Friday, 16 April 2021

Majaliwa: Watendaji Jiepusheni Na Rushwa


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watendaji wajiepushe na vitendo vya kuomba rushwa na urasimu usiokuwa wa lazima katika kuwahudumia wawekezaji ili kujenga imani baina ya sekta binafsi na sekta ya umma

Pia, Waziri Mkuu amezitaka Wizara na taasisi zote zinazohudumia wawekezaji kuhakikisha wanawezesha wawekezaji katika maeneo yao kwa kutoa huduma na taarifa muhimu kwa wakati.

Ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Aprili 16, 2021) wakati akihitimisha hoja ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka wa 2021/2022 mwaka wa Fedha 2021/2022, Bungeni jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema tarehe 6 Aprili 2021, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan Tanzania akiwaapisha Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu na Wakuu wa baadhi ya Taasisi za Serikali alisisitiza masuala mbalimbali ikiwemo uwekezaji na vibali vya kazi.

“Mheshimiwa Rais aliielekeza Ofisi ya Waziri Mkuu kuimarisha huduma za pamoja (One Stop Centre), kushughulikia malalamiko kuhusu kodi, kuondoa vikwazo katika uwekezaji, kuhamasisha uwekezaji kupitia mazungumzo, ushawishi, kudhibiti rushwa na kuondoa urasimu kwenye maombi ya vibali vya kazi”.

Amesema maelekezo hayo ya Mheshimiwa Rais yenye kujali maslahi mapana ya nchi hii yalikwenda sambamba na uamuzi wake wa tarehe 31 Machi 2021 wa kuunda rasmi Wizara ya Uwekezaji chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa lengo la kuhakikisha kuwa Wizara hiyo inasimamia kikamilifu masuala ya uwekezaji.

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kueleza hatua mbalimbali za utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia kuhusu Wizara ya Uwekezaji ambazo tayari zimechukuliwa kuwa ni pamoja na pamoja na kuandaa Muundo wa Wizara ambao utaainisha majukumu na mgawanyo wa Idara na Taasisi zitakazokuwa chini ya uwekezaji.

“Hatua ya pili ni kupitia Sera ya Uwekezaji ya mwaka 1996 na Sheria ya Uwekezaji ya mwaka 1997 ili kubainisha maeneo yenye kuhitaji maboresho ambapo tayari tathmini ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996 imekamilika na kuandaa Mkakati wa Kitaifa wa Maendeleo ya Uwekezaji ili kuimarisha uratibu, usimamizi, uhamasishaji na ufuatiliaji wa masuala ya uwekezaji nchini”.

Waziri Mkuu amesema kukamilika kwa hatua hizo kutaiwezesha Serikali kushiriki kikamilifu katika mikutano na majadiliano ya jumuiya za kikanda yanayohusu masuala ya uwekezaji ikiwemo maandalizi ya Sera ya Uwekezaji ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Pia, Waziri Mkuu ameongeza kuwa hatua hizo zitaiwezesha Serikali kushiriki katika utungaji wa Sera za Uwekezaji kwa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na Itifaki ya Uwekezaji ya Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika.

“Kujenga  mazingira rafiki ya uwekezaji na uchumi shindani nchini kwa kutekeleza programu mbalimbali za kuimarisha mazingira wezeshi ya biashara na uwekezaji kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi na kuandaa mfumo wa kielektroniki wa kupokea na kushughulikia malalamiko ya wawekezaji (Online Investors Feedback Platform)”.

“Kutatua changamoto za wafanyabiashara kupitia Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) kwa kuratibu majadiliano ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, kutoa elimu na hamasa kuhusu huduma zitolewazo kwenye Kituo cha Huduma za Mahala Pamoja (One Stop Facilitation Centre-OSFC).”

Amesema kupitia hatua hizo, Serikali itaweza kuimarisha mifumo ya usajili wa miradi na kutoa Cheti cha Vivutio (Certificate of Incentives), kuunganisha mifumo inayotumika TIC na makao makuu ya Taasisi na kuboresha mfumo wa kuchakata rufaa za vibali vya kazi na ukaazi kwa njia ya mtandao.

“Nitumie fursa hii tena kuwakumbusha watendaji wenzangu wakiwemo Waheshimiwa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu kuhakikisha kuwa muundo na mifumo ya masuala ya uwekezaji inakamilika ndani ya muda ulioelekezwa na Mheshimiwa Rais”.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,



Share:

Waziri Mkuu Awatoa Wasiwasi Watanzania ......Ni Kuhusu Mfumo Wa Kuyaendeleza Makao Makuu Ya Nchi Dodoma


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewatoa hofu Watanzania kuhusu kuendelezwa kwa Makao Makuu ya nchi Dodoma kwa kuwaeleza kwamba Serikali imeweka mfumo mzuri utakaohakikisha yanajengwa kuendana na mipango ya maendeleo ya Jiji la Dodoma.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Aprili 16, 2021) wakati akihitimisha hoja ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka wa fedha 2021/2022, Bungeni jijini Dodoma.

Amesema mfumo huo, unahusisha Kikosi Kazi cha Taifa cha Kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma ambacho kinajumuisha wajumbe kutoka Wizara na Taasisi za Serikali. “Kikosi Kazi hicho kina jukumu la kushauri namna bora ya kupanga na kuendeleza Mji wa Serikali na Jiji la Dodoma kwa ujumla”.

Waziri Mkuu amesema utekelezaji huo, unahusisha miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na maji, kiwanja cha ndege, barabara na utoaji wa huduma za jamii. “Niwahakikishie Watanzania wote kuwa Dodoma inaendelea kujengwa”.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wabunge na Watanzania warejee kauli ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kuwa waendelee kushikamana, kusimama na kuwa wamoja kama taifa, kuoneshana upendo na undugu, kudumisha amani yetu, kuenzi utu wetu, uzalendo wetu, utanzania wetu na kutazama mbele kwa matumaini na kujiamini.

“Huu si wakati wa kunyoosheana vidole bali ni wakati wa kushikana mikono na kusonga mbele. Kwa msingi huo, tuendelee kudumisha na kuilinda amani ya nchi yetu ikiwa ni sehemu ya kuenzi jitihada za waasisi wa Taifa hili. Tutumie muda mwingi kwa kazi zaidi za kujipatia kipato na kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja.”

Vilevile, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwatakia Waislamu wote nchini mfungo mwema na wenye mafanikio wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ulioanza katikati ya wiki hii. “Nitoe rai kwamba tutumie kipindi hiki kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kuibariki nchi yetu na watu wake”.

“Kadhalika, tumuombe Mwenyezi Mungu awajalie viongozi wetu hekima na busara ili waendelee kuliongoza Taifa letu kwa haki, kujenga umoja na mshikamano, kudumisha amani katika nchi yetu pamoja na kuimarisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii”.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

WATANZANIA TUMUUNGE MKONO RAIS WETU MHE.SAMIA SULUHU-BW.FESTO

 

Kijana Mzalendo Bw.Frank Festo (Kulia)akiwa pamoja na rais wa Chuo cha Bahari (DMI) Bw.Salim Awali wakionesha stika yenye ujumbe "MIMI NASIMAMA NA MAMA SAMIA,WEWE JE".

Kijana Mzalendo Bw.Frank Festo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam baada ya kukutana kwaajili ya uzinduzi wa stika yenye ujumbe "MIMI NASIMAMA NA MAMA SAMIA,WEWE JE".

(Picha na Emmanuel Mbatilo)


NA EMMANUEL MBATILO

Ili kuweza kuunga mkono Juhudi za Rais Mhe.Samia Suluhu Hassani, Kijana Mzalendo Bw.Frank Festo amezindua stika yenye ujumbe "MIMI NASIMAMA NA MAMA SAMIA,WEWE JE". Lengo kuhamasisha mshikamano, umoja, upendo, amani na furaha kama kipaumbele cha Rais Mhe.Samia Suluhu.

Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es Salaam, Bw.Festo amesema sote kwa pamoja tunapaswa kumuunga mkono ili kuweza kufanikisha kuiongoza Tanzania katika amani na upendo tulionayo toka zamani.

"Tusikae pembeni kwa kuchungulia na kumsikiliza eti huyu mama ataweza?.Kila mmoja awajibike kwa nafasi yake ipasavyo ndiyo njia pekee ya kumuunga mkono Mama yetu mpendwa". Amesema Bw.Festo.

Aidha Bw.Festo amesema stika hiyo itasambazwa nchi nzima kupitia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii, vyombo vya usafiri, kutembelea ofisi za Umma na Binafsi,Bunge, Shule,Vyuo na nyumba za ibada ikiwa lengo ni kuhakikisha ujumbe huo unamfikia kila mtanzania mahali popote alipo.

Pamoja na hayo Bw.Festo amesema kuwa pamoja na taifa letu kujaliwa rasilimali nyingi, rasilimali kubwa tuliokuwa nayo ni amani na hatuna mbadala wa amani.

Kwa upande wake rais wa Chuo cha Bahari (DMI) Bw.Salim Awali amewasihi viongozi ambao wamepewa dhamana serikalini kufanya kazi kwa bidii bila kumkatisha tamaa Rais kwa masirahi ya nchi yetu.

"Sisi kama vijana tunamuahidi Rais wetu tutaliendeleza taifa hili kwa umoja na kumshauri ni nini kifanyike ili tuweze kufika sehemu ambayo tunaitaka kwasababu kiongozi wetu Rais Mhe.Samia ni mtu ambaye anapokea ushauri na ni mtu ambaye msikivu". Amesema Bw.Awali.

Share:

MBUNGE NEEMA LUNGANGIRA AIKUMBUSHA SERIKALI KUHUSU UMUHIMU WA LISHE BORA KWA MAENDELEO YA TAIFA

 


MBUNGE wa Viti Maalumu kupitia Asasi za Kiraia (NGOs) Mhe Neema Lugangira ameishauri Ofisi ya Waziri Mkuu kutoa mwelekezo wa mapambano dhidi ya udumavu na utapiamlo wa aina zote na kuzikaribisha rasmi Sekta ya Asasi za Kiraia kuandaa mpango kazi kwa kushirikiana nao kama ilivyofanya kwa Sekta Binafsi.

Alitoa ushauri huo Bungeni Jijini Dodoma wakati akichangia kwenye Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ambapo Mh Neema Lugangira alijikita kwenye mambo mawili ya Lishe na Sekta ya Asasi za Kiraia (NGOs) kwa kutoa mchango wake.

Akizungumza wakati akichangia mambo hayo Mbunge Neema Lugangira aliipongeza Serikali kwa jitihada kubwa inayofanya kwa kuboresha hali ya lishe hapa nchini na kutokomeza udumavu na aina yoze utapiamlo.

“Napenda kupongeza jitihada kubwa zilizofanywa na Rais Samia Suluhu wakati akiwa Makamu wa Rais ambaye ilipelekea kumuagiza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamiseni kusaini mikataba ya Lishe kwa niaba yake na Wakuu wa Mikoa. Hivyohivyo namshukuru sana Mhe Waziri Mkuu Kasim Majaliwa na Mhe Waziri Jenista Mhagama kwa namna ambayo wanavyoendelea kuratibu Masuala ya Lishe ambayo yanaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu” Alisema

Mbunge Neema Lugangira alisema wanafanya hivyo kwa kupitia maeneo manne ambayo ni (1) kusimamia utekelezaji wa mpango jumuishi wa Lishe wa Kitaifa; (2) kusimamia  vuguvugu la uongezeji kasi ya kuboresha hali ya lishe duniani; (3) kujuimisha jumbe la lishe kwenye jumbe Mbio za Mwenge wa Uhuru; na (4) katika kutekeleza vipaumbele vya lishe vilivyowekwa kwenye mpango wa maendeleo ya Taifa.

“Kipekee napenda kukishukuru Chama changu, Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwa Chama pekee ambacho kimeweka kipaumbele kikubwa  kwenye lishe na mnaweza kurejea ukurasa wa 7,40,139 hadi 141 ambapo Chama hicho kimeweka malengo madhubuti ya namna gani itaekeleza serikali ya kuboresha hali ya lishe nchini na kutokomeza udumavu na aina zote za utapiamlo” Alisema

Hata hivyo Mbunge Neema Lugangira alisema hivi sasa Tanzania kuna changamoto kubwa sana ya Lishe Duni inayopelekea kutuweka kwenye hatari ya kutokuwa kizazi chenye nguvu kazi shindani kwa siku zijazo.

“Wengi tunaongelea ajira lakini ikiwa watoto wana lishe duni na wapo na udumavu hivyo nguvu kazi na kizazi cha kesho kitapatikana vipi ndio maana ya kuipa kipaumbele suala la Lishe hivyo nitumie fursa hii kuikumbusha Ofisi ya Waziri Mkuu itamke rasmi ina maoni gani kuhusu janga hilo la lishe bora” Alisema

Alienda mbali zaidi na kueleza kwamba pia Ofisi ya Waziri Mkuu itakwenda kufanya nini ili ihakikishe kwamba Sekta na Wizara zote zinakwenda kuhusika na suala hilo na wanakwenda kutekeleza yale yote yaliyoandikwa kwenye Ilani ya CCM.
Share:

Jobs at NGARA District Council

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Various Jobs at NGARA District Council April, 2021. Ngara District is one of the eight districts of the Kagera Region of Tanzania. It is bordered to the north by Karagwe District, to the east by Biharamulo District, to the south by the Kigoma Region, to the northeast by Muleba District and to the we   […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

WAFANYABIASHARA WAOMBWA KUWA NA HURUMA MWEZI WA RAMADHAN

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo

**

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaomba wafanyabiashara nawatoa huduma mbalimbali mkoani humo kutopandisha gharama za mazao na mahitaji mbalimbali katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan ili kuwahurumia Waislamu wanaoendelea na mfungo wa Mwezi wa Ramadhan.

“Niwaombe sana wafanyabiashara na watoa huduma, hiki sio kipindi cha kujineemesha ni kipindi cha tafakari, ni kipindi cha kuwa Pamoja, kipindi cha kuhurumiana, kipindi cha sadaka, sio kipindi cha kuona kwamba sasa ni kipindi cha kupata mapato zaidi, niwaombe msiongeze bei za vyakula, niwaombe msiongeze bei za huduma mbalimbali, mwaka jana mlinisikiliza, hali ilikuwa nzuri, ni matarajio yangu hata mwaka huu pia, bei za vyakula sokoni, viazi, mihogo, sukari na bidhaa nyingine hazitapanda,”

“Lakini kama itatokea watu wataokwenda kinyume, niwatahadharishe, serikali ipo na itafuatilia kila mahali, ili tusitese watu ambao tayari wanajitesa, mtu anajinyima, anashinda njaa, anakula jioni ile na wewe unaamua kumtesa zaidi, kuwabebesha mzigo mkubwa zaidi, hii haikubaliki, tuhurumiane, tupendane, bila ya shaka ujumbe huu utafika kwa kila mwananchi na kila mwanarukwa,” alisisitiza.

Mh. Wangabo alitoa ujumbe huo tarehe 14.5.2021 ambapo Waislamu kote nchini walikuwa wameuanza mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani kwa kipindi cha siku 30 ama 29 kutemea mwandamo wa mwezi.

Share:

Field Officers (18 Posts) at Ifakara Health Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Summary Position:          Field Officers (18 Posts) Reports to:  Research Officer/Project Leader Work station:    Tanga District (Tanga Municipality), Kaliua District (Tabora) and  Sengerema District (Mwanza) Apply by: April 23rd 2021 Institute overview  Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Technology Procurement & Asset Manager at NBC

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Job Summary The role is responsible to ensure that new and existing IT Assets and Services are procured and renewed cost-effectively. It will also ensure […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Programme Finance Assistant at UNCDF

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Eligibility criteriaCandidate age: between 18 and 29 throughout the entire duration of their assignment. Applicants must be nationals of or legal residents in the country of assignment.  Description of task Assist in financial management activities of the office – 25% Support the preparation of the various financial reports based on our reporting calendar. Ensure that […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Finance and Admin Manager at REDESO

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

About REDESO: Relief to Development Society (REDESO) is a Tanzanian National Non-Governmental Organization dully registered under the Society Ordinance of 1954 with registration number S.O. No. 9459. The organization is engaged in Humanitarian and Community Development projects implemented under the humanitarian to development nexus concept. In the areas of our operation, Local Government has been […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Deputy Director Finance at International Rescue Committee

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Requisition ID: req14307 Job Title: Deputy Director Finance Sector: Finance Employment Category: Fixed Term Employment Type: Full-Time Open to Expatriates: Yes Location: Dar es Salaam, Tanzania Job Description The International Rescue Committee responds to the world’s worst humanitarian crises and helps people whose lives and livelihoods are shattered by conflict and disaster to survive, recover and gain control of their future. We […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MKAGUZI MKUU WA MIGODI AIDHINISHA MPANGO WA UCHIMBAJI MADINI WA GGML MWAKA 2021


Mkurugenzi Mtendaji wa GGML Bw.  Richard Jordinson

Na Mwandishi wetu

Geita Gold Mining Limited (GGML) imepokea ruhusa ya mpango wa uchimbaji madini wa mwaka 2021 unaohusisha uchimbaji wa wazi na wa chini kwa chini.

Mkaguzi Mkuu wa Migodi yote nchini Dkt Abdul Rahman Mwanga ameruhusu mpango huo baada ya GGML kupeleka nyaraka zote Tume ya Madini na kupatiwa vibali.

Kufuatia ruhusa hiyo, GGML sasa inatarajiwa kufanya shughuli zake za uchimbaji kama zinavyoainishwa kwenye kijitabu kilichokamilika na kutiwa saini na Mkaguzi Mkuu wa migodi yote nchini.

GGML inapaswa pia kuendesha shughuli zake kwa kuzingatia masharti na miongozo ya sheria za nchi ya Tanzania.

Vile vile, Kampuni itaweka taarifa mpya kila mwaka katika mpango wa uchimbaji uliothibitishwa na kwa kuzingatia mabadiliko makubwa katika shughuli za uchimbaji.

Akizungumzia ruhusa hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa GGML Bw. Richard Jordinson ameipongeza serikali kwa kuendeleza ushirikiano wa miaka mingi na kufafanua kuwa GGML sasa itapata fursa ya kupanua wigo zaidi wa uzalishaji na kutimiza matarajio ya wadau wake.

“Kupata kibali cha mpango huu wa uchimbaji ni ushahidi wa rekodi yetu nzuri ya uchimbaji madini nchini. Hii inaonyesha pia imani iliyonayo Serikali kwa kampuni yetu kama mdau wa maendeleo,” alisema Bw Jordinson.

Miradi inayotajwa katika mpango wa uchimbaji wa GGML ni pamoja na Mradi wa Nyamulilima utakaohusisha maeneo ya kituo cha nane (8), Star and Comet, Xanadu, Selous, Mabe pamoja na Roberts.

Uchimbaji wa wazi katika eneo la Nyamulilima unatarajiwa kuongeza uzalishaji dhahabu katika mgodi wa GGML ambapo uchimbaji unaweza kuendelea hadi mwaka 2027.

Ruhusa ya kuanza shughuli za uchimbaji katika eneo la Nyamulilima ni habari njema kwa wadau wetu, wafanyakazi na wakandarasi.

Inatoa pia fursa nyingi kwa jamii inayotuzunguka kufaidika kutokana na shughuli za AngloGold Ashanti. Tunatarajia kuendelea kufanya uwekezaji kwenye jamii inayotuzunguka kwa kuwa hiyo ni mojawapo ya tunu zetu,” aliongeza Bw Jordinson.

Hivi karibuni GGML iliibuka mshindi wa jumla wa kampuni zinazofanya vizuri kwenye sekta ya madini nchini Tanzania kwa mwaka 2019/2020. GGML iliibuka mshindi katika vipengele vya Wajibu wa Kampuni kwa Jamii (CSR), Utunzaji mazingira na usalama, ukusanyaji wa mapato ya Serikali (kodi) pamoja na uwezeshaji wa wazawa.


Share:

Inventory and Asset Assistant at ICAP

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job no: 495106 Work type: Regular Full-Time Location: Tanzania – Dar es Salam Categories: Finance/Administration ICAP at Columbia University, a global health leader situated within the Columbia University Mailman School of Public Health in New York City, seeks Inventory and Asset Assistant  to be based in Dar es Salaam, Tanzania. Inventory and Asset Assistant with safety, efficiency and customer […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Information System (IS) Specialist at Médecins Sans Frontières

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

   JOB VACANCY – INFORMATION SYSTEM (IS) SPECIALIST     Médecins Sans Frontières (MSF) is an international, independent, medical humanitarian organisation that delivers emergency aid to people affected by armed conflict, epidemics, natural disasters and exclusion from healthcare. MSF offers assistance to people based on need, irrespective of race, religion, gender or political affiliation. MSF […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Commercial Specialist at U.S. Embassy Dar es Salaam

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The U.S. Mission in Dar es Salaam is seeking eligible and Qualified applicants for the position below. Position Title: Commercial Specialist Vacancy Number: DaresSalaam-2021 -018   Duties 25% – Trade facilitation through business matchmaking, including identifying potential partners (incl., distributors, agents, etc.) The incumbent identifies potential distributors, representatives, joint venture partners, or other professional contacts […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Mechanic Cum Driver at HJFMRI

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Join us in our efforts to end the HIV epidemic in Tanzania. Be part of the winning team to advance global health and save the lives of people living with HIV. About HJFMRI Tanzania Program The Walter Reed Program Tanzania (WRP-T) is a collaborative effort that supports PEPFAR-funded HIV prevention and treatment activities in the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Financial Analyst at HJFMRI

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Join us in our efforts to end the HIV epidemic in Tanzania. Be part of the winning team to advance global health and save the lives of people living with HIV. About HJFMRI Tanzania Program The Walter Reed Program Tanzania (WRP-T) is a collaborative effort that supports PEPFAR-funded HIV prevention and treatment activities in the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger