Friday, 10 April 2026

MUYINGA AISHUKIA CHADEMA KUHUSU KIINI CHA VURUGU ZA OKTOBA 29

...


Na mwandishi wetu, Dar

Mwanaharakati wa kijamii, Alphonce Patrick Muyinga ameonya kuhusu baadhi ya wanasiasa na wanaharakati kutumia nguvu kubwa kuvuruga na kuanzisha chokochoko dhidi ya Tume huru ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akiwataka kuiacha Tume hiyo kukamilisha kazi yake kwa mustakabali wa amani na haki ya Watanzania.

Muyinga amebainisha hayo leo Ijumaa Aprili 10, 2026, siku moja mara baada ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuzungumza na wanahabari na kuhamasisha maandamano nchini pamoja na kuishutumu serikali kuhusu kuendelea kushikiliwa kwa mwanasiasa Tundu Lissu, akisema zote hizo ni njama za kuvuruga utendaji wa Tume ya Oktoba 29.

"Watanzania wote tunajua Rais Samia aliunda Tume hii kuchunguza yaliyotokea Oktoba 29, leo Tume inakaribia kumaliza kazi tujiulize kwanini Heche na genge lake la wanakaa kuchochea, kutengeneza propaganda, kutumia nguvu kubwa kuvuruga uchunguzi wa tume. Wanaficha nini? Kuna nini hawataki tume ije kusema? Tuache! Tume imalize kazi yake ije iseme. Suala la Lissu ni la kisheria na lipo mahakamani kama zlivyo kesi za wengine." Amesema Muyinga.

Muyinga amemkosoa Makamu Mwenyekiti huyo wa Chadema pia kuhusu namna ambavyo amekuwa akikwepa kuzungumzia ajenda za maendeleo nchini na badala yake kuhamasisha vurugu na kutaka Vijana kupinga na kuharibu jitihada mbalimbali za maendeleo nchini, akiwataka Vijana kuzinduka na kujifunza kuhusu Chadema na siasa zao za mihemko wanazofanya wao pamoja na washika wao.

Mwanaharakati huyo amehimiza utulivu kwa watanzania na wapenda haki wote wa ndani na nje ya nchi katika kipindi hiki ambacho Tume ya Oktoba 29 inapokwenda kukamilisha jukumu lake, akiwasihi pia kuwakataa kwa nguvu wale wote wanaoanzisha uchochezi na tuhuma mbalimbali dhidi ya Tume na serikali kwa lengo la kuikwamisha Tume hiyo kumaliza kazi yake na kukabidhi kwa mamlaka kwa hatua zaidi.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger