Sunday, 25 April 2021

WAZIRI UMMY AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI WA TEMEKE LUSUBILO MWAKABIBI..DED SUMBAWANGA



Share:

TIC : UWEKEZAJI WA BILIONI 624 ULIOFANYWA NA GRUMET RESERVE (T) LTD UNA TIJA

Share:

TSC QUEENS BINGWA BONANZA LA MEI MOSI


Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Pete kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC Queens) wakiwa katika pozi la ushindi baada ya kuichakaza Timu kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa mabao 25 kwa 01, katika fainali za Bonanza la Michezo ya Mei Mosi lililoshirikisha Taasisi mbalimbali za Serikali, Mkoa wa Dodoma, Aprili 24, 2021.
Dafroza Luhwoga ambaye ni mchezaji wa Timu ya Mpira wa Pete kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC Queens), akifunga goli wakati wa mchezo wa fainali baina ya timu hiyo na wapinzani wao kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa. TSC Queens ilishinda kwa mabao 25 kwa 01. Mashindano hayo yalifanyika Aprili 24 wakati wa Bonanza la Michezo lililoshirikisha Taasisi mbalimbali za Serikali Mkoa wa Dodoma.
Kikosi cha Mpira wa Miguu kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC Sports Club), kikiwa uwanjani muda mfupi kabla ya kuchuana na Timu kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa katika Bonanza la Michezo ya Mei Mosi lililoshirikisha Taasisi mbalimbali za Serikali Mkoa wa Dodoma, Aprili 24, 2021.
Wafanyakazi kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) wakishangilia baada ya Timu yake ya Mpira wa Miguu (TSC Sports Club) kuichakaza timu kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa mikwaju 5 ya penati dhidi ya 2 katika Bonanza la Michezo ya Mei Mosi lililoshirikisha Taasisi mbalimbali za Serikali Mkoa wa Dodoma, Aprili 24, 2021.
Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Pete kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC Queens) wakiwa na nyuso za furaha baada ya kuichakaza Timu kutoka Wizara ya Fedha kwa mabao 29 kwa 05, katika Bonanza la Michezo ya Mei Mosi lililoshirikisha Taasisi mbalimbali za Serikali, Mkoa wa Dodoma, Aprili 24, 2021.
Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Miguu kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC Sports Club), wakimsikiliza Kapteni wao Bitwalihat Magota (kushoto) akiwapatia maelekezo kabla ya kuchuana na Timu kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa katika Bonanza la Michezo ya Mei Mosi lililoshirikisha Taasisi mbalimbali za Serikali, Mkoa wa Dodoma, Aprili 24, 2021.

******************

Na Veronica Simba - TSC

Timu ya Mpira wa Pete kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC Queens), imetwaa ushindi wa kwanza katika bonanza maalum la michezo kwa Taasisi za Serikali, lililofanyika Aprili 24 mwaka huu, jijini Dodoma.

TSC Queens ilitwaa ushindi huo baada ya kuwabwaga washindani wao kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa waliochuana nao vikali katika ngazi ya fainali kwa magoli 25 kwa moja.

Awali, Timu hiyo machachari ilipambana na Timu kutoka Wizara ya Fedha na kufanikiwa kuwachakaza mabao 29 kwa 05, hatua iliyowawezesha kufuzu kuingia ngazi ya fainali.

Akizungumzia siri ya ushindi huo wa kishindo, Mlezi wa TSC Queens ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimaliwatu, Shani Kamala alisema ni kutokana na kujituma katika kufanya mazoezi ya mara kwa mara.

“TSC tunathamini michezo kwani tunaamini ina mchango mkubwa katika kujenga afya za watumishi wetu. Ndiyo maana sisi kama viongozi tumeweka mikakati ya kuhakikisha watumishi wanafanya mazoezi mara kwa mara na kushiriki katika michezo mbalimbali,” alifafanua.

Wakati huohuo, Timu ya Mpira wa Miguu kutoka TSC (TSC Sports Club) waliibuka washindi wa tatu baada ya kuwachabanga mikwaju 5 ya Penalti wapinzani wao ngazi ya nusu fainali, Timu kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa ambao waliambulia mikwaju 2 tu.

Kwa upande wake, Kapteni wa TSC Sports Club, Bitwalihat Magota amesema kikosi chake Kiko vizuri isipokuwa wanahitaji kuongeza zaidi mazoezi na mbinu za kimchezo.

Bonanza hilo liliandaliwa na Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE), Mkoa wa Dodoma ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani maarufu kama Mei Mosi, ambayo huadhimishwa tarehe moja ya kila mwezi Mei.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRILI 25,2021







Share:

Saturday, 24 April 2021

SIMBA SC YAPAA KILELENI LIGI KUU TANZANIA BARA...YAITWANGA GWAMBINA FC 1-0 MISUNGWI


MABINGWA watetezi, Simba SC wamepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Gwambina FC Uwanja wa Gwambina wilayani Misungwi mkoani Mwanza.

Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, beki wa kushoto na Nahodha Msaidizi, Mohammed Hussein 'Tshabalala' aliyefunga dakika ya 29 kwa shuti la umbali wa mita 35 baada ya pasi ya kiungo Muzamil Yassin.

Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 58 baada ya kucheza mechi 24, ikiwazidi pointi moja vigogo, Yanga SC ambao pia wamecheza mechi mbili zaidi.

Tshabalala anafunga bao hilo siku mbili tu baada ya kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumia klabu hiyo hadi mwaka 2024.

CHANZO- BINZUBEIRY BLOG
Share:

MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED WAANDAMANA


Baadhi ya mashabiki wa Manchester United walioandamana jioni ya leo wakiwa na bango lenye ujumbe wa kuwataka wamiliki wake waachie ngazi.
**
Licha ya wamiliki wa klabu ya Manchester United kuomba radhi siku chache zilizopita baada ya kukubali kushiriki kwenye michuano mipya ya European Super Ligi , lakini mamia ya mashabiki wa klabu hiyo wameandama jioni ya leo Aprili 24, 2021 kuutaka uongozi huo uachie ngazi.

Mashabiki hao wameandamana wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe ulioandikwa kwa lugha ya kiingereza unaosomeka “Glazers Out. Edwoord ward Out” ukiwa na tafsiri ya kutaka wamiliki wao waachie ngazi pamoja na makamu mwenyekiti mtendaji Edwoord ward ajiengue.

Mgomo huo umekuja siku tatu baada ya klabu hiyo kutangaza kujitoa kwenye michuano hiyo mpya na wamiliki hao kuomba radhi kwa mashabiki kupitia vyanzo mbalimbali vya habari lakini mashabiki hao hawaoonekani kuridhishwa na namna klabu hiyo inavyoendeshwa.

Ikumbukwe kuwa, Jumapili ya Aprili 18, 2021 waandaaji wa michuano hiyo mipya kwa kushirikiana na benki ya Street Bank JP Morgan, waliorodhesha vilabu 12 vilivyothibtisha kushiriki mihchuano hiyo na klabu ya Manchester United ikiwemo.

Mashabiki hao mbali na kuwapinga wamiliki wa klabu hiyo, lakini wanapinga klabu yao kushiriki kwenye michuano hiyo kwasababu itaondoa msisimko na kuondoa mahusiano ya mashabiki na klabu yao hiyo.
Share:

MCHEZAJI WA SOKA SOSPETER MAIGA AFARIKI DUNIA AKIFANYA MAZOEZI MUSOMA MJINI


Mchezaji wa zamani wa klabu ya Biashara United Mara, Sospeter Maiga Mandala amefariki dunia asubuhi ya leo wakati akifanya mazoezi katika uwanja wa Posta mjini Musoma.

Kwa mujibu wa wachezaji waliokuwa mazoezini na mchezaji huyo, Mandala alifika mazoezini kama kawaida akiendesha baiskeli yake na kufanya mazoezi vizuri bila kuonyesha dalali zozote lakini ghafla aliinama na kushika kifua.

"Tumeanza mazoezi vizuri asubuhi na leo alikuwa anakimbia sana na kutoa pasi, lakini ghafla aliinama na kushika kifua, tulipokimbia kumuona akaonekana amepoteza fahamu, lakini tulipomfikisha hospitali ikaonekana amefariki dunia," alisema mchezaji huyo.

"Hata hivyo, hadi. sasa bado hatujapata taarifa za daktari aliyempokea ili kubaini nini kimesababisha kifo chake,".

Mchezaji huyo inaelezwa hii ilikuwa Mara ya tatu kuanguka lakini wakati wote hakuwa wazi ili kupata matibabu ya tatizo la moyo linalosemekana lilikuwa linamsumbua, “ alisema mmoja wa wachezaji aliokuwa nao mazoezini kabla ya kifo chake.

Mbali na Biashara, marehemu Mandala pia amewahi kuchezea timu za Nyakato FC, Kigera FC, JK FC, Pamba FC za Mwanza, Geita FC ya Geita, Stand United ya Shinyanga na Njombe Mji FC ya Njombe.

Share:

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA ASHIRIKI MKUTANO WA 37 WA DHARURA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI KWA MTANDAO.

 

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (katikati), Naibu Waziri wa Madini Mhe. Prof Shukran Manya (kulia) na Mkurugenzi Mkurugenzi Idara ya Mtangamano wa Biashara ya wizara Bw. Ali Gugu (kushoto) wakishiriki Mkutano wa 37 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri kwa Sekta za Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulifanyika kwa njia ya mtandao 23/04/2021, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mtumba, Dodoma.

Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa 37 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri kwa Sekta za Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulifanyika kwa njia ya mtandao 23/04/2021, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mtumba, Dodoma

Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo (kulia) akisikiliza kwa makini mjadala wakati wa Mkutano wa 37 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri kwa Sekta za Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulifanyika kwa njia ya mtandao 23/04/2021, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mtumba, Dodoma.


Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo na Naibu Waziri wa Madini Mhe. Prof Shukran Manya ameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki Mkutano wa 37 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri kwa Sekta za Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 23 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma.

Mkutano huo wa 37 ulilenga kujadili uendelezaji wa Sekta ya Viwanda katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuzingatia maelekezo yaliyopita ya Wakuu wa Nchi na Baraza la Mawaziri la Jumuiya kupitia mikutano mbalimbali iliyopita na kwa kuzingatia utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Aidha, Mkutano huo ulihudhuriwa na nchi zote sita (6) Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, na Sudani Kusini ulikuwa chini ya uenyekiti wa Jamhuri ya Kenya na Katibu wa Mkutano huo alitoka nchi ya Burundi.

Ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (Mb.), aliyeambatana na Naibu Waziri wa Madini Mhe. Prof. Shukurani Manya (Mb.) ulijumuisha Maafisa Waandamizi kutoka Wizara za Viwanda na Biashara; Wizara ya Fedha na Mipango; Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki; Wizara ya Kilimo; Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) na Wizara Madini.

Pia, Mkutano huo wa 37 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji ulitanguliwa na mkutano ngazi ya Watendaji Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika sekta hizo uliofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 22 Aprili, 2021 na ngazi ya Wataalam wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Mahsusi katika eneo la Viwanda uliofanyika kwa njia ya mtandao kuanzia tarehe 20 hadi 21 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, uliopo katika Mji wa Magufuli Mtumba, Jijini Dodoma.

Ujumbe wa Tanzania katika ngazi ya wataalamu katika mkutano huo uliongozwa na Wizara ya Viwanda na Biashara na ulihudhuriwa na Wataalam kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Madini, Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO), Chama cha wazalishaji nguo na bidhaa za nguo Tanzania (TEGAMAT) na Mfamasia Mkuu wa Serikali.

Share:

SITAKI WALA SITAMANI KUITWA MWANAUME MASURUALI TENA MWAKA HUU

 

Baada ya kuhitimu masomo yangu ya Chuo Kikuu (UDOM) niliingia mtaani na kuanza kutafuta ajira ili niweze kuendesha maisha yangu bila kuomba au kutegemea wazazi wangu tena.

Niliweza kupata GPA ya 3.5 kutoka chuoni kwangu.Nilitafuta kazi kwa mwaka mmoja bila mafanikio ila sikuweza kukata tamaa kwa sababu nilikuwa na vigezo vya kutosha kupata kazi nzuri.

 Kulingana siku zinasonga mbele ilinibidi nipate mwenza wangu wa kuishi nae na family yangu ilisimamia Harusi yangu mwanzo hadi mwisho.Tuliishi na amani na upendo na mke wangu nikiwa bado nazidi kutafuta ajira.

Mungu si Athumani niliweza ajiriwa kwa department ya IT (Information Technology) katika kampuni flani hapa Jijini. Nilichapa kazi kwa bidii kubwa sana ili niweze kupata hata cheo kwa sababu mshahara wangu ulikuwa hautoshi kabisa kulingana na mahitaji yangu.

Hali yangu ilikuwa ngumu sana kimaisha na mke wangu kabadilika ,amani na upendo ukakosekana kwa nyumba kisa sina pesa ya kuacha hata nyumbani kwa ajili ya kupata chakula.

Mke wangu alikuwa akaniomba pesa ya Saloon ili apendeze sina kila kukicha maisha yangu baada ya kusonga mbele kimaendeleo yalikuwa yanarudi nyuma.Niliweza kubana pesa yangu na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ila pesa bado haionekani,sababu kubwa zaidi nilikuwa nafanya kazi mbali sana na ninapoishi ,nilikuwa napanda gari 2 tofauti kufika kazini na 2 tofauti kurudi nyumbani.

 Nusu ya mshahara wangu ulikuwa unaishia katika usafiri.Mwisho wa mwezi nikipokea mshahara wangu najikuta nina madeni katika maduka mbalimbali hapa mtaani kwangu.Nilikuwa najitahidi kulipa hivyo kabla ya kufika katikati ya mwezi mimi pesa sina tena.

Mke wangu aliweza kunivumilia kwa kila namna ila ilifika hatua ndiyo akasema, Sitaki wala sitamani kuishi na mwanaume masuruali mwaka huu.

 Ni baada ya kutoka kazini ndipo aliniambia kuwa mtoto wetu anaumwa hivyo inahitajika kuchukuliwa Hospitali ndiyo nikasema sina pesa,iliniuma sana lakini sikuwa na namna lazima nimwambie ukweli kuwa mfukoni sina chochote.

Ndipo nikampiga rafiki yangu Datius ili anikope Tshs 100,000 Datius arinitumia TShs 200,000 wakati niliomba Tshs 100,000 Nilikutana na Datius University na baada ya masomo alifanikiwa kufanya kazi katika kampuni ya Vodacom mkoa wa Tanga kama meneja.

 Kesho yake niliamua kufungua moyo wangu na kumwambia rafiki yangu kuwa nimefanya kazi kwa miaka 3 sasa ila sipanishwi cheo kazini kwangu. Mshahara wangu mdogo na mambo mengine.

 Rafiki yangu alinieleza mtu ambaye alimsaidia kupata nafasi ya kuwa Meneja wa mkoa wa Tanga akiwa bado kijana mdogo hata bila kufanya kazi kwa kampuni hiyo kwa muda mrefu. Alinipatia namba hii +254 769404965 ya Dr. Kiwanga nikajieleza kadiri nilivyoweza,pia Dr. Kiwanga akaniuliza maswali kidogo kuhusu kazini kwangu nikamjibu pia.

Hapo Dr. Kiwanga ndiyo alisema kuwa atanisaidia na Promotion spell na kuniambia ndani ya masaa 24 nitakuwa nimepata majibu sahihi. Baada ya chakula cha mchana Boss alikuja kwa Department yetu na kutupa taarifa kuwa tuna kikao saa 4:30 za jioni.

Muda ulipotimia wote na department mbalimbali tulijumuika na kusubiri kipi Boss anataka kusema. Ndipo alipoanza kutuambia kuwa Meneja wa kampuni amehamishiwa mkoa wa Pwani kulingana na mambo ya family na atakaye chukua nafasi yake ni Dickson Kato ambaye ni mimi.

Nilishtuka na kufurahi sana,nikasimamishwa ili niweze kutoa neno nikatoa na kutoa ahadi mbalimbali kwa kampuni. Baada ya wiki 2 nikapewa nyumba pamoja na gari. Maisha yangu kwa sasa yamejaa furaha na upendo.

Natoa shukrani zangu za dhati kwa kiwangadoctors bila kusahau rafiki yangu Datius. Dr. Kiwanga aliniambia anaweza kusaidia mtu akiwa mbali bila kufika ofisini kwake Kenya-Nakuru. Pia alisema kuwa anatatua shida mbalimbali kama Kurudisha mpenzi,kuwa na mvuto kwa mwanaume,kuinua biashara yako,nguvu za kiume,kupata mimba kwa waliokosa,kunasa mwizi na Kusafisha Nyota.

 Unaweza kumpata Dr. Kiwanga kwa kumpigia/WhatsApp +254 769404965 au tembelea website yao www.kiwangadoctors.com



Share:

JITIBU TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER.. UUME MDOGO ZAT 50 NDIYO SULUHISHO



Zati 50


Full Power



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:

⇒Ngiri,


⇒Henia


⇒Kisukari


⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri


⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu


⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi


⇒Msongo wa mawazo 

⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

ZAT 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

Zanzibar yasitisha safari za baharini


Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesitisha usafiri wa baharini na shughuli nyinginezo za baharini kuanzia leo Jumamosi, saa tatu asubuhi hadi pale taarifa nyingine zitakapotolewa na mamlaka husika.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Dkt. Khalid Salum Mohamed amesema serikali imefikia uamuzi huo ili kuchukua tahadhari ya dhidi ya Kimbunga Jobo.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kimbunga hicho kipo umbali wa kilomita 200 kutoka Kisiwa cha Mafia kikisafiri kwa kasi ya kilomita 18 kwa saa.

TMA imeeleza kuwa kasi hiyo imepungua kutoka ile iliyokuwa ikitarajiwa kutokana na kimbunga hicho kuingia katika mazingira yenye upepo kinzani.


Share:

Waziri Biteko Atoa Wito Mabenki Ya Ndani Kuungana Kukopesha Wawekezaji


Nuru Mwasampeta na Steven Nyamiti – Dodoma
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampuni kubwa na ndogo zinazowekeza kwenye sekta ya madini.

Waziri Biteko ametoa wito huo  tarehe 23 Aprili, 2021 alipokutana na uongozi wa juu wa Benki ya NMB uliofika kwa nia ya kutaka kujua maeneo ya ushirikiano baina ya wizara na benki hiyo ili waweze kushiriki katika kuinua uchumi wa nchi kupitia sekta ya madini kwa kutoa mikopo kwa wawekezaji hao.

“Niwasihi sana ndugu zangu, unganeni mfanye kazi kwa pamoja Benki hii itatoa asilimia 20 nyingine 30, 40, 10   kwa mwekezaji na hivyo manufaa ya uwekezaji kupitia sekta ya madini yataonekana zikikopwa nje ya nchi manufaa wanapata mataifa mengine” alisisitiza.  

Amesema wizara imekuwa ikipokea wawekezaji wengi wenye changamoto za mitaji na wakielekezwa kukopa kwenye benki za ndani kutokana na sera yetu ya local content wanakiri benki za ndani hazina uwezo wa kukopesha kiasi cha pesa wanachokihitaji.

Akizungumza katika kikao hicho Waziri Biteko ameweka wazi kuwa biashara ya uchimbaji wa madini inahitaji mtaji mkubwa na kubainisha sifa kuu tatu za biashara hiyo kuwa ni biashara inayohitaji mtaji mkubwa (capital intensive), muda wa kutosha mpaka kuona matokeo pamoja na uwepo wa rasilimali watu ya kutosha.

Biteko ameushukuru uongozi wa Benki ya NMB kwa kuona umuhimu wa kufika na kuzungumzia masuala ya muhimu kama ya mitaji  na kuona kuwa Sekta ya Madini ni mahala wanapoweza kuwekeza fedha zao.

Aidha, amesema Wizara pamoja na taasisi zake wako tayari kufanya kazi bega kwa bega na benki za ndani na kuwaongoza mahala penye viashiria vizuri ili waweze kuwekeza pesa zao na kukiri kuwa wizara yake haitakuwa tayari kuziingiza benki katika kutoa mikopo mahala ambapo kuna viashiria hatarishi vya hali ya juu maana haipendi benki hizo kupata hasara. “Kazi ya wizara ni kuzishauri benki nasisi tutafanya hivyo” alisisitiza.

Akibainisha maeneo ambayo yana viashiria vizuri katika biashara ya madini Biteko amesema ni pamoja na eneo la uchakataji wa madini, uongezaji thamani wa madini biashara ya madini na kubainisha kuwa katika hatua hizo tayari mwekezaji anakuwa na uhakika wa kile anachokifanya hivyo ni rahisi kuuza madini aliyonayo na kupata pesa ya kulipia deni la mkopo aliouchukua.

Ameitaka Sekta ya Benki kushirikiana na wizara katika kusukuma gurudumu la maendeleo na kusema kazi haiwezi kwenda mbele wala kujulikana kusipokuwa na ushirikiano baina ya sekta hizo mbili. Tushirikiane kwa pamoja, tusukume gurudumu, sekta iende mbele ili sote tuone manufaa, alisema.

Akibainisha vipaumbele vya wizara, Biteko amesema kuwa kwanza ni kutengeneza ajira kwa watanzania. Amebainisha kuwa endapo kuna leseni imetolewa kwa mwekezaji na haifanyiwi kazi leseni hiyo inanyang’anywa na kupewa wachimbaji wadogo walio tayari kufanya kazi.

Pili amesema kipaumbele kingine ni kubadilisha mtazamo wa wachimbaji wadogo katika suala zima la nidhamu ya pesa. Katika hilo ameitaka benki hiyo kuendesha mafunzo mbalimbali kwa wachimbaji wadogo katika eneo hilo ili kuwawezesha na kuwasaidia kuweza kufanya kazi kwa weledi na baadaye walipe kodi zitakazochangia katika maendeleo ya nchi.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila ameutaka uongozi wa benki hiyo kuwasilisha chati inayoonesha viwango vya chini na vya juu vya mikopo inayoweza kutolewa na benki hiyo kwa wawekezaji ili pindi wawekezaji wenye nia ya kukopa wanapotembelea ofisi yake wanakuta taarifa hizo muhimu na kufanya mawasiliano.

Aidha, ameishauri benki ya NMB kujihusisha na biashara ya bima na kukiri kwamba biashara hiyo ni fursa ya wazi na itawawezesha kutengeneza pesa na kuendeleza benki yao kiurahisi.

Akiwasilisha hoja zake kwa uongozi wa wizara, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna ameanza kwa kutoa pongezi kwa Sekta ya Madini na kusema kwamba sekta ya madini imeibeba nchi hususani katika kipindi cha janga la corona katika suala zima la kuiingizia nchi pesa za kigeni. Amesema sekta hii imekuwa ni tegemeo sana katika suala zima la pesa za kigeni. “Sisi tupo kwenye sekta ya fedha hivyo tunaona namna sekta hii ilivyokuwa mkombozi” amesisitiza.

Amesema awali benki ya NMB ilikuwa ikisita kuingiza mkono wake kwenye sekta ya madini lakini kutokana na namna bora zilivyowekwa katika suala zima la mnyororo wa biashara ya madini benki hiyo imeamua kuingia na kutoa mikopo ili kuwawezesha wafanyabiashara na wachimbaji wa madini kufanya biashara kwa ufanisi ambapo mpaka sasa tayari benki hiyo imetoa mikopo ya shilingi bilioni 10 kwa wachimbaji wadogo.

Aidha, amesema benki hiyo ikishirikiana na benki kutoka Afrika ya Kusini wametoa mkopo wa dola za kimarekani milioni 22 kwa mgodi wa Uchimbaji Mkubwa wa madini wa Geita (GGM).

Zaipuna amebainisha kuwa, kwa sasa benki yao ina mtaji wa shilingi trilioni 1.1 ambapo ameonesha imani yake ya kuchangia katika miradi mikubwa ya uchimbaji na kuboresha maisha ya watanzania.

Amesema benki yake inaweza kutoa mkopo wa kiasi cha shilingi bilioni 240 bila shida yoyote.

Amekiri kuwa biashara ya madini ina changamoto kubwa katika kuielewa, kutokana na changamoto hiyo benki hiyo imefanya jitihada ya kuwasaidia watumishi wake kuielewa biashara ya madini kwa kuandaa mafunzo kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali ikiwepo wizara na taasisi zake ili kuwajengea uwezo na uelewa wa namna biashara ya madini inavyofanyika.

Akihitimisha mazungumzo yake Ruth Zaipuna amesema ofisi yake ipo tayari kuisikiliza wizara kadri itakavyoona inafaa kuona ni maeneo yapi yapewe kipaumbele ili waweze kushirki katika kulisukuma gurudumu la maendeleo kupitia benki anayoisimamia.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Yahya Samamba amekiri kufanya mafunzo kwa wataalamu wa benki hiyo na kuwaelimisha juu ya mnyororo mzima wa biashara ya madini unavyofanyika.


Share:

TMA yasema kimbunga Jobo kimekuwa hafifu


Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema kimbunga Jobo kimepungua nguvu kwa haraka baada ya kuingia katika mazingira yenye mzunguko wa upepo kinzani.

Taarifa iliyotolewa na TMA leo Jumamosi Aprili 24, 2021  imeeleza kuwa kimbunga hicho kimekuwa hafifu na kinasafiri kwa kasi ya kilometa 18 kwa saa baharini tofauti na spidi ya kilometa 60 kwa saa iliyokuwa imetabiriwa awali.

TMA imesema kimbunga hicho kilichopo Bahari ya Hindi kwa sasa kipo umbali wa kilomita 200 mashariki mwa kisiwa cha Mafia.

“Kimbunga hafifu cha Jobo kinatarajiwa kusababisha vipindi vya mvua kubwa katika maeneo machache hususan ya ukanda wa Pwani kadri kinavyosogea nchi kavu kwa siku ya leo Aprili 24 na kesho Aprili 25, 2021,” inaeleza taarifa hiyo.

Maeneo yanayotarajiwa kupata athari za moja kwa moja ni pamoja na mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani ikiwemo kisiwa cha Mafia, Dar es Salaam pamoja na kisiwa cha Unguja.

Aidha TMA imetahadhalisha kuwa uwepo wa kimbunga hafifu baharini, unatarajiwa kusababisha mawimbi makubwa.


Share:

ASKOFU AKIRI HADHARANI KUCHOVYA ASALI YA MKE WA ASKOFU MWENZAKE



Ntagali alisimamishwa kazi ya kuhudumu kama askofu mwezi Januari mwaka huu baada ya kubainika kwamba alikuwa na uhusiano Judith Tukamuhabwa. Picha: The Observer
***
Askofu Mkuu mstaafu wa kanisa la Kiangilikana nchini Uganda, Stanley Ntagali ameomba msamaha hadharani baada ya kukiri kwamba alichovya asali (alishiriki ngono) na mke wa Askofu mwezake.

Ntagali alisimamishwa kazi ya kuhudumu kama askofu mwezi Januari mwaka huu baada ya kubainika kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke wa mwenyewe aliyetambulika kwa majina kama Judith Tukamuhabwa.

Ntagali ambaye alitangaza kwamba aliokoka mwaka wa 1974, alikiri kwamba alipotoshwa na shetani kutekeleza kitendo hicho na anaamini Mungu na waumini watamsamehea.

 "Mimi nilimkubali Mungu mwaka wa 1974 siku ya Krismasi, nampenda Mungu na nitazidi kumtumikia, najua Mungu pia ananipenda, Najutia kujiingiza katika uzinzi na kwa sasa naomba msamaha mbele ya Mungu na pia ningependa kanisa linisamehe," Askofu huyo alisema.

 " Askofu wenzangu, kaka, dada zangu katika kristu, naomba mnisamehe, maaskofu wote dunia naomba msamaha na ningependa kuendelea kumtumikia Yesu," Aliongezea Ntagali. 

Kwenye habari zingine, Judith alikuwa amedai kwamba kabla ya kuwa mpenzi wa askofu Ntagali, alikuwa amewasilisha kortini ombi la kutaka kumpa mumewe talaka mwezi Disemba 2020.

 Judith alidai kwamba mumewe alikuwa mkatili, hakuwa anamheshimu na hangestahimili maisha waliokuwa wakiishi.

 Mwanamke huyo na mumewe walioana kwenye harusi ya kifahari katika kanisa la Rugarama Cathedral mjini Kabale Disemba 15, 2018 siku chache baada ya askofu mumewe kufiwa na mkewe.

 CHANZO - TUKO NEWS
Share:

PADRE LIVINUS AFARIKI DUNIA



Na r. Angela Rwezaula – Vatican.

Mtawa wa Nigeria wa Shirika la "Mater Dei" aliyekuwa amepewa wakfu wa kikuhani na Askofu Libanori kwa utashi wa Papa Francisko,mara baada ya kuomba ruhusa ya kupewa daraja la ukuhani kabla ya muda wake,kutokana na afya yake kuwa mbaya,ameaga dunia siku ya Ijumaa 23 Aprili 2021.

Amekuwa Kuhani kwa siku 23 tu tangu Alhamisi Kuu, lakini atakuwa kuhani hata milele kwa sababu ndivyo ilivyo Sakramenti ya daraja ambalo linamfananisha na Kristo kuhani ambaye anajitoa mwenyewe kama sadaka. Kwa utulivu akiwa anasindikizwa na jumuiya yake, amezima kama mshumaa Padre Livinus Esomchi Nnamani, mwenye umri wa miaka 31.

 Miaka kumi iliyopita alikuwa amejiunga na Jumuiya ya Shirika la “Mater Dei” yaani “Mama wa Mungu”, katika jiji la wa Owerri, nchini Nigeria, kwa malezi ya kidini. Mara baada ya nadhiri za kwanza, aligunduliwa kuwa na tatizo la saratani ya damu, lakini haikumfanya kutoendelea na mchakato wake wa mafunzo na maandalizi ya ukuhani ambayo mnamo 2019, yalimfikisha jijini Roma. Aliendelea na mapambano makubwa dhidi ya gonjwa hili, lakini ambayo miezi kadhaa, ugonjwa huo ulilazimisha kijana huyu kulazwa katika Kituo cha kiafya cha Group Casilino.

Akiwa hapo katika kituo cha kiafya, binafsi kwa hamu yake ya kuwa kuhani alimwandikia Papa Francisko mnamo tarehe 31 Machi, Jumatano Kuu. Alifanya hivyo alipoona kwamba nguvu zake zinaanza kudhoofika na akaomba aweze kupewa daraja la ukuhani mapema. Jibu la Baba Mtakatifu lilikuwa karibu mara moja, kwa maana lilikuja masaa machache baadaya kupitia kwa mmoja wa maaskofu wasaidizi wa Roma, Askofu Daniele Libanori. Askofu huyo huyo alikutana na Baba Mtakatifu siku iliyofuata wakati wa Misa ya Krismasi, (yaani ya kubariki mafuta matakatifu) akipokea jukumu la kuendelea siku hiyo hiyo ya Alhamisi kuu Takatifu, kumweka wakfu Padre Livinus.

Ilikuwa sherehe rahisi sana hospitalini, ikiongozwa na askofu msaidizi wa Roma, ambayo ilihudhuriwa na baadhi ya mapadre wa shirika lake na wafanyakazi wa matibabu ambao walimtunza kwa mapenzi mema. Alipokea kikombe na paten na mikono yake ilipakwa mafuta na Krismasi baada ya sala ya majitoleo ambayo ilimfanya awe ‘alter Christus’ aliyebadilishwa kuwa Kristo mwingine kwa maana, ya kufanana na Yesu aliye kuhani mkuu. Kuanzia siku hiyo, alitumia nguvu zake kidogo alizokuwa nayo ili kuadhimisha Misa akiwa kitandani kwake. Aliunganisha dhabihu yake na ile ya Kristo, kama vile Askofu Libanori alivyomshauri siku ya kuwekwa wakfu. Na ndivyo alivyofanya hadi Jumatano iliyopita isipokuwa jana tarehe 22 Aprili, kwa sababu ya hali yake kuwa mbaya. Akitambua juu ya kile kilichokuwa kinamtokea, Padre Livinus aliomba kuungama na kupokea kumunio.

Asubuhi ya leo Ijumaa tarehe 23 Aprili, mkuu wake mkuu wa shirika, kuhani mwingine wa Mater Dei na kijana mmoja anayefanya mang’amuzi ya wito wake wamesali rosari ya Huruma ya Mungu karibu naye hospitalini. Mara tu, baada ya saa 5:10 asubuhi, Padre Livinus ameaga dunia na ndugu zake wa Jumuiya wamemkabidhi mikononi mwa Mamama kwa sala ya “Sub tuum praesidium”. Maadhimisho maziko yanatarajiwa kufanyika Jumatatu tarehe 26 Aprili saa 5.00 katika Parokia ya Mtakatifu Giovanni Leonardi, Sekta ya Torre Maura, Roma. Na baadaye Mwili wake utasafirishwa kurudi katika ardhi yake nchini Nigeria. Raha ya Milele uumpe Ee Bwana na Mwana wa Milele umwangazie apumzike kwa amani, Amina.

Share:

MTANDAO WA WANAWAKE, KATIBA, UONGOZI, NA UCHAGUZI WACHAMBUA HOTUBA YA RAIS SAMIA…WATOA TAMKO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akilihutubia Bunge la 12 na kuelezea Muelekeo wa Serikali ya Awamu ya Sita 22 Aprili, 2021 Jijini Dodoma

TAMKO UCHAMBUZI WA HOTUBA YA MHE. RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGENI KWA MTIZAMO WA KIJINSIA 24 APRILI 2021

Mtandao wa Wanawake, Katiba, Uongozi na Uchaguzi, kwa kushirikiana na wadau wengine wanaoshughulika na masuala ya usawa wa jinsia na haki za wanawake, tunayo furaha kubwa kuendelea kumpongeza Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ameandika Historia katika nchi yetu na ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuwa Rais wa kwanza mwanamke Tanzania. 

Halikadhalika, tunampongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa ujasiri wake wa kupokea Serikali na kuongoza taifa katika kipindi kigumu cha majonzi baada ya kifo cha Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amin. 

Sisi, Wanamtandao tunaoshugulika kutetea na kukuza uongozi uliojengeka katika misingi ya haki na usawa wa jinsia, tumemfuatilia kwa karibu Mheshimiwa Rais akilihutubia Bunge kwa mara ya kwanza tangu aapishwe tarehe 19 Machi 2021 na kutoa mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Sita kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

 Hotuba hii imeonesha vipaumbele ambavyo vimegusa maeneo mbalimbali ya maendeleo katika nchi yetu, yakiwemo yale ya kuneemesha maisha, haki, na usawa katika makundi mbalimbali ya kijamii.

 Kipekee tumefurahishwa na Mheshimiwa Rais Samia kwa kuonesha bayana tunu za kuongoza taifa ambazo zimejumuisha masuala ya haki, demokrasia, na usawa. 

Ni matumaini yetu kuwa tunu hizi muhimu zikidumishwa, kulindwa na kutetewa, zitatoa mwanga mkubwa katika kuongoza utekelezaji wa vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya sita, ambavyo vimejumuisha kukuza uchumi na kupambana na umasikini nchini, kupambana na rushwa na ubaridhifu wa mali ya umma, ulipaji wa kodi usio na bughudha, kukuza na kuongeza tija katika sekta ya kilimo na mifugo, kukuza ajira na mapato kwa kukuza na kulinda sekta ya Madini, utalii, viwanda na kwingineko, kuendeleza na kukuza miundo mbinu mbalimbali, kuboresha na kuleta mapinduzi zaidi ya teknolojia, TEHAMA na mawasiliano, kuongezea uwekezaji katika sekta za nishati, elimu, afya (na haswa afya ya uzazi), kukuza na kudumisha misingi ya demokrasia, amani na uhuru, na zaidi kuhakikisha misingi ya haki na sheria zinatumika kulinda wananchi.

Tunapenda kusisitiza kuwa, katika uchambuzi wetu kuhusu Hotuba hii ya kwanza ya Mhe. Rais Samia, unaonesha kuwa maeneo yote yaliyopewa kipaumbele katika Serikali yake, yanatoa fursa kubwa ya kukuza maendeleo yatakayowafikia na kuwanufaisha wanawake, wasichana na makundi mengi mengi ya wanyonge nchini, kama utekelezaji wa vipaumbele hivi utajengeka na kutekelezeka katika misingi ya haki na usawa, ukiwemo usawa wa jinsia.

 Kwa kutumia mifano michache tu hapo chini, tunaonesha jinsi maeneo yaliyobainishwa na Mheshimiwa Rais yanavyotoa fursa za kukuza misingi na matokeo ya maendeleo yatakayopelekea kukua kwa misingi inayojumuisha usawa wa jinsia, na kwa uhakika Mhe. Samia Suluhu Hassan anastahili pongezi kwa hayo: 

i) Tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa ahadi ya kulinda misingi ya demokrasia na uhuru wa watu pamoja na wanasiasa na vyombo vya habari.

 Katika utekelezaji wa hili, tunaona fursa kubwa ya kujenga misingi na mikakati ambayo haitaacha nyuma ushiriki na sauti za wanawake kama wanajamii wa Taifa hili. 

Hivyo, tunamuomba Mheshimiwa Rais kwamba katika kukutana na vyama vya siasa, kuwe na msisitizo wa kuhakikisha mkakati wa usawa wa jinsia na demokrasia ndani ya vyama inatekelezwa kama ajenda yao kimkakati. 

ii) Kipaumbele cha kuboresha Sekta ya madini, utalii na nyinginezo ni cha kupongezwa sana. Kwa bahati mbaya, kwa muda mrefu sekta hizi zimekuwa zikitoa kipaumbele na kuwanufaisha zaidi wanaume kuliko wanawake. Ni matumaini yetu kuwa utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamuya Sita, utatilia mkazo kuhakikisha kuwa wanawake wananufaika na fursa zitokanazo na sekta hizo.

 iii) Juhudi za kuboresha kilimo ili kufungamanisha maendeleo ya kilimo na viwanda kwa lengo la kuwezesha mazao ya kilimo yatumike kama malighafi za viwanda. Jambo hili litasaidia wakulima, wakiwemo wakulima wanawake vijijini kuweza kuuza mazao yao viwandani na kununua bidhaa za viwandani. 

iv) Kutoa kipaumbele katika uwekezaji, na umiliki wa ardhi ni suala nyeti na tete ambalo linahitaji umakini mkubwa. Tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuainisha kipaumbele hiki na kuahidi kuwa ushiriki wa wanawake katika suala hili ni wa muhimu sana kwani ardhi imekuwa msingi mkuu wa ushiriki wa wanawake katika maendeleo. Tunatarajia kwamba wanawake ambao wamekuwa wakilisha taifa hili kwa muda mrefu watapewa kipaumbele katika fursa zitokanazo na kilimo cha biashara tofauti na walivyokuwa wakiachwa nyuma kwa muda mrefu.

 v) Kuongeza usawa wa kijinsia kwa kuongeza wanawake wengi zaidi katika nafasi za uongozi kwa kuzingatia vigezo na sifa stahiki. Juhudi hizi zitapunguza pengo la usawa wa kijinsia katika nafasi za uongozi na kuongeza tija katika kuingiza masuala ya kijinsia katika sera, bajeti, mipango na michakato yote ya maendeleo. Hii itasaidia katika kuongeza kasi ya maendeleo jumuishi na endelevu nchini. 

vi) Kuongeza juhudi katika kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto. Pia, kuimarisha huduma za afya kwa kujenga miundo mbinu, kuongeza watumishi, vifaa-tiba, dawa na vitendanishi, pamoja na kuboresha Bima ya afya kwa wazee na kwa wote. Juhudi hizi zitawasaidia wanawake kwani ndio wanaobeba mzigo mzito katika masuala ya afya katika familia na jamii kwa ujumla.

 vii) Kuongeza uwajibikaji wa watendaji katika miradi ya maji, kuhakikisha upatikanaji wa maji sehemu zisizo na maji kwa kupitia mabwawa ya kuvuna maji ya mvua na kuimarisha kamati za maji za mitaa na vijiji ili ziweze kutimiza majukumu yao kwa ufanisi. Juhudi hizi zitawapunguzia wanawake mzigo wa kutumia muda mwingi kutafuta maji badala ya kutumia muda huo kwenye shughuli za uzalishaji. 

viii) Kuboresha mfumo wa elimu nchini kwa kufanya mapitio ya Sera ya Elimu na Ufundi ya mwaka 2014 na mitaaala ya elimu ili iendane na muktadha wa sasa.

 Tunatarajia mapitio haya yatakuwa jumuishi na yatatoa kipaumbele kwa watoto wa kike na wenye ulemavu ili waweze kunufaika na haki yao ya msingi ya kupata elimu bora.

 Sisi wanamtandao tunaahidi kuendelea kufanya kazi na Serikali ya Awamu ya Sita kwa njia mbalimbali ikiwemo kutoa ushirikiano kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Awamu ya Sita katika kufuatilia na kutoa ushauri juu ya utekelezaji wa vipaumbele vilivyoainishwa katika hotuba ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan.

 Imetolewa na: 
Mtandao wa Wanawake, Katiba, Uongozi, na Uchaguzi.




Share:

SAFARI ZA KWENDA, KUTOKA ZANZIBAR BAHARINI ZASITISHWA TAHADHARI YA KIMBUNGA JOBO... TMA YATOA NENO

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesitisha shughuli za usafiri wa baharini zikiwemo safari za meli na vyombo vingine vya usafiri baharini kuanzia leo Jumamosi Aprili 24, 2021 saa tatu asubuhi.

Taarifa iliyotolewa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Dkt Khalid Salum Mohamed inaeleza kuwa Serikali ya Zanzibar  imesitisha shughuli hizo kuchukua tahadhari ya kimbunga Jobo kinachotarajiwa kupiga mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Lindi, Mtwara na kisiwani Zanzibar pamoja na Mafia kesho Jumapili Aprili 25, 2021.

Inaeleza kuwa katazo hilo litadumu hadi hadi pale taarifa nyingine zitakapotolewa na mamlaka husika.

Hata hivyo Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini TMA imesema Kimbunga JOBO kimepunguza kasi mara baada ya kuingia kwenye mazingira ya upepo kinzani hivyo kwasasa kimbunga hicho ni hafifu.

TMA imetoa taarifa hiyo leo April 24, ikielezea mwenendo wa kimbunga “Jobo” kilichopo bahari ya Hindi ambacho kipo umbali wa kilomita 200 mashariki mwa kisiwa cha Mafia na kusema kuwa kimbunga hicho kimekuwa hafifu kinachosafiri kwa kasi ya kilometa 18 kwa saa baharini.

TMA imesema kimbunga hicho hafifu kinatarjia kusababisha vipindi vya mvua kubwa katika maeneo machache hususan ya ukanda wa Pwani kadri kinavyosogea nchi kavu kwa siku ya leo tarehe 24 na kesho 25 mwezi Aprili, 2021 na kusababisha mawimbi makubwa.

Pia Mamlaka hiyo imesema maeneo yanayotarajiwa kupata athari za moja kwa moja ni pamoja na mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani (ikiwemo kisiwa cha Mafia), Dar es Salaam pamoja na kisiwa cha Unguja.

Aidha wananchi wameshauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka hiyo pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam katika sekta husika ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger