Saturday 31 August 2019

Aua Mkewe Kwa kumnyonga shingo kisha kujiua kwa kunywa sumu.

Mkazi wa kijiji cha Iponya katika Halmashauri ya Mji wa Kahama, Paschal Clement (32), amemuua mkewe Ashura Paschal (30) kwa kumnyonga shingo kisha kujiua kwa kunywa sumu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Richard Abwao, alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa moja jioni katika kijiji cha Iponya.

Alisema chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi na kwamba kabla ya tukio hilo, wanandoa hao walikuwa na ugomvi huku mume akimtuhumu mkewe kuwa si mwaminifu kwenye ndoa.

Abwao alisema Paschal baada ya kutekeleza mauaji hayo, alijiiua kwa kunywa sumu ambayo mpaka sasa bado haijafahamika ni ya aina gani na kukutwa chumbani kwake akiwa amelala sakafuni.


Share:

Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi aridhishwa na miradi ya SUMA JKT Kanda ya Ziwa

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi amesema anaridhishwa na kazi nzuri inayofanywa na miradi inayotekelezwa na SUMA JKT kanda ya Ziwa.

Dkt. Mwinyi akiwa kwenye ziara yake ya kukagua miradi inayotekelezwa na SUMA JKT pamoja na makampuni mengine yaliyo chini ya Wizara hiyo kanda ya Ziwa  tarehe 30/08/2019 katika Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga amesema kwa kiwango kikubwa ameridhishwa na kazi zinazofanywa na sehemu kubwa kazi zimekwenda kwa kiwango kinachotarajiwa na kuwa changamoto zilizopo zitafanyiwa kazi.

“Niwahakikishie Mikoa na Halmashauri zinazohusika na miradi inayotekelezwa na SUMA JKT changamoto zote zitafanyiwa kazi” amesema Dkt. Mwinyi.

Aidha, amemshukuru Mhe. Rais John Magufuli kwa kuiamini kampuni hiyo iliyo chini ya Wizara yake na ndiyo sababu ya yeye kufanya ziara hiyo ili kuhakikisha imani hiyo inadumu pamoja na kuwaomba viongozi wote wa Mikoa na Halmashauri kuendelea kuiamini.

Aidha, amewataka SUMA JKT kuongeza kazi ya ziada mara watakapopata fedha ili kukamilisha jengo la Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambalo ujenzi wake umesimama kutokana na changamoto ya fedha.

Naye Mkurugenzi wa SUMA JKT Kanali Rajab Mabele amesema kuwa, kampuni hiyo imepiga hatua kubwa hasa katika nyanja ya ujenzi lakini pia inajihusisha na kazi nyingine mbalimbali ikiwemo kilimo na ufugaji.

Awali, akimkaribisha Dkt. Mwinyi Mkoani hapa, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amemuomba kupitia kampuni ya SUMA JKT kuangalia jinsi ya kuwa na miradi ya kuvuna maji ili wananchi waweze kujishughulisha na kilimo cha umwagiliaji.

“Pamoja na kiangazi kilichopo, tunapata mvua nyingi sana na tunavuna mpunga unaoweza kulisha nchi yote, sasa tuone namna bora ya kuvuna hayo maji na tayari baadhi ya wananchi wameshaanza kuchimba mashimo makubwa ya kuvuna maji, tumeona kama Mkoa tufanye hilo ili wananchi wetu waweze kupata mpunga” amesema Telack.


Share:

Polisi Pwani Yakamata Shehena Ya Vipodozi Feki

NA MWAMVUA MWINYI,PWANI
JESHI la polisi mkoani Pwani, linamshikilia Albert Kiwia (45) mkazi wa Kimara Dar es salaam kwa kosa la kusafirisha shehena ya vipodozi feki mbalimbali ,kwa kutumia gari aina ya Toyota Nissan.

Katika hatua nyingine, jeshi hilo limefanikiwa kukamata madumu saba ya mafuta ya diezel yakiwa na ujazo wa lita 20 kila moja mali inayodhaniwa kuwa ni ya wizi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani,Wankyo Nyigesa aliwaambia waandishi wa habari kuwa ,mtuhumiwa huyo amekamatwa agost 29 mwaka huu, katika eneo la Mizani ya zamani -Kibaha Mji .

Alifafanua, licha ya tuhuma hiyo ya kusafirisha vipodozi hivyo ,jeshi hilo likamtaka aonyeshe kwa TRA stakabadhi alizolipia ushuru katika mipaka ya nchi wakati akiingiza vipodozi na hakuwa navyo

Aliwataka ,wafanyabiashara wenye tabia ya kuingiza bidhaa zao nchini kwa kukwepa kulipa kodi ,kuacha mara moja .

Wankyo alisema ,wamedhibiti mianya yote kwa wale wanaojaribu kukwepa kulipa kodi katika barabara zote za mkoa na wale watakaokamatwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Hata hivyo, akielezea kuhusiana na tukio la kukamatwa madumu ya mafuta ya diezel ,alisema madumu hayo yamekamatwa ,eneo la Misugusugu ,Kibaha baada ya mtu aliyekuwa na mafuta hayo kuyatelekeza na kukimbia baada ya kuona gari la polisi likielekea mahali alikokuwa .

Wankyo alitoa wito kwa jamii kuacha kuhifadhi madumu ya mafuta aina ya diezel na petrol ndani ya nyumba kwani ni hatari.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi August 31




Share:

Friday 30 August 2019

MWENDESHA BODABODA ALIYEFARIKI KWA AJALI AZUA GUMZO KUACHA WAJANE 6 NA WATOTO 30

Siri nyingi hufichuka wakati ambapo binadamu anafariki kwani licha ya kuwa ni kinyume na itikadi kumuanika aliyeaga dunia, mambo mengine hasa ya kifamilia huwa vigumu kuyaficha. 

Hayo ndiyo yalifichuka baada ya dereva mmoja wa bodaboda aitwaye Hassan Mafabi (51) mkazi wa Nakatundu Kangulumira nchini Uganda kufariki dunia kwenye ajali ya barabarani pikipiki yake kugongana na gari siku ya Jumamosi wiki iliyopita.

Bodaboda huyo alikuwa na wake 6 na watoto 30 licha ya kazi yake yenye malipo ya wastani hali iliyosababisha watu wengi kushangaa ni vipi aliweza kutekeleza mahitaji ya wake hao wote. 

 Wengi wamepigwa na butwaa baada ya matangazo kuwafikia kuhusu mchango wa kusaidia familia ya marehemu kwani ameacha wajane sita na watoto 30.

Hassan Mafabi mwenye umri wa miaka 51 alikuwa akiishi na wake hao sita na watoto wake na kuchapa kazi kama kawaida huku wengi wasijue kuwa alikuwa na familia kiasi hicho.

 Kulingana na Ugandanz.com, Mafibi aliishi katika kijiji kimoja nchini humo tangu kifo chake barabarani ambapo aligongwa na gari. 

Askofu wa kanisa la Mukono nchini humo alidhibitisha kisa hicho na kuwataka marafiki kujitokeza kuisaidia familia ya Mafibi kwani yeye ndiye alitegemewa kuilisha. 

Wengi hata hivyo walishangaa ni vipi mwendesha bodaboda huyo aliweza kuwalisha wake hao pamoja na watoto 30 ikizingatiwa mapato ya biashara ya bodaboda ni ya wastani tu.
Share:

SANAMU TATA YA TRUMP YAZUA GUMZO

Sanamu ya mbao ya Donald Trump, iliyotengenezwa na Tomaz Schlegl, ilisimamishwa wiki kadhaa baada ya sanamu ya Melania Trump

Sanamu ya mbao ya rais wa Marekani imejengwa katika nchi alikozaliwa mkewe ya Slovenia, imeibua maoni tofauti.

Ikiwa na urefu wa karibu futi 26, sanamu hiyo ilijengwa katika ardhi ya kibinafsi na inamuonyesha Donald Trump akiwa na kichwa cha muundo wa mraba na kidevu huku akiwa anyenyenyua kichwa juu.

Msanii aliyeitengeneza amekiambia shirika la habari la AFP kuwa alitaka iwe kama kielelezo cha maoni ya kisasa ya wanaohisi kuwa watawala wa kisiasa hawawajali.

Sanamu hii imewekwa baada ya ile ya mke wa trump, Melania inayomuonyesha akiwa na ulimi uliojaa ndani ya mashabu.

Sanamu ya Melania, iliyochongwa ndani ya mti viungani mwa mji alikozaliwa wa Sevnica, inamuonyesha akiwa amevalia koti la rangi ya blu huku mkno wake ukionyesha angani. baadhi ya wakazi wanaichukulia kama ''aibu'', na wanasema inaonekana zaidi kama katuni kuliko mke wa rais wa Marekani.Mnara huu wa Trump unaripotiwa kujengw ana msanii wa Slovenia Tomaz Schlegl


Sanamu mpya ya rais wa Marekani ilijengwa katika kijiji cha Sela pri Kamniku, yapata kilomita 30 kusini -mashariki mwa mji mkuu wa Slovania -Ljubljana.

Mbunifu wake, Tomaz Schleglameliambia shirika la habari la AFP kwamba alilenga kutoa maoni ya wengi kupitia sanamu.

"Kwa mara ya kwanza ttangu Vita ya II ya dunia ndio mara ya kwanzamaoni ya wengi yanajitokeza kupinga utawala uliopo : Mtazame waziri mkuu wa Uingere za Boris Johnson, tazama Trump, rais wetu au waziri mkuu wa Hungary Viktor Orban. Dunia hii inaelekea wapi ?," alisema. "Tunataka kufungua macho ya watu kuelewa demokrasia ni nini ."
sanamu ya Bwana Trump inamuonyesha akiwa amevalia shati la blu na tai nyekundu, huku akiwa amesimama mithili ya mnara wa uhuru wa New York.

Bwana Schlegl anasema muundo wa ndani ya sanamu ya mbao unairuhusu kubadilika kutoka "sura ya urafiki mnamo siku za kazi za wiki na kuwa na sura ya kutisha sana katika siku za wikendi ", ikiwa ni sihara ya unafiki wa wanasiasa wanaotaka kuonyesha kuwa wanawajali wale wanaohisi kuwa wamesahaulika.

Lakini mnara huu umeibua maoni tofauti . Shirika la habari la AFP ililishuhudia mkazi mwenye hasira akiendesha gari lake la trekta na kugonga mnara huo wa sanamu wiki hii wakati maandalizi ya kuufungua rasmi Jumamosi yakiendelea.

Baadhi ya wakosoaji wa sanamu hiyo wamelalamikia juu ya "uharibifu wa mbao " na wakasema isingepaswa kujengwa .

"Majirani zetu wanadai sanamu hii ina sura mbaya na kwamba haifai katika eneo letu hili zuri tambalale ," Alisema Bwana Mr SchleglMnara huu wa Trump unaripotiwa kujengwa na msanii wa Slovenia Tomaz Schlegl

Watu wa Slovania wana maoni tofauti kumuhusu Rais wa Marekani . Mji anakotoka mkewe Mellania umekuwa ni kitovu cha utalii tangu alipochaguliwa mwaka 2016.

Huku wageni wakija kupata taswira ya mahali alikozaliwa na kuishi enzi za utoto wake , wakazi wametengeneza bidhaa zenye nembo ya melania zikiwemo kandambili, keki na baga zenye sura ya Trump na zilizopambwa na jibini iliyotengenezwa kama " nyweli" za Trump.

Japokuwa sanamu ya Mke wa rais ikiibua ukosoaji mwezi uliopita , mmoja wa wakazi wa eneo hilo ameliambia shirika la habari la AFP n kwamba kazi ya sanaa kuihusu lilikuwa ni " wazo zuri".

"Melania ni shujaa wa Slovenian , amefikia mafanikio ya juu nchini Marekani ," alisema Katarina, mwenye umri wa miaka 66.
Chanzo - BBC
Share:

RAIS MAGUFULI AKERWA NA CHANGAMOTO ZA UMASKINI BARA LA AFRIKA

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia Mkutano wa Sita Jukwaa la Uongozi la Afrika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam, Tanzania.


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Rais John Magufuli wa Tanzania amesema masalia ya fikra za kikoloni walizonazo Waafrika wengi ni miongoni mwa sababu zinazofanya Bara la Afrika kushindwa kusimamia rasilimali zake ili kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi.

Ameyasema hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akihutubia kongamano la viongozi la 2019 akisema dhana ya uhuru haiwezi kutenganishwa na kujitegemea.

“Kama hujitegemei huwezi kuwa huru, kwani uhuru wako utakuwa mikononi mwa unayemtegemea.”

“Maana hasa ya kupigania uhuru ni kurejesha rasilimali zetu na hasa rasilimali zetu, lakini pia kuwa na uamuzi kamili wa namna ya kuzisimamia na kuzitumia wa kuzitumia ili kuleta ukombozi wa kiuchumi,” amesema Rais Magufuli.

Amesema kutokana na kutoelewa dhana kamili ya uhuru, nchi za Afrika zinadhani watawala wa zamani ndiyo wenye uwezo wa kusimamia na kusaidia na kuendeleza rasilimali.

Ametaja pia sababu ya kushindwa kusimamia rasilimali na kuleta mageuzi ya kiuchumi, akisema fedha siyo msingi wa rasilimali.

“Fedha ni matokeo ya mwisho kabisa ya matumizi ya rasilimali zetu na siyo msingi wa maendeleo. Hata hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alisema ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Hakutaja pesa, alijua itakuja tu kama yale tutayatimiza,” amesema.

Ametaja pia ukosefu wa ubunifu na teknolojia ya viwanda akisema Afrika haitaweza kusimamia na kutumia rasilimali zake kiuendelevu bila kuwa na viwanda.

Mbali na viwanda, ametaja kukithiri kwa migogoro na hali tete ya siasa barani Afrika akisema inasababishwa na mabeberu wanaotaka kuendelea kutumia maliasili za Afrika kwa manufaa yao.

“Wakati sisi tunapigana wao wanakula na kamwe hawatataka tuwe na amani, kwani migogoro ndiyo mtaji wao,” amesema.

Ameendelea kutaja pia tatizo la mikataba na makubaliano yanayoingiwa na wawekezaji katika kutumia rasilimali akisema, “Na hapa nchi yetu imeliwa sana kutokana na mikataba mibovu na hasa kwenye madini.”

Kuhusu uharibifu wa mazingira, Rais Magufuli amesema unasababishwa na ukataji hovyo wa msitu kwa ajili ya nishati ya majumbani kutokana na gharama kubwa za umeme na gesi asilia.

“Chanzo kingine ni uchafuzi wa mazingira unaofanywa na mataifa mengine yaliyoendelea na yenye viwanda vingi, lakini Afrika ndiyo inayoathirika zaidi a machafuko hayo,” amesema.

Akizungumzia hatua zilizochukuliwa na Serikali, Rais Magufuli amesema imetungwa sheria ya kulinda utajiri na rasilimali na maliasili ya 2017 na kupitiwa upya na kurekebisha mikataba ya uchimbaji na madini isiyo na manufaa kwa Taifa.

“Tumeweka msukumo mkubwa kwenye ujenzi wa viwanda na ukuzaji wa teknolojia ya viwanda ili mazao yanayotokana na rasilimali zetu yasindikwe kwanza kabla ya kuuzwa nje,” amesema

Alitaja pia uanzishwaji wa mradi wa bwawa la Nyerere utakaozalisha MW 2115 kwenye bonde la mto Rufiji kama njia ya kutunza mazingira, kudhibiti nidhamu za watumishi wa umma na kupamba na rushwa na ufisadi.

Wageni maarufu waliohudhuria mkutano huo walikuwa marais wastaafu kutoka baadhi ya nchi za Afrika akiwemo Thabo Mbeki wa Afrika Kusini, Olusegun Obasanjo wa Nigeria, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete wa Tanzania.
Share:

KAMPUNI ZA JAPAN ZENYE UZOEFU KWENYE MIRADI YA GESI ASILIA ZAONESHA NIA YA KUWEKEZA TANZANIA


Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dkt. James Mataragio akipeana mkono na Mtendaji Mkuu wa Chiyoda Corporation Ndg. Ken Nagao baada ya kikao baina ya ujumbe wa Tanzania na Kampuni ya Chiyoda. Wengine pichani kutoka kushoto ni Ndg. Pius Gasper (TANESCO), Dkt. Tito Mwinuka, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Mhandisi Innocent Luoga, Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu (Wizara ya Nishati), Ndg. Katsuo Nagasaka (Chiyoda) na Ndg. Koji Nishita (Chiyoda).
Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika kikao na Kampuni ya JGC kilichofanyika sambamba na kilele cha Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD7). Upande wa kushoto ni Ndg. Kenji Yamamoto (JGC), Ndg. Masayuki Sato (JGC), Ndg. Yanamaka (JGC) na Ndg. Taketoshi Shogenji (JGC). Upande wa Kulia ni Mhandisi Innocent Luoga, Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu (Wizara ya Nishati), Dkt. James Mataragio, Mkurugenzi Mtendaji (TPDC) na Ndg. Pius Gasper (Tanesco).
***
Yokohama, Japan.

Kampuni kubwa za Japan zenye uzoefu wa miaka mingi katika miradi ya gesi asilia zimeonesha nia ya kuwekeza nchini Tanzania hususan katika mradi mkubwa wa kusindika gesi asilia (Liquefied Natural Gas-LNG). Kampuni za JGC na Chiyoda zenye uzoefu wa miaka mingi katika kazi za uhandisi, manunuzi na ukandarasi (EPC) hususan katika kutekeleza miradi ya LNG duniani zimekutana na ujumbe wa Tanzania uliohudhuria kilele cha Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD7) zikionyesha nia ya kushiriki katika mradi wa ujenzi wa mitambo ya kusindika gesi asilia (LNG).

Katika kikao hicho kilichofanyika sambamba na TICAD7, Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Dkt. James Mataragio alisema “katika kipindi cha muongo mmoja, Tanzania imepiga hatua kubwa katika sekta ya mafuta na gesi asilia ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu mikubwa ya kusambaza gesi kwa ajili ya umeme, viwanda na majumbani”.

Dkt. Mataragio pia alieleza nia ya Serikali ya Tanzania kuwekeza katika utekelezaji wa mradi wa kimkakati unaokadiriwa kugharimu dola za marekani bilioni 30 na utahusisha uendelezaji wa kiasi kikubwa cha gesi asilia kilichogunduliwa katika kina kirefu cha bahari.

Dkt. Mataragio alieleza kwamba kwa sasa Serikali iko katika hatua za majadiliano ya vipengele muhimu vya mkataba wa Serikali mwenyeji (Host Government Agreemet-HGA) na kampuni za kimataifa zilizogundua gesi asilia katika kitalu namba 1, 2 na 4. Kitalu namba 1 na 4 vinaendeshwa na Kampuni ya Shell ikishirikiana na Ophir Energy na Pavilion wakati kitalu namba 2 kinaendeshwa na Kampuni ya Equinor ikishirikiana na ExxonMobil.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Chiyoda Corporation, Ndg. Ken Nagao alisema “Kwa miaka kadhaa sasa tumeshirikiana na Tanzania katika kuendeleza sekta ya gesi asilia na tunadhani tunaweza kushirikiana zaidi katika kutoa uzoefu tulionao wa zaidi ya miaka 50 katika ujenzi wa mitambo ya LNG”.

Kampuni ya Chiyoda imehusika katika ujenzi wa miradi mikubwa ya LNG ikiwemo Australia, Nigeria, Qatar na nchi nyingine nyingi ikiwa na pato ghafi la takribani Trilioni 7.2. Nae Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya JGC, Ndg. Masayuki Sato alieleza nia ya kampuni yake kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha Wananchi wake wanafaidika na rasilimali ya gesi asilia kwa kujenga mitambo ya LNG itakayowezesha uvunaji wa gesi asilia iliyogunduliwa katika kina kirefu cha bahari ya Hindi.

Akizungumza katika kikao hicho, Ndg. Sato alisema “Tumeshirikiana na Tanzania katika maandalizi ya mpango kabambe wa matumizi ya gesi asilia (NGUMP) na tusingependa kuishia hapo kwani tunadhani Tanzania ina fursa ya kuwa kituo kikubwa cha kuzalisha na kusambaza gesi asilia kwa nchi zenye mahitaji makubwa ya nishati na hivyo kukuza uchumi na pato la Taifa”.

JGC ni miongoni mwa kampuni kubwa katika ujenzi wa mitambo ya LNG na ujenzi wa miundombinu mingine katika mnyororo wa thamani wa gesi asilia, alifafanua zaidi Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa JGC.

Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga nae alieleza nia ya Wizara ya Nishati kuhakikisha gesi asilia inatumika katika kukuza uchumi wa ndani kwa kuisambaza kwa viwanda vingi zaidi ili kuchochea ajenda ya uchumi wa viwanda itakayosaidia Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

“Mpango kabambe wa matumizi ya gesi asilia unaainisha wazi kwamba tutatumia gesi yetu kusaidia kukuza uchumi na kunyanyua sekta nyingine kama vile viwanda, kilimo, uvuvi, usafirishaji na nyinginezo ili kubadilisha uchumi wa Taifa na watu wetu” alisema Mhandisi Luoga.
Share:

MTOTO MWINGINE ALIYEANGUKIWA NA BOMBA LA MAJI AFARIKI DUNIA


Mfano wa Bomba lililomwangukia mtoto.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora ACP Brnabas Mwakalukwa, amesema kuwa mtoto aliyeangukiwa na bomba kubwa la maji mkoani humo, amefariki dunia wakati akipelekwa hospitali ya Bugando kwa ajili ya matibabu.

Mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya msingi Kiyungi iliyopo Manispaa ya Tabora, alipata majeraha siku ya Agosti 28 baada ya kuangukiwa na bomba kubwa la kupitisha maji, walipokuwa wakicheza na wenzao hali iliyopelekea mtoto mwenzake kufariki muda huo huo.

''Yule mtoto aliyelazwa ICU walifanya utaratibu wa kumpeleka Bugando lakini bahati mbaya akafariki njiani maeneo ya Nzega, na daktari akathibitisha kufariki kwake'' amesema ACP Mwakalukwa.

Mabomba yaliyosababisha madhira hayo ni ya mradi mpya wa usambazaji wa maji mkoani humo kutoka Ziwa Victoria, yaliyokuwa yamehifadhiwa kwenye kiwanja cha shule hiyo.
Share:

Job opportunities at I&M Bank

Information Security Officer l&M Bank (T) Ltd, a subsidiary of l&M Group which has presence in Kenya, Tanzania, Rwanda and Mauritius invites applications from suitably qualified candidates to fill the following available positions. JOB TITLE:  INFORMATION SECURITY OFFICER REPORTS TO:  HEAD OF RISK JOB PURPOSE: Protecting organization’s computers, networks and data against threats, such as security breaches, computer viruses… Read More »

The post Job opportunities at I&M Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Nafasi za kazi TADEPA- Jobs at TADEPA August 2019

Information about TADEPA Tanzania Development and AIDS Prevention Association (TADEPA) is a Tanzanian Nongovernmental organization (NGO) currently offices in Kagera, Geita, Shinyanga and Dodoma regions. Was formed and registered in 1997 and acquired mandated to work in all regions of Tanzania mainland. The main purpose of TADEPA is to promote development in totality through and fight against public… Read More »

The post Nafasi za kazi TADEPA- Jobs at TADEPA August 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at Vodacom, Head of Revenue Assurance

Head of Revenue Assurance   Role purpose: The key purpose of the Head of Revenue Assurance is to ensure completeness and accuracy of the company revenue streams across CBU, EBU and M-Pesa Units. In addition to checking on the integrity of systems in place, the position requires an inclination towards continuous improvements in revenue chain, proactive design and implementation… Read More »

The post Job Opportunity at Vodacom, Head of Revenue Assurance appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at NETIS Tanzania, Project Sheq officer

JOB TITLE: Project Sheq officer INDUSTRY: Telecommunication LOCATION: Dar es Salaam. ROLE PURPOSE To ensure that NETIS’s Quality, Safety, Health, Social, Security, Cultural, Environmental and Risk Management systems are defined, implemented, maintained and adhered to according to best practice standards at all levels of the organisation within Tanzania. KEY PEFORMANCE AREAS Document and communicate all SHERQ manuals and policies… Read More »

The post Job Opportunity at NETIS Tanzania, Project Sheq officer appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

11 Job Vacancies at BAK-AID Tanzania

EXCITING CAREER OPPORTUNITIES OVERVIEW BAKWATA NATIONAL HIV/AIDS PROGRAM (BAK-AIDS) is a Faith Based Organization (FBO) implementing HIV programs to support Tanzania Government efforts to reduce the rate of HIV pandemic in Tanzania. Since inception, BAK-AIDS has played a big role in supporting Tanzania’s social development initiatives by implementing health programs which include HIV and AIDS education and other… Read More »

The post 11 Job Vacancies at BAK-AID Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Wizara ya elimu (MOE): Commonwealth scholarships tenable in the United Kingdom 2020

Wizara ya elimu (MOE): Commonwealth scholarships tenable in the United Kingdom 2020: scholarships for tanzanians to study in tanzania, how to apply for commonwealth scholarship, commonwealth scholarship 2019/2020, tanzania scholarship 2019, how to apply for commonwealth scholarship 2019, what is commonwealth scholarship, commonwealth scholarship 2020, commonwealth scholarship application portal. The Ministry of Education, Science, and Technology as a… Read More »

The post Wizara ya elimu (MOE): Commonwealth scholarships tenable in the United Kingdom 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Ardhi University- How to confirm selection 2020- Maelekezo jinsi ya kuthibitisha udahili kwa waliodahiliwa zaidi ya chuo kimoja

Ardhi University- How to confirm selection 2020- Maelekezo jinsi ya kuthibitisha udahili kwa waliodahiliwa zaidi ya chuo kimoja- Ardhi University (ARU) 2019. The Ardhi University (ARU) was established after transforming the former University College of Lands and Architectural Studies (UCLAS) which was then a constituent college of the University of Dar es Salaam from 1st July 1996. The… Read More »

The post Ardhi University- How to confirm selection 2020- Maelekezo jinsi ya kuthibitisha udahili kwa waliodahiliwa zaidi ya chuo kimoja appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Ardhi University 2nd Round selection release date

Ardhi University 2nd Round selection release date 2019 The Ardhi University (ARU) was established after transforming the former University College of Lands and Architectural Studies (UCLAS) which was then a constituent college of the University of Dar es Salaam from 1st July 1996. The history of Ardhi University, however, dates back to 1956 when the then Surveying Training… Read More »

The post Ardhi University 2nd Round selection release date appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger