkoa wa Manyara (wilaya ya Hanang).

 Bashe amemalizia kwa kusema kwamba Udhibiti umefanywa na Wizara Kilimo kwa kushirikiana na shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nzige wa Jangwani (Desert Locust Control Organization for East Africa) kutoka Nairobi Kenya kwa kutumia ndege ya kunyunyizia aina ya beaver 5Y DLD ambapo ilianza kufanya kazi Dodoma na inaelekea Mvomero Morogoro kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.


Share:

MAMA ALIYEPEWA MIMBA NA KUTELEKEZWA MBARONI KWA KUMUUA NA KUMZIKA MTOTO WAKE MVUA IKINYESHA KISHAPU

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mwanamke aliyejulikana kwa jina la Lucia Lukenya Mahizi (42) mkazi wa Kitongoji cha Wizunza kijiji cha Seke Ididi kata ya Sekebugoro wilayani Kishapu mkoani Shinyanga anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua kisha kumzika mtoto wake mwenye umri wa siku mbili kwa madai kuwa ni ugumu wa maisha baada ya kutelekezwa na aliyempa mimba.

Akitoa taarifa kwa Vyombo vya Habari leo Alhamis Mei 28,2020 Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema mtuhumiwa amekamatwa Mei 26,2020 baada ya wananchi kubaini kuwa mwanamke huyo hana mtoto aliyejifungua. 

“Tunamshikilia Lucia Lukenya Mahizi (42) mkazi wa kitongoji cha Wizunza kijiji cha Seke Ididi kwa kosa la mauaji ya mtoto wake mchanga, jinsia ya kiume anayekadiriwa kuwa na umri wa siku 02 baada ya kuzaliwa kwake kisha kumzika mwenyewe pekee yake wakati mvua kubwa ikiendelea kunyesha ili watu wasimuone”,amesema Kamanda Magiligimba. 

Akisimulia kuhusu tukio hilo Kamanda Magiligimba amesema tarehe 26.05.2020 majira ya saa kumi na mbili jioni (12:00) katika maeneo ya kitongoji cha Wizunza kijiji cha Seke Ididi wananchi wa maeneo hayo walibaini kuwa mtuhumiwa Lucia Lukenya Mahizi hana mtoto aliyejifungua tarehe 17/04/2020. 

“Baada ya wananchi kubaini kuwa Lucia hana mtoto ndipo wananchi hao waliamua kutoa taarifa kwa jeshi la polisi na mtuhumiwa huyo alikamatwa siku hiyo ya tarehe 26/05/2020”,ameeleza Kamanda Magiligimba. 

Kamanda Magiligimba amesema chanzo cha mauaji hayo ni ugumu wa maisha baada ya kutelekezwa na aliyempa mimba. 

Kamanda huyo wa polisi amesema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa mtuhumiwa alijifungua mtoto huyo tarehe 17/04/2020 na kumuua tarehe 19/04/2020 na kumzika mwenyewe pekee yake huko maeneo ya shule ya msingi ididi majira ya saa kumi na mbili na kasoro robo (11:45) jioni wakati mvua kubwa ikiendelea kunyesha ili watu wasimuone. 

“Mabaki ya mwili wa marehemu yalipatikana tarehe 26/05/2020 majira saa tisa alasiri katika kaburi alilozikwa na mtuhumiwa huyo na kukabidhiwa kwa ndugu kwa taratibu za mazishi”,ameongeza Kamanda Magiligimba. 

Kamanda Magiligimba anatoa wito kwa wananchi hususani wanawake kuacha kukatisha uhai wa watoto kwa sababu tu ya kutelekezwa na wenza wao bali wafike katika madawati jinsia na watoto yaliyopo vituo vya polisi na ofisi za ustawi wa jamii ili kupata ufumbuzi wa matatizo yanayowakabili.
Share:

Trump atishia kufunga mitandao ya kijamii nchini Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump anatarajia leo Alhamisi kutia saini kwenye agizo linalolenga mitandao ya kijamii, maafisa wa Ikulu ya White House wamesema, saa chahe baada ya rais huyo kutishia  kufunga makampuni ya mitandao yote ya kijamii, akiyatuhumu kujaribu kuzuia uhuru wa kujieleza.

Wawakilishi hao hawakutoa maelezo zaidi kuhusu yaliyomo kwenye agizo hilo la rais Trump. Haijulikani kwa wakati huu jinsi Donald Trump atakavyopitisha  tishio lake la kufunga kampuni binafsi, ikiwa ni pamoja na Mtandao wa Twitter.

Mzozo huo uliibuka Jumanne wakati Mtandao wa Twitter ulihakiki ukweli wa baadhi ya ujumbe wa Rais wa Marekani Donald Trump alioundika katika ukurasa wake. Ni mara ya kwanza mtandao huo ambao Trump anapendelea zaidi kuutumia unafanya hivyo.

Rais wa Marekani alighadhibishwa na jambo hilo na kushumu mtandao huo kwa kile alichokiita ‘kuingilia kati' uchaguzi wa urais wa mwezi Novemba pamoja na uhuru wa kujieleza.

Twitter ilichukua hatua hiyo ambayo haraka ilichochea mvutano kati yake na Trump, baada ya rais huyo wa Marekani kuandika Tweet mbili akidai kwamba mtindo wa kupiga kura kwa njia ya posta huwa una udanganyifu mwingi.

Ilichofanya Twitter ni kuweka kiungo kingine chini ya ujumbe wa Trump kinachosema "Pata taarifa za ukweli juu ya kura ya njia ya posta,” na baadae kiungo hicho kinampeleka mtumiaji kwenye makala ya habari inayompa taarifa za ukweli kuhusu suala hilo, na orodha ya maelezo yanayopinga madai ya Trump.

Trump mwenye wafuasi wapatao milioni 80 katika ukurasa wake wa Twitter, anasema anautumia mtandao huo wa kijamii kupinga kile anachodai kuwa ni taarifa za upendeleo zinazotolewa na vyombo vya habari.

Trump amekuwa akidai kwamba mtindo wa kupiga kura kwa njia ya posta, una viwango vya juu vya udanganyifu katika wakati ambapo majimbo mengi yanazingatia kuitumia njia hiyo ili kulinda afya ya raia dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 wakati taifa hilo likiwa linaelekea katika uchaguzi wa rais wa mwezi Novemba.

Credit:RFI


Share:

WAGONJWA WA CORONA UGANDA WAFIKA 281 BAADA YA WENGINE 28 KUONGEZEKA


Wizara ya Afya nchini humo imetangaza ongezeko la Wagonjwa wengine 28 na kufanya jumla ya visa vya Corona nchini humo kufikia 281.

Wagonjwa 21 ni madereva wa malori walioingia Uganda kupitia mpaka wa Elegu wakitokea Sudan Kusini huku 7 ni waliokuwa Karantini baada ya kukutana na madereva waliotangazwa awali.

Kati ya madereva 21, 7 ni raia wa kigeni kutoka Tanzania (4), Congo (1), Burundi (1) na Eritrea (1). Wote wamekabidhiwa kwa nchi zao.

Aidha, Wizara hiyo pia imetangaza jumla ya Wagonjwa waliopona kuwa 69. Jumla ya sampuli zilizopimwa jana na kuleta matokeo hayo ni 2,004.


Share:

VIFO VYA CORONA MAREKANI VYAPINDUKIA 102,107


 Idadi ya wagonjwa waliofariki kutokana na virusi vya corona nchini Marekani imefika  102,107 katika kipindi cha chini ya miezi minne.

Taifa hilo limeandikisha vifo vingi zaidi ya taifa lolote lile huku watu 1,745,803  wakithibitishwa kuambukizwa virusi hivyo idadi ambayo ni asilimia 30 ya maambukizi yote duniani.

Maambukizi ya kwanza nchini Marekani yaliripotiwa mjini Washington tarehe 21 mwezi Januari.

Kufikia sasa idadi ya waliofariki nchini Marekani imefikia 102,107, kulingana na Chuo kikuu cha John Hopkins mjini Maryland ,ambacho kimekuwa kikifuatilia mlipuko huo. Waliopona 490,130


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger