Saturday 17 August 2024

UMMY AMSHUKURU RAIS DKT SAMIA

 
 Na Hadija Bagasha Tanga, 

Aliyekuwa Waziri wa afya ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumpa heshima kubwa ya kuwa Waziri wake kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu akiitumikia nafasi ya waziri ofisi ya Rais Tamisemi na baadaye wizara ya afya huku akisema ameyapokea mabadiliko hayo kwa moyo mkunjufu na kwa moyo wa shukrani. 

Ummy ametoa shukrani hizo wakati akizungumza kwenye mkutano wa ndani katika ziara ya Makamu wa pili wa Rais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hemed Suleiman Abdullah ambaye ni mlezi wa kichama katika Mkoa wa Tanga.

Ummy amesema kuwa ameyapokea mabadiliko yaliyotokea kwa moyo mkunjufu na kwa moyo wa shukrani kwani Rais Samia ameonyesha Imani yake kwake Kwa kiwango kikubwa huku akiahidi sasa kuwatumikia wanatanga ipasavyo. 

"Nimeyapokea mabadiliko haya kwa moyo mkunjufu lakini kwa moyo wa shukrani namshukuru Mwenyezi Mungu kwa yaliyotokea kubwa nikuahidi mheshimiwa Makamu wa Rais nitaendelea kuwa mwaminifu na mtiifu kwa Mwenyekiti wangu wa chama na chama kwaujumla lakini pia nikuahidi kwamba sasa nitafanya kazi kwa karibu sana na wananchi wangu ambao ndio walionipa heshima ya kuweka rekodi ya kuwa mbunge wa kwanza mwanamke katika jimbo la Tanga,"alisisitiza Ummy. 

Aidha Ummy amesema kwamba kazi kubwa sasa iliyopo mbele yao ni kuendelea kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi katika jimbo la Tanga kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa ccm Wilaya Tanga Meja Hamis Mkoba. 

"Tunasimama kifua mbele watu wa Tanga kwa jinsi Rais Samia alivyorubeba ksa kuboresha bandari ya Tanga hili jambo nililisema kwa sauti kubwa na kwa nguvu kubwa wakati naomba kura tunamshukuru Rais kazi hii aliianza Rais Magufuli na sasa Rais Samia anaendeleza Bilioni 429 zimewekwa katika bandari ya Tanga,  bandari ya Tanga imeboreshwa niliwaambia watu wa Tanga kwamba nataka Tanga iwe kama Singapore maana yake mameli makubwa yatie nanga katika bandari ya Tanga ndugu zangu wanatanga na sasa meli kubwa tunashuhudia zikitia nanga hapa, "alisema Ummy. 

"Mheshimiwa Makamu wa Rais kwetu sisi hili moja tu tuna deni kubwa kwa Rais Samia kwani hatumdai lakini yeye anatudai ushindi wa kishindo kwa sababu mameli makubwa sasa yanatia nanga katika bandari yetu ya Tanga juzi imekuja meli ya magari 500 yamechochea ajira nimepokea vijana wa Tanga 200 na siku nyingine tutakuletea madereva wa kuendesha gari za IST wanasema kwanini wanaoendesha watoke Daresalaam wameanzisha umoja tunawafungulia ofisi ili sasa madereva wa IST watoke jiji la Tanga, "alisema Ummy. 

"Nikuhakikishie Makamu wa, Rais tutakwenda nyumba kwa nyumba,  shuka kwa shuka,  kitanda kwa kitanda,  kata kwa kata kutafuta ushindi wa chama cha mapinduzi katika mitaa yote 181 ya jiji la Tanga na kata zote 27,"alisema Ummy. 

Aidha amewashukuru wanatanga  Kwa kumuwezesha kutimiza historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kugombea Jimbo la Tanga na kushinda. 

Share:

KIJANA AFARIKI WAKATI AKIHONDOMOLA TENDO LA NDOA NA BINTI GHETONI... CHANZO CHADAIWA DAWA ZA KUBOOST NGUVU




Kijana mwenye umri wa miaka 23 Raia wa Burundi amepoteza maisha wakati akifanya mapenzi.

Tukio hilo limeripotiwa kutokea Jumanne 12 August 2024 katika tarafa ya Kayogoro mkoani Makamba kusini mwa nchi ya Burundi.

Kijana huyo ajulikanae kwa jina la Eric(23) alipata mgeni ambaye pia alikuwa mpenzi wake aliyetambulika kwa jina la Grace (17) ndipo walipoanza kufanya mapenzi nyumbani kwa kijana huo baada ya mda Éric alipoteza maisha

Kwa mujibu wa mamlaka za vyombo vya dola na idara ya afya nchini Burundi chanzo cha kifo ni mshtuko wa moyo ambapo imedhibitishwa na daktari mkuu wa mkoa wa Makamba ambaye alifika eneo la tukio.

Majirani wa marehemu wakihisi kuwa kijana huo alitumia vidonge vya kuongeza nguvu kwenye tendo kitu ambacho hakijaweza kudhibitishwa.

Marehemu atazikwa jumamosi 17 August 2027 huku mwanamke aliyeshiriki naye mapenzi akishikiliwa na jeshi la polisi.

Kamishina wa jeshi la polisi mkoa wa makamba amefahamisha vyombo vya habari kuwa msichana huyo amewekwa kizuizini kwa ajili ya kulinda usalama wake.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AGOSTI 17,2024













Share:

Friday 16 August 2024

KANISA KATOLIKI LATOA MUONGOZO IBADA NA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MISA YA MAZIKO


Kanisa Katoliki la Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari Makongo Juu Jimbo Kuu la Dar es Salaam.


DAR ES SALAAM – Kanisa Katoliki Tanzania limetoa muongozo mpya kuhusu shughuli za ki imani zikihusisha utaratibu wa ibada na salamu za rambirambi katika misa ya miziko.

Taarifa iliyotolewa na Mratibu wa Liturujia Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Padri Stefano Kaombe likirejea kikao kilichoongozwa na Askofu Mkuu Jude Thadeus Ruwa’ichi imesema utaratibu wa salamu hizo kwa sasa utahusu wawakilishi watano pekee.

Wawakilishi hao ni mmoja kutoka parokia, Jumuiya, Chama chake cha Kitume, Ajira na Kiongozi wa jamii (mtendaji, diwani).

Pd. Kaombe amesema katika mkutano wa Waklero wote uliofanyika Juni 25, 2024, katika Kituo cha Msimbazi, mkutano ulielekeza kuwa kabla ya komunyo katika tukio la msiba maelekezo yatolewe kwa kuzingatia kuwa wanajumuika waamini wa madhehebu na imani mbali mbali.

“Sasa tunaingia hatua ya kupokea Ekaristi Takatifu. Hili ni tendo la pekee la kiimani. Wanaalikwa kushiriki Wakristo Wakatoliki waliojiandaa kiroho ipasavyo,” ilisema taarifa ya Pd. Kaombe.

Amefafanua kuwa salamu za rambirambi katika Misa ya maziko zitolewe na wawakilishi tu zikifuatiwa na neno la shukrani toka katika familia.

“Rambirambi zingine zaweza kutolewa nyumbani na makaburini baada ya ibada,” imesema taarifa hiyo.

Vile vile Kanisa limesema Ibada ya marehemu katika Misa ina sehemu nne: nyumbani, mlangoni, Misa inaendelea bila ibada ya toba, sala ya buriani. Misa inahitimishwa bila baraka kanisani, kwani makaburini kuna maziko na Baraka ya mwisho.

Kuhusu jeneza, taarifa hiyo imesema litengenezwe kwa namna nzuri, liweze kufunuliwa kutoka kushoto kuelekea kulia kwa marehemu, kama kuna sababu za msingi si lazima kufungua jeneza wakati wa sala ya buriani.

Aidha wakati wa kunyunyizia maji ya Baraka na kufukiza ubani, ni kipindi cha ukimya na maombolezi ya moyoni, hakuna sala ya hadhara katika maombezi kwa marehemu wetu.

Chanzo - Habarileo 


Share:

Thursday 15 August 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA AGOSTI 16, 2024






Share:

DK. BITEKO ASHIRIKI KIKAO CHA MAWAZIRI WA NISHATI NCHINI UGANDA




Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto BIteko leo tarehe 15 Agosti, 2024 ameshiriki kikao cha 19 cha pamoja cha Mawaziri wa Nishati ambao ni Wanachama wa Umoja wa soko la pamoja la kuuziana umeme na kuimarisha mifumo ya Gridi ya EAPP (Eastern Africa Power Pool) unaofanyika nchini Uganda.

Mkutano huo unajadili masuala mbalimbali ikiwemo kupitisha mabadiliko ya mikataba ya uongozi wa EAPP, kuridhia kanuni za uanzishwaji wa kitengo kinachojitegemea cha kusimamia soko la biashara ya umeme kwa nchi wanachama (Marketing and Trading unit) na kuridhia kanuni na taratibu za uendeshaji wa vikao vya Baraza la Mawaziri, Makatibu wakuu, na kamati ya uongozi.

Mkutano huo umehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Dennis Londo, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba, Mkurugenzi wa Shirika la Umeme (TANESCO) Mha. Gissima Nyamo-Hanga, Naibu Mkurugenzi Mipango, utafiti na uwekezaji CPA Renatha Ndege, na viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Nishati na taasisi zake.
Share:

Video Mpya : KUSEKWA LUKUBHA - BHUHABE

 

Share:

WATENDAJI VILABU VYA LIGI KUU WANUFAIKA NA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII KUTOKA NSSF

 


*Karia avitaka vilabu vyote ligi kuu kuchangamkia fursa ya kujiwekea akiba

*NSSF waeleza namna  watakavyonufaika kupata mafao, matibabu

Na MWANDISHI WETU,
Dar es Salaam. Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Bw. Wallace Karia amevitaka vilabu vinavyoshiriki ligi kuu Tanzania Bara kuwaandikisha wachezaji, makocha na wafanyakazi wao katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) ili waweze kunufaika na mafao mbalimbali yanayotolewa na Mfuko huo ikiwemo matibabu.

Bw. Karia amesema hayo tarehe 14 Agosti 2024 wakati akifungua semina kwa watendaji wakuu wa vilabu vinavyoshiriki ligi kuu, ambayo imeandaliwa na TFF, Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPBL) pamoja na NSSF, iliyofanyika katika ukumbi wa Mafao House Ilala, Dar es Salaam.

Amesema zipo faida nyingi za wachezaji na wadau wengine wa mpira kujiunga na kuchangia NSSF ikiwemo kupata mafao pamoja na huduma za matibabu na wategemezi wao na kuwa jambo hilo litawasaidia kipindi ambacho hawana nguvu za kucheza mpira.

Bw. Karia amevitaka vilabu vyote kuchangamkia fursa hiyo yenye manufaa kwa wachezaji, na kuwa vielekeze nguvu zaidi ya kuandikisha NSSF wachezaji vijana walio chini ya umri wa miaka 20 ili wanapostaafu mpira wanufaike na pensheni ya uzeeni inayotolewa na NSSF.

“Tunawashukuru wenzetu wa NSSF kwa kuja na jambo hili kwetu sisi litatuepusha na zile lawama tulizokuwa tunatupiwa ambazo hazituhusu za wachezaji wa zamani kuishi maisha magumu kwa kukosa kukidhi gharama za matibabu na gharama za maisha, angalau sisi tunaosimamia mpira tutahakikisha wachezaji wanaocheza kipindi hiki wasipate changamoto ambazo wanazipata wenzao,” amesema Bw. Karia.

Naye, Bw. Cosmasi Sasi, Meneja Uandikishaji, Ukaguzi na Michango wa NSSF, amesema kwa mujibu wa mabadiliko ya sheria ya hifadhi ya jamii sura ya 50 ya mwaka 2018, NSSF ndio Mfuko pekee uliopewa jukumu la kuandikisha wanachama waliopo katika sekta rasmi na sekta isiyo rasmi wakiwemo wachezaji wa mpira pamoja na wajasiriamali wengine wote.

“Lengo la NSSF ni kuwafikia wafanyakazi waliopo katika sekta binafsi na tayari kazi hiyo tunaifanya kwa njia mbalimbali, lakini ili tuweze kumfikia kila mmoja tuna jukumu la kutoa elimu ya hifadhi ya jamii, mafao tunayotoa na faida zake. Tunashukuru kupata fursa hii ya kujumuika na wenzetu TFF, TPBL pamoja na watendaji wakuu wa vilabu vinavyoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara kwa lengo la kutoa elimu hii ili waweze kujiunga na kuchangia,” amesema Bw. Sasi.

Amesema wachezaji na watendaji wa vilabu vya mpira ni wadau muhimu ambao wanatakiwa wapate kinga ya hifadhi ya jamii ili waweze kunufaika moja kwa moja kipindi ambacho hawana uwezo wa kucheza mpira kwa kupata mafao yatakayowasaidia kuishi maisha bora uzeeni.

Bw. Sasi amesema sheria ya NSSF imezungumzia mahususi wanaopaswa kujiunga na Mfuko kuwa ni wafanyakazi wote walioajiriwa katika sekta binafsi, raia wa kigeni wanaofanya kazi Tanzania bara, watumishi wa taasisi za kimataifa zinazofanya kazi Tanzania bara na watu waliojiajiri katika sekta isiyo rasmi.

“Tutahakikisha elimu ya hifadhi ya jamii inawafikia wana michezo wote hata waliopo vilabu vya chini, lengo waweze kujiunga na kujiwekea akiba kwa ajili ya kesho yao iliyokuwa njema,” amesema Bw. Sasi.

Naye, Meneja wa NSSF Mkoa wa Temeke, Bw. Ferouz Mtika ameishukuru Bodi ya Ligi, TFF na vilabu vya mpira wa miguu kwa kushiriki semina hiyo yenye lengo la kupata elimu ya hifadhi ya jamii.



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger