Thursday, 9 April 2026

JAMII YATAKIWA KUSHIRIKIANA NA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KULINDA AMANI

...


Jamii imetakiwa kushirikiana kwa karibu na Vyombo vya ulinzi na usalama na mamlaka nyingine za uongozi zilizopo nchini katika kutoa taarifa za matukio ya uvunjifu wa amani, uhalifu na wahalifu pamoja na kutumia vyema mitandao ya Kijamii ili kudumisha na kuendeleza amani, utulivu na usalama wa nchi kama msingi mkuu wa uhai, maendeleo ya kiuchumi, kijamii na ustawi wa haki.

Kadhalika Waandishi wa habari hapa nchini wamehimizwa kutumia kalamu zao vyema na kuandaa maudhui kwenye majukwaa yao ya habari ya kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kudumisha amani nchini ili kuhakikisha kuwa amani hiyo inaendelea kuwepo pamoja na kuendeleza mshikamano wa Watanzania kwa kuuhabarisha kuhusu hatua mbalimbali za maendeleo na namna wanavyoweza kunufaika na amani na utulivu unaoendelea kuwepo nchini.

Wito huo umetolewa na  Epimark Aqwesso na  Gabriel Hilonga Silo, wakazi wa Wilayani Karatu Mkoani Arusha, wakitahadharisha watanzania kurejea katika matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 na kadhia waliyokutana nayo kutokana na kukwama kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.

"Amani tuliyonayo hapa nchini kwetu ndio inatufanya tuendelee kukusanyika na kufanya shughuli zetu nyingine za kijamii na kiuchumi. Mnakumbuka tukio la Oktoba 29, 2025? wengi wetu tulishindwa kufanya shughuli zetu, hofu ilitanda na wengi waliingia mitini na kujificha, hali hii isijirudie tena, Vijana wa sasa (GenZ) tukumbuke kuna maisha kesho na kamwe tusiharibu amani ya nchi yetu." Amesema Bw. Aqwesso.

Kwa upande wake Bw. Silo amehimiza Vijana kutumia vyema fursa ya amani iliyopo nchini kwa kujiendeleza kiuchumi, akieleza namna ambavyo serikali imeendelea kuwezesha wananchi kiuchumi kupitia sekta mbalimbali ikiwemo kilimo na ufugaji, akisisitiza kuwa amani ndio uhai wa Nchi na wananchi wake na kutaka jamii kushirikiana kuilinda.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger