Friday 9 August 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI AGOSTI 9,2024

Share:

Thursday 8 August 2024

PPAA YAOKOA BILIONI 567.6 KATIKA MICHAKATO YA ZABUNI ZA UMMA





Na Zena Mohamed,Dodoma

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imefanikiwa kuokoa upotevu wa fedha za serikali kiasi cha TZS: 567,636,151,996.00 katika mshauri 140 yaliyokuwa katika hatua mbalimbali za michakato ya ununuzi wa umma kwa kipindi cha miaka mitatu (2021 – 2024).

Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando amebainisha hayo alipozungumza na waandishi wa Habari katika maonesho ya Kilimo ya Kimataifa (Nane Nane), yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni, Jijini Dodoma.

“PPAA imeendelea kudhibiti taasisi nunuzi kukiuka taratibu za kisheria hasa katika kufanya tathmini ya zabuni (tender evaluation); katika baadhi ya mashauri ambapo ilifanikiwa kubaini ukiukwaji wa taratibu za kufanya tathimini uliofanywa na taasisi nunuzi ikiwemo kutokuzingatia vigezo vilivyowekwa katika kabrasha la zabuni au kuongeza vigezo vipya ambavyo havikuwepo awali,” alisema Bw. Sando.

Bw. Sando aliongeza kuwa kwa kufanya hivyo, Mamlaka hiyo ilihakikisha kuwa zabuni zinatolewa kwa wazabuni wenye sifa na hivyo kuiwezesha Serikali kupata thamani halisi ya fedha na kuepusha upotevu wa fedha za serikali kiasi cha TZS: 567,636,151,996.00 katika michakato ya ununuzi wa umma kwa kipindi cha miaka mitatu.

“PPAA imeweza kushughulikia jumla ya mashauri 140 yaliyotokana na michakato ya Ununuzi wa Umma kwa kudhibiti utoaji wa tuzo kwa wazabuni ambao walipendekezwa kupata zabuni bila kuwa na sifa stahiki,” aliongeza Bw. Sando.

Aidha, Bw. Sando aliongeza kuwa PPAA ilizuia utoaji tuzo kwa wazabuni 32 wasio na uwezo wa kifedha pamoja na wale waliokosa sifa za kitaalamu za kutekeleza zabuni husika na kuiwezesha Serikali kupata thamani halisi ya fedha. Hatua hiyo iliepusha utekelezaji usioridhisha wa miradi ambao ungesababisha upotevu wa fedha za umma na kuchelewesha maendeleo kwa wananchi.

“Serikali ya awamu ya Sita inaamini kuwa usuluhishi wa migogoro hauwezi kupatikana penye ubaguzi na pale ambapo kuna wanaokosa fursa na haki zao za kiuchumi na kiraia. Hivyo, kitendo cha PPAA kuzuia utoaji wa tuzo kwa wazabuni 32 waliokosa sifa kinaweka uzito katika usuluhishi wa migogoro ambayo ni moja kati ya falsafa za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan,” alisema Bw. Sando.

Katibu Mtendaji wa PPAA ameongeza kuwa Mamlaka hiyo kwa kushirikiana na Mamlaya ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imejenga moduli mpya ya kuwasilisha Rufaa/Malalamiko kwa njia ya kieletroniki (Complaint & Appeal Management). “Moduli hiyo inarahisisha uwasilishaji wa malalamiko na kutoa fursa kwa wazabuni wengi zaidi kuwasilisha malalamiko yao, ni rafiki na inaokoa muda wa kuwasilisha rufaa,” alisema Bw. Sando.

Aidha, Moduli ya Complaint & Appeal Management imewekwa kwenye Mfumo wa Ununuzi wa Umma Kieletroniki (NeST), uliojengwa chini ya Uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) ni Taasisi iliyo chini ya Wizara ya Fedha iliyoundwa kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi ya Umma Na. 3 ya Mwaka 2001 ambapo baada ya Sheria hiyo kufutwa, Mamlaka ya Rufani ilihuishwa chini ya Sheria ya Ununuzi ya Umma Na. 21 ya Mwaka 2004 na kuhuishwa tena kupitia Sheria ya Ununuzi wa Umma Na. 7 ya Mwaka 2011 baada ya ile Sheria Na. 21 ya Mwaka 2004 nayo kufutwa. Mwaka 2023 Sheria ya Ununuzi wa Umma Na. 7 ya Mwaka 2011 nayo ilifutwa na Mamlaka ya Rufani ilihuishwa tena kupitia Sheria ya Ununuzi wa Umma Na. 10 ya Mwaka 2023.

Share:

HALMASHAURI YA USHETU WAJIANDAA KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA

NA MWANDISHI WETU

Katika kuelekea zoezi la Uboreshaji wa Daftari la mpiga kura, Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama Mkoani Shinyanga imekutana na wadau mbalimbali likiwemo Shirika la Huheso katika kujadili namna Bora ya uhamasishaji wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo linalotarajia kuanza hivi karibuni.

Kikao hicho kimefanyika Agosti 7, 2024 katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, huku zoezi hilo likitarajia kushika hatamu kuanzia Agosti 21 mpaka 27 mwaka, huku kukiwa na Vituo 249 vya uandikishaji katika Halmashauri hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu ambae pia ni Afisa Muandikishaji Mkuu katika zoezi Hilo Bi Khadija Mohamed Kabojela amewaomba wadau wote waliojitokeza kuwa mabalozi Wazuri katika kuihamasisha Jamii kuona umuhimu wa kushiriki Zoezi Hilo la kuboresha taarifa zao , sambamba na kujiandikisha upya kwa wale wenye sifa.

Bi Khadija amesema wadau ni chachu ya maendeleo hivyo Wana wajibu wa kushiriki zoezi la uhamasishaji wa Uboreshaji wa Daftari la mpiga kura kwa kutoa taarifa na Elimu sahihi juu ya umuhimu huo wa kujiandikisha kwani kwa kufanya hivyo kutamsaidia raia kutimiza haki yake ya msingi katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2025 kwa kupiga kura kwa Kiongozi anayemtaka.

Kwa Upande wake Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Ushetu Bw. ELISHA MAHUNGO ametaja wenye sifa za kushiriki katika Zoezi Hilo la Uboreshaji wa Daftari la mpiga kura ni pamoja na Wapiga Kura wapya ambao hawajawahi kujiandikisha lakini Wana sifa za kupiga kura kuanzia miaka 18 na kuendelea, wale wote watakaotimiza miaka 18 ifikapo Oktoba kipindi Cha uchaguzi Mkuu mwaka 2025, lakini pia wale waliohamia kwa makazi ya kuishi katika Halmashauri hiyo, waliopoteza kadi zao, sambamba na kufuta taarifa za wapiga kura waliokosa sifa za kuendelea kuwepo katika daftari Hilo hasa waliotangulia mbele za haki.

Sambamba na Hilo alisema zoezi Hilo halitawahusu wananchi walio na vitambulisho visivyohitaji maboresho, hivyo amewasihi kuendelea kuvitunza kwa umakini mkubwa.

Kikao hicho kimehudhuliwa na wadau mbalimbali likiwemo Shirika la Huheso lenye makao yake makuu Mjini Kahama na ofisi yake ndogo iliyopo Halmashauri ya Ushetu inayotekeleza mradi wa EpiC unaofadhiliwa na USAID na kuratibiwa na FHI360 unaojihusisha na Upimaji wa VVU, huku wadau wengine wakiwa ni Jeshi la Polisi Ushetu ,Viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya Siasa, wawakilishi wa vijana pamoja na Vikundi vya hamasa vinavyopatikana ndani ya Halmashauri ya Ushetu.



Share:

RAIS SAMIA APONGEZA NSSF NA JESHI LA MAGEREZA KUKAMILISHA MRADI WA KIWANDA CHA SUKARI MKULAZI

 


*Asema mradi huu una umuhimu wa kipekee
*Asema kiwanda hicho kinaenda kutoa uhakika wa sukari nchini, awapongeza NSSF na Jeshi la Magereza kwa kufanikisha mradi huo

Na MWANDISHI WETU,
MOROGORO.

 Historia imeandikwa na hakika hakuna kilichokwama! Unaweza kusema hivyo baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuzindua rasmi mradi wa kiwanda cha sukari Mkulazi, kilichopo Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro na kusema mradi huo anataka uwe endelevu kwa maslahi mapana ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Uzinduzi wa kiwanda hicho chenye uwezo wa kuzalisha sukari tani 50,000 kwa mwaka umefanyika tarehe 7 Agosti, 2024 na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali.

Akizungumza na wananchi waliohudhuria hafla hiyo Mhe. Rais Dkt. Samia amewapongeza wana hisa wa kiwanda hicho ambao ni NSSF na Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Uzalishaji Mali (SHIMA), kwa kukamilisha mradi huo wenye manufaa makubwa na kuwa Serikali inafanya kila jitihada kutanua mradi huo.

Aidha, amepongeza mradi huo kutoa ajira kwa vijana wa Tanzania pamoja na wakulima kupata soko la uhakika wa kuuza miwa. Pamoja na hilo amepongeza mradi huo kutumia umeme ambao unaozalishwa kiwandani hapo.  Amesema dhamira na malengo ya Serikali ni kuhakikisha mradi huo unakua na kuleta tija kubwa kwa jamii na Taifa kwa ujumla.

Naye, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema ujenzi wa kiwanda hicho unatokana na maono ya Rais Dkt. Samia ambaye aliahidi kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ukiwemo wa Mkulazi. Amesema baada ya Rais Dkt. Samia kuingia madarakani mwezi Machi 2021, aliridhia mradi huo kuendelea na kuwa unaenda kupunguza nakisi ya sukari nchini na kutatua changamoto ya ajira.

Amesema uwekezaji wa mradi huo umeongeza wigo wa kodi na umechechemua uchumi wa mwananchi mmoja mmoja.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima amemshukuru Rais Dkt. Samia kwa ziara yake katika mkoa huo ambayo imekuwa na mafanikio makubwa hasa katika kuzindua miradi ya kimkakati ukiwemo wa kiwanda cha sukari Mkulazi ambao umetoa fursa nyingi kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Akitoa taarifa ya mradi wa kiwanda hicho, Dkt. Hildelitha Msita, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Mkulazi, amesema wataendelea kutekeleza dhamira ya Serikali ya kuondoa nakisi ya sukari nchini pamoja na kuongeza ajira kwa Watanzania kwa kusimamia uendeshaji wa kiwanda hicho chenye uwezo wa kuzalisha tani 50,000 za sukari kwa mwaka na tayari uzalishaji wa sukari ya majumbani ulianza tarehe 1 Julai, 2024 ambapo kwa siku kinazalisha tani 250.

Kwa upande wake Mhandisi Hamad Masauni, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, amesema mradi huo umekuwa na faida kwa Jeshi la Magereza na kuwa faida hizo zinatokana na maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia kuhakikisha wanatumia vizuri rasilimali za Jeshi hilo kwa kuleta tija na kutoa mchango kwa jamii na Taifa.

Naye Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe amesema uwepo wa mradi wa kiwanda hicho unatoa fursa mbalimbali kwa wananchi, hivyo watahakikisha kiwanda hicho kinazalisha sukari ya majumbani na viwandani na kinalindwa kwa maslahi mapana ya Taifa.

Aidha, Mhe. Dkt. Suleiman Jafo, Waziri wa Viwanda na Biashara, amesema Serikali ya awamu ya sita imeweka historia kubwa ikiwemo kuongeza idadi ya viwanda takribani 18,000 ndani ya miaka mitatu.

Mbunge wa Jimbo la Kilosa, Profesa Kalamagamba Kabudi amesema wananchi wa jimbo hilo wanashukuru ujio wa kiwanda hicho ambacho kinawasaidia kupata ajira na kupata soko la uhakika la kuuza miwa yao.


Share:

Wednesday 7 August 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI AGOSTI 8,2024

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger