Thursday 28 May 2020

NEC yakutana vyama vya siasa kujadili na kupitisha kanuni na maadili kwa uchaguzi Mkuu 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imejizatiti na imejipanga kuhakikisha kuwa inatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba, Sheria, Kanuni pamoja na kuzingatia masharti ya Kanuni za Maadili ya Uchaguzi.

Hayo yamesemwa jana  Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Mhe.Jaji Semistocles Kaijage katika kikao na vyama vua Siasa na Wadau wengine wa Uchaguzi kujadili na kupitisha Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2020.

Akizungumza katika kikao hicho Jaji Kaijage alisema kuwa NEC kwa kushirikiana na vyama vya Siasa na Serikali huandaa Maadili ya Uchaguzi kwa shabaha ya kuwa na Uchaguzi ulio huru, wa haki, wa wazi na wa kuaminika.

“Maadili yatasaidia kuwa na uwanja sawa wa ushindani katika Uchaguzi.Maadili hayo huandaliwa kwa mujibu wa kifungu Cha 124A Cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 ya sheria za Tanzania kwa kuzingatia mahitaji yaliyopo”. Alisema Jaji Kaijage.

Jaji amesema kuwa ni muda mwafaka tena kwa vyama vya siasa, Tume na Serikali kama wadau wa Uchaguzi kuandaa Maadili hayo kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

“Natambua kuwa vyama na Serikali mlipewa Rasimu ya Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2020 ambapo mlipata fursa ya kupitia na kutoa maoni na mapendekezo yenu ambayo yamezingatiwa katika Rasimu hii ya Maadili”. Alisema Jaji Kaijage.

Pamoja na hayo Mhe.Kaijage aliwaaomba Wadau mbalimbali wa Uchaguzi baada ya majadiliano hayo na kuridhiwa kwa Maadili,wahusika wataweka saini ya kuyakubali, kuyaheshimu na kuyatekeleza kuanzia wakati was kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu na chaguzi ndogo zitakazofuata.


Share:

Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) Chasema Corona Imepungua Sana Nchini, Champongeza Rais Magufuli

Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) kimesema kinafanya uchambuzi ili kubaini tiba mbadala ambazo zimetumika kwenye kukabiliana na virusi vya corona zina mchango gani katika kupungua kwa maradhi hayo Tanzania.

Rais wa chama hicho, Dk. Elisha Osati, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati MAT ikitoa tathmini ya kitaaluma kuhusu mwenendo wa corona.

Dk. Osati alisema tathmini waliyoifanya kuhusu mwenendo wa corona, wamebaini idadi ya wagonjwa imepungua kwa kiasi kikubwa katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma wakiwamo wanaohitaji kuwekewa oksijeni.

“Tunafanya uchambuzi ambao tutautoa unaolenga kujua kitu gani kimechangia na kwa namna gani kimepunguza corona Tanzania.

“Hatuwezi kudharau njia mbadala kwa sababu Watanzania wengi wanatumia miti shamba, wengi walikuwa wanatumia limao, tangawizi ambavyo vina vitamin C kwa wingi inayosaidia kujenga kinga ya mwili ili kupambana na wadudu mbalimbali wakiwamo corona.”

Alisema inawezekana tiba mbadala imekuwa na nafasi yake, hivyo uchambuzi kuhusu hilo utakuja.

“Watanzania tumewaelekeza vitu vingi vya kufanya watu wananawa mikono, wiki tatu mfululizo watu wamevaa barakoa, tunaamini hiyo imesaidia kupunguza tatizo pia. Kila kimoja tutakifanyia uchambuzi ikiwa ni pamoja matumizi ya tangawizi na limao,” alisema.

Akizungumza ugonjwa huo, Dk. Osati alisema Aprili sampuli zilizokuwa zikipelekwa maabara takribani 90 zilikuwa na corona wakati kwa sasa ni chini ya asilimia 10.

“Idadi ndani ya jamii zimepungua, kwa kuangalia idadi ya simu zinazopigwa kwa kuuliza au kuomba msaada wa kitaalamu kuhusu wagonjwa wenye dalili za ugonjwa huu. Pia idadi ya vifo imepungua,” alisema.

Alisema MAT kimempongeza Rais John Magufuli, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kwa kuwaongoza Watanzania katika kipindi hicho kigumu.

“Tunawapongeza madaktari na watumishi wa sekta ya afya kwa kuwa askari wa mbele kupambana na corona.

“Tunawaomba wagonjwa walioko nyumbani kwa matatizo ya corona au magonjwa mengine waje hospitali tuwahudumie, kwani corona imepungua kwa kiasi kikubwa. Madaktari tupo tayari kuwahudumia.”

Chama hicho kimewaeleza Watanzania kuwa ugonjwa huo bado upo, hivyo waendelee kuchukua tahadhari hasa wakati huu wa wanafunzi wanaporudi vyuoni.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 28,2020





















Share:

Wednesday 27 May 2020

Rais Magufuli Aongoza Kikao Cha Baraza La Mawaziri Ikulu Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ameongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Mawaziri Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mawaziri pamoja na Manaibu Mawaziri tarehe 27 Mei 2020.

Awali kabla ya kikao hicho Mhesimiwa Rais aliwaongoza wajumbe kusimama kwa dakika moja ili kumkumbuka na kumuombea aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Marehemu Balozi Dkt. Augustine Mahiga kabla ya kuanza kwa Kikao hicho.


Share:

SADC Wapendekeza Kuondolewa Kwa Vikwazo Vya Kibiashara Mipakani

Eric Msuya – MAELEZO
Katibu Mkuu Wizara  ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge amewataka watanzania kuendelea kudumisha umoja na Ushirikiano wa Kibiashara katika ukanda wa Jumuiya ya maendeleo Kusini mwa Afrika SADC.
 
Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kufungua Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC kwa ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika kwa njia ya Mtandao (video conference) leo jijini Dar es Salaam, amesema Mkutano huo ni mahususi kwa kujadili na kuondoa vikwazo vyote vya Kibiashara ili kuweza kuendeleza Uchumi ndani ya Jumuiya.
 
“Kikao cha makatibu wakuu cha leo, kimekubaliana kuondoa kikwazo cha bidhaa mahususi tu kupita katika mipaka yetu badala yake bidhaa zote zinazowezesha wananchi wetu kuendelea na maisha ni lazima ziruhusiwe kupita katika mipaka ya nchi wanachama wa SADC” Amesema Balozi Ibuge
 
Aidha, Katibu Mkuu ameongeza kuwa ni muhimu wa wanaSADC kujumuika katika wakati huu na kuona ni jinsi gani wanaweza kushirkikiana na kuhakikisha kuwa Uchumi wa Nchi Wanachama wa SADC unakua na kuongeza juhudi za kibiashara kuendelea kufunguka.
 
“kwa mfano halisi sisi kama Tanzania hatukufunga mipaka yetu, na katika kutokufunga mipaka yetu bado tunatambua kwamba tunaendelea kuwategemea wenzetu kama wanavyotutegemea sisi, tuna bandari inayohudumia Nchi nane za SADC na zisizokuwa za SADC na ambazo ndizo hasa tunapozungumzia utengamano na mazingiara ya kufanya biashara na kuzingataia zile tahadhari mbalimbali ambazo nchi hizo zimekuwa zikichukua” amesema Balozi Ibuge
 
Mkutano huo wa siku tatu 27 hadi 29 Mei, 2019 unajadili Hali ya kifedha ndani ya Jumuiya, Utekelezaji wa Maazimio yaliyotokana na kikao cha Baraza la Mawaziri wa SADC ambayo ni Menejimenti ya Maafa, utekelezaji wa kaulimbiu ya Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC isemayo "Mazingira Wezeshi kwa ajili ya Maendeleo Endelevu na Jumuishi ya Viwanda, Kukuza Biashara na Ajira ndani ya SADC" na mapitio ya hali halisi ya biashara baina ya nchi, maendeleo ya viwanda ndani ya Jumuiya na taarifa ya utekelezaji wa Mkakati wa Maendeleo ya Viwanda wa Jumuiya na Mpango kazi wake.
 
Pia, Mkutano huo unahusisha wataalamu kutoka nchi 12 wanachama wa SADC kutoka sekta za Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Fedha na Mipango, Uchukuzi na Mawasiliano, Viwanda na Biashara, Maliasili na Utalii pamoja na Afya. Mkutano huo pia utatoka na maazimio ambayo nchi wanachama watatakiwa kuyatekeleza ndani ya muda utakaokubaliwa.
 
Nchi zinazoshiriki Mkutano huo ni Angola, Afrika Kusini, Comoro, Eswatini, Mauritius, Msumbiji, Madagascar, Namibia, Visiwa vya Shelisheli, Zambia, Zimbabwe na Mwenyekiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
MWISHO.


Share:

Ufaransa Yaipatia Serikali Mkopo Nafuu Wa Euro Milioni 70 Kujenga Mradi Wa Maji Mjini Morogoro

Na Farida Ramadhani-WFM, Dodoma
Serikali ya Tanzania na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) zimetiliana saini mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Euro milioni 70, sawa na takriban shilingi za Tanzania bilioni 175.6 kwa ajili ya kugharamia Mradi wa Maji Safi na Usafi wa Mazigira Mjini Morogoro (MORUWASA).

Mkataba wa mkopo huo umesainiwa Jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James kwa upande wa Serikali na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa, Bi. Stephanie Mouen Essombe.

Bw. James alisema mkopo huo utawezesha wakazi wa Mjini Morogoro wapatao 722,010 kupata maji safi na salama kupitia upanuzi wa mfumo wa usambazaji wa Maji kutoka Bwawa la Mindu.

Alisema kukamilika kwa mradi huo kutawezesha upatikanaji wa Maji kutoka mita za ujazo 33,000 hadi kufikia mita za ujazo 108,000 kwa siku pamoja na kuwezesha Mji wa Morogoro kupata kiwango cha mahitaji ya maji safi kinachokadiriwa kuwa mita za ujazo 126,253 kwa siku, ifikapo mwaka 2035.

“Mradi pia utaongeza upatikanaji wa huduma za majitaka kutoka kiwango cha sasa cha asilimia 5 hadi asilimia 15 kwa wakazi wa mjini Morogoro”, alifafanua.

Bw. James alisema Tanzania imekuwa ikinufaika na ufadhili wa AFD hususan katika sekta za Nishati, Maji, Usafirishaji na Kilimo kupitia idadi ya miradi  mbalimbali inayoendelea na ile inayotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Alisema miradi 7 inayoendelea kutekelezwa katika sekta mbalimbali hapa nchini kupitia misaada na mikopo inayotolewa wa Shirika hilo inafikia takriban Euro milioni 154.5 sawa na shilingi bilioni 387.6.



“Miradi 6 yenye thamani ya Euro milioni 141.4 kupitia ufadhili wa AFD imekamilika na kuna miradi mingine 12 yenye thamani ya Euro milioni 1,021.7 ambayo tuko kwenye mazungumzo na AFD katika sekta ya Nishati, Maji, Kilimo Usafiri wa mwendokasi Jijini Dar es Salaam, miundombinu ya viwanja vya ndege na Usafi wa mazingira Jijini Dare salaam” alisema Bw. James.



Aliishukuru Serikali ya Ufaransa kupitia Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) kwa ufadhili huo muhimu, ambao utachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya nchi na kupunguza umaskini na kuahidi kuwa Serikali itafuatilia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo ili kuhakikisha kwamba fedha zitakazotolewa zinatumika kama ilivyokusudiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), Bi. Stephanie Mouen Essombe aliahidi kuwa shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania ili kuhakikisha inafikia malengo yake katika kuboresha maisha ya wananchi hasa katika upatikanaji wa maji.

“Ushirikiano wa Tanzania na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) ulioanza miaka 20 iliyopita umezidi kuimarika ambapo katika kipindi cha miaka 10 iliyopita Shirika limewekeza kiasi cha Euro milioni 258 sawa na takriban Sh. bilioni za Tanzania 655” alisema Bi. Essombe.

Alisema mradi huo umelenga kupanua Bwawa la Mindu linalochangia upatikanaji wa maji yanayotumika katika Mji wa Morogoro kwa asilimia 70 pamoja na kuboresha mfumo wa huduma ya maji taka katika mji huo.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Prof. Kitila Mkumbo alisema kuwa mkopo huo utatatua changamoto ya maji ambayo ilikuwa kilio cha muda mrefu kwa wananchi wa Morogoro.

Alisema mkopo huu unafaida nyingi nchini ikiwemo kutoa ajira pamoja na kutoa fursa kwa viwanda vya ndani kwa sababu vifaa vitakavyotumika kutekeleza mradi huo wa kihistoria vitanunuliwa ndani ya nchi.

Alisema hivi sasa Serikali inatekeleza miradi ya maji 1,423, miradi 792 imekamilika na miradi 631 inaendelea na kwamba mradi huo wa maji wa Mji wa Morogoro utakuwa mkombozi mkubwa wa wananchi wa mji huo.

Alisema upatikanaji wa fedha hizo ambazo mjadala wa kupata mkopo umechukua zaidi ya miaka minne utawezesha kuongeza kiwango cha upatikanaji wa maji nchini ambapo hivi sasa kiwango cha upatikanaji wa maji vijijini kimefikia asilimia 85 ya lengo la asilimia 95 iliyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM huku katika miji kiwango kimefikia asilimia 70.1 kati ya lengo la asilimia 85 ifikapo mwishoni mwa mwaka 2020

Mwisho.


Share:

Riwaya Kali ya Kusisimua....SIN- Sehemu Ya Nne (04)

ILIPOISHIA
“Wamesema ni kiasi gani?”   
“Milioni mia sita hamsini, ila nimezungumza nao, hadi kwenye milioni miatano watauza”
“Mage umaipenda hii nyumba”
“Ndio baba ila mbona kodi yao ni garama kiasi hicho?”
“Hapana, jana usiku nilibadilisha mawazo, nikaona nisichukue nyumba ya kupangisha ila ninunue kabisa. Nina imani utaishi kwa amani kabisa kwenye hii nyumba”
Maneno ya nabii Sanga kidogo, yakabakisha kidogo yamuangushe Magreth kwa furaha. Katika maisha yaku hakutarajia hata siku moja kuja kumiliki nyumba ya kwake peke yake, tena nyumba yenye hathi ya mamilioni ya pesa.

ENDELEA
“Au hujapenda mimi kukununulia hii nyumba?”
Nabii Sanga alimuuliza Magreth swali la mtego ikiwa jibu ana lifahamu kwamba ni lazima atahitaji kumiliki nyumba kama hiyo.
“Yaani baba sina hata cha kuzungumza”
“Usijali, hivi ndivyo jinsi Mungu anavyo fungua baraka kwa kila mja wake. Hivyo Mungu amezipitisha baraka zako kupitia mimi”
“Asante sana Mungu na ninazidi kukuombea baba Mungu azidi kukubariki kwenye kila hatua ya huduma yako”
“Nashukuru sana mwanangu”
Tomas akawatembeza kwenye nyumba hiyo yenye vyumba vitatu vya kulala huku vyote vikiwa ni master room na seble mbili za kupumzikia, pamoja na jiko kubwa.
“Kutokana muda umwekwenda, kesho tutakutana na mmiliki wa hii nyumba”
“Sawa baba mchungaji na uzuri ni kwamba hii nyumba ni mpya kabisa, nimali ya shirika moja la ujenzi”
“Ahaa kumbe”
“Ndio kwa hiyo hatununui kwa mbabaishaji, ila tuna nunua kwa shirika ambalo hapo baadaye hawato weza kutudhulumu”
“Ndio maana nina kupenda sana Tomas, huwa una fanya kazi zako kwa uhakika na uaminifu mzuri. Endelea hivyo hivyo, Mungu atazidi kukufungulia milango ya baraka”
“Amen”
Wakarudi ndani ya gari, wakamrudisha Tomas hadi eneo alipo liacha gari lake na kuagana naye.
“Baba mchungaji nina weza kuuliza swali?”
“Uliza tu?”
“Kwa nini una nifanya haya yote kwa wakati mfupi, yaani kuanzia jana nimeona maisha yangu yamebadilika kwa kiasi fulani?”
“Swali zuri sana mwanangu. Unatambua kwenye maisha, hususani haya maisha ya kumcha Mungu, yana changamoto zake na faida zake. Ngoja nikusimulie kisa kidogo ambacho kinahusiana na misha yangu.”
Nabii Sanga alizungumza huku akipunguza mwendo kasi wa gari lake.
“Kipindi nilipo kuwa nina ianza hii hudumua. Nilianza kwenye maisha ya chini sana tena maisha ya ufukara. Watu wengi walinisimanga, ikiwemo ndugu zangu wa tumbo moja. Walidai kwamba nina igiza igiza. Sikumuacha Mungu, na nilikutana na mke wangu, barabarani akishambuliwa na wasichana wezake”
“Akishambuliwa kwa nini alikuwa anashambuliwa?”
“Ahaa alichukua mwanaume wa mtu. Hivyo siku hiyo alikutana na mwenye mume wake. Niliweza kuuamua ugomvi ule huku akiwa amejeruhiwa sana kwa kucha. Hakuwa na sehemu ya kuishia kwa maana huyo mwenye mume wake, aligundua kwamba mume wake ame mpangishia nyumba nzima na alifanya kila analo liweza kuhakikisha ana mfukuza ndani ya hiyo nyumba”
“Basi nilimsaidia na kipindi hicho nilikuwa na kachumba kamoja tu. Takribani miezi tisa tulikuwa tuna ishi kama mtu na dada yake. Niliweza kumbadilisha tabia yake na akwa mcha Mungu kweli kweli. Baada ya kuridhika naye basi nilifanya taratibu zote za kanisa na nikamuoa. Hivyo katika kipindi chote hicho hicho sikuweza kukutana naye kimwili hadi nikamuoa na yeye ndio alikuwa mwanamke wangu wa kwanza kukutana naye kimwili”
“Aiseee!!”
“Yaa. Ona sasa Mungu alivyo kuwa wa ajabu. Mara baada ya kufunga naye ndoa. Huduma yangu ikaanza kutanuka, wadhamini kutoka ndani na nje ya nchi wakazidi kunisaidia. Nikaanza kutajirika taratibu hadi sasa hivi nina utajiri mkubwa sana, ambao hata nikiwaambia wanangu na mimi tisifanye kazi yoyote ya kutuingizia kipato. Basi tunaweza kukaa na pesa niliyo nayo kwa zaidi ya miaka mia moja, tukiwa tuna kula, kunywa na kulala”
“Sasa maana yangu ya kukuadithia wewe hivyo ni ili uweze kujua kwamba Mungu ana makusudi yake kwa kila hatua ya mafanikio kwenye maisha yako. Mimi lango la uchumi lipo kwa mke wangu na wewe lango la uchumi lipo kwa yule Evans aliye lala pale kitandani. Laiti kama asinge kutana na wewe, muda huu usinge kuwemo ndani ya gari langu na wala nisinge jua matatizo yako”
“Ni kweli baba mchungaji”
Magreth alijibu kwa unyonge sana huku akimtazama nabii Sanga usoni mwake.
“Hivyo weza kutambua makusudi ya kila jambo kwenye maisha yako”
“Amen”
Wakapitia katika hospitali ya Mwanayamala kumjulia hali Evans. Walipo ridhishwa na afya yake, nabii Sanga akamrudisha Magreth nyumbani kwake kisha yeye akaelekea kwake.
‘……….wewe lango la uchumi lipo kwa yule Evans aliye lala pale kitandani. Laiti kama asinge kutana na wewe, muda huu usinge kuwemo ndani ya gari langu na wala nisinge jua matatizo yako’
Maneno ya nabii Sanga yakajirudia akilini mwa Magreth na kujikuta akihisi hali ya tofauti sana kwenye moyo wake. Hali hii hakuwahi kuihisi toka abalehe.
‘Nahisi nina mpenda Evans’
Magreth alizungumza kimya kimya huku akielekea kwa muuza chips katika mtaa huo. Akanunua chipsi mayai na soda.
“Da Mage chupa yangu hukunirudishia”
“Usijali mdogo wangu nitakuletea”
“Fanya hivyo, kesho nitaagizia kreti la soda”
“Sawa miskaki hivi ni bei gani?”
“Mia tano”
“Niwekee miwili”
Japo Magreth ana pesa ya kutosha, ila maisha yake ya kuishi kwa bajeti bado yapo pale pale. Akapita dukani kwa Mangi na kununua daftari kubwa na kalamu, kisha akarudi nyumbani. Akapata chakula hicho cha usiku, kisha akaanza kuandika mipango atakayo ifanya kwenye Mgahawa wake. Alipo hakikisha kwamba bajeti hiyo anayo taka kuanza nayo ime mtosheleza akatamani kumujulisha nabii Sanga muda huo, ila moyo wake ukasita na akajipa matumaini ya kumpatia bajeti hiyo siku inayo fwata.
                            ***
    Gari aina ya Ford Ranger, ikalipita kwa spidi gari la nabii Sanga na kulizuia gari la nabii Sanga kwa mbele. Kitendo hicho kikamfanya nabii Sanga kufunga breki za gafla huku akiwa na wasiwasi mkubwa sana. Wanaume wanne wenye bunduki huku sura zao wakiwa wamezifunika, wakashuka kwenye gari hilo na kumuamrisha kwa ishara nabii Sanga kushuka ndani ya gari hilo.
‘Ehee Mungu ni nini hichi kinacho endelea?’
Nabii Sanga alizungumza huku akifungua mkanda wa siti ya gari lake. Wanaume hao mmoja wao akapiga risasi kwenye kioo cha mbele upande ambao hakuna mtu. Tobo la risasi hiyo likamfanya nabii Sanga kushuka kwenye gari bilia kushurutishwa.
“Jamani kama muna taka pesa chukueni, chukueni tu”
Nabii Sanga alilalama huku mwili mzima ukimtetemeka kwa woga.
“Hatutaki pesa zako na tuna kutaka wewe”
Wakamfunga mikono yake kwa nyuma, kisha wakamfunga kitambaa na kumuigiza kwenye gari lao na kuondoka eneo hilo kwa mwendo wa kasi sana huku wakilitekeleza gari la nabii Sanga eneo hilo. 
Gari hiyo inayo endeshwa kwa mwendo wa kasi sana ikazidi kuchanja Mbuga usiku kwa usiku, huku nabii Sanga akiwa amewekwa chini ya ulinzi mkali sana.
“Jamani nyinyi ni kina nani, mbona mme niteka ikiwa sina uadui na mtu”
Nabii Sanga alilalama, ila kisuku suku alicho pigwa kwenye mbavu za kulia kilimfanya atulie tuli.
“Ukirudia kuuliza swali jingine basi utakufa kabla ya masaa yako”
Gari hilo likafika katika wilaya ya Mkinga. Wakasimamisha gari hilo kwenye moja ya pori ambalo lina nyumba nne tu zilizo jengwa na kikundi cha watekaji wanao fanya kazi zao kwa kulipwa na watu binafsi au makampuni. Wakamshusha nabii Sanga, mzoga mzoga na wakamuingiza kwenye moja ya chumba na kuifunga mikono yake juu na taratibu wakaanza kumvuta na kumfanya nabii Sanga aning’inie hewani, juu asifike wala chini asikanyage.
                            ***
‘Done’
Meseji hiyo ikaufanya moyo wa mrs Sanga kutawaliwa kwa tabasamu pana sana. Akamtazama mfanyakazi wake wa ndani anaye fatilia tamthiia ya kikorea.
“Hivi wewe una jua wanacho kizungumza hao watu?”
“Ndio mama”
“Wewe Rose kweli unataka kuniambia kwamba una jua kikorea? Hembu acha kunitania bwana”
“Najua kidogo kidogo”
“Umejifunzia wapi wewe mtoto?”
“Si kwenye hizi tamthilia. Wakisema jonaaaaa ni sawa sawa na kusema mfalmeeeee”
Maneno ya Rose yakamfanya mrs Sanga kucheka kwa furaha sana. Akaondoka sebleni na kuingia chumbani kwake. Haraka akatoa line iliyopo kwenye simu hiyo, akafungua pochi na kutoa line nyingine ambayo hata mume wake huwa haifahamu wala mwana familia wake yoyote yule. Baada ya kuiingiza line hiyo, akatafuta jina lililo andikwa T.
“Niambie mpenzi wangu”
“Salama, kazi vijana wame ikamilisha”
“Weee eheee imendaje endaje?”
“Mara baada ya mimi na wao kuachana. Nikaanza kuwafuatilia taratubu hadi sehemu aliopo mpeleka msichana yule. Nikawapa vijana ratiba nzima na wamemteka karibu kabisa na hapo kwenu”
“Kazi nzuri Tomas, ndio maana nina kupenda. Mwanaume ana taka kuniletea upuuzi wa kijinga. Hatosheki na mimi hadi anataka  huko nje, ana taka hadi kufungua migahawa na kumnunulia nyumba mtu, haiwezekani kwa kweli”
“Usijali mpenzi wangu, mpango acha uendelee”
“Sawa, ila Tomas ile mechi ya jana mwenzio, unajua nilisahau kuondoka huko kwako hata sija chana nywele”
“Weee ehee ilikuwaje sasa?”
“Huyo mkn** si ndio nikamkuta amekaa sebleni kama kibwengo. Alinitakia tu usiku mwema kisha akenda zake kulala.”
“Usijali mpenzi wangu. Hakikisha kwamba unakuwa makini na hakuna mtu ambaye ana weza kugundua juu ya mahusiano yetu”
“Wala usijali katika hilo. Ila Tomas nina hamu sana na wewe
“Hahaa usijali, kesho ukipata muda kidogo njoo mama”
“Nakupendea hapo. Hakikisha kwamba huyo mpuuzi hajulikani alipo, hadi wiki ijayo”
“Nimekuelewa mke wangu”
“Yaani najisikia vizuri sana unapo niita mke”
“Kweli?”
“Haki ya Mungu vile. Najisikia amani na furaha kabisa.”
“Ehee na kale kabinti vipi nikapoteze?”
“Achana nako, nitapambana naye huku huku kanisani. Nitamuwekea vizingiti hadi ajute ni kwa nini alikaa karibu na mume wangu”
“Sawa mpenzi. Nakupenda sana”
“Nakupenda pia. Mwaaaaa”
Mrs Sanga akakata simu huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana moyoni mwake. Mapenzi yake ya siri na Tomas, dalali wa nabii Sanga, yana miezi saba toka walipo yaanzisha. Tabia mbaya za kufanya mapenzi kinyume na maumbile anazo fanyiwa mrs Sanga na Tomas, zimempagawisha hadi ana jikuta akitamani hata leo mume wake aweze kutoweka duniani.
“Na bado mwaka huu ata koma”
Mrs Sanga alizungumza huku akibadilisha laini hiyo na simu na kuirudisha laini yake halisi. Hazikupita hata dakika mbili simu yake ikaanza kuita. Moyo ukamstuka sana, kwani ni simu kutoka kwa mume wake Mr Sanga. Akaitazama kwa muda simu hiyo kisha akaipokea.
“Ndio mume wangu, upo wapi mbona hurudi nyumbani?”
“Samahani, mimi ni afisa wa polisi kanda maalumu. Ninaitwa ispeka Mussa Rjab. Tumepewa taarifa na wasamaria wema kwamba gari la mume wako limeshambuliwa kwa risasi na hadi ninavyo zungumza hatujajua ni wapi mume wako alipo”
“Ameshambuliwa kwa risasi….Ohooo Mungu waangu, jamani mume wangu”
Mrs Sanga akaanza kujiliza kinafki ila ukweli wa mambo ana utambua kwamba yeye na Tomas wamehusika katika kumteka mume wake.
“Usilie mama, unacho paswa ni kufika hapa eneo la tukio ili kuweza kutusaidia, kwa maana si eneo la mbali sana na hapo nyumbani kwenu.”
“Sawa nina kuja sasa hivi”
Mrs Sanga, akajifunga matenge mawili huku ndani akiwa amevalia suruali na tisheti. Akatoka kwa haraka haraka, akaingia kwenye moja ya gari la familia na kufika eneo la tukio ambalo si mbali na nyumbani kwake. Akakuta polisi pamoja na waandishi wa habari wakiendelea kufanya mahojiano japo kwa baadhi ya watu walio weza kushuhudia tukio hilo.
“Ohoo jamani mume wangu”
Mrs Sanga aliangua kilio huku akishuka ndani ya gari hilo. Askari wawili wa kike waka muwahi iku kumzuia asisogee eneo la tukio.
“Mama tafadhali baki kwenye gari lako. Hili eneo si salama.”
Askari mmoja wa kike alizungumza huku akimshika mrs Sanga mkono.
“Jamani huyo ni mume wangu”
“Ndio ni mume wako ila hapa hayupo kabisa. Jambo la msingi ni kuhakikisha kwamba una kuwa salama wewe na familia yako. Kama watekaji wamemteka mume wako basi kitakacho fatia hapo ni familia yako.”
Baadhi ya askari pamoja na mkuu wao wakaondoka na mrs Sanga na kuelekea nyumbani kwake.
“Watoto wako wapo wapi?”
“Mmoja yupo chuo. Wawili wapo nje ya nchi”
“Huyu wa chuo, yupo chuo gani?”
“Hapo mlimani”
“Hakikisheni kwamba ana wekewa ulinzi wa kutosha huyo binti”
Mkuu wa kikosi hicho cha polisi alizungumza.
“Sawa mkuu”
“Ikiwezekana akachukuliwe na kuletwa hapa nyumbani”
“Tumekupata mkuu”
“Hembu niambie mume wako ana tatizo japo na mtu au kikundi cha watu?”
“Jamani kama munavyo tambua. Mume wangu ni mtumishi wa Mungu. Hana shida na mtu yoyote, yeye ni mcha Mungu kisawa sawa. Yaani sijui kwa nini wamamteka mume wangu ohooo”
Mrs Sanga alizungumza na kunza kuangua kilio kilicho mfanya mkuu wa kikosi hicho cha polisi kumuacha kwa muda apunguze machungu yake kisha mahojiano yaendelee.
“Mama Sanga, je unaweza hisi kidogo kwa nini watekaji wamemteka mume wako”
“Hapo itakuwa ni pesa tu. Hakuna jengine, oohooo Mungu wangu, ohoo jehova, muokoe mume wangu. Damu ya Yesu kristo, imfunike, wasimfanye jambo lolote baya. Mungu simama naye”
Mrs Sanga alisali maombi ya kinafki na laiti kama mioyo ya binadamu ingekuwa na uwezo wa kuoenaka na bindamu mwengine kwamba ina panga nini juu ya kila tukio. Basi polisi wasinge jisumbua kumuhoji mrs Sanga na siku nyingi sana wangekuwa wamemsweka rumande.
                                ***   
    Katika siku ambazo Magreth amejawa na furaha pamoja hamu ya kupata kile alicho ahidiwa na nabii Sanga ni siku ya leo. Akajiandaa vizuri huku mdomoni mwake, akitawaliwa na mapambio ya kumsifu Mungu. Akaelekea kwenye kituo cha waegesha bajaji huku moyoni mwake akiamini sasa maisha ya kupanda dalala dala yanakwenda kuisha.
“Ila hii nchi sasa imetawaliwa na mambo ya ajabu sana.”
Muendesha bajaji alizungumza huku wakiendelea na safari ya kuelekea hospitali ya Mwananyamala.
“Kwa nini kaka?”
“Kuna watu wana wateka watu na wanavishwa jina .... Yaani nashindwa hata kuelewa, tunaelekea wapi?”
“Nani mwengine ametekwa?”
“Si yule nabii Sanga wa kanisa la Heaven light ministry”
Mapigo ya moyo wa Magreth, yakasimama kwa sekunde kadhaa, kisha yakaanza kumuenda kasi, mwili mzima ukaanza kumtetemeka na jasho likimtiririka usoni mwake, hadi muendesha bajaji akabaki akiwa ameshikwa na butwaa kwa nini hali ya abiria wake imebadilika gafla mara ya kusikia taarifa hiyo.
                                                                                                   ITAENDELEA
Ndoto, matumaini na matarajio ya Magreth sasa yameingia giza. Mwanga alio kuwa akiuhisi mbele ya macho yake sasa umebadilika na kuwa giza nene. Nini kitatokea? Endelea kufatilia kisa hiki cha kusisimua, usikose sehemu ya 05



Share:

TASAF KUANZA UTEKELEZAJI WA KIPINDI CHA PILI CHA AWAMU YAKE YA TATU NCHINI KOTE



Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Ladislaus Mwamanga (aliyeketi katikati) akimsikiliza Mtaalamu wa Mawasiliano wa TASAF , Zuhura Mdungi aliyesimama akitoa neno la kuwakaribisha Wandishi wa Habari (hawapo pichani) kwenye ofisi ndogo taasisi hiyo jijini Dar es salaam. Kulia kwa kwake ni Mkurugenzi wa Miradi wa TASAF, Amadeus Kamagenge. 

***
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF umekamilisha mipango itakayowezesha kuanza kwa utekelezaji wa Kipindi cha Pili cha Awamu yake ya TATU kufuatia uzinduzi uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Ladislaus Mwamanga amekutana na Wandishi wa Habari jijini Dar es salaam na kuwajulisha kuwa mipango ya kuanza utekelezaji wa kipindi cha pili ambayo imezingatia maelekezo ya Serikali inaelekea kukamilika.

Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF amesema katika kutekeleza kipindi hicho cha pili, Mfuko huo utajikita zaidi katika kuhamasisha Walengwa kutumia zaidi huduma za kielektroniki hususani katika suala la ulipwaji wa ruzuku.

Aidha Mwamanga amesema mkazo mkubwa utawekwa katika kuhamasisha Walengwa kushiriki kwenye miradi ya maendeleo hususani katika sekta za elimu,afya maji na shughuli za miradi ya kiuchumi kwa kutumia utaratibu wa Ajira ya Muda na kisha kulipwa kwa mujibu wa taratibu zilizopo.

Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF ametoa wito maalum kwa Walengwa wa Mfuko huo kuhakikisha kuwa wanapata huduma za simu ili waweze kunufaika na utaratibu mpya wa kulipwa kwa njia ya kielektroniki ambao umefanyiwa majaribio kwenye halmashauri za wilaya zipatazo 16 kwa mafanikio.

Bwana Mwamanga amezitaja halmashauri ambazo Walengwa wa TASAF hulipwa kwa njia ya kieleketroniki kuwa ni pamoja na Arusha, Ilala,Temeke, Kinondoni,Mpanda na Kigoma Manispaa. Nyingine ni Bagamoyo,Songea Manispaa,Kisarawe, Kilwa, Muheza ,Mkuranga, Bahi,Urambo, Siha na Unguja.

Mfuko wa Maendeleo yas Jamii-TASAF unatekeleza kipindi cha pili cha awamu ya tatu ambacho kilizinduliwa na Rais John Pombe Magufuli jijini Dar es salaam ambacho kinatarajiwa kutumia kiasi cha shilingi trilioni 2.032 ambazo zitatumika kutekeleza miradi inayolenga kuboresha huduma za miundombinu kwenye sekta za afya,elimu na maji na kutoa ruzuku kwa kaya zinazoishi katika mazingira duni sana ili ziweze kuboresha maisha.
Share:

Kenya yatangaza idadi kubwa zaidi ya wagonjwa wa Corona Kwa Kipindi Cha Masaa 24

Waziri wa Afya nchini Kenya Mutahi Kagwe leo Jumatano Mei 27 ametangaza watu 123 zaidi kuambukizwa virusi vya corona.

Hiyo ndiyo idadi kubwa zaidi ya maambukizi ya corona kuwahi kutangazwa kwa siku moja nchini humo tangu ugonjwa huo uingie Kenya mwezi Machi.

Mpaka kufikia sasa Kenya imethibitisha watu 1,471 kuambukizwa virusi hivyo.

Waziri Kagwe pia ametangaza watu watatu zaidi wamefariki kutokana na corona katika saa 24 zilizopita na kufanya watu waliopoteza Maisha kutokana na virusi hivyo nchini Kenya kufikia 55.


Share:

TAKUKURU Yaanza Kuichunguza CHADEMA Juu Ya Tuhuma Za Matumizi Mabaya Ya Fedha.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), imeanza kuchunguza tuhuma za matumizi mabaya ya fedha, inazokikabili Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
 
Hivi karibuni, kumekuwepo na madai yanayotolewa na baadhi ya wabunge juu ya matumizi mabaya ya fedha walizochanga kila mwezi kwa mujibu wa Katiba.

Baadhi ya waliotoa shutuma hizo ni; wabunge wa viti maalum; Susan Maselle, Joyce Sokombi na Peter Lijualikali wa Kilombero ambao wote wametangaza kukihama chama hicho.

Kwa nyakati tofauti, wabunge hao, Maselle na Sokombi walisema mara baada ya Bunge kuvunjwa watahamia NCCR-Mageuzi huku wakisema, hawana shida na kuchangia fedha hizo lakini matumizi yake hayaeleweki.

Leo Jumatano, tarehe 27 Mei 2020, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru  Brigedia Jenerali John Mbungo amesema wameanza kuwahoji baadhi ya watu.

 “Kwa mujibu wa taarifa tulizo nazo, kuna matumizi mabaya ya fedha za michango ya wanachama, ambayo kwa mujibu wa katiba yao wanadai imeanishwa wachangie.”

“Lakini, matumizi yake ndio wanatilia mashaka, kuna fedha nyingi zinatumika ndivyo sivyo, kwa mujibu wa makubaliano yao,” amesema Jenerali Mbungo.

“Kwa hiyo, tunachunguza matumizi yasiyo sahihi ya fedha zao, Takukuru inayomamlaka ya kuchunguza taasisi yoyote iwe ya umma, watu binafsi, chama, klabu, iwe chochote Takukuru wanaingia kufanya uchunguzi, ilimradi kuwe na ubadhirifu au matumizi mabaya ya fedha na rushwa,” amesema bosi huyo wa Takukuru.

Amesema, wameanza kuwahoji wanachama waandamizi  na viongozi wa Chadema, wabunge waliotoa tuhuma hizo, pamoja na maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Mbungo amewataja baadhi ya watakaohojiwa ni; Dk. Vincent Mashinji, aliyekuwa Katibu Mkuu Chadema, ambaye kwa sasa amehamia Chama cha Mapinduzi (CCM), John Mrema, Mkurugenzi wa Itifaki na Mambo ya Nje Chadema, pamoja na mhasibu mkuu wa chama hicho, Dk. Roderick Lutembeka.

Aidha, Jenerali Mbungo amesema wameshindwa kumhoji Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, kuhusu sakata hilo, kwa kuwa aliieleza TAKUKURU kwamba yuko nje ya jiji la Dar es Salaam.

Amesema, taasisi hiyo imeshaanza kukusanya nyaraka mbalimbali, zinazohusiana na tuhuma hizo.

Credit: Mwanahalisi


Share:

Vyuo Vikuu Zanzibar Kufunguliwa Juni Mosi, Michezo kuanzia tarehe 5 juni, 2020

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaungana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhakikisha kuwa kuanzia tarehe 01 juni, 2020 vyuo vyote vya elimu ya juu vitafunguliwa na kuendelea na programau zao kama kawaida kwa upande wa Zanzibar.

Hayo yameelezwe na Makamo wa pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari amesema wanafunzi wa kidato cha sita nao wataanza masomo yao tarehe 01 juni, 2020 ili kuwawezesha kufanya mitihani yao ya taifa.

“Kufuatia maamuzi haya Serikali imeiagiza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kushirikiana kikamilifu na wizara ya afya katika kuandaa miongozo ya kiafya itakayopaswa kuzingatiwa ili kuepuka maambukizo ya maradhi Corona”-Amesema

Aidha Balozi Seif amesema kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha tano pamoja na wanafunzi wa skuli za msingi, maandalizi na madrasa, zitaendelea kufungwa hadi yatakapotolewa maelekezo mengine ya Serikali.

Kwa upande wa michezo, ligi kuu ya mpira wa miguu Zanzibar itaendelea kuanzia tarehe 5 juni, 2020 na kuiagiza Wizara ya Vijana, Utamaduni Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na ZFF pamoja na Wizara ya Afya kuandaa muongozo na namna bora ya kuendesha ligi hiyo.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger