Sunday 2 June 2019

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili June 2




Share:

Tamisemi: All girls who passed Form four will Join Form Five or Technical Colleges

Form Five selection, Selection form five 2019/2020 , form five selection 2019/20 first selection form five 2019 pdf tamisemi form five selection 2019 form five second selection 2019/2020 post form five 2019, necta form five selection 2019, www.tamisemi.go.tz form five selection, form 5 selection 2019 pdf download, form five second selection 2019/20

Tamisemi: All girls who passed the Form 4 to  join Form Five, Technical Colleges

Minister of State President’s Office Regional Administration and Local Government Hon. Seleman Jafo said all the girls who succeeded in the Fourth Form exam in 2018 last year have been selected to join the Form five with various technical colleges in the country.

Jafo, he made the same statement today in Dodoma while announcing students selected to join Form Five with vocational education colleges in the year of study that will begin in July, 2019.

“I would like to announce to you the good news that, for this year all the successful girls have been selected to join the Form five with various technical universities, of which a total of 45,816 girls.

Given the performance of the Fourth Form candidates for 2018, from grade one to third, he said 113,825 candidates among them are 47, 779 and 66,046 boys equal to 31.76 percent of all candidates who did the test.

In another phase, the Minister Jafo has called on the councils, especially those of the science and mathematics studies to complete Form five and six classes by March, 2020, which cited Councils as Kyerwa DC, Kilindi DC, DC, Handeni DC, Malinyi, Mtwara DC, Momba DC, Nanyumbu DC and Nanyamba DC, urging Regional Heads and District Heads and Directors of Local Government Authorities to manage closely and ensure the Government’s mandate for each of them and the Formula School is being fulfilled.

Last Minister Jafo has asked all selected students to take into account all the necessary precautions in the case of their final pre-deadline especially for those who are to join the prestigious universities (NACTE).

“We have given a date from 09 June, 2019 to 30 August to have all agreed to join the technical colleges and will fail to do so their positions will be filled with other students.” Said Jafo Minister.

President TAMISEMI’s office has been tasked with the responsibility of overseeing the election of five Formal students and technical colleges from 2014 after the announcement of the Fourth Form Outcomes.

Source: Tamisemi

YOU MAY ALSO LIKE

MORE NEWS ABOUT FORM FIVE SELECTIONS AND JOINING INSTRUCTIONS

The post Tamisemi: All girls who passed Form four will Join Form Five or Technical Colleges appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Saturday 1 June 2019

[FULL PDF DOWNLOAD] Form Five selection 2019

[FULL PDF DOWNLOAD] Form Five selection, Selection form five 2019/2020 , form five selection 2019/20 first selection form five 2019 pdf tamisemi form five selection 2019 form five second selection 2019/2020 post form five 2019, necta form five selection 2019, www.tamisemi.go.tz form five selection, form 5 selection 2019 pdf download, form five second selection 2019/20

Students selected to join form five and Technical Colleges 2019/20 academic year

 

GOOD NEWS!!: YOU CAN NOW EASILY FIND YOUR NAME (FORM FIVE SELECTION NAMES 2019) IN THE PDF FILE ATTACHMENT BELOW, SINCE IT IS NOW AVAILABLE AT UDAHILIPORTAL.COM

CLICK HERE TO ACCESS FULL PDF FILE- FORM 5 SELECTION 2019

 

MORE NEWS ABOUT FORM FIVE SELECTIONS AND JOINING INSTRUCTIONS

The post [FULL PDF DOWNLOAD] Form Five selection 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano 2019

Share:

Yanafunguka Fasta : ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO 2019

Share:

Breaking : HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI 2019

Share:

WAVUTAJI SIGARA HATARINI KUSHINDWA KUSHIRIKI TENDO LA NDOA


Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani na Upasuaji Harisson Chuwa kutoka Hospitali ya Agakhan, amesema miongoni mwa madhara yanayosababishwa na matumizi ya Tumbaku ni wanaume kushindwa kushiriki tendo la ndoa kutokana zao hilo kuathiri zoezi la kusukuma damu mwilini.

Akizungumza kwenye kipindi cha Supamix cha East Africa Radio, Dr Chuwa amesema mbali na wanaume kudai mfumo wa maisha, ikiwemo lishe bora hupelekea kukosa nguvu za kiume lakini pia matumizi ya Sigara na mazao ya Tumbaku, hupunguza nguvu za kiume.

"Madhara mengine ya matumizi ya tumbaku inaweza kusababisha mwanaume kushindwa kushiriki tendo, kwa sababu mishipa ya damu inashindwa kufanya kazi vizuri, ndiyo maana tunasingizia tuna upungufu wa nguvu za kiume, lakini si kweli ni mfumo wa maisha tu wa uvutaji wa sigara" amesema Dr Chuwa.

Aidha Dr Chuwa amesema kuwa "moshi wa sigara una madhara kwa mvutaji mwenyewe na aliyekuwa naye karibu, madhara yanaanzia kwenye saratani ya mapafu, hii ndiyo saratani inayosababishwa na 95% ya matumizi ya sigara, ndiyo maana utakuta wake, waume au watoto wa watu wanaovuta sigara wanapata saratani hii"

Madhara mengine yanayoweza kutokana na matumizi ya tumbaku ni mtoto anapokuwa tumboni, moshi wa sigara unaweza kumuathiri kukua kwa mapafu yake, anaweza kupata pumu na mapafu yanaweza kujaa makamasi, na wakati mwingine inamfanya ashindwe kupumua.

Chanzo- EATV
Share:

ATUPWA JELA MIAKA 30 KWA KUKUTWA NA BANGI


Mkazi wa Kijiji cha Majengo, Kata na Tarafa ya Mtama, Wilaya ya Lindi Ramadhani Haji Juma, amehukumiwa kwenda gerezani kutumikia kifungo cha miaka 30, baada ya kupatikana na hatia ya kujihusisha na madawa ya kulevya aina ya Bangi yenye uzito wa Kilo 7.8 kinyume cha sheria.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Lindi, Liliani Rugalabamo,baada ya Mshtakiwa kukiri kosa lililomkabiri bila ya kulazimishwa.

Baada ya mshitakiwa kukiri kosa, Hakimu Rugalabamo alimuuliza mshtakiwa kama anazo sababu zitakazoishawishi Mahakama isimpe adhabu kali, Ramadhani Haji Juma aliomba asipewe adhabu kali, akidai ni mkosaji wa mara ya kwanza na alilazimika kujiingiza kwenye Biashara hiyo kwa lengo la kujipatia riziki ya kila siku.

"Mh,Hakimu naiomba Mahakama yako tukufu inisamehe na sitarudia kufanya kosa la aina hii tena kushiriki kazi hii "Amesema Ramadhani.

Kufuatia utetezi huo, hakimu Rugalabamo alirejea kwa Mwanasheria wa Serikali, Yahaya Gumbo iwapo anazo kumbukumbu za makosa ya zamani kwa mshtakiwa na kujibu hana, huku akiiomba mahakama impatie adhabu kali ili iwe fundisho kwake na wengine walio na tabia ya aina hiyo.

Hakimu Rugalabamo akimpatia mshitakiwa adhabu katika kesi hiyo Namba 41/2019, alipinga utetezi huo kwa kusema hauna mashiko, kwani zipo njia nyingi za halali kama vile kuitumia ardhi iliyopo kuzalisha mali, yakiwemo mazao ya chakula na biashara ili kuondokana na umasikini.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya June 1




Share:

Friday 31 May 2019

WADAU WAANZA KUJITOKEZA KUMSAIDIA BINTI ANAYEUGUA UGONJWA WA NGOZI MWAKA WA 16 SASA

Share:

NAMNA WAKULIMA WANAVYOPOTEZA FURSA KWA KUTOKUCHANGAMKIA FURSA


Kaimu Mkurugenzi Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dk Fortunatus Kapinga akionyesha maziwa yanayotegenezwa kwa kutumia korosho.
Kaimu Mkurugenzi Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dk Fortunatus Kapinga akionyesha maziwa yanayotegenezwa kwa kutumia korosho.
Mtafiti kutoka kituo cha utafiti wa kilimo Tari- Naliendele, Regina Msoka akinyesha bidhaa zinazotengenezwa kwa kutumia mabibo ya korosho, juisi kusho na kulia ni mvinyo.
Mtafiti kutoka kituo cha utafiti wa kilimo Tari- Naliendele, Regina Msoka akinyesha bidhaa zinazotengenezwa kwa kutumia mabibo ya korosho, juisi kusho na kulia ni mvinyo.
Chupa zenye mvinyo ulio tayari kwa ajili ya kwenda sokoni.

Chupa zenye maziwa yanayotengenezwa kwa kutumia korosho.
****
Mara nyingi wakulima wa korosho hulima zao hilo kwa lengo la kuuza korosho ghafi ambazo kwa kiasi kikubwa husafirishwa kwenda nje nchi na baadhi yao wachache huzibangua ili kuziongezea thamani.
Lakini bado wamekuwa wakipoteza mapato kwa kiasi kikubwa kutokana na kutotumia vyema fursa inayopatikana kwenye korosho.
Kutokana na utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele katika zao hilo mkulima anaweza kuzalisha bidhaa nyingine kwa mbali na ile korosho anayoiuza ikiwa ghafi.
Katika zao hilo kuna tunda la bibo ambalo wakati wa mavuno mkulima hulazimika kutenganisha bibo na korosho ndipo apeleke korosho ghalani. Wakulima wengi huyateketeza kwa moto licha ya kuwa yanafaa kuzalisha bidhaa kama mvinyo, jam na juise’
Mtaalamu kutoka kituo cha utafiti wa kilimo Tari- Naliendele, Regina Msoka anasema mkulima anapopata kilo moja ya korosho ghafi shambani anaacha mabibo kilo tisa huku akiambulia kati ya Sh 2,400 hadi 4,000 kulingana na bei ya mnada.
“Mkulima akipata kilo moja ya korosho  ghafi maana yake ameacha kilo tisa za mabibo shambani unaweza kuona ni jinsi gani anaacha bidhaa ambayo ni muhimu shambani,”anasema Msoka
Anabainisha katika katika kilo tisa ya mabibo yakisindikwa na kutengenezea mvinyo na kuuthaminisha ana uwezo wa kupata Sh 100,000 huku kilo moja pekee ya korosho hazidi Sh 4,000.
“Ukipiga hesabu za haraka katika kilo kumi za korosho ana mabibo kilo 90 maana yake ana Sh 40,000 ya korosho na ambaye anatumia mabibo kutengeneza mvinyo ana Sh 1milioni kwa hiyo hapo unaona ni faida gani iliyopo kwenye mabibo,”anasema Msoka na kuongeza;
“Tumefanya utafiti teknolojia zipo tuna uwezo wa kutengeneza juisi ya mabibo ambayo haina ukakasi, ambapo katika mabibo kilo moja unapata nusu lita ya juisi,wengi wanakimbia bibo sababu ya ule ukakasi wake,sisi tumefanikiwa kuutoa na pia tunapata juisi nzuri, tunapata jam na pia mashine zinapatikana Sido na tunaendelea kutoa mafunzo kwa badhi ya wakulima,”anasema
Kutokana na bibo kutohifadhika kirahisi anasema baadhi ya wakulima huyakausha na kutenegenezea pombe za kienyeji maarufu kama ulaka ambazo hazijathibitishwa kwani kiutaalamu.Anasema kitaalamu yanapaswa kutunzwa sehemu yenye ubaridi (cold room).
Muda wa kupata mvinyo, jam na juisi
Ili kupata mvinyo uliokamilika inahitajika miezi mitatu ili kuyasindika mabibo ili ukomae ambapo kilo moja ya mabibo una uwezo wa kuzalisha lita moja ya mvinyo.
Ili kupata juisi zinahitajika siku mbili ambapo mtengenezaji anahitaji mabibo kilo moja ili kupata nusu lita ya juisi na kwa jam ni siku moja.
Utengenezaji  siagi ya korosho na maziwa
Mtafiti Msoka anasema kwa kutumia  kilo moja ya daraja la mwisho ambalo ni vipande vidogo vya korosho (small pieces WW450) baada ya kubanguliwa na kupangwa katika madaraja unaweza kutengeneza siagi kilo moja ambayo huuzwa Sh 20,000 na korosho hizo thamani yake ni Sh 10,000 kwa kilo.
 “Badala ya kuuza korosho Sh 10,000 natengeneza siagi kilo moja na kuuza Sh 20,000,nikitoa gharama za uzalishaji bado nitakuwa na faida, na nikitumia kilo moja hiyo hiyo ya korosho nina uwezo wa kupata maziwa takribani lita tatu ambazo nitaziuza Sh 25,000,”anasema
Kuhusu madaraja ya korosho,Kaimu Mkurugenzi Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dk Fortunatus Kapinga anasema kwenye saizi ya mbegu kiutafiti wamefanikiwa kuwa na mbegu ambazo zina ukubwa unaostahili  kwenye soko kwa maana zinazokidhi daraja kubwa na kuvutia wanunuzi kutoka nje.
Anafafanua daraja la mbegu 500 nchini hazipo na badala yake zipo zinazokidhi daraja kubwa la mbegu 180 huku zile za daraja la 450 zikiwa ni chache sana na ndizo hutengenezea maziwa na siag.
“Korosho za Tanzania zina ubora wa kimataifa unaokubalika kwa sababu tuna mbegu ambazo tumezizalisha na tumezigundua zina sifa za soko la kimataifa na ndio maana tunahimiza wakulima wetu wapande mbegu bora kutoka Naliendele il tunapoenda kwenye ushindani soko lolote la kimataifa hakuna anayetushinda,”anasisitiza Dk Kapinga
Anafafanua kutokana na baadhi ya watu kama watoto kushindwa kutafuna korosho au kuwa na mzio (allergy) ya maziwa ya ng’ombe ndio sababu za wao kuwa na utafit wa maziwa ya korosho.
Upatikanaji wa malighafi
Msoka anasema malighafi wanazotumia kutengeneza mvinyo,jam na juisi hupatkana katika mashamba yao ya utafiti huku korosho zinazotengenea ,maziwa na pinetbutter hutokana na korosho zinazobanguliwa katika kiwanda kilichopo kwenye taasisi hiyo kwa ajili ya utafiti.
Mwakilishi wa mkurugenzi mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Dk Bakari Msangi anasema kwa kuwa Taasisi ya Utafiti wa kilimo Naliendele imeshafanya utafiti na kuthibitisha teknolojia inayoweza kutumika watu wachangamkie fursa.
Anasema wafanyabiashara wakubwa wanatakiwa kuona fursa na kuweka viwanda katika mikoa inayozalisha korosho kwa kuanzisha viwanda vitakavyozalisha bidhaa zitakazotokana na mabibo.
“Wanachotakiwa ni kuona tayari katika level ya research tumeprove teknolojia kwamba inaweza na tumeshatoa product zinazoingia sokoni, kwa hiyo tunawavutia wawekezaji wa ndani na nje waone umuhimu wa kuweka viwanda,”anasema Dk Msangi
Hata hivyo, anasema kwa kuwa sasa ni uchumi wa viwanda hawawalengi tu wajasiriamali wadogo, bali wafanyabiashara wakubwa na watunga sera wote.
“Watu wote wanaoongelea sera za nchi wajitahidi kuitangaza teknolojia hii ambayo imeshahakikiwa na Naliendele kuhamasisha watu kuwekeza katika maeneo yanayozalisha korosho ili kutumia hii product (bidhaa) ambayo inapotea,ni potential area,”amesema Dk Msangi
Wakulima
Mkulima Elisha Millanzi anasema katika msimu mmoja ana uwezo wa kupata korosho tani mbili hadi tatu na mabibo yatokanayo na korosho hizo hutengeneza juisi ya kunywa wawapo shmbani na yanayosalia ambayo ni mengi huyateketeza kwa moto pindi yanapokauka.
Pia, anasema wapo baadhi ya watu huyatumia kutengenezea pombe maarufu kama ulaka pindi yanapokuwa mabichi na hutumika katika familia na hutumika kama burudani ya familia na wengine huyakaush na kutengenezea pombe ya gongo ambayo hairuhusiwi.
“Unapokula bibo linakuwa na asili ya sukari, mara nyingi tunakamua na kuchuja na kunywa bila hata kuweka sukari wala kuongeza maji, hata kama uko shambani umekosa maji ya kunywa unayakamua na kunywa,”anasema Millanzi
“Kama serikali ikituletea viwanda vya kutengeneza bidhaa nyingine itakuwa imetusaidia kwa sababu tunatupa rasilimali nyingi, mtu akivuna tani kumi ina maana kila korosho moja ilikuwa na bibo lake moja hapo mabibo na yenyewe ni tani kumi au zaidi,”
Mikakati iliyopo
Mbunge wa Tandahimba, Katani Katani anasema baadhi ya wakulima hutengeneza pombe asili ya gongo ambayo haina viango na hairuhisiwi nchini na hivyo kupelekea mabibo mengi kuteketezwa.
Anasema utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa kilimo Naliendele unahitaji mashine zitakazotakiwa kufanya uzalishaji.

“Bahati nzuri waziri wa kilimo tulifika naye Naliendele anajua mabibo yanaweza kutengeneza mvinyo, kwa hiyo tunajaribu kuangalia namna iliyo sahihi tuweke kwenye sera ya kuona hilo jambo linaweza kuwanufaisha wakulima kwa namna nyingine,”anasema Katani

Share:

WAZIRI BITEKO ASHUHUDIA MAKABIDHIANO YA DHAHABU ILIYOKAMATWA MWANZA


Na GB Pazzo, BMG

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameshuhudia makabidhiano ya mali ikiwemo dhahabu iliyokamatwa katika Wilaya Sengerema mkoani Mwanza, ikisafirishwa kinyume na sheria baada ya kutaifishwa na mahakama kuwa mali ya Serikali.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Mei 31, 2019 jijini Mwanza baina ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP), Biswalo Mganga na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na
Mipango aliyewakilishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Khatibu Kazungu.

Akizungumza baada ya makabidhiano hayo, Biteko amewasihi wachimbaji na wafanyabiashara wa madini nchini kuachana na utoroshaji wa madini kwani biashara hiyo kwa sasa ni zilipendwa hivyo wafanye shughuli zao kwa kuzingatia sheria.

Naye DPP Biswalo Mganga amesema mali zilizotaifishwa ni dhahamu kilo 319 yenye thamani ya shilingi bilioni 27.018, fedha taslimu shilingi 305, mzani wa kupimia ubora wa
madini, mizani ya kupimia madini pamoja na magari mawili ambapo vyote kwa pamoja vilikamatwa mwezi januari mwaka huu wilayani Sengerema. 

Aidha ameongeza kwamba dhahabu kilo tano iliyokamatwa mkoani Geita nayo imekabidhiwa serikalini baada ya kutaifishwa pia.

Baada ya kupokea mali hizo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Khatibu Kazungu ametoa shukrani kwa mamlaka zote zilizofanikisha kukamatwa, kutoa ushahidi na kutaifishwa na kwamba zitatumika kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo.
Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP), Biswalo Mganga (wa pili kushoto) pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Madini, Khatibu Kazungu (wa kwanza kulia) wakishuhudia vipimo vya madini yaliyokamatwa wilayani Sengerema kabla ya kufanya makabidhiano.
Makabidhiano ya mali hizo yamefanyika leo jijini Mwanza na kushuhudiwa pia na viongozi wengine akiwemo Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella.
Madini yaliyokamatwa yakipimwa kabla ya makabidhiano kufanyika, hatua hii inajiri maada ya mahakama kutaifisha madini hayo.
Watuhumiwa 12 wakiwemo wenye mali wanne na askari polisi wanane walikamatwa wakihusishwa kuhusika na utoroshaji wa madini hayo wilayani Sengerema ambapo wenye mali walipatikana na hatia na kuhukumiwa huku askari polisi wakikana mashtaka dhidi yao ambapo bado kesi yao inaendelea mahakamani.
Viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa Madini, Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella wakishuhudiano vipimo vya madini hayo kabla ya kufanyika makabidhiano.
Viongozi mbalimbali wakishuhudia makabidhiano ya madini hayo.
Tazama video hapa chini



Share:

MJAMZITO AJIPASUA TUMBO KUTOA MTOTO TUMBONI RUKWA

Mwanamke mmoja anadaiwa kujipasua tumbo kwa kitu chenye ncha kali na kumtoa mtoto, wilayani Nkasi mkoani Rukwa Kusini Magharibi mwa Tanzania.

Tukio hilo limevuta hisia za wengi na wengine wakiwa katika taharuki wengi wakifika katika kituo cha afya kushuhudia ukweli wa tukio hilo linalodaiwa kutekelezwa na bi Joyce Kalinda.

Wakati taarifa za awali zikisema kuwa mwanamke huyo alijipasua umbo, Mganga mkuu wa wiaya ya Nkasi Dokta Hashi Mvogogo alizungumza na gazeti la Habari Leo alisema bado uchunguzi unafanyika ili kujua ukweli wa kilichotokea kwa mama huyo.

Uchunguzi unafanyika kubaini kama alijifanyia upasuaj mwenyewe kutoa mtoto au kuna mtu mwingine alifanya hivyo.

Daktari huyo amesema saa tisa alfajiri ya kuamkia siku ya Alhamisi, mwanamke huyo alifika katika kituo cha afya cha Kirando na kuanza kupiga kelele, akimtaka muuguzi aliyekuwa zamu ampe huduma za kumsaidia kujifungua.

Alisema kutokana na kuwepo kwa wagonjwa wengine kituoni hapo, muuguzi alimshauri mama huyo mja mzito kusubiri kidogo kisha alikwenda kumhudumia mgonjaw mwingine, lakini aliporejea mahali apokuwepo hakumkuta.

Kwa mujibu wa Dokta Mvogogo,ilipotimu alfajiri saa 11 mja mzito huyo alirudishwa hospitalini hapo akiwa amepasuka sehemu ya tumbo, huku watu waliomfikisha hospitalini hapo wakiwa wamembeba mtoto mchanga.

Watu hao walisema mwanamke huyo alikuwa amejipasua tumbo na kumtoa mtoto tumboni.

''Tumbo lilionekana limepasuliwa na kitu chenye ncha kali.Alipofika aliwekewa dripu tatu za damu ili kuokoa maisha yakekwani alikua amepoteza damu nyingi, lakini pia mtoto alipewa matibabu kutokana na kutolewa tumboni bila kufuata utaalamu unaotakiwa na sasa wote wanaendelea vizuri na matibabu,'' Dokta Mvogogo aliiambia Habari Leo.

Dokta Mvogogo amesema tukio hilo limeripotiwa polisi ili uchunguzi wa kina ufanyike kubaini ni nini kilichotokea kwa mama huyo.

''Uchunguzi unaofanywa pia unahusisha mtaalamu wa magonjwa wa akili ambaye tunataka achunguze ili kubaini kama mama huyo ambaye huo ni uzao wake wa nane ana ugonjwa wa akili au la,'' alieleza Daktari huyo.

Chanzo - BBC
Share:

MTOTO ACHOMWA MOTO,AKATWA VIWEMBE KISA KAKOMBA MBOGA YA KISAMVU

Mkazi wa Kata ya Buhalahala mjini Geita, Magreth Digugulo, anadaiwa kumchoma moto na kisha kumkatakata na wembe mjukuu wake kwenye mkono wa kulia kwa madai ya kukomba mboga.

Mtoto huyo (jina linahifadhiwa) alizungumza na Nipashe jana nyumbani kwao alitaja sababu za kufanyiwa kitendo hicho kuwa ni kujipakulia mboga aina ya kisamvu.

Alisema siku ya tukio, hakuwa amekwenda shuleni ila hakuwapo nyumbani na baada ya kurudi alipakua mboga kidogo akala na baada ya bibi yake kurudi, alimwita na kumkaripia ndipo akamchoma moto na kumkatakata vidole na wembe.

"Sikuwa nimeenda shuleni siku hiyo. Baada ya kutoka kucheza nilikuja nyumbani kula, sikumkuta bibi hivyo nikajipakulia mboga kidogo nikala. Bibi aliporudi akasema nimekomba mboga ndiyo akanifanyia hiki kitendo," alisema.

Baadhi ya majirani ambao walishuhudia tukio hilo, akiwamo Ayoub Bwanamadi, ambaye ni Mratibu wa Mtandao wa Marafiki wa Elimu, alisema walipata taarifa za tukio hilo na baada ya kusogea eneo la tukio, walitafuta namna yakumsaidia mtoto huyo.

Kwanza, alisema walitaka kujua nini chanzo cha tatizo na walimuuliza bibi yake akawajibu mtoto amekomba mboga ndiyo maana amemchoma moto.

Alisema tabia hiyo inaonekana imezoeleka kwa bibi huyo kutokana na mtoto kuonekana na majeraha mengine makubwa kwenye mwili wake ambayo yamekwisha pona.

"Hali ilivyo kwa huyu mtoto ni kama matukio haya ni ya kujirudia. Ukitazama kwenye kiganja cha mkono wake kuna kovu moja na mtoto anavyodai bibi alishawahi kumchoma kwenye majivu kabla ya tukio hili," alisema Bwanamadi.

Naye Ofisa Maendeleo ya Jamii wa Kata hiyo, Neema Emmanuel, alisema alipokea taarifa ya tukio hilo na kumpeleka mtuhumiwa polisi kisha kumpeleka mtoto hosptalini kwa ajili ya matibabu.

"Mwezi huu wa tano (Mei) matukio kama haya yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara. Hili ni tukio la nne kutokea kwenye kata yangu, mengine tumeshayafikisha kwenye ngazi husika. Hata hivyo tunawashukuru wananchi wamekuwa wakitoa taarifa za matukio haya," alisema.

Babu mzazi wa mtoto huyo, Stephano Matata, alisema tukio hilo limemsikitisha kutokana na mtoto huyo kutokuwa na msaada wowote wa malezi ya wazazi wake kwa kuwa anaishi na bibi yake kwa sababu mama yake mzazi ameshatokomea kwenye machimbo huku baba akiwa hajulikani ni nani.

"Mimi huwa sikai hapa nyumbani, lakini nilivyopata taarifa hizi zilinisikitisha kwani huyu mtoto ni kama hana wazazi. Mimi nitamchukua nikae naye kwa sababu hana msaada mwingine," alisema Matata.

Kutokana na kitendo hicho, bibi huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili kuhojiwa kabla ya kuchukuliwa hatua zaidi za kisheria.
Share:

NEC YATANGAZA NAFASI ZA AJIRA ZA MUDA ZA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza nafasi za kazi za muda kwa ajili ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura.

Kwa mujibu wa tangazo la maombi ya ajira hizo lililosainiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi Mabamba Rajabu Moses, Watanzania wenye umri kuanzia miaka 18 na wasiozidi miaka 45 wametakiwa kuomba.

Sifa zingine za waombaji ni kuwa na elimu ya kidato cha nne na kuendelea na awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.

“Awe na uwezo wa kutambua matatizo ya kompyuta ya hardware na software an kuyatatua” ilisema sehemu ya tangazo hilo.

“Awe na uwezo wa ku-istall programu za kompyuta an kutoa msaada wa kuifundi wa TEHAMA kwa watumiaji. Awe hajawahi kutiwa hatiani kwa makosa ya jinai an awe na uwezo wa kufanya kazi katika mazingira yenye usimamizi mdogo”,ameongeza.

Sifa nyingine za ziada za kazi hiyo zimetajwa kwenye tangazo hilo linalopatikana kwenye Tovuti ya NEC ya www.nec.go.tz na mitandao ya kijamii ya NEC.
Share:

ARIF TANZANIA ATAKA WENYE KIPATO KUSAIDIA WASIO NA KIPATO


Na Shushu Joel,Chalinze.

Taasisi ya Miraj Islamic Centre yenye makao yake mkuu jijini Dar es Salaam imetoa wito kwa watu wote walio na nafasi ya kipato kuwasaidia wasio na kipato kama ilivyoagizwa katika vitabu vya Mungu.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa taasisi hiyo Sheikh Arif Yusuf Abdulrehman maarufu Arif Tanzania alipokuwa akizungumza na baadhi ya waislamu wakati wa zoezi la kuwagawia futari wakazi wa Vikindu wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani. 

Arif Tanzania alisema taasisi yake imekuwa miongoni mwa taasisi za kuigwa nchini na nje kwa jinsi inavyojitolea kuwasaidia Watanzania wote pasipo kujali dini zao wala kabila huku lengo likiwa ni kuwaonyesha wale wasio na uwezo kuona ni sawa na wenye uwezo.

"Unaposaidia wenzako Mwenyekiti Mungu anakuongezea kutokana na jinsi wale unaowasaidia wanakuombea uweze kupata ili uendelee kuwasaidia zaidi",alisema Arif Tanzania.

Aliongeza kuwa kwa kipindi hiki cha mwezi huu wa Ramadhan taasisi ya Miraj Islamic imewezesha sehemu mbalimbali kwa ajili wananchi vyakula na tende kwa baadhi ya mikoa kama vile Arusha,Pwani,Mwanza,Kigoma,Zanzibar na mikoa mingine kwa kusudi la kuwasaidia wasio na uwezo wa kipato ila wamefunga katika mwezi Mtukufu wa Ramadhan. 

Aidha alisema Taasisi yake imekuwa msaada mkubwa kwa serikali kutokana na jinsi inavyojitoa katika masuala ya kusaidia watu mbalimbali ili waweze kujikwamua katika maisha yao,watu hao ni pamoja na kuwasaidia usafiri walemavu,vijana kuwapatia mashine za kukamulia juisi na wengine kuwapatia pikipiki kwa ajili ya kufanya shughuli za boda boda, akinamama kuwawezesha kwa vyerehani ya ushonaji.

Alisema kama kila mwenye nafasi ya kipato akijitolea kwa moyo mmoja basi Watanzania wengi watafikiwa na kuwawezesha ili nao waondokane na umaskini walionao.

Arif Tanzania pia aliipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa jinsi inavyofanya kazi zake na viongozi wa dini zote na kuwakomboa watanzania wa hali za chini kwenye imani zao pasipo kubagua. 

Kwa upande wake Ashura Juma (81) mkazi wa Vikindu katika wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani aliipongeza taasisi ya Miraj Islamic Centre kwa jinsi inavyojitolea katika kutoa misaada mbalimbali kwa wanyonge.

Aliongeza kuwa kwa kipindi hiki cha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kupitia taasisi hiyo familia yake imekuwa moja ya wanufaikaji wakubwa kwa kupata misaada mingi ikiwemo chakula kwa ajili ya futari,fedha na mahitaji mengine mengi ya kibinadamu.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa halmashauri ya Chalinze katika wilaya ya Bagamoyo, Mbunge wa jimbo hilo Ridhiwani Kikwete amesema kuwa misaada hiyo inayotolewa na taasisi hiyo imekuwa na tija kubwa kwa waumini wa dini ya kiislamu kutokana na uhitaji wa futari kwenye kipindi hiki.

Mbali na hilo Kikwete alisema pongezi hizo si kwa wananchi bali hata serikali imekuwa ikinufaika na Arif Tanzania kupitia taasisi zake zinazojitolea kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya wanyonge.

"Kutokana na jinsi taasisi hii inavyojitolea katika ufanikishaji wa wa misaada ni lazima sisi kama wawakilishi tuisemee vizuri ili wengine wajitokeze "alisema .
Share:

MHUBIRI ATUKANA MAASKOFU WASIOMHESHIMU...WAUMINI WANAOMVIZIA MKEWE

Mhubiri mwenye utata James Ng'ang'a wa Kanisa la Neno Evangelism Center nchini Kenya ametishia kuchukua hatua mikononi mwake na kuyafunga matawi mengine ya kanisa lake kwa kile alichokitaja kama kukosewa heshima. 


Wakati wa ibada, Ng'ang'a amewaonya waumini, maaskofu dhidi ya kummezea mate mkewe.

Ng'ang'a aliyekuwa mwingi wa hasira aliyataja majina ya baadhi ya waumini wa kanisa hilo la Neno Evangelism Center.

 "Mengi yamekuwa yakisemwa. Iwapo mtashindwa kumheshimu mke wangu nitawafukuza katika kanisa hili. Wakati huu sasa nitawaonesha uwezo wangu,You will know my true colour" Ng'ang'a alitishia. 

Haijabainika wazi kile mtumishi huyo alimaanisha kwa kutamka kukosewa heshima lakini aliwakemea baadhi ya waumini kwa madai ya kumvizia mkewe.

Hakukomea hapo tu bali alizidi kuwaonya baadhi yao kwamba iwapo hawatabadili mienendo atawachukulia hatua. 

"Vile vile, mwanamke yeyote ambaye atamkosea heshima mke wangu nitamfurusha humu kanisani. Utaondoka katika kanisa langu na kuanzisha lako,"aliongeza.

 Matamshi yake yaliwashtua waumini kanisani humo, ambao hawakuwa na la kufanya ila kuketi kitako na kumsikiza kwa makini huku wakisalia kumkodolea tu macho.

 Machi, 2019 alijipata pabaya baada ya kushtakiwa kwa kumtishia mwanahabari Linus Kaikai wa Citizen TV, baada ya Linus kupendekeza wachungaji wote ni sharti wawe na shahada ndipo wahudumu kama mapasta.

 Mhubiri huyo ambaye amezongwa na utata si haba alifunga ndoa na mkewe Mercy Murugi kwenye sherehe ya kifahari ilyoandaliwa Windsor Golf Club na kuhudhuriwa na wanasiasa mashuhuri. 

MSIKILIZE HAPA

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger