Friday, 18 August 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA AGOSTI 18,2023



























Share:

Thursday, 17 August 2023

MKOA WA TANGA UNA CHANGAMOTO KUBWA YA MATUKIO YA AJALI ZA BARABARANI HUSUSANI ZA WANAFUNZI

 Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoani Tanga (RTO) Wiliam Mwamasika akizungumza wakati kuelezea mpango kazi wa Usalama barabara kwa Jiji la Tanga unaendeshwa na Shirika la Amend Tanzania ambao umefikia asilimia 90.
Meneja wa Shirika la Amend Tanzania Simon Kalolo akielezea  Mpango Kazi wa Usalama Barabarani
Mmoja wa madereva waliokiuka sheria za usalama barabara Avishai kushoto akiandika maelezo ya kutokurudia kosa la kutokusimama kwenye kivuko cha waenda kwa miguu baada ya kukamatwa kwa kosa hilo leo na kufikishwa kwenye mahakama ya watoto iliyokuwa ikishikiliza kesi za madereva waliovunja sheria za barabarani kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa Tanga William Mwamasika
Mahakama ikiendelea
Elimu ikitolewa kwa waendesha bodaboda

Wanafunzi wakifiatilia mahakama hiyo





Na Oscar Assenga,TANGA

JESHI la Kitengo cha Usalama barabarani mkoani Tanga limesema kwamba mkoa huo una changamoto kubwa ya matukio ya ajali hususani kwa watoto na wanafunzi wanapotoka majumbani kwenda shuleni na wanaporejea.

Hayo yalibainishwa leo na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoani Tanga (RTO) Wiliam Mwamasika wakati wa kuelezea mpango kazi wa Usalama barabara kwa Jiji la Tanga unaendeshwa na Shirika la Amend Tanzania ambao umefikia asilimia 90.

Kabla ya kueleza mpango huo kulishuhudiwa uendeshaji kesi katika Mahakama ya Watoto( Mahakama Kifani) kwa madereva waliovunja sheria za usalama barabarani kwa kutosimama maeneo yenye alama za watembea kwa miguu yanayotumiwa kuvuka wanafunzi.

Mpango huo umekwenda sambamba na kufadhili mafunzo kwa waendesha bodaboda 300 katika Jiji la Tanga ili kuweza kuzijua sheria za usalama barabarani na namna ya kuweza kuziepuka.

Alisema mara nyingi ajali hizo zimekuwa zikisababishwa na waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda kutokana na baadhi yao kushindwa kufuata sheria za usalama barabarani

Alisema kufuatia uwepo wa changamoto hiyo, Jeshi hilo limendelea kujipanga na kuimarisha usalama hususani kwenye vivuko wavyovukia wanafunzi nyakati za asubuhi wanapovuka ikiwa ni mkakati wa kutokomeza ajali ambazo zimekuwa zikipoteza ndoto zao.

“Kwa kweli sisi kama Mkoa wa Tanga tumejipanga vizuri kuhakikisha tunatokemeza ajali za barabarani hususani kwa watoto na wanafunzi kwa kuhakikisha kila siku hususani nyakati za asubuhi kuna kuwa na askarti wa usalama kwenye vivuto vya watembea kwa miguu kwa lengo kuondosha ajali hizo”Alisema

Alisema watumiaji wa vyombo vya moto wamekuwa wakipuuzia sheria za usalama barabarani licha ya kuzifahamu hivyo ni jukumu la kila mwananchi sasa wahakikishe wanazingatie na kufuata sheria za usalama ili kuweza kupunguza ajali

Awali Meneja wa Shirika la Amend Tanzania Simon Kalolo alisema hilo limetekeleza Mpango Kazi wa Usalama Barabarani kwa Halmashauri ya Jiji la Tanga kwa asilimia 90 huku likitumia nafasi hiyo kueleza hatua mbalimbali za kuutekeleza mpango huo ikiwemo kutoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa 350 wa shule za msingi.

Alisema Shirika hilo linajishughulisha na usalama barabarani nchini tangu mwaka 2009 na kwa ufadhili wa Shirika la Fondation Botnar jijini Tanga, shirika hilo limekuwa likishirikiana na Halmashauri ya Jiji katika kuboresha miundombinu ya barabara kwenye maeneo ya shule.

“Pia kutoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi,kuanzisha klabu za usalama barabarani na mahakama kifani za watoto, mafunzo kwa madereva pikipiki , kuandaa makongamano ya wadau wa usalama barabarani, kufanya tafiti huhusu ajali za barabarani, na kuandaa Mpango Kazi wa usalama barabarani kwa Jiji hilo”Alisema

Akizungumzia Mpango Kazi huo wa usalama barabarani wenye lengo la kuboresha safari salama na endelevu kwa jiji la Tanga alisema ulizinduliwa Novemba 11 ,2022 na tangu ulipozinduliwa kuna mambo kadha yametekelezwa.

Alisema baada ya uzinduzi huo amesema shirika la Amend limefanikia kuzindua miundumbinu katika shule tatu za msingi za Shaaban Robert, Mabawa na Majengo.

“Mpaka sasa tumetoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi 3,501 wa shule za msingi Mabawa, Majengo and Shabaan Robert na wengine 3,247 wa shule za sekondari Toledi, Kihere and Kiomoni”Alisema

“Tumeanzisha klabu mbili za shule za usalama barabarani katika Shule ya Msingi Usagara na klabu ya usalama wa baiskeli katika Shule ya Sekondari Usagara, yenye watoto 20 katika kila klabu na tumetoa mafunzo ya usalama barabarani kwa watoto hawa, baada ya kuhitimu kuwa mabalozi, wakipokea vyeti katika hafla ndogo”Alisema

"Shughuli za vilabu hivi zimejumuisha mafunzo, midahalo ya usalama barabarani, michezo, mijadala ya mezani na kushiriki katika kampeni za vyombo vya habari na mafunzo ya msasa kwa madereva wa pikipiki 350 kufanya jumla ya madereva waliopata mafunzo haya kufikia 950."

Kalolo alisema Februari mwaka huu wamesambaza vifaa vya kufundishia usalama barabarani kwa maofisa maendeleo ya jamii katika kata 22 kati ya 27 za Jiji la Tanga.


MWisho.
Share:

TAMKO LA KULAANI KUSHAMBULIWA KWA WAANDISHI WA HABARI



 Chama  Cha  Waandishi wa Habari wa Kupiga  Vita  Matumizi  ya  Dawa za  Kulevya na Uhalifu Tanzania  (OJADACT) kinalaani  tukio  la  kijinai  lililofanywa  na  vijana  wa  jamii ya  kimasai  dhidi  ya  waandishi wa  habari lililotekea  Agosti, 15,  2023  katika Kijiji cha  Enduleni, Wilaya  ya  Ngorongoro, Jijini Arusha.
 

Tukio  hilo   lilihusishwa  kujeruhiwa  kwa  Waandishi wa  habari    wafuatao, Ferdnand   Shayo  (ITV), Dennis  Msacky (Media  Brain),Habib  Mchange (Jamvi  la  Habari),Elia  Kinian (Channel  Ten),Janeth  Joseph (Mwananchi), Dickson Busagaga (Clouds   Media)  na  Mkalimani  wao  Lengai  Ngoishiye,

 

Waandishi  hao  walikutwa  na madhila  hayo   wakati  wakitekeleza  majukumu  yao  ya  kikazi ya  kutafuta  taarifa za  wamasai wanaoishi  Ngorongoro   na  kutaka  kuhama   kwa  hiari  yao  toka  Kijiji cha  Enduleni kilichopo  ndani  ya  hifadhi  ya  Ngorongoro.

 

OJADACT  inaamini   kuwa  Jeshi la  Polisi  Mkoa wa Arusha  pamoja na Mamlaka  nyingine  za  ulinzi  na usalama    zitawatafuta  na  kuwakamata  watuhumiwa  wa  tukio hilo  na kuwafikisha  kwenye   mkono wa  sheria  ili  wawajibishwe na  iwe  funzo  kwa  watu  wengine  wenye  nia  ovu  dhidi  ya  waandishi wa  habari.

 

Pia  OJADACT inawakumbusha  waandishi wa  habari  na  vyombo  vya  habari  kufanya  tathimini  ya  ulinzi  na  usalama  wa  maeneo  wanayotakiwa  kwenda  kufanya  kazi  zao  ili  kupungunza  madhila  yanayoweza  kuwapata  na  pia  OJADACT inatia  pole  majeruhi  wote.

 

 Edwin  Soko

 Mwenyekiti,  OJADACT

 Julai Agosti 17, 2023

Share:

JUMLA YA WAZABUNI 4,350 WAMEJISAJILI KWENYE MFUMO WA NeST.



Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma PPRA yawasisitiza Wafanya biashara na Wazabuni wote nchini Kuendelea kujisajili katika Mfumo mpya wa Ununuzi wa Umma kwa njia ya mtandao NeST ili kuongeza ushindani na kupanua wigo Mpana katika kuboresha uendeshaji wa Michakato ya ugawaji wa zabuni za umma.
Akizungumza hayo Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA Bw. Eliakim Maswi amesema kuwa, Idadi ya Wazabuni wanaojisajili kwenye Mfumo inazidi kuongezeka siku hadi siku jambo linalotoa taswira Chanya juu ya muitikio na mapokeo ya Wananchi katika ujio wa Mfumo huo mpya wa NeST katika sekta ya Ununuzi wa Umma.

“Tunashkuru kupitia juhudi za Serikali yetu Kuona idadi ya Wazabuni wanaojisajili ndani ya Mfumo inaongezeka siku hadi siku suala ambalo hata sisi kama Mamlaka tunalitazama kwenye mtazamo Chanya, Mpaka sasa Jumla ya Wazabuni 4,350 tayari wameshajisajili kwenye Mfumo” Alisema Maswi.

Sambamba na suala hilo, Maswi amewataka Wazabuni Pamoja na Taasisi za Umma kuendelea kushiriki mafunzo yanayoendelea kutolewa katika mikoa mbalimbali nchini ambayo yanalenga kutoa muongozo wa namna ya matumizi sahihi ya Mfumo huo wa NeST kwa Taasisi za Umma sambamba na Wazabuni wake.

“Utaratibu wetu wa utoaji Mafunzo ya jinsi ya kutumia mfumo bado unaendelea, Kwahivyo niwasihi Wazabuni Pamoja na Taasisi mbalimbali za Umma kuweza kushiriki mafunzo hayo kwa mujibu wa ratiba zinazopangwa” Aliongezea

Aidha amesema kuwa, Sambamba na Utoaji wa mafunzo hayo wanahakikisha kila Taasisi inayopatiwa mafunzo inasajiliwa ndani ya Mfumo mpya wa NeST ili mapema kuanza kutumia Mfumo huo bila kuwa na urasimu wa aina yoyote.

“Kila Taasisi tunayoipatia mafunzo ya Mfumo mpya tunahakikisha tunaisajili pia kwenye mfumo ili ikibidi waanze kutumia mfumo huu haraka” Alisema

Ifikapo tarehe 30 Septemba Taasisi zote za Umma zinatakiwa ziwe tayari zimeshajisajili kwenye Mfumo kwani Mpaka tarehe 1 Oktoba hakutakuwa na Taasisi yoyote ya Umma itakayoweza kufanya michakato ya Ununuzi nje ya mfumo wa NeST.
Share:

MIAKA 20 YA PEPFAR: KITUO CHA BIKIRA MARIA MAMA WA TUMAINI - MASANGA KIMBILIO SALAMA LA TOHARA KINGA KWA WANAUME


Msimamizi wa kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT) na Mkurugenzi Mtendaji wa asasi ya ATFGM,  Sister Jacqueline Gbanga akielezea namna wanavyoshirikiana na PEPFAR kukabiliana na Maambukizi ya VVU kupitia Tohara Kinga ya Kitabibu kwa Wanaume

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Kituo cha Bikra Maria Mama wa Tumaini kilichopo katika Kijiji cha Masanga kata ya Goronga Halmashauri ya Tarime Mkoani Mara kimeeleza kupata mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka 20 tangu kuanzishwa kwa Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) kwa kutoa bure huduma ya kitabibu kwa wanaume wanaokimbia tohara ya kimila ili kupunguza maambukizi ya VVU.

Akizungumza Jumatano Agosti 16,2023 na Waandishi wa Habari wanaofanya ziara mkoani Mara, Msimamizi wa kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT) na asasi ya ATFGM inayopinga ukatili wa kijinsia kwa watoto wa kike, Sister Jacqueline Gbanga amesema Kituo hicho kimekuwa kikitumika kama hifadhi ya wanaume waliokimbia tohara ya kimila wakiwa na uhitaji wa kufanya tohara ya kitabibu.


Amesema Kituo hicho kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma Mkoa wa Mara na kusimamiwa na Daughters of Charity of Vincent de Paul kinatumika kama hifadhi ya wanaume waliokimbia tohara ya kimila wakiwa na uhitaji wa kufanya tohara ya kitabibu kwa sababu ya usalama na kuepuka utokwaji wa damu, maambukizi yanayotokana na kifaa kimoja cha tohara, maumivu makali na wakati mwingine vifo.

Sr. Jacqueline ameeleza kuwa tangu waanzishe huduma ya tohara mwaka 2018 jumla ya vijana na wanaume 88 waliokimbia huduma za tohara ya kimila wamepata huduma ya tohara ya kitabibu bure katika kituo hicho kwa njia ya huduma mkoba ya tohara (Informed facility led outreach).
Msimamizi wa kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT), Sister Jacqueline Gbanga akisoma taarifa kuhusu Tohara Kinga ya Kitabibu kwa Wanaume

Amebainisha kuwa kwa kushirikiana na hospitali ya wilaya ya Nyamwaga inayotoa huduma endelevu za tohara, wamefanikiwa kupata watoa huduma pamoja na vifaa tiba ikiwa ni ushirikiano mkubwa unaotolewa na Shirika la Amref Health Africa Tanzania linalopata ufadhili wa PEPFAR kupitia CDC.


“Tunapoadhimisha miaka 20 toka tulipoanza kupata msaada kutoka Serikali ya Marekani kupitia Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kupambana na UKIMWI (PEPFAR) kwa ajili ya kupigana na janga la VVU/UKIMWI, tunashukru sana kwa maana bila msaada wenu tusingeweza kufanikisha Tohara kinga ya kitabibu. Tunashukuru vijana wamepata na wanaendelea kufanyiwa tohara ya kitabibu”,amesema Sr. Jacqueline.


“Mchango wa PEPFAR kupitia CDC, kwa kushirikiana na Amref pamoja na Wizara ya Afya vimeongeza tumaini kwa wananchi ambao pia ni maskini wasiokua na uwezo wa kipato kwa ajili ya gharama za matibabu lakini wanapata huduma zote bure katika kituo hiki”,ameongeza.


Katika kupinga mila kandamizi kwa watoto ikiwemo ukeketaji na tohara ya jadi ambayo haizingatii afya ya mtu, Sr. Jacqueline amesema kituo hicho kimekuwa kikihamasisha makundi mbalimbali wakiwemo wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, wazee wa mila, wachungaji, walimu, watalamu wa afya, watu maarufu katika jamii, viongozi wa vijiji na vitongoji na serikali kuendelea kuhamasisha tohara kinga ya kitabibu (VMMC) kuweza kupunguza maambukizi ya VVU.


“Mila hii ya tohara kwa Wakurya zimejenga hofu kwa watoto na vijana. Tunaendelea kupiga vita mila kandamizi kukeketa watoto wa kike na kulazimisha watoto wa kiume kutahiriwa bila ganzi na kupata maumivu makali, kuvuja damu nyingi na hata kupelekea kupoteza uhai”,ameeleza.
Mratibu Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) Tanzania, Bi. Jessica Greene akizungumza katika kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini Masanga 

Mratibu Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI - The U.S. President’s Emergency Plan for AIDS Relief (PEPFAR) Tanzania, Bi. Jessica Greene amesema tohara kinga ya kitabibu inalenga kupunguza maambukizi ya VVU.


Ameongeza kuwa Serikali ya Marekani inaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kufikia malengo ya shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Kupambana na Ukimwi Duniani (UNAIDS) 95/95/95 (95% (ya watu wanaoishi na VVU wanajua hali zao, 95% ya waliogundulika wako kwenye matibabu, 95% ya wanaopata matibabu virusi vitakuwa vimefubazwa ifikapo 2025.

Mkurugenzi Msaidizi wa CDC Tanzania Dkt. George Mgomella amesema huduma za tohara kinga ya kitabibu Mkoani Mara zimekuwa zikifanyika kwa ushirikiano wa Serikali ya Marekani na Tanzania kupitia Amref Health Africa Tanzania inayotekeleza Mradi wa Afya Kamilifu kupitia CDC kwa ufadhili lengo likiwa ni kupunguza maambukizi ya VVU.

Naye Mhamasishaji wa tohara kinga ya kitabibu kutoka Kijiji cha Masanga, Mwalimu Baraka Joseph amesema Amref Health Africa Tanzania kupitia CDC kwa ufadhili wa PEPFAR wamesaidia kwa kiasi kikubwa vijana kuondokana na hali ya ukimbizi kwenye jamii yao wakikwepa tohara ya kimila.

“Tohara ya kimila imekuwa ikiwafanya wanaume kuwa wakimbizi kwenye jamii yao, tunashukuru katika eneo hili la Masanga na kata hii ya Goronga ambayo ilikuwa na Mangariba na wazee wengi wa mila elimu ya tohara ya kitabibu inazidi kusambaa na wanaume wameendelea kujitokeza kupata huduma hii bure”,amesema Mwl Joseph.

Mratibu wa Masuala ya UKIMWI Halmashauri ya Tarime ,Dkt. Rebeca Mngumi ameeleza kuwa kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini ni kati ya vituo 6 vinavyotoa huduma ya tohara kinga ya kitabibu katika halmashauri hiyo na kimekuwa msaada mkubwa katika kuwakomboa vijana dhidi ya tohara ya kimila.

“ Masanga kuna wazee wengi wanaofanya tohara za kimila katika wilaya ya Tarime, kutokana na hali hii tumekuwa tukitoa elimu ya tohara ya kitabibu katika jamii. Kipindi cha tohara za kimila ambazo hufanyika miezi ya Oktoba hadi Februari vijana wengi wamekuwa wakikimbilia kwenye kituo hiki ili kukwepa tohara hiyo isiyo salama kutokana na vifaa vinavyotumika kufanyia tohara”,amesema Dkt. Rebeca.

Kwa upande wake, Mhudumu Ngazi ya jamii, Rose Chikaka ambaye anafanya kazi ya uhamasishaji wa tohara nyumba kwa nyumba amesema huduma ya tohara kinga bure sasa inachangamkiwa na wanaume wengi wanaotoka kwenye jamii iliyoamini tohara ya kimila ambayo ilikuwa inawapotezea gharaa na muda mwingi kujiandaa kwa ajili ya shughuli tohara,kuwa hatarini kupata maambukizi ya VVU, kutokwa damu nyingi na wakati mwingine kifo.
Mhudumu Ngazi ya jamii, Rose Chikaka.
Naye mtoa huduma za tohara katika kituo cha BMMT ,Godfrey Mago amesema vijana wengi wanakimbilia huduma ya tohara kinga ya kitabibu ili kuepuka maumivu wakati wa tohara ya kimila, kupoteza muda mwingi na gharama za tohara za kimila mfano kutozwa sh. 25,000/= ili upatiwe huduma lakini pia kupigwa faini ya hadi sh. 30,000/= endapo utalia au kupiga kelele wakati ukifanyiwa tohara ya kimila.


“Nilitoroka nyumbani nikaja BMMT kufanyiwa tohara salama tofauti na tohara ya kimila ambayo hata kidonda kinachukua muda mrefu kupona. Naishukuru sana PEPFAR kwa kuleta huduma hii bure”,ameongeza Juma Magaiwa Msenda ambaye ni mnufaika wa huduma za tohara kinga ya kitabibu.


Kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Zabron Masatu amesema kupitia PEPFAR mpaka sasa wamefanikiwa kuwafanyia tohara kinga ya kitabibu wanaume wapatao 63,000 mkoani humo ambapo hayo yote yanatokana na uhamasishaji wa tohara ya kitabibu inayotolewa bure kwa wanaume ikiwa ni juhudi za kukabiliana na maambukizi ya VVU.
Msimamizi wa kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT) na Mkurugenzi Mtendaji wa asasi ya ATFGM,  Sister Jacqueline Gbanga akisoma taarifa namna wanavyoshirikiana na PEPFAR kukabiliana na Maambukizi ya VVU kupitia Tohara Kinga ya Kitabibu kwa Wanaume. Kushoto ni Mratibu Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) Tanzania, Bi. Jessica Greene.
Msimamizi wa kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT) na Mkurugenzi Mtendaji wa asasi ya ATFGM,  Sister Jacqueline Gbanga akisoma taarifa namna wanavyoshirikiana na PEPFAR kukabiliana na Maambukizi ya VVU kupitia Tohara Kinga ya Kitabibu kwa Wanaume.
Mratibu Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) Tanzania, Bi. Jessica Greene akizungumza katika kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT). Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa CDC Tanzania Dkt. George Mgomella.
Mratibu Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) Tanzania, Bi. Jessica Greene akizungumza katika kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT).
Waandishi wa habari wakichukua matukio katika kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT).
Mkurugenzi Msaidizi wa CDC Tanzania Dkt. George Mgomella katika kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT)
Mhamasishaji wa tohara kinga ya kitabibu kutoka Kijiji cha Masanga, Mwalimu Baraka Joseph akielezea kuhusu huduma ya tohara kinga ya kitabibu kwa wanaume
Mhamasishaji wa tohara kinga ya kitabibu kutoka Kijiji cha Masanga, Mwalimu Baraka Joseph akielezea kuhusu huduma ya tohara kinga ya kitabibu kwa wanaume
Juma Magaiwa Msenda ambaye ni mnufaika wa huduma za tohara kinga ya kitabibu akielezea kuhusu huduma ya tohara kinga ya kitabibu kwa wanaume
Mratibu wa Masuala ya UKIMWI Halmashauri ya Tarime , Dkt. Rebeca Mngumi akielezea kuhusu huduma ya tohara kinga ya kitabibu kwa wanaume
Mtoa huduma za tohara katika kituo cha BMMT ,Godfrey Mago akielezea kuhusu huduma ya tohara kinga ya kitabibu kwa wanaume
Bango katika kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT)
Viongozi wakipiga picha ya kumbukumbu katika kituo cha Afya cha Bikra Maria Mama wa Tumaini (BMMT).

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

JK ATETA NA KAMATI YA SADC-TROIKA ANGOLA

 

*Na Mwandishi Wetu, Angola*


Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, (SADC Panel of Elders) akiwa pamoja na Viongozi wanaounda Kamati ya Utatu ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC- TROIKA) wakijiandaa na Mkutano wa Kamati hiyo unaofanyika leo tarehe 16 Agosti, 2023, Luanda, Angola. 


Viongozi hao ni pamoja na Mhe. Hage Geingob, Rais wa Namibia ambaye ndiye Mwenyekiti wa sasa wa SADC TROIKA, Mhe. Haikande Hichilema wa Zambia ambaye anatarajiwa kuchukua Uenyekiti wa Kamati hiyo na Mhe. Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ambaye ni Mwenyekiti anayemaliza muda wake wa Kamati hiyo ya SADC TROIKA. Pichani pia ni Mhe. Samuel Matekane, Waziri Mkuu wa Lesotho (wa pili kutoka kulia) na Katibu Mtendaji wa SADC, Mhe. Elias Magosi (wa kwanza kushoto).


Rais Mstaafu Kikwete amewasilisha katika Kamati hiyo ya SADC TROIKA Ripoti ya Kamati ya Uangalizi (Oversight Committee) anayoiongoza katika kufuatilia hatua za kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa kiasiasa ulipo katika Ufalme wa Lesotho.

Share:

DAWA ITAKAYOKUSAIDIA KUJIKINGA NA MAADUI ZAKO!

 

Kitu ambacho hatuwezi kukipinga ni kusema kwamba hakuna maadui katika maisha yetu, ukweli ni kwamba maadui wapo na wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana kuhakikisha maisha yetu wanarudi nyuma.

Maadui wamekuwa wakiumiza wasio na hati katika maisha yetu, ubaya ni kwamba ni vigumu sana kufahamu maaduni wetu, hivyo naweza kusema maadui wetu tunaishi nao katika kazi, biashara na hata mahusiano.

Jina langu ni Fadhili kutokea Nyeri, nina miaka 24, katika familia yangu tulipitia changamoto nyingi sana kiasi kwamba nilitaka hadi kukimbia nyumbani maana changamoto zilikuwa haziishi.

Kila mara utakuta wazazi wanaumwa, natumia fedha zangu zote kuwatibu hadi nakosa nauli ya kwenda kazini, hilo likiishi mara utasikia kuna changamoto nyingine kubwa ipo ambayo inahitaji fedha kuitatua.

Kila siku maisha yakawa ni kurudi nyuma badala ya kusonga mbele, hakuna jambo la kimaendeleo ambalo kama familia tuliweza kulifanya.

Hata wadogo zangu wote hawakuweza kwenda shule, wengine wa kike walipata na ujauzito wakiwa hapo hapo nyumbani bila ya kuolewa na hata wanaume waliowapa ujauzito waliwatelekeza, hivyo kazi ikawa tena kwetu kama familia kuwahudumia.

Kuna siku niliweza kusikia tangazo katika redio kuwa  African Doctors anaweza kuikinga familia na maadui, nilitegemea sikio kwa makini hadi pale Mtangazaji alipotaja namba yake ambayo ni +254 769404965. Nilinakili namba hiyo ili baadaye niweze kumpigia.

Hatimaye niliweza kuwasiliana naye na kumuelezea kuhusu shida yangu, aliniambia ningoje baada ya muda, alinipigia na kuniambia kuna jirani yetu ambaye mara nyingi huwa anakuja nyumbani kwetu ndiye ambaye anatuchezea mchezo huo.

African Doctors alinipatia dawa ya kuweza kujikinga na adui huyu na kweli nashukuru dawa yake imeweza kuzaa matunda maana tangu wakati huo huyu jirani haji tena nyumbani kwetu kwa madai ni mgonjwa lakini mimi najua langu moyoni kuwa dawa ya  African Doctors imeweza kufanya kazi yake vilivyo.

Tangu wakati huo hakuna chochote kile ambacho kimeweza kuleta shida pale nyumbani, mambo yamekuwa yakienda sawa kama ambavyo tulipanga na kutarajia.

Kumbuka African Doctors ana uwezo kumfanya mtu kuwa na bahati maishani mwake, kushinda michezo ya bahati nasibu, kukukinga na maadui zako, kukufanya ushinde migogoro kama ya ardhi, kuwa na mvuto wa kimapenzi, kuongeza mauzo katika biashara.

Pia anatibu magonjwa kama kaswende, kisonono, kifua kikuu, presha, kifafa, upungufu wa nguvu za kiume, kuvimba miguu, kaswende, vile vile anawezesha wanawake kubaba ujautizo, wanaume kutungisha mimba n.k.

Wasiliana na African Doctors kwa namba; +254 769 404965, tembelea tovuti yao; www.african-doctors.com au watumie email; africandoctorheals@gmail.com.

Mwisho.



Share:

Wednesday, 16 August 2023

AFYA CHECK , OFISI YA MBUNGE WA JIMBO LA TANGA KUZINDUA KAMBI MAALUMU YA MATIBABU BURE


MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari mapema leo
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo akizungumza wakati wa mkutano huo

Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shiloo akizungumza




TAASISI ya  Afya Check kwa kushirikiana na ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Tanga wanatarajia kuzindua kambi maalum ya kupima afya  bure kwa wananchi wa Jiji la Tanga  kwa siku tano ikiwa ni mpango wa kuihamasisha  jamii kuwa na desturi ya kupima afya zao mara kwa mara ili pale wanapogundulika kuwa na matatizo mbalimbali waweze kupata matibabu ya haraka.


Akizungumza na waandishi wa Habari leo Waziri wa Afya ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu amesema kambi hiyo itafanyika kwa muda wa siku tano kuanzia Augost 21 ambapo wananchi 5000 wanatarajiwa kufanyiwa uchunguzi katika magonjwa ya Kisukari,  shinikizo la damu, Saratani ya tezi dume,saratani ya mlango wa kizazi.

Waziri Ummy amesema magonjwa yatayopimwa ni yale yanayoambukiza na yasiyoambukizwa na endapo mtu atakutwa na ugonjwa atapatiwa tiba bure na kwa wale ambao watakuwa na magonjwa yatakayohitaji  upasuaji watapatiwa tiba watakapokuja madaktari bingwa huku akiipongeza banki ya CRDB ambao ndio wadhamini wakuu wa kambi hiyo. 

"Takwimu inaonesha wapo watu laki mbili ambao hawajajitambua afya zao katika upimaji wa vvu, tunawashauri na kuwahamasisha watu kupima na kama watu wote ambao wana maambukizi wangekuwa wanafuata masharti ya kumeza dawa tunaweza kuutokomeza kabisa" amesema.

"Niwapongeze sana sana wadau wetu wakubwa CRDB, benki yetu kwa kujitolea na kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan,  katika kufadhili huduma zinazowasaidia wananchi" amebainisha.

"Sasa, nitoe wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Tanga kujitokeza, wilaya zote kujitokeza kuja kupima katika viwanja vya shule ya sekondari ya Usagara, lengo ni watu 5000 lakini hata tukipata zaidi itakuwa vizuri" amesisitiza.

Awali akizungumza Mratibu mkuu wa Afya check Isack Maro amesema lengo la kuweka kambi mkoani hapa ni kutaka kuwajengea wananchi tabia ya kupima afya kwa hiyari mara kwa mara na hii ni mara baada ya kumaliza mkoani Dar es salaam ambapo zaidi ya wananchi 9324 walifanyiwa vipimo.

"Kitakwimu watanzania tunatumia gharama kubwa sana kujitibu na mara nyingi ni kwa sababu tumechelewa kugundua tatizo sasa kampeni hizi zilianzishwa kuhakikisha kwamba watanzania  wanajenga tabia ya kuoenda kupima afya zao mara kwa mara na hii inaonyesha kuyokana na matukio tunayoyaona  kutokana na hizi kambi ambazo tumezifanya kwa muda mrefu"

"Kwa  sasa hivi ndio tumetoka kumaliza vipimo kwa wakazi wa mkoa wa Dar es salaam na wilaya zake zote na tukafanikiwa kuwapatia huduma za afya za bure wananchi takriban 9324 walifanikiwa kupatiwa  huduma zote za kibingwa pamoja na hufuma za kawaida  bila kusahau wakapatiwa dawa na vipimo"
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger