Saturday, 24 April 2021
SAFARI ZA KWENDA, KUTOKA ZANZIBAR BAHARINI ZASITISHWA TAHADHARI YA KIMBUNGA JOBO... TMA YATOA NENO
WAZIRI UMMY AZIONYA HALMASHAURI ZILIZOKUSANYA CHINI YA ASILIMIA 75
Angela Msimbira TAMISEMI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Ummy Mwalimu ameagiza Halmashauri ambazo zimekusanya mapato chini ya asilimia 75 ya makisio yake kufanya tathmini na kuhakikisha inaweka mikakati madhubuti ya kufikia malengo yao ifikapo 30 Juni, 2021.
Akitoa taarifa ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kipindi cha Julai, 2020 hadi machi, 2021 Waziri ummy amesema kila Halmashauri ihakikishe inatumia kwa usahihi mifumo ya kielektroniki ya ukusanyaji wa mapato ya ndani na mifumo ya uhasibu ili kutoa taarifa kwa kufuata matakwa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya uhasibu katika sekta ya umma (IPSAS).
Waziri Ummy ameiagiza Mikoa kuendelea kusimamia, kutoa ushauri na maelekezo kuhusu suala zima la ukusanyaji na matumizi ya mapato ya ndani ya Halmashauri kabla ya viongozi wa juu kubaini matatizo ya halmashauri nchini.
Amezielekeza Halmashauri zote nchini kuzuia na kudhibiti matumizi ya fedha mbichi kabla ya makusanyo hayajapelekwa benki, kwa kuwa kwa mujibu wa sheria fedha inatakiwa kukusanywa na kupelekwa benki ndipo kuanza kutumika.
Waziri Ummy amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri kuacha kutumia fedha mbichi za makusanyo kabla ya kupelekwa benki na atakayekiuka hatua kali zitachukuliwa dhidi yake kwa kuwa atakuwa amekiunka miongozo ya kifedha inayomtaka kuhakikisha wanankusanya na kupeleka benki ndipo kuanza kutumika.
Ameielekeza Mikoa kuendelea kusimamia Halmashauri kwa kutoa taarifa kupitia mifumo ya kielektroniki, kusisitiza usuluhishi wa taarifa na usahihishaji wa takwimu katika mifumo mbalimbali na kuongeza jitihada katika usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Hata hivyo, amezitaka Sekretarieti za Mikoa kuhakikisha wanatoa ushauri stahiki kwa wakati, kutatua changamoto zilizopo katika suala zima la ukusanyaji wa mapato katika halmashauri wanazoziongoza, kutoa miongozo kwa lengo za kuhakikisha Mamlaka za Serikali za Mitaa zinafanya vizuri katika suala zima la ukusanyaji wa mapato ili kuleta maendeleo kwa wananchi
Akizungumzia ukusanyaji wa Mapato hayo Waziri Ummy ameeleza kwa mwaka wa fedha 2020/21 Halmashauri zilipanga kukusanya Shilingi Bilioni 814.96 kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani katika kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021 Halmashauri zimeweza kukusanya jumla ya shilingi bilioni 557.45 sawa na asilimia 68 ys makisio ya mwaka
Amefafanua kuwa taarifa za mapato ya vyanzo vya ndani vya Halmashauri katika kipindi cha Julai 2020 hadi Machi, 2021 imeonesha uwepo wa ongezeko la mapato yaliyokusanywa kuwa ni shilingi bilioni 30.14 ikilinganishwa na kiasi kilichokusanywa katika kipindi kama hicho cha Julai – Machi , 2020 sawa na ongezeko la asilimia 6.
Waziri Ummy ameongeza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala imeongoza kwa kukusanya mapato kwa asilimia 117 ya makisio yake ya mwaka wakati Halmashauri za Wilaya za Ngorongoro imekuwa ya mwisho kwa kukusanya chini ya asilimia 34 ya makisio yake ya mwaka.
Katika kuzipima Halmashauri zote kwa kigezo cha wingi wa mapato (pato ghafi), Halmashauri ya Jiji la Dar-es-salaam imekusanya mapato mengi zaidi kuliko Halmashauri zote kwa kukusanya shilingi bilioni 52.78 na Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe imekusanya mapato kidogo kuliko Halmashauri zote kwa kukusanya Shilingi Milioni 453.72
Hata hivyo katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri Kimkoa kwa kuzingatia asilimia ya makusanyo Waziri Ummy amebainisha kuwa Mkoa wa Geita umefanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ambapo umekusanya kwa wastani wa asilimia 82 ya makisio ya mwaka ya Halmashauri za Mkoa huo wakati Mkoa wa mwisho kwa kigezo hicho ni Mkoa wa Singida ambao umekusanya wastani wa asilimia 48 ya makisio ya mwaka ya Halmashauri za Mkoa huo.
Katika hatua nyingine Waziri Ummy ameweka wazi Ukusanyaji wa Mapato ya Ndani ya Halmashauri Kimkoa kwa Kuzingatia Wingi wa Mapato kuwa Mkoa wa Dar es Salaam umefanya vizuri kwa kigezo cha wingi wa mapato ambapo imekusanya kiasi cha Shilingi Bilioni 133.90 huku Mkoa wa mwisho katika wingi wa mapato ni Mkoa wa Rukwa ambao umekusanya Shilingi Bilioni 5.57.
Vile vile Ukusanyaji wa mapato kwa Halmashauri kwa Kuzingatia aina ya Halmashauri kwa Kigezo cha asilimia ya makusanyo ukilinganisha na makisio ya mwaka Waziri Ummy amesema kwa upande wa Majiji Halmashauri ya Dar-es-salaam imeongoza kwa kukusanya mapato kwa asilimia 78 ya makisio yake ya mwaka na Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa ya mwisho katika kundi hili ambapo imekusanya kwa asilimia 58 ya makisio yake ya mwaka.
Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni imeongoza kundi la Halmashauri za Manispaa ambayo imekusanya asilimia 101 ya makisio yake na Katika kundi hilo Halmashauri ya Manispaa ya Lindi imekuwa ya mwisho ambapo imekusanya kwa asilimia 36 ya makisio yake ya mwaka.
“Kwa kundi la Halmashauri za Miji , Halmashauri ya Mji Kibaha imeongoza kwa kukusanya kwa asilimia 93 ya makisio ya mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2020/21 ambapo Halmashauri ya Mji wa Bariadi imekuwa ya mwisho kwa kukusanya asilimia 36 ya makisio ya mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2020/21” amesema Waziri Ummy
Aidha, kwa upande wa Halmashauri za Wilaya amesema Halmashauri ya Wilaya ya Msalala imeongoza kwa kukusanya asilimia 117 ya makisio ya mapato ya ndani huku Halmashauri za Wilaya za Ngorongoro kuwa ya mwisho katika kundi hilo kwa kukusanya asilimia 34 ya makisio ya mapato ya ndani kwa mwaka wa Fedha 2020/21.
“Halmashauri ya Jiji la Dar-es-salaam a imeongoza kwa kundi la Halmashauri za Majiji kwa kigezo cha wingi wa mapato kwa kukusanya Shilingi bilioni 52.78 na Halmashauri ya Jiji la Tanga imekuwa ya mwisho katika kundi hili ambapo imekusanya Shilingi bilioni 9.93.” ameeleza Waziri Ummy
Kwa kuongezea Waziri Ummy amesema kwa upande wa Halmashauri za Manispaa,Manispaa ya Kinondoni imeongoza kwa kukusanya Shilingi bilioni 33.25 na Halmashauri ya Manispaa ya Lindi imekuwa ya mwisho katika kundi hili ambapo imekusanya Shilingi bilioni 1. 26
Huku katika kundi la Halmashauri ya Wilaya, Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze imeongoza kwa kukusanya mapato mengi ambapo imekusanya Shilingi Bilioni 6.48. Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe imekuwa ya mwisho katika kundi hili ambapo imekusanya Shilingi Milioni 453.72
JESHI LA MAGEREZA TARIME LAZIDI KUBUNI MIRADI ILI KUJITEGEMEA KIUCHUMI KATIKA KUWAHUDUMIA WAFUNGWA NA MAHABUSU
Na Dinna Maningo,Tarime.
JESHI la Magereza wilaya ya Tarime mkoa wa Mara linaendelea na utekelezaji wa shughuli za kiuchumi kwa kubuni miradi mbalimbali kwa ajili ya kujitegemea ili kuwawezesha wafungwa na mahabusu kupata chakula cha kutosha.
Akizungumza na Malunde 1 blog ofisini kwake, Mkuu wa Gereza la wilaya ya Tarime ASP Sebastian Dionis aliyehamishiwa wilaya hiyo Machi, 20,2021 akitokea gereza la wilaya ya Chato-Geita alisema kuwa tayari wameanza rasmi kulima zao la mahindi ekali 20 katika mlima Nkongoro kata ya Kitare.
Alisema mlima wa Nkongore ni eneo lililokuwa likitumiwa na baadhi ya wananchi kulima kilimo cha bangi na hivyo serikali kulikabidhi kwa Jeshi la Magereza mwaka 2017 kwa ajili ya shughuli za kilimo.
"Eneo hilo lina ukubwa wa ekari 150 kati ya hizo ekali 20 tumelima mahindi eneo jingine tuko kwenye maandalizi ya kilimo cha kahawa,mlima huo wa Nkongore baadhi ya wananchi waliutumia kulima bangi.
"Hali iliyopelekea serikali kulichukua eneo hilo na kuwakabidhi jeshi la Magereza,kilimo kitasaidia kuwezesha wafungwa na mahabusu kupata chakula istoshe tulikuwa hatuna eneo la kilimo tunalima mahindi kwenye eneo la kuazima kutoka katika Jeshi la JWTZ -Nyandoto lenye ekali 30", alisema Dionis.
Mkuu huyo wa magereza alisema kuwa mbali na kujishughulisha na kilimo jeshi hilo limekuwa likiendelea kubuni miradi mbalimbali ambapo lina mradi wa zahanati ya afya inayotoa huduma ya jamii ndani ya magereza na nje ya magereza,kufanya usafi katika hospitali ya wilaya.
Miradi mingine ni huduma ya Bima ya afya na ushauri nasaha,hoteli,huduma ya vinywaji (Bar) duka la magereza, Bucha ya kuuza nyama ya ng'ombe, bustani ya mbogamboga, uchomeleaji wa vyuma kwa kutengeneza madirisha,vitanda na milango, utengenezaji wa majiko ya kupikia na ujenzi.
"Bado tutaendelea kubuni miradi mingine tunajihusisha na ujenzi kupitia mafundi ambao ni wafungwa katika gereza letu, tunawaomba wananchi watuchangie miradi yetu ili tupate fedha ambazo zitasaidia kufanikisha huduma za magereza ikiwa ni pamoja na kutupatia kazi za ujenzi tuna mafundi wa kutosha ambao ni wataalamu katika ujenzi watakujengea mradi wako na utakamilika kwa wakati ,uchomeleaji wa vifaa na miradi mingineyo",alisema.
Dionis alisema kuwa magereza ya wilaya ya Tarime linahudumia wafungwa na mahabusu wapatao 512 kati ya hao wafungwa ni 112 na mahabusu 400 na kwamba miradi hiyo imekuwa inasaidia kuendesha shughuli za magereza na kujitegemea kiuchumi hivyo anawakaribisha wananchi kununua bidhaa za magereza na kupata huduma ya afya.
RAS MOROGORO: HALMASHAURI ZOTE MOROGORO TUMIENI WATAALAM WANAOZALISHWA NA CHUO CHA ARDHI MOROGORO KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI
Mgeni Rasmi, Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emanuel Kalobelo.
Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Emanuel Kalobelo akisaini kitabu cha wageni alipofika Chuo cha Ardhi Morogoro.
Mgeni Rasmi Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Emanuel Kalobelo (wa pili toka kushoto) akipata maelekezo ya kifaa cha upimaji (total station) kutoka kwa mmoja wa wanafunzi. Upande wa Mgeni Rasmi yupo Kamishna wa Ardhi Mkoa wa Morogoro na upande wa Kushoto yupo Mkuu wa Chuo
TBS YAWAFUNDA WADAU WA MAFUTA YA KULA MKOANI MOROGORO
![]() |
| Wakaguzi wa TBS wakielimisha baadhi ya wauzaji wa maduka ya chakula mkoani Morogoro, namna ya kusajili katika mfumo na umuhimu wa kutumia vifungashio sahihi katika bidhaa zao. |
Wakaguzi wa TBS wakielimisha baadhi ya wauzaji wa maduka ya chakula mkoani Morogoro, namna ya kusajili katika mfumo na umuhimu wa kutumia vifungashio sahihi katika bidhaa zao.
![]() |
| Washiriki wa mafunzo kwa wadau wa mafuta ya kula mkoani Morogoro wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo. |
Washiriki wa mafunzo kwa wadau wa mafuta ya kula mkoani Morogoro wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo.
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kutoa mafunzo maalum kwa wajasiriamali na wafanyabiashara kwa ujumla wanaojishughulisha na sekta ya mafuta ya kula 282 kutoka katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero na Halmashauri ya Mji ya Gairo za mkoani Morogoro.
Mafunzo haya maalum yamewalenga wajasiriamali na wafanyabiashara wanaojishughulisha na uzalishaji, usambazaji na uuzaji wa mafuta ya kula katika masoko ya ndani na ya nje katika mkoa wa Morogoro.
Akimuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TBS Dkt. Athuman Y. Ngenya, Meneja wa Utafiti na Mafunzo wa TBS Bw. Hamisi Mwanasala alisema mafunzo haya ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya Shirika sambamba na agizo la Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara kulitaka Shirika kuendesha mafunzo haya maaalum mikoa yote nchini.
Bw. Sudi alisema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa wajasiriamali ikiwa ni pamoja na wanaojishughulisha na sekta mafuta ya kula katika kukuza uchumi wa nchi.Hivyo mafunzo haya ni mahsusi kuwajengea uwezo wadau wa mafuta ya kula nchini ili waweze kuzalisha mafuta kwa wingi na yenye ubora unaokidhi matakwa ya viwango vya mafuta ya kula.
"Mafunzo haya yataenda sambamba na utoaji wa elimu maeneo ya kwenye masoko na vituo vya pembezoni mwa barabara ambapo wauzaji wengi wanauza mafuta ya kula" alisisitiza Bw. Sudi.
Kwa upande wake Afisa Udhibiti Ubora wa TBS, Bi Gudila Boniface alisema ili mafuta ya kula yakidhi viwango ni lazima kufuata kanuni za kilimo bora, usindikaji na usafi.
Bi. Gudila alisema kanuni za kilimo bora zinahusisha matumizi ya mbegu bora, kuvuna kwa wakati mazao yalikomaa.
Kwa upande wa kanuni bora za usindikaji kwa mujibu wa Bi. Gudila ni pamoja na kutumia malighafi bora, vifaa vya kusindikia ambavyo havishiki kutu na vilivyoshauriwa na wataalam.
Akizungumzia kanuni bora za usafi, Bi. Gudila alisema wazalishaji wanatakiwa kuhakikisha vifaa vya kuhifadhi mafuta ni safi ikiwa ni pamoja na madumu yanayotumika kuhifadhi mafuta hayo yawe yamesafishwa vizuri pamoja na usafi wa mazingira.
" Vifungashio/Madumu wanayoweka mafuta wahakikishe wameyasafisha vizuri na waweke lebo zinazoeleza bidhaa hizo ni za aina gani," alisema na kuongeza kwamba haikubaliki kwenye vifungashio ambavyo wazalishaji wanaweka mafuta iwe lebo inayohusu bidhaa nyingine.
Aidha, alisema mafuta ya kula hayatakiwi kuwekwa juani, kwani yanapokuwa juani kuna kemikali zinazozalishwa na zinaweza kusababisha mafuta kuharibika ambayo yakitumiwa na walaji yanaleta athari za kiafya.
Kwa upande wake Afisa Udhibiti Ubora Mwandamizi wa TBS, Bi. Flora Luvanda alitoa wito kwa wadau hao kuthibitisha ubora wa bidhaa zao, kusajili bidhaa za chakula na vipodozi na majengo yanayojihusisha na bidhaa za vyakula na vipodozi.
" Tunatoa wito kwa wadau kuwasiliana na TBS endapo wanakutana na changamoto yeyote wakati wa usajili tutawaelekeza na kuwasaidia mpaka usajili utakapokamilika," alisema Bi Flora.
Alisema ni muhimu kwa wafanyabishara kusajili bidhaa na majengo ya vyakula na vipodozi kwa mujibu wa sheria ambayo imetokana na mabadiliko ya Sheria ya fedha ya mwaka 2019 iliyohamisha majukumu ya usimamizi wa usalama na ubora wa vyakula na vipodozi kwa TBS kutoka kwa iliyokua Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA).
Alisema usajili wa bidhaa na majengo ya vyakula na vipodozi ni takwa la kisheria na hivyo kwa kufanya hivyo kutawafanya wafanye biashara zao kwa uhuru na uhakika.
Katika mafunzo haya, TBS imewashirikisha watoa mada kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara na Taasisi nyingine ikiwa ni pamoja na Wakala wa Vipimo (WMA), BRELA, Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) pamoja na maafisa kutoka dawati la Halmashauri husika ikijumuisha Afisa Biashara, Afisa Afya na Afisa Maendeleo ya Jamii.
Mafunzo haya maalum kwa wadau wa mafuta ya kula mkoani Morogoro ni mwendelezo wa mafunzo kama haya yaliyokwisha kutolewa katika mikoa ya Dodoma, Singida, Tabora, Kigoma, Iringa, Njombe, Mbeya na Songwe.
PROF SHEMDOE AWAONYA MATAPELI KUHUSU AJIRA ELFU SITA ZA WALIMU
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe (katikati), akizungumza na Wajumbe wa Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Walimu – TSC (hawapo pichani), alipotembelea Taasisi hiyo jijini Dodoma Aprili 23, 2021 kujionea utekelezaji wa majukumu. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, anayehusika na masuala ya Elimu, Gerald Mweli na kulia kwake ni Katibu wa TSC Mwl. Paulina Nkwama.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe (mbele-katikati), akizungumza na Wajumbe wa Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), alipotembelea Taasisi hiyo jijini Dodoma Aprili 23, 2021 kujionea utekelezaji wa majukumu. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, anayehusika na masuala ya Elimu, Gerald Mweli na kulia kwake ni Katibu wa TSC Mwl. Paulina Nkwama.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, anayehusika na masuala ya Elimu, Gerald Mweli (katikati), akizungumza na watumishi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), wakati wa ziara ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe (wa pili-kushoto), Aprili 23, 2021 Makao Makuu ya Tume Dodoma. Wa kwanza kushoto ni Katibu wa TSC, Mwl Paulina Nkwama.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Mwl Paulina Nkwama akimkaribisha Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe (wa tatu-kushoto) kuzungumza na Wajumbe wa Menejimenti ya Tume hiyo. Prof Shemdoe alitembelea Makao Makuu ya TSC jijini Dodoma, Aprili 23, 2021 kujionea utekelezaji wa majukumu yao. Kushoto kwa Katibu Mkuu ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI, anayehusika na masuala ya Elimu, Gerald Mweli.
Baadhi ya wafanyakazi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe (wa pili-kushoto) alipotembelea Makao Makuu ya TSC jijini Dodoma, Aprili 23, 2021 kujionea utekelezaji wa majukumu yao. Kushoto kwa Katibu Mkuu ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI, anayehusika na masuala ya Elimu, Gerald Mweli na wa kwanza kushoto ni Katibu wa TSC, Mwl Paulina Nkwama.

Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Mwl Paulina Nkwama (kushoto), akimkaribisha Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe (katikati) na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI, anayehusika na masuala ya Elimu, Gerald Mweli (kulia), walipowasili Makao Makuu ya Tume jijini Ddoma, Aprili 23, 2021 wakiwa katika ziara ya kazi.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, akisaini Kitabu cha Wageni, Ofisini kwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Mwl Paulina Nkwama (wa pili-kulia). Katibu Mkuu alitembelea Makao Makuu ya Tume jijini Dodoma, Aprili 23, 2021. Wa pili kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, anayehusika na masuala ya Elimu, Gerald Mweli, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu TSC, Moses Chitama na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Idara ya Ajira, Maadili na Maendeleo ya Walimu TSC, Christina Hape.
![]() |

Baadhi ya wafanyakazi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe (hayupo pichani), aliyekuwa akizungumza nao alipotembelea Makao Makuu ya TSC jijini Dodoma, Aprili 23, 2021 kujionea utekelezaji wa majukumu yao.
************************
Veronica Simba na Atley Kuni
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, ametoa onyo kwa watu wanaowatapeli wananchi sehemu mbalimbali kwamba wanahusika kwa namna moja ama nyingine katika zoezi la kuajiri walimu 6,000 ili kujaza nafasi zilizoachwa wazi, kama ilivyoagizwa na Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni.
Ametoa onyo hilo leo Aprili 23, 2021 mbele ya waandishi wa habari wakati wa ziara yake ya kwanza Makao Makuu ya Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Dodoma, iliyolenga kujionea utekelezaji wa majukumu yao pamoja na kuzungumza na watumishi.
Prof. Shemdoe amewataka watumishi wa umma kuepuka kujihusisha na utapeli huo kwani wakibainika watachukuliwa hatua kali za kinidhamu na kisheria ikiwemo kufukuzwa kazi. Aidha, kuhusu vishoka wanaojihusisha na utapeli huo, Prof. Shemdoe amesisitiza kuwa TAMISEMI itapambana nao vikali.
“Mtumishi atakayebainika kujiingiza kwenye suala hili la utapeli anaweza kupoteza kazi. Kwa wale vishoka ambao wameamua kujichukulia fedha za watanzania wenzetu wakiwahadaa kuwa watawatafutia ajira, tutapambana nao vikali na tutahakikisha sheria inachukua mkondo wake.”
Kufuatia hali hiyo, Prof Shemdoe amebainisha kuwa ajira husika zitatolewa kwa kuzingatia vigezo vitakavyoainishwa katika tangazo litakalotolewa na Ofisi yake, na kwamba hakutakuwa na upendeleo wa aina yoyote.
“Hakuna mtu atakayependelewa na hatutaangalia nani katoka wapi. Hizi ni ajira za watanzania wote, hivyo tutaangalia vigezo ambavyo tutaviainisha katika tangazo ambalo tutalitoa kwa wananchi na siyo vinginevyo,” amesisitiza.
Aidha, amemwagiza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, anayehusika na masuala ya Elimu, Gerald Mweli pamoja na Katibu wa TSC, Mwl Paulina Nkwama kukaa pamoja na kuunda timu itakayoshughulikia ajira hizo, huku akisisitiza kuwa timu hiyo iundwe na watu wenye hofu ya Mungu ili watende haki.
Amesema Ofisi yake itaendelea kuomba nafasi zaidi za ajira kwani inatambua kuwa wapo vijana wengi waliohitimu nab ado hawapata ajira.
Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu ameipongeza TSC kwa kazi nzuri inayofanya hususani katika kusimamia maadili kwa walimu walioko katika utumishi wa umma. Amewataka watendaji wa Taasisi hiyo kuendelea kutimiza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu hasa wakati wa kufanya maamuzi katika mashauri ya walimu yanayofikishwa kwao.
“Serikali imewapa dhamana na imani kubwa kwenu katika kusimamia maadili ya walimu. Nawaomba muendelee kufanya kazi hiyo kwa imani ileile ambayo mmepewa.”
Prof Shemdoe amempongeza Katibu wa TSC, Mwl Paulina Nkwama kwa kuaminiwa na kuteuliwa na Rais Samia kushika wadhifa huo. Amewataka watumishi wote kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu yake.
Akizungumza katika ziara hiyo, Naibu Katibu Mkuu Mweli, alimweleza Katibu Mkuu kuwa TSC imekuwa ikifanya kazi nzuri ambapo alibainisha kuwa tangu ashike nafasi hiyo, Tume imetekeleza kazi walizokubaliana kwa asilimia 90.
Kwa upande wake, akizungumza kwa niaba ya watumishi wote wa TSC, Katibu wa Tume Mwl Nkwama alisema kuwa wamefarijika sana kupata heshima ya kuwa miongoni mwa taasisi za mwanzo zilizo chini ya TAMISEMI, kutembelewa na Katibu Mkuu ili kujionea utendaji wao.
“Tumefarijika sana na ujio wako hasa kwa kuzingatia kuwa ni takriban majuma mawili tu tangu ulipoapishwa na Mhe. Rais kushika wadhifa wa Katibu Mkuu TAMISEMI. Kwa kuthamini, mchango wa kada ya walimu, umeona ziara yako ya kwanza ujielekeze kwenye Ofisi ya Tume ambayo ndiyo yenye kushughulikia masuala mbalimbali ya walimu. Tunaskushukuru sana,” amesema.
Tume ya Utumishi wa Walimu ndiyo Mamlaka ya Ajira na Nidhamu kwa walimu walioko katika utumishi wa umma Tanzania Bara.
Friday, 23 April 2021
AJICHOMA KISU MARA 12 KIFUANI BAADA YA KUMUUA MPENZI WAKE
MHUNI ALIYEZOEA KUPAPASA WANAWAKE KWENYE MAGARI ASHAMBULIWA NYETI ZAKE BILA HURUMA
Baraza La Mawaziri La Kisekta La Afya La Ahidi Kuendelea Kushirikiana Katika Kukabiliana Na Changamoto Za Afya
Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya ngazi ya Mawaziri uliofanyika leo katika Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha, Tanzania; umekubaliana na kuahidi kuendelea kushirikiana katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya afya katika Jumuiya.
Mkutano huu uliotimishwa leo tarehe 23 Aprili 2021, umefanyika kwa siku tano kuanzia tarehe 19 hadi 23 Aprili 2021, ulikuwa na lengo la kufanya mapitio ya hatua ya maendeleo iliyofikiwa katika utekelezaji wa maamuzi na maagizo yaliyotolewa na Mkutano uliopita wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na la Kisekta, sambamba na kuibua maeneo mapya yanayohitajika kupewa kipaumbele kulingana na mapendekezo yaliyotolewa na Kamati za Wataalamu.
Mkutano huu uliokuwa ukiongozwa na Mhe. Mutahi Kagwe Waziri wa Afya wa Kenya ambale pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo, pamoja na masuala mengine umepitia kujadili na kutoa maelekezo katika kutatua changamoto mbalimbali, zinazokwamisha utekelezaji wa mikakati ya pamoja ya kukabiliana na Ugonjwa wa Homa kali ya Mapafu unaosababishwa na Virusi vya Korona (UVIKO-19), na usalama wa dawa na chakula katika Jumuiya.
Kila Nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa nyakati tofauti katika mkutano huo imeeleza utayari wake wa kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mikakati na mipango mbalimbali waliyokubaliana kuitumia katika kutatua changamoto za sekta ya afya.
Mkutano huu umehudhuriwa na Mawaziri kutoka Nchi zote Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaosimamia masuala ya Afya. Tanzania imewakilishwa na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mhe. Dkt. Dorothy O. Gwajima (Mb)
Tanzania Yapokea Nyongeza Ya Euro Milioni 4 Kutoka Ubelgijikwa Ajili Ya Mradi Wa Maji Kigoma
Na, Farida Ramadhani
Serikali ya Tanzania imepokea nyongeza ya kiasi cha Euro milioni nne kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa maji mkoani Kigoma kutoka Serikali ya Ubelgiji.
Hafla fupi ya utiaji saini wa mkataba wa marekebisho ya nyongeza ya mradi huo ilifanyika jijini Dodoma kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Bw. Emmanuel Tutuba kwa upande wa Serikali na Balozi wa Ubelgiji nchini, Bw. Peter Van Acker.
Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba alisema mradi huo ambao ulianzishwa kwa ajili ya Wilaya zote sita za Mkoa wa Kigoma, mwanzoni ulitarajiwa kugharimu Euro milioni nane.
“Sasa hizi Euro milioni nne zitakwenda kuongezea na kufanya jumla ya Euro milioni 12 sawa na takribani Shilingi bilioni 33 za kitanzania ambazo zitatumika kwa ajili ya kuongeza upatikanaji wa maji maeneo ya vijijini na mijini mkoani humo”, alifafanua.
Alisema katika Mkoa wa Kigoma, Serikali ya Ubelgiji pia imefadhili mradi mwingine wa kilimo ambao unaendelea na umegharimu Euro milioni nane sawa na takribani Shilingi bilioni 22, hivyo miradi yote miwili (mradi wa maji na kilimo) inagharimu jumla ya takribani Shilingi bilioni 55.
Aidha aliipongeza Serikali ya Ubelgiji kwa kubuni njia nzuri ya kupunguza gharama za utekelezaji wa mradi wa kilimo kwa kujenga madaraja ya mawe ambayo yanaweza kuunganisha sehemu ya mashamba na sehemu ya makazi na kupunguza gharama za ujenzi wa daraja moja kwa takribani asilimia 80.
Bw. Tutuba aliihakikishia Serikali ya Ubelgiji kuwa fedha hizo zitatumika kikamilifu na utekelezaji wa miradi hiyo utakamilika kwa wakati.
Naye Balozi wa Ubelgiji nchini, Bw. Peter Van Acker alisema Serikali ya nchi yake itaendeleza ushirikiano na Tanzania kwa kuendelea kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo.
Alisema anaamini mradi wa maji mkoani Kigoma utatatua changamoto ya maji mkoani humo na ameahidi kuwajibika katika masuala ya maji kama hotuba ya Mhe. Rais, Samia Suluhu Hassan ilivyosisitiza.
Akipokea kwa shukrani nyongeza hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga, aliishukuru Serikali ya Ubelgiji kwa kuendeleza ushirikiano mzuri na Tanzania na kubainisha utekelezaji wa mradi wa maji mkoani Kigoma utanufaisha watu takribani laki moja na 30.
Aliahidi kusimamia matumizi ya fedha hizo kikamilifu ili kuhakikisha malengo ya utekelezaji wa mradi huo yanatimia kwa wakati.
Mwisho.
SUPER – NHESHA: Dawa Bora Ya Kutibu Tatizo La Kisukari
Ni dawa ya kutibu tatizo la sukari au jina la kitaalamu (Diabetes Mellitus) ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo Mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya Glucose katika mwili kutokana na mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza Insulin ya kutosha au seli za mwili wake kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote kwa pamoja na kupelekea mgonjwa wa sukari kupata haja ndogo mara kwa mara (Polyuria) uhisi kiu kila wakati (Polydipsia) Na (Polyphagia).
AINA YA KISUKARI
Kuna aina chache tofauti za ugonjwa wa kisukari (1) ni ugonjwa wa Auto hii aina mgonjwa wa Auto hushambulia mfumo wa kinga na kuharibu seli katika kongosho ambako insulin huzalishwa asilimia 10% ya watu wenye ungonjwa wa kisukari wanayo aina hii (Auto).
AINA YA PILI
Hii hutokea wakati mwili wako unakuwa sugu kwa insulin na sukari hujenga katika damu yako hii husababishwa na kuwa na sukari nyingi kwenye damu yako kuliko kawaida.
CHANZO CHA UGONJWA SUKARI
Viko vyanzo vingi mbalimbali vya sukari
1. Shinikizo la damu (B.P)
2. Viwango vya juu vya triglyceride (mafuta)
3. Lishe yenye mafuta mengi na wanga
4. Utumiaji mkubwa wa pombe kupita kiasi
5. Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
6. Mtindo wa maisha usiofaa kiafya
7. Uzito na unene uliozidi
8. Kutofanya mazoezi
9. Umri
10. Kurith
UNAJUAJE KUWA UNADALILI ZA KISUKARI
1. Kusikia njaa mara kwa mara
2. Kusikia kiu mara kwa mara
3. Kupungua uzito
4. Maono machafu
5. Uchovu mara kwa mara
6. Ukipata kidonda hakiponi
7. Kushuka kwa kinga mwili
DALILI ZA KISUKARI KWA MWANAUME
Mbali na dalili za jumla za ugonjwa wa sukari wanaume wenye tatizo hilo wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa uume hushindwa kusimama misuri hulegea na kusinyaa, maumivu ya mgongo, kiuno, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kupata choo kama cha mbuzi
DALILI ZA WANAWAKE
Wanawake wenye ugonjwa wa sukari wanaweza pia kuwa na dalili kama vile maambukizi kwa njia ya mkojo (U.T.I) maambukizi ya gonzi kukakamaa
TIBA YA MAGONJWA YA SUKARI
Ugonjwa wa sukari unatibika bila kujali ni mda gani umepata hilo tatizo wengi wamekata tama na kuwa wabishi amini tatizo hili linatibika vizuri sana wengi wemepona.
Tumia dawa ya SUPER-NHESHAambayo ni dawa ya miti shamba yaani (asilia) ambayo humfanya mtu kupona na kuimalika kabisa.
Tutakuelekeza pia mfumo wa mtindo wa maisha utakao takiwa kutumia ili kutoluhusu tatizo hilo kurudi tena.
BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO/KANISANI NJIA PANDA YA KWENDA SINZA SIMU: 0652 102 152/0788 330 105/ 0755 684 297 NYOTE MNAKARIBISHWA PIA TUNATUMA MIKOANI WHATAPPS NO 0652 102 152






















