Monday, 27 September 2021

Tanzia : NAIBU WAZIRI WILLIAM OLE NASHA AFARIKI DUNIA



Habari zilizotufikia hivi punde ni kuwa Mbunge na Ngorongoro ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, William Ole Nasha amefariki dunia leo Septemba 27, 2021 nyumbani kwake jijini Dodoma.
Share:

DAKTARI ATUPWA JELA KWA KUMDUNGA MKEWE SINDANO YA MAPEPO




DAKTARI mmoja nchini Uingereza ambaye ni raia wa Misri, Hossam Metwally amehukumiwa kwenda jela miaka 14 baada ya kukutwa na hatia ya kumdunga mke wake sumu akiwa katika harakati za ‘kumuondoa mapepo’ yaliyokuwa yakimsumbua.

Hossam mwenye umri wa miaka 34, alipewa adhabu hiyo baada ya kumdunga mke wake Wilson sindano ya sumu aina ya Nicortin kwa lazima akidai anamtoa mashetani nyumbani kwao katika eneo la Grimsby.

Kufuatia ushahidi uliotolewa katika Mahakama ya Sheffield, Metwally alidaiwa kumshutumu mke wake kuwa na ‘majini ndani ya mwili wake.

Daktari huyo alipatikana na makosa nane ikiwemo kujaribu kumuua mke wake, ulaghai na pia kutazama picha za utupu baada ya kunaswa na kamera za siri alizoziweka katika ndani ya kliniki yake ya kibinafsi.

Metwally alikamatwa baada ya Wilson kupatikana akiwa mahututi na kupoteza fahamu mnamo Julai 4, 2019 na kulazimka kulazwa.

Kufuatia uchunguzi uliofanywa na polisi, ilibainika kuwa kiwango kikubwa cha sumu za nircotics, zikiwemo zile za aina ya ketamine, propofol na fentanyl zilitumika.

Hata hivyo, jambo la kushangaza zaidi ni kwamba daktari huyo bingwa wa upasuaji, hakuonyesha kujutia kitendo hicho alipokuwa akijitetea kortini.
Share:

RAIS SAMIA AMUAPISHA MATHEW KIRAMA KUWA KATIBU WA TUME YA UTUMISHI WA UMMA NA BALOZI MHE. TOGOLANI MAVURA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mathew Modest Kilama kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 27 Septemba, 2021.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Balozi Togolani Edriss Mavura kuwa Balozi wa Tanzania nchini Korea ya Kusini katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 27 Septemba, 2021.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma Mathew Modest Kilama akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Korea ya Kusini Togolani Edriss Mavura wakila Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 27 Septemba, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na Viongozi katika picha ya pamoja baada ya kuwaapisha katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Mathew M. Kirama na Balozi Mhe. Togolani E. Mavura, leo Ikulu, Chamwino Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na Viongozi katika picha ya pamoja baada ya kuwaapisha katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Mathew M. Kirama na Balozi Mhe. Togolani E. Mavura, leo Ikulu, Chamwino Dodoma.

Share:

MBUNGE AWATAKA WANAWAKE KUKATAA MAHUSIANO YA KINGONO NA WANAUME AMBAO HAWAJAFANYIWA TOHARA


Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma, Jaqueline Msongozi amewataka wanawake nchini kutokubali kuwa na mahusiano ya kingono na wanaume ambao hawajafanyiwa tohara ili kuondoa hatari ya kupata magonjwa.

Ameyasema hayo leo Septemba 27,2021 wakati Kamati ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI, Kifua Kikuu, Dawa za Kulevya na Magonjwa yasiyoambukiza ilipotembelea na kukutana na viongozi pamoja na wadau wa mkoa huo.


Pia kamati hiyo imeupongeza mkoa huo kwa mafanikio iliyoyapata katika kupambana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI ambapo mkoa una maambukizi ya asilimia 4.4 chini ya kiwango cha kitaifa cha 4.7.

"Niwashauri wanawake wenzangu wa Rukwa na kote nchini kabla ya kuwa na mahusiano ni vizuri kujua endapo mwanaume amepata tohara au la.Ukikuta hajapata tohara basi usitoe huduma," amesema Mbunge Msongozi.

Mheshimiwa Msongozi amekuwa miongoni mwa wabunge wasiopenda kukaa na jambo moyoni, kwani hivi karibuni alipaza sauti bungeni akilalamikia kitendo cha wabunge wa viti maalumu kunyanyaswa kijinsia, kunyanyapaliwa na kufanyiwa ukatili na vitisho juu na wabunge wa majimbo wanapowajibika kuwatumikia wananchi katika maeneo yao.


Kwa mujibu wa Mganga Mkuu Mkoa wa Rukwa, Dkt. Boniface Kasululu, wanaume 34,549 kati ya lengo la watu 35,999 wamepatiwa huduma ya tohara kwenye mkoa huo ikiwa ni mkakati wa kupungunza maambuzi ya VVU/Ukimwi.
Share:

DAKTARI AWAUA WATOTO WAKE WAWILI KWA KUWACHOMA SINDANO




DAKTARI mmoja katika eneo la Nakuru nchini Kenya anadaiwa kuwaua wanawe wawili wenye umri wa miaka mitano na mitatu kwa kuwachoma sindano.

Dk. James Gakara alikutwa amelala kando ya wanawe akiwa amepoteza fahamu katika kisa ambacho anashukiwa kutekeleza mauaji na kujaribu kujiua.

Dk. Gakara ambaye alikimbizwa ili kupata matibabu katika Hospitali ya Nakuru Level Five, naye aliaga dunia Jumatano, Septemba 22, 2021.

Kulingana na ripoti ya upasuaji wa maiti, Gakara alimeza kemikali isiyojulikana ambayo huenda ilisababisha kifo chake.

Daktari aliyeendesha zoezi la upasuaji kubaini chanzo chake, Dkt. Titus Ngulungu amesema kwamba huenda marehemu alikunywa dawa.
Share:

TADB yatoa mkopo wa milioni 436 ujenzi kiwanda kusindika korosho Tanga

 Na Mwandishi Wetu, Tanga
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeidhinisha mkopo wa kiasi cha shilingi 435,500,000/- kwaajili ya uanzishwaji wa kiwanda kidogo cha kusindika korosho ili kuliongezea thamani zao sambamba na kuongeza pato la taifa pamoja na kuinua pato la mkulima..

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa mradi wa Ubunifu katika mnyororo wa thamani wa zao la Korosho chini ya Taasisi ya Care Tanzania wilayani Mkinga,Jijini Tanga, Meneja wa Kanda ya Mashariki wa TADB,Bw  Jeremiah Jeremiah Mhada alisema kuwa benki hiyo imeidhinisha mkopo  huoambapo zitatumika katika ujenzi wa kiwanda na ununuzi wa mashine na vifaa mbalimbali za kuendesha kiwanda hicho.

“Fedha hizo zitatoka kwa awamu ikiwa ni kujenga miundombinu ya kiwanda na awamu ya pili kufadhili wakulima wa korosho pembejeo zitakazowawezesha kuzalisha korosho kwa tija na kupata bei nzuri sokoni,” alisema Bw.Mhada  

Alieleza kuwa fedha ziizotolewa zitakwenda kusaidia katika kutengeneza ajira kupitia kazi ya ujenzi wa majengo ya kiwanda pia kukiwezesha kiwanda Mtaji wa kununua korosho kutoka kwa Wakulima wadogo wa  Kilimo Viwanda Sigaya Limited.

“TADB imetoa mkopo huu kwa lengo la kuongeza thamani ya zao la korosho hali itakayopelekea kuongezeka kwa mapato ya wakulima wa korosho Wilayani Mkinga, alisema Bw.Mhada na kuongezea kuwa kiwanda hicho kitaongeza thamani ya zao na kuhamasisha wakulima kufanya kilimo cha korosho kutokana na uhakika wa soko.

Bw .Mhada alisisitiza kuwa majukumu ya TADB ni kuhakikisha mageuzi yanafanyika katika sekta ya kilimo na kuwabadilisha wakulima kutoka kilimo cha mazoea na kufanya kilimo biashara na kuwafanya waweze kupita hatua kiuchumi kupitia shughuli za kilimo na kuwaunganisha na masoko kupitia chama cha msingi cha ushirika cha DUGA.

“Uchakataji wa korosho hapa nchini utasaidia kuzalisha bidhaa nyingine kama mafuta kwa asilimia 15 ambayo hutumika kama dawa na matumzi ya viwandani jambo litakalopelekea kuongeza thamani ya zao la korosho hapa nchini,” alisema

Alieleza kwa sasa mafuta ghafi ya korosho yanauzwa katika soko la Umoja wa Ulaya, Marekani, Japan, Korea ambapo wasambazaji wakuu ni India na Brazil. Hivyo tukiweza kuzalisha wenyewe mafuta haya Tanzania itakuwa miongoni mwa wasambazaji wakuu wa bidhaa hiyo Duniani.

“Kwa mujibu wa ANSAF mwaka 2016/17 Tanzania ni namba 3 kwa uzalishaji wa korosho Duniani, sasa hivi ipo namba 4 kwa Afrika ambapo zaidi ya asilimia 90 inasafirishwa kama malighafi,” alisema Bw.Mhada

“TADB tutaendelea kuhamasisha kuongeza na kukuza uzalishaji nah ii ni muendelezo wa uwekezaji wa zaidi ya bilioni 33 ambazo zimetolewa katika mnyororo wa thamani wa uzalishaji, alieleza Bw.Mhada

Mwenyekiti wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha DUGA, Bw.Said Hassan Tuwano aliishukuru benki ya TADB pamoja na Wawekezaji walioamua kuwekeza katika Wilaya yao na kusema hii imeonyesha dhamira ya dhati ya kusaidia wakulima wadogo nchini.

“Nashukuru zaidi kwa kutupa asilimia 45 ya hisa kwenye kiwanda hivyo zaidi ya wakulima 200 tutakuwa sehemu ya kiwanda na tumejipanga kuhakikisha tunaongeza idadi ya wakulima mpaka kufikia 2,500 katika Wilaya yetu ili tunufaike wote,” alisema Bw.Tuwano

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Kanali Maulid Surumbu aliwataka wadau wote kutekeleza majukumu yao kuhakikisha uzalishaji wa zao la korosho unaongezeka pia kuhakikisha kiwanda kinakamilika ili uzalishaji uanze msimu ujao wa mavuno.

“Tunachotaka kutoka kwenu ni uwazi na uwajibikaji, niwahakikishe Serikali ipo pamoja na nyinyi kutoa mchango ili kuhakikisha tija katika uzalishaji inaongezeka na kufanya korosho yetu izidi kukubalika katika soko la ndani na masoko ya kimataifa jambo litakalo ongeza kipato kwa wakulima Wilayani Mkinga,” alisema Kanali Surumbu.



Share:

Rais Samia Awaasa Viongozi ALAT kutoa elimu ya Uviko 19

 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi wa serikali za mitaa kutoa elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa chanjo ya UVIKO 19 kwa wananchi.

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi hao kutotumia mabavu katika utoaji wa chanjo bali kuwaelimisha wananchi wapate chanjo kwa hiari.

Rais ametoa kauli hiyo leo Septemba 27, 2021wakati akifungua mkutano mkuu maalum wa uchaguzi wa viongozi wa jumuiya ya serikali za mitaa- ALAT Taifa Mkoani Dodoma.

“Tulisema hili jambo ni la hiari, ukipita nyumba kwa nyumba anayetaka mchome asiyetaka usichome Lakini kubwa ninalotaka kusema mtu ana hiyari ya kukubali au kukataa na kama ana elimu ya kutosha ,hawezi kukataa”

Katika mkutano huo maalum Rais Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi hao kushirikiana na kuondoa tofauti Zao ambazo nyingi hutokana na maslahi binafsi.



Share:

Serikali Yaitaka TPA Na Mscl Kuandaa Maegesho Ya Meli Ya Mv Mwanza Hapa Kazi Tu


 Serikali imeiagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) kuandaa miundombinu ya maegesho ya meli kwa ajili ya meli mpya ya MV MWANZA “Hapa Kazi Tu” inayojengwa katika Bandari ya Mwanza.

Akikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa meli hiyo Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema kuwa kazi za ujenzi wa meli hiyo kwa sasa zimefikia asilimia 53.8 na ifikapo mwezi Aprili, 2022 meli hiyo itaingizwa majini kwa mara ya kwanza na kuendelea kumaliziwa ujenzi wake ambao unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2022 na baadae kufanyiwa majaribio na kukaguliwa na Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kabla ya kuanza kutoa huduma.

“Meli hii ni kubwa kuliko meli zote zinazofanya safari katika Ziwa Victoria kwani ina urefu wa mita 92.6, upana mita 17 na kimo mita 20, hivyo MSCL kwa kushirikiana na TPA hakikisheni miundombinu ya maegesho kwa ajili ya meli hii inaboreshwa ili meli itakapokuwa tayari iweze kuanza kazi mara moja kwani meli hii ni inatarajia kutatua changamoto za upatikanaji wa huduma za usafiri wa maji katika Ziwa Victoria” amesema Kasekenya

Ameongeza kuwa hadi kufikia sasa Serikali tayari imemlipa mkandarasi zaidi ya asilimia 70 na kuwa anamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, kwa kuwezesha upatikanaji wa fedha hizo na kwamba kwa sasa kazi ya ujenzi wa meli hiyo inaendelea vizuri.

Aidha, Mhandisi Kasekenya amesema kuwa meli hiyo itakapokamilika itafungua fursa za kiuchumi na kibiashara kati ya jiji la wa Mwanza, mikoa jirani ya Musoma, Bukoba kupitia Bandari ya Kemondo Bay pamoja na nchi jirani za Uganda na Kenya.

Kwa Upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), Bw. Philemon Bagambilana amemueleza Naibu Waziri Kasekenya kuwa ujenzi wa meli ya MV MWANZA “Hapa Kazi Tu” unagharimu dola za kimarekani milioni 39 sawa na shilingi Bilioni 89.7 na umeenda sambamba na ujenzi wa chelezo kipya kinachotumika kwenye ujenzi wa meli hiyo ambacho pia kimegharimu dola za Kimarekani milioni15.

Bw. Bagambilana ameongeza kuwa Kampuni yake imekwishakamilisha ukarabati wa meli ya “New Victoria Hapa Kazi Tu” kwa gharama ya Shilingi Bilioni 25.5 na “New Butiama Hapa Kazi Tu” kwa Shilingi Bilioni 5.7 na tayari meli hizo zinaendelea kufanya kazi katika Ziwa hilo.

Naye, Kaimu Meneja wa Bandari ya Ziwa Victoria, Bw. Vicent Steven, amemueleza Naibu Waziri Kasekenya kuwa tayari TPA imeshafanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kupanua na kuboresha miundombinu ya maegesho yote yatakayopokea meli hiyo na kwamba kwa sasa wako kwenye hatua za manunuzi yatakayo wezesha kumpata mkandarasi atakayeifanya kazi hiyo.

Meli mpya ya MV MWANZA “Hapa Kazi Tu” inajengwa na wakandarasi kutoka kampuni ya GAS Entec Company na KANGNAM Corporation za Korea Kusini na itakapokamilika inatarajiwa kuwa na madaraja sita (6) yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200, magari madogo 20, magari makubwa 3 pamoja na mizigo tani 400 na hivyo inatarajiwa kuwa meli kubwa kuliko zote katika Ziwa Victoria.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi


Share:

AOMBA APEWE DHAMANA MAHAKAMANI BAADA YA SEHEMU ZAKE ZA SIRI KUPOTEA

 

Mshtakiwa Faraji Ramadhani mwenye umri wa miaka 27 ameiomba Mahakama imruhusu ajidhamini mwenyewe kutokana na sehemu zake za siri kutoweka hivyo kupata maumivu makali anapokuwa Mahabusu.

“Hakimu nilikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Mtoto wa Shekhe, Ustadhi huyo alinionya sana kuachana na Binti yake lakini sikusikia ndio chanzo cha sehemu zangu za siri kupotea, nikiwa nyumbani natumia dawa za miti shamba kutuliza maumivu”.

Kutokana na malalamiko hayo Hakimu Manase aliamuru mtuhumiwa huyo aliyefikishwa Mahakamani hapo kwa kosa la wizi wa Kompyuta akaguliwe na baada ya askari kumkagua ilibainika anachokisema ni kweli.

Hata hivyo Hakimu Diana Manase wa Mahakama hiyo ya Mwanzo Jijini Mbeya aligoma kumruhusu kujidhamini kwa madai akitoroka hawezi kujua wapi kwa kumpata na kumtaka avumilie kwakuwa tatizo kalitafuta mwenyewe maana shekhe alimuonya aachane na Binti yake akakaidi, Kesi iliahirishwa na itasikilizwa tena leo September 27,2021.

Share:

RAIS SAMIA ATANGAZA RASMI MADIWANI KUANZA KULIPWA POSHO KILA MWEZI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa serikali imeridhia madiwani kulipwa posho ya kila mwezi ili iwasaidie kuacha kuhangaika kukusanya fedha kwenye Halmashauri.

Ameyasema hayo leo Septemba 27 , 2021 akiwa katika Mkutano Mkuu Maalum wa Uchaguzi wa Viongozi wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania-ALAT, unaofanyika kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Center, Jijini Dodoma.

“Kwenye bajeti ya mwaka huu, Serikali imeridhia madiwani kuanza kulipwa posho ya kila mwezi, na hii itasaidia madiwani kuacha kuhangaika na pesa inayokusanywa kule ili wajilipe posho, posho yenu sasa imehakikishwa ipo”,amesema Rais Samia.

“Kwa kadri uwezo wa Serikali utakavyokuwa ukiongezeka tutaangalia kuboresha maslahi ya madiwani na watendaji wengine kwenye halmashauri zetu”, ameongeza Rais Samia.
Share:

HII NDIYO FAIDA YA KU - RESTART SMART PHONE YAKO



Ni wazi kuwa Smartphone zimekuwa ni sehemu ya maisha ya watu wengi kila siku, lakini ni vizuri ukafahamu kuwa washauri wa masuala ya Teknolojia wanasema ku-restart (kuwasha tena) simu yako angalau mara moja kwa wiki kunarahisisha utendaji kazi wa kifaa hicho.

Bob Motamedi ambaye ni mshauri wa teknolojia anasema kufanya hivyo husaidia simu kudumu na chaji lakini pia kufanya kazi haraka na vizuri zaidi ukilinganisha na simu ambayo hauja-restart.
Share:

BAADA YA KUCHEKWA SANA NA MAJIRANI, SASA BIBI YANGU ANAZAA

 

Naitwa Mohamed Peter mzaliwa wa Kijitopanga kule Tanzania ambako familia yangu pia imekita mizizi. 

Nilimpata mrenbo flani ambaye tulianza maisha naye lakini kuna jambo moja lililotusumbua kwa muda mrefu. Tatizo hilo ni la kupata watoto. 

Tumetafuta mtoto tangu mwaka jana lakini hatujafanikiwa. Mimba ya kwanza ilitoka kisha ya pili pia ikatoka tukabaki kwa masononeko. 

Sijajua ni nini hasa mbaya lakini nilimpeleka bibi hospitalini ili afanyiwe uchunguzi lakini suluhu haikupatikana na ikafika wakati wa kuanza kulaumiana naye. 

Nilimuambia kila mara simtaki sababu hawezi nizalia watoto hata nikamfukuza na akaenda kwao. Bila kuficha, amekuwa kwao kwa muda wa miezi nane nilipoambiwa anahudhuria matibabu ya kienyeji kwa daktri Kiwanga.

 Hata nilipoambiwa hilo nilipuuzilia mbali lakini dadaangu akaniambia nitafute huyo bibi haraka huenda akafanikiwa kupata mtoto baada ya kupata matibabu kwa Kiwanga.

 Kwa sababu nilimuheshimu dadaangu huyo nilimtuma amuite bibi yangu arudi. Na la kushangaza aliporudi tumekuwa naye kwa muda wa mwaka mmoja na tayari tumepata mtoto.

 Kiwanga Doctors ni madaktari wa kiasili ambao wanaweza kutatuwa changamoto nyingi kama uzazi utasa na kadhalika. Tunapoongea nawe sasa hivi tunatafuta mtoto wa nne na maisha yetu ya ndoa inanawiri bila mvutano.

 Kiwanga nimewaaamini. Kama unajuwa una matatizo na mapenzi, ndoa, kazi, cheo na magonjwa kwa nyumba yako mbona usitafute matibabu ya Kiwanga? Kiwanga Doctors ni shujaa wa mambo yote. Tuvuti au Website yao ni: www.kiwangadoctors.com; Simu: +254 769404965 au wasiliana kwa barua pepe yaani Email kwa: kiwangadoctors@gmail.com

Sio lazima usafiri hadi ofisi zao. Ongea nao kwa njia ya simu na utasaidika kwa haraka kama vile watu wengine wanavyopata usaidizi.  

Share:

Sales Specialist (SA) at Alistair Group

Sales Specialist (SA)     Are you someone with a “hunger for growth”, a “whatever it takes mentality” and understand the advantages of a team environment and what it takes to thrive in one? Are you someone who “Questions things” and “looks for improvements”? Do you have experience in taking a fast growing business to a […]

This post Sales Specialist (SA) at Alistair Group has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Social Performance Manager at Dangote

Description   Develop, implement and maintain a consistent strategy on stakeholder’s engagement establishing cordial relationship with host communities and other relevant stakeholders. Key Duties and Responsibilities   Manage, direct and inspire a team of independent professionals in order to achieve Departmental goals Manage identification, mapping and proactive engagements with stakeholders Negotiate and manage Community Development […]

This post Social Performance Manager at Dangote has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

MAZISHI YA ASKARI POLISI ALIYEFARIKI AKISHANGILIA MECHI YA SIMBA NA YANGA KUFANYIKE KESHO



ASKARI wa Jeshi la Polisi, Kituo cha Polisi Mpwapwa mkoani Dodoma, Afande Rashid Mohamed Juma ambaye ni shabiki wa Timu ya Yanga amefariki dunia juzi Jumamosi, Septemba 25, 2021 wakati akitazama mchezo wa Simba na Yanga kwenye runinga.
Shuhuda aliyekuwa akitazama mpira na Rashid aitwaye Joseph Ndani Mutalima, Mkazi wa Mpwapwa amesema alifika pale dakika ya pili ya mchezo na hakuchukua zaidi ya dakika tano alianza kuishiwa nguvu.
“Alianza kuguna akiwa amesimama na nikamdaka baada ya kumlaza chini ndio akaendelea kuguna kama ng’ombe na kurusha mikono baadaye akaguna mara ya mwisho na kunyoosha miguu na mikono.
“Dakika chache baadaye walikuja Askari kumchukua, baadaye wakasema ameshafariki, sio kwamba amefariki baada ya goli hapana, wakati anaendelea kurusha mikono goli ndio lilikuwa linaingia,” amesema Joseph.
Mwili wa Rashid umeagwa jana Mpwapwa na kusafirishwa jana Jumapili kwenda nyumbani kwao wilayani Nkasi mkoani Rukwa kwa ajili ya mazishi. Marehemu ameacha mjane na watoto wawili na mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho Jumanne.
Mechi ya Simba na Yanga iliisha kwa Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0, bao la Yanga likifungwa na Fiston Mayele dakika ya 11 tu ya mchezo huo.
Kwa matokeo hayo Yanga walifanikiwa kutwaa taji la Ngao ya Jamii mbele ya wapinzani wao hao wa jadi katika Dimba la Mkapa jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma.
Share:

Media and Communications Coordinator at Children in Crossfire

NOW RECRUITING TO DELIVER AN EXCITING EARLY CHILDHOOD DEVELOPMENT (ECD) NATIONAL PROGRAM! Children in Crossfire is a registered charity in Ireland that facilitates International Development and Development Education/Public Engagement activities. Our vision is a compassionate world where every child can reach his or her potential. We work in partnership with local organisations in Tanzania and […]

This post Media and Communications Coordinator at Children in Crossfire has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Senior Specialist Monitoring, Evaluation And Learning (MEL) at Children in Crossfire

NOW RECRUITING TO DELIVER AN EXCITING EARLY CHILDHOOD DEVELOPMENT (ECD) NATIONAL PROGRAM!   Children in Crossfire is a registered charity in Ireland that facilitates International Development and Development Education/Public Engagement activities. Our vision is a compassionate world where every child can reach his or her potential. We work in partnership with local organisations in Tanzania […]

This post Senior Specialist Monitoring, Evaluation And Learning (MEL) at Children in Crossfire has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger