Thursday 19 September 2024

JAMBO FOOD PRODUCTS YAJA NA MUONEKANO MPYA WA BIDHAA ZAKE

...

Kampuni ya Jambo Group imezindua muonekano mpya wa bidhaa zake za Jambo Food Products ‘Jamukaya’ zenye muonekano mzuri na wa kuvutia wenye radha ile ie.

Hafla ya uzinduzi huo umefanyika Septemba 17, 2024 kwenye kiwanda hicho ukiongozwa na Mkurugenzi Nassoro Salum Hamis pamoja na Meneja Mkuu wa Jambo Fm ambaye pia ni msimamizi wa Chapa group Nickson George, huku ukihudhuriwa na wananchi pamoja na wafanyakazi wa jambo.

Akizungmza wakati wa uzinduzi huo George amesema mbali na uzalishaji wa bidhaa bora pia imejidhatiti kutoa ajira za kudumu 400,000 ukijumlisha na wale wa ajira ya muda mfupi wanakuwa 600,000 hivyo kila siku watu hao wako kazini na serikali inapata mapato yake.

“Tumeamua kubadilisha muonekana wa sura ya mpya ya bidhaa baada ya kampuni kufikisha miaka 20 ya uzalishaji wa bidhaa zake hivyo tumeheshimu wateja wetu na hatua hiyi llni kuunga mkono juhudi za serikali kupunguza wimbi la vijana wasio na ajira,” amesema George.

Ameongeza kuwa mteja akiona muonekano mpya asiwe na mashaka kwani kuna usemi unaoeleza ‘Hawa ndio sisi’ ikimaanisha muonekano huo usiwape wasiwasi bali ni kampuni hiyo hiyo ikiendelea kuwapa furaha wateja wake.

Nao baadhi ya wananchi waliohudhuria hafla hiyo, wamepongeza muonekano mpya wa bidhaa za jambo, huku wakitoa wito kwa watanzania kwamba wawaunge wawekezaji wazawa kwa kununua bidhaa zao.

Kauli mbiu ya uzinduzi wa sura mpya bidhaa za jambo inasema “Jambo hawa ni sisi,dukani mpaka nyumbani,sisi ndio sura mpya ya furaha na maisha mazuri”.

Meneja Mkuu wa Jambo Fm ambaye pia ni msimamizi wa chapa group Nickson George akizungumza wakati wa uzinduzi huo.



Meneja Mkuu wa Jambo Fm ambaye pia ni msimamizi wa chapa group Nickson George akizungumza wakati wa uzinduzi huo.

Baadhi ya watu waliojitokeza kwenye uzinduzi huo.




Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger