Saturday 6 February 2016

Magazeti ya Leo Jumamosi 06 Februari 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Share:

Friday 5 February 2016

DOWNLOAD ALIKIBA-LUPELA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

DOWNLOAD via MKITO
https://mkito.com/song/lupela/18700/bwi-1-36537
Share:

Mbunge Godbless Lema Awachana CCM Laivu

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mbunge wa arusha mjini Godbless lema amesema leo bungeni swala la Zanzibar si la kichama,Ni swala la nchi na lisipotafutiwa ufumbuzi lina athari kwa kila mtu,

Lema ameenda mbali zaidi na kuwaambia Wabunge Wa CCM hii nchi ikiharibika hata watoto wao wataharibikiwa na hawawezi kukaa madarakani kwa maisha yao yote.

Lema amemtolea mafano mbunge Marry nagu na kumwambia akumbuke serakali iliyopita alikuwa waziri,Lakini leo naye anauliza maswali ya nyongeza.

Lema alienda mbali zaidi na kumwambia Mwenyekiti wa bunge Chenge asijione ni mdogo wake mungu kwa kukalia kiti cha spika.
Share:

Wednesday 3 February 2016

MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARY 03 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Tuesday 2 February 2016

AJIRA MPYA ZA WALIMU 2016;SERIKALI KUAJIRI WALIMU ZAIDI YA 40000

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Serikali katika mwaka wa fedha 2016/2017 imepanga kuongeza ajira kwa vijana ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana wengi wa kitanzania kwa kuongeza ajira na kuwezesha wengine kujiajiri kupitia mifuko ya uwezeshaji toka Halmashauri za Wilaya nchini.

Akijibu swali la Mhe.Mgumba Tebweta Omary Mbunge wa Morogoro Kusini (CCM) lenye sehemu a na b lililouliza Serikali itaanza lini kuwawezesha vijana wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki  kifedha ili waweze kujiajiri na kuondokana na tatizo la ajira na umaskini ,Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe  Suleiman Jafo amesema vijana katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Kusini Mashariki wamekuwa wakiwezeshwa kiuchumi kupitia fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ambapo kila Halmashauri hupaswa kutenga asilimia 5 ya mapato yake ya ndani kila mwaka kwa ajili ya vijana.

Mhe  Suleiman Jafo ameongeza kuwa katika Bajeti ya mwaka 2014/2015,Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ilifanikiwa kutoa Shillingi Millioni 10.3 kwa vikundi vya vijana 19 kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za kiuchumi na katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2015/2016 vikundi vya vijana vilitengewa Shilllingi Millioni 87.5 ili kuviwezesha kiuchumi kwa kujiajiri.

“Katika kutatua changamoto zilizopo kwa vijana tunawawezesha  kifedha ili kujiajiri ili kumekuwa na tatizo la fedha kuchelewa kufika kwa walengwa ila Serikali kupitia Wizara yangu tunalifanyia kazi ili fedha zifike kwa wakati na tumetenga Shillingi Millioni 50 kwa kila kijiji kwa ajili ya kuwezesha vijana walioko katika vikundi mbalimbali mfano SACCOS ili waweze kujiajiri na kujikwamua kiuchumi kwa kujiondoa katika hali ya umaskini”

“Napenda kuwaomba wabunge tusaidiane sababu wao  wanahusika katika kamati za fedha za Halmashauri za Wilaya, waende wakasimamie hizo fedha kwa ajili ya kuwezesha vijana  zitoke na ziwasaidie walengwa” Alisema Mhe Jafo.

Aidha Mhe  Suleiman Jafo amesema kuwa Serikali imetenga Shillingi Billioni 233 kwa ajiri ya kuajiri vijana wapya takribani 71,408 kati ya hao watumishi wapya wa Afya wanatarajiwa kuwa takribani 10,871 na Waalimu 40,000 kwa nchi nzima ili kupunguza tatizo la ajira kwa vijana wanaomaliza vyuo mbalimbali nchini.

Serikali kupitia Halmashauri za Wilaya imejipanga katika kuwawezesha vijana katika maeneo yao kujikwamua kiuchumi kwa kujiajiri na kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali itaboresha zaidi mifuko ya kuwezesha vijana katika Halmashauri za Wilaya kwa kununua vifaa zaidi vya kujifunza stadi mbalimbali za kazi zitakazowezesha vijana wengi zaidi kuwa na ujuzi utakaowasaidia kujipatia kipato na kujikwamua kiuchumi.
Share:

UTARATIBU WA KUSHUGHULIKIA MALALAMIKO YA WANAFUNZI -MAAFISA MIKOPO WAGUSWA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
1.0    UTANGULIZI
Imebainika kwamba bado malalamiko ya baadhi ya wanafunzi hayashughulikiwi ipasavyo katika muda mfupi na kupelekea wanafunzi kwenda kulalamika ofisi za juu hata kwa masuala ambayo yako wazi na ambayo maelezo yake wangepaswa kuyapata katika ngazi za vyuo au katika Ofisi za Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.
Aidha, itakumbukwa kuwa, ili kuboresha ufanisi wa utoaji mikopo, mwezi Agosti mwaka 2011, Serikali kupitia iliyokuwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilivielekeza vyuo vyote za elimu ya juu kuanzisha madawati yatakayoratibu na kusimamia masuala ya mikopo na ruzuku kwa wanafunzi wa vyuo husika. Agizo hili limetekelezwa vizuri kiasi na hivi sasa kila chuo cha elimu ya juu kina Afisa anayesimamia masuala ya mikopo na ruzuku kwa wanafunzi wao wanaokopesheka.
Hivyo, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuwakumbusha wadau wake wote, wakiwemo wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, kuhusu utaratibu wa kuwasilisha malalamiko au maswali yanayohusu mikopo na ruzuku kwa wanafunzi wa elimu ya juu kama ifuatavyo hapa chini.

2.0    UTARATIBU WA KUWASILISHA MALALAMIKO

i.    KWANZA, mwanafunzi yeyote anayefadhiliwa na Serikali kupitia Bodi ya Mikopo mwenye swali au malalamiko anatakiwa kuwasilisha suala lake kwa Afisa mhusika anayesimamia Dawati la Mikopo/Ruzuku (Loan Officer) aliyepo chuoni kwake. Hao ‘Loan Officers’ hivi sasa wana uzoefu wa masuala ya mikopo na ruzuku zitolewazo na Bodi;
ii.    PILI, baada ya swali au malalamiko kupokelewa, ‘Loan Officer’ huyo anapaswa kuyapokea na kuyatafutia suluhisho malalamiko hayo na kumjibu mwanafunzi ndani ya siku mbili (02), kama siyo siku hiyo hiyo, tangu apokee swali au malalamiko hayo;
iii.    TATU, ikiwa siku mbili (02) zitapita bila mwanafunzi kupata jibu, mwanafunzi awasilishe malalamiko yake kwa mamlaka ya juu ya huyo ‘Loan Officer’ ambaye naye anapaswa kutoa majibu au kuchukua  hatua ndani ya siku mbili (02), kama siyo siku hiyo hiyo;
iv.    NNE, ikiwa kiongozi wa chuo husika cha elimu ya juu atakuwa hana jibu la swali au malalamiko yaliyowasilishwa kwake, anapaswa kuwasilisha suala hilo Ofisi ya Bodi ya Mikopo ya Kanda iliyo karibu na chuo chake. Ofisi ya Kanda itawajibika kutoa jibu siku hiyo hiyo ya kupokea maswali au malalamiko hayo au kuwasilisha suala hilo Makao Makuu ya Bodi ya Mikopo kama hana maelezo yake;
v.    TANO, kwa vyuo vya elimu ya juu ambavyo havipo karibu na ofisi za Kanda za Bodi ya Mikopo, uongozi wa chuo husika unapaswa kuwasiliana na makao Makuu ya Bodi ya Mikopo moja kwa moja kwa njia ya barua pepe ifuatayo: malalamiko@heslb.go.tz ;
vi.    SITA, baada ya kupokea malalamiko hayo, Bodi ya Mikopo Makao Makuu  itatoa majibu kwa malalamiko/maswali yaliyowasilishwa siku hiyo hiyo au ndani ya siku mbili (02) tangu kupokelewa kwa malalamiko au maswali hayo; na
vii.    SABA, mara tu baada ya kupokea majibu ya swali au malalamiko yaliyowasilishwa kutoka Bodi ya Mikopo, uongozi wa chuo cha elimu ya juu utayafikisha majibu hayo kwa mwanafunzi husika siku hiyo hiyo kupitia kwa ‘Loan Officer’ wa chuo husika.

3.0    HITIMISHO

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inasisitiza kuwa ni muhimu kwa wanafunzi na wadau wote kuzingatia utaratibu huu ili kuongeza ufanisi katika kushughulikia malalamiko ya wanafunzi.


IMETOLEWA NA:
MKURUGENZI MTENDAJI,
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

Share:

New AUDIO | Mh Temba Feat.Yamoto Band & Jokate - Fundi | Download

Share:

Monday 1 February 2016

New AUDIO | Real Jofu Ft. Nay wamitego - UNANIONEA | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
DOWNLOAD via HULKSHARE
http://old.hulkshare.com/dl/lrhqh2vfiznk/Real_jofu_ft_Nay_wamitego_-_UNANIONEA.mp3?d=1
Share:

UKAWA Wapinduliwa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Wabunge wa upinzani, wakiwamo wanaootoka vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wamepata pigo la aina yake baada ya jukumu mojawapo muhimu la kamati wanayopaswa kuiongoza kuondolewa kwao, imefahamika.

Kamati hiyo ni ya Hesabu za Serikali na Mashirika ya Umma (PAC) ambayo imehamishiwa kwenye kamati mpya inayoongozwa na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Majukumu hayo muhimu yaliyohamishwa PAC ni yale yanayohusiana na hesabu za mashirika ya umma.
Majukumu hayo sasa yamehamishiwa kwenye kamati mpya ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC), chini ya uenyekiti wa Mbunge wa Jimbo la Sumve (CCM), Richard Ndasa, huku makamu mwenyekiti akiwa Lolesia Bukwimba (Busanda-CCM).

Naibu Katibu wa Bunge anayeshughulikia masuala ya Bunge, John Joel, amethibitisha  juu ya kuwapo kwa mabadiliko hayo, akisema kwamba ni kweli PIC imepewa jukumu la kusimamia hesabu za mashirika ya umma kutokana na kanuni za Bunge, toleo la Januari 2016.

Alisema uamuzi wa kupeleka jukumu hilo PIC, umetokana na pendekezo la Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) kutokana na PAC iliyopita kushindwa kutimiza majukumu yake iliyopewa.

Katika mabunge yaliyotangulia, hesabu za mashirika ya umma zilikuwa zikisimamiwa na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia (Chadema), Zitto Kabwe. Hivi sasa, Zitto ni Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT-Wazalendo.

Kamati hiyo pia iliwahi kuongozwa na aliyekuwa Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), John Cheyo.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa mara zote PAC ndiyo iliyokuwa mstari wa mbele katika kuibua ‘madudu’ mbalimbali yanayohusiana na rushwa na ufisadi bungeni na kuilazimu serikali kubadili mawaziri wake mara kadhaa.

Baadhi ya mambo yaliyowahi kuibuliwa na PAC ni pamoja na kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow ambayo ripoti yake ilisababisha mawaziri wawili wa serikali ya awamu ya nne ya Rais Jakaya Kikwete na maofisa wengine kadhaa wa juu kuachia ngazi. 

Taarifa ya PAC kuhusiana na ripoti ya CAG mwaka 2012 pia ilisababisha vigogo kadhaa, wakiwamo mawaziri, kung’olewa.

Zitto Atoa ufafanuzi
Aliyekuwa Mwenyekiti wa PAC kwenye Bunge la 10, Zitto, amesema si kweli kwamba kuna jukumu walilopewa na kushindwa kulitimiza.

 “Kwa kweli tulitimiza majukumu yetu yote. Na ili tufanye kazi yetu kwa ufanisi, tuliigawa kamati, eneo moja likawa chini ya Makamu Mwenyekiti (Deo Filikunjombe) na moja chini yangu. Deo mashirika na mimi serikali.

"Hata hivyo, kazi ilikuwa kubwa na muhimu kugawa PAC kuwa na PIAC na PAC. Isipokuwa, PIC ya sasa haina mamlaka ya kushughulikia hesabu za mashirika ya umma kwa mujibu wa kanuni. Kamati za mahesabu ni mbili tu, PAC na LAAC,” alisema Zitto.

Aliongeza kuwa iwapo Bunge linataka PIC ishughulike na hesabu za mashirika ya umma, itabidi iitwe Public Investments Account Committee (PIAC) na itabidi iongozwe na mbunge wa upinzani na siyo wa CCM.

“Kanuni za Bunge za sasa hazielekezi PIC kushughulikia taarifa ya CAG kuhusu mahesabu ya mashirika ya umma. Pia kanuni haziipi PAC mamlaka hayo pia. Kikanuni, hivi sasa mahesabu ya mashirika ya umma hayana kamati,” alisema Zitto.
Share:

VIDEO:ESAYA FT BEST NASSO-KIGODORO

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjzYv1_AiSrXRQB5f0uSJc0ReNTQj4rY_PxfnOfAA09o3QqtGHOsMT_FzIFPhtDYbNzHwKh28fRoNC0WEVtj_Vd8XRkw4ju_x1iWOvv3BHxv8DY3pvxy6hcWD1e7bpvdEDFpVo0maNQx2s/s1600/vlcsnap-2016-02-01-08h06m14s130.png
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Official VIDEO | Shilole - Nyang'anyang'a

https://www.youtube.com/watch?v=ZA22teuu5-QINNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Chimbo la unga la Ray c!

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Ray-newMwanadada Rehema Chalamila ‘Ray C.
Stori: Mayasa Mariwata, Wikienda
Dar es Salaam: Inauma sana! Baada ya kuwepo kwa madai kuwa mwanadada Rehema Chalamila ‘Ray C’ amerudia matumizi ya madawa ya kulevya ‘unga’, Kikosi cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers kiliingia mzigoni kujua kama anaendelea na dozi ya kuacha ishu hiyo na kujua anakopatia ulevi huo kwa sasa.
Katika kusaka majibu ya mambo hayo mawili, yalipatikana madai kuwa kwa sasa ameacha kwenda kuchukua dozi ya kupona ya Methadone kwenye Hospitali ya Mwanayamala, Dar kama alivyokuwa akifanya awali.
Habari zilizopatikana kutoka kwa vyanzo vyetu zilieleza kwamba, msanii huyo ambaye tangu alipoanza kupatiwa matibabu ya kuacha unga alikuwa akihudhuria hospitalini hapo kuchukua lakini sasa haendi.
Ili kung’amua ukweli wa madai hayo, OFM ilizama kwenye Hospitali ya Mwananyamala na kuongea na Mganga Mkuu, Dk. Delila Moshi aliyethibitisha Ray C kutofika tena hospitali hapo kwa ajili ya kupatiwa dozi.
“Ray C haji tena hapa siku hizi labda amehamia Muhimbili,” alisema Dk. Delila.
OFM ilifika Muhimbili ili kujua maendeleo ya mwanadada huyo ambapo Afisa Habari aliyejitambulisha kwa jina moja la John alidai kuwa Ray C si miongoni mwa watu waliohamishiwa hapo.
“Kuna wagonjwa wamehamishiwa hapa lakini Ray C hayupo,” alijibu kwa kifupi na hata alipobananishwa kuwa mwanadada huyo amehamishiwa hapo na huenda ameamua kuacha dozi aliishia kucheka.
Katika fukunyuafukunyua, OFM ilipokea madai kwamba, baada ya kuacha dozi kwa sasa ana machimbo yake ambayo huwa anakwenda kununua unga.
Katika hilo, yalitajwa maeneo mawili, Magomeni na Mwananyamala nyuma ya hospitali hiyo.
OFM ilifika maeneo hayo yote na kushuhudia pilika za watu wasioeleweka huku wakijishtukia na kumshangaa Kamanda wa OFM, wakiambizana kuwa kulikuwa na sura ngeni katika maeneo yao hivyo wachukue tahadhari.
Kwenye eneo hilo la Mwananyamala, OFM ilibaini nyumba moja iliyodaiwa kuwa ndilo chimbo la ‘mambo hayo meupe’.
Katika kujiridhisha na mzani wa habari hiyo, OFM ilimtafuta Ray C ili kueleza juu ya madai ya kuacha tiba hiyo huku akitajiwa maeneo anayokwenda kuchukua unga ambapo aliwaka akidai kwamba hajaacha kwenda kuchukua dozi Mwananyamala.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger