Sunday, 5 April 2020

WABUNGE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI WATEMBELEA MPAKA WA KENYA NA TANZANIA KUONA HATUA ZINAZOCHUKULIWA

 Mwenyekiti wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Abdulla Makame akizungumza mara baada ya wabunge wa bunge la Afrika Mashariki kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wametembelea mpaka wa Kenya na Tanzania eneo la Horohoro –Lungalunga kuangalia umeathirika vipi kutokana na janga la Virusi vya Corona na hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa kuweza kukabiliana nao huku wakiridhishwa na hatua zinazochukuliwa kulia ni Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure
  Mwenyekiti wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Abdulla Makame akisisitiza jambo wakati walipotembelea mpaka wa Kenya na Tanzania eneo la Horohoro ikiwemo upande wa pili wa nchi ya Kenya
 Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure akifuatilia jambo wakati wa ziara hiyo
 Sehemu ya watumishi wa TRA mkoa wa Tanga wakifuatilia matukio mbalimbali
 Mwenyekiti wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Abdulla Makame kushoto akisalimiana na Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure wakati walipoingia kwenye Kituo cha Forodha Horohoro


 WABUNGE wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Abdulla
Makame na Mhandisi Mohamed Habibu Mnyaa
 WABUNGE wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Abdulla Makame na Mhandisi Mohamed Habibu Mnyaa  katikati wakiangalia bidhaa mbalimbali mpakani hapo
 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhandisi Mohamed Habibu Mnyaa katikati akinawa na santize kabla ya kuingia kwenye ofisi mbalimbali zilizopo mpakani hapo
 Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure kulia akiwa na Mbunge  wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Abdulla Makame wakitoka nje mara baada ya kufanya ziara yao
 Wakipata picha ya pamoja mara baada ya kutembelea eneo hilo
 Wakiwa kwenye picha ya pamoja na Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki


WABUNGE wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wametembelea mpaka wa Kenya na Tanzania eneo la Horohoro –Lungalunga kuangalia umeathirika vipi kutokana na janga la Virusi vya Corona na hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa kuweza kukabiliana nao huku wakiridhishwa na hatua zinazochukuliwa.

Mpaka wa Horohoro upo wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga na Kenya ambao umekuwa ukitumiwa na wananchi wa nchi hizo mbili kuweza kuvuka upande mmoja hadi mwengine lakini hivi sasa inaelezwa huwezi kuvuka bila kuwekwa chini ya uangalizi kwa kipindi cha siku 14.

Akizungumza mara baada ya kutembelea eneo hilo  hivi karibuni Mwenyekiti wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Abdulla Makame ambayo pia walikuwa wameambatana na Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure huku akizipongeza mamlaka zilizopo mpakani hapo kutokana na hatua inazochukua kukabiliana na janga hilo lakini kwa kuzingatia taratibu zilizotolewa na Serikali.

Mwenyekiti huyo pia aliwapongeza watumishi wanaofanya kazi kwenye sekta ya afya nchini kutokana na kuwa mstari wa mbele kutoa huduma ikiwemo kuweka maisha yao rehani kuhakikihs wanatuokoa na janga hilo hatari ambalo limekuwa tishio kubwa duniani.

Aidha alisema mpaka sasa nchi haijafunga mipaka yake na watu wanaendeela kuvuka lakini kwa tahadhari ya afya wanaovuka wataendelea kuwekwa chini ya uangalizi kwa siku 14 ili waweze kujiridhika kama ana maambukizi au la .

“Mpaka sasa hapa kwetu nchi haijafunga mipaka yake sababu serikali inataka bidhaa muhimu ikiwemo vifaa tiba kwa kipindi hiki vinahitajika vitaendelea kuvuka lakini watu wanaovuka watakwenda karatini”Alisema Dkt Abdulla.

Mwenyekiti huyo alisema kwamba sio kwamba watu wanazuiwa ili waonewe wanachoifanya ni kupambana na janga la kitaifa ambalo limefanya mataifa makubwa watu wanalia, wanakufa hali ni hatari na lazima hatua hizo zichukuliwe.

“Lakini pia tumeambiwa hapa kwamba abiria wakivuka wanakaa karantine siku 14 katika uangalizi kabla ya kuvuka tumeonyeshwaa maeneo na mengine tumeambiwea yapo Tanga mjini kabla ya kuendelea na safari zao hilo zoezi lilikuwa ni kuangalia abiria”Alisema

“Madereva walikuwa na utaratibu tofauti kwa sababu wanapeleka mizigo na walisema hawataki mizigo isivuke kutokana na baadhi yake ni vifaa ikiwemo tiba na vyakula ambavyo vinahitajika kila siku na kuweka maisha yakawe sawasawa “Alisema

Mwenyekiti huyo alisema kwamba lakini waraka namba 2 umetoka na kwa sasa madereva nao watakuwa wakikaa karantine huo waraka utaanza kutekeleza kutokana na hilo wameona maelekezo yanazidi kuwa makali lakini pamoja na ukali wanasema mipaka bado ipo wazi na bidhaa muhimu zitaendelea kuvuka.

Hata hivyo alisema watatumia utaratibu mwengine kwamba ama gari zishushe mizigo mipakani ipandishwe magari mengine au gari ije ibadilishe madereva mipakani na kuwekwa dawa na madereva kubaki kwenye nchi zao.

“Kimsingi maelekezo ya serikali yanaendelea kufuatwa na mpaka sasa kwenye mpaka huo hajapatikana mgonjwa yoyote wa Corona lakini tumeambiwa wapo karatine watu 47 na watu wanne walishukiwa kuonyesha dalili walipimwa wakawa hawana na waliruhusiwa”Alisema

Awali akizungumza kwa upande wake Mbunge mwengine wa Bunge hilo Mhandisi Mohamed Habibu Mnyaa alisema wamefika eneo hilo kwa lengo la kuona uelewa upo kiasi gani na taratibu zilizotangazwa na serikali za kujilinda na virusi vya Corona umeeleweka kiasi gani na watu wanayafuata kwa kiasi gani.

Alisema wao kama wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki wamelazimika wote kufanya kazi ndani ya nchi zao kushirikiana na serikali na wananchi kuhusu kupiga vita maradhi ya virusi vya Corona kwa hiyoi kwa upande wa Tanzania wamegawana vikundi vya watu wawili wawili maeneo mengine mmoja kutembelea mipaka mbalimbali iliyopo nchini lengo kusaidia uelewa wa wananchi kupiga vita maradhi hayo.


 Naye kwa upande wake Afisa Afya Mfawidhi Huruma Kimaro alisema katika mpaka huo hakuna mtu yoyote anayepita na wanaofika hapo wanapelekwa karatini na mpaka sasa watu 47 wapo karatine huku akieleza kwamba walipata washukiwa wanne walipopelekwa maabara walikuwa hawajaambukizwa waliwaruhusu na kuwapa maelekezo ikiwemo kutoa ushauri kwao kwa kuendelea kuwa mabalozi wazuri.
Share:

Trump Awataka Wamarekani kujiandaa kwa idadi ya kutisha sana ya vifo vya Corona

Rais wa Marekani Donald Trump amewaonya Wamarekani kujiandaa kwa idadi ya kutisha sana ya vifo kutokana na virusi vya corona katika siku chache zijazo. 

Trump amesema Marekani inaingia katika kipindi ambacho idadi ya vifo itapanda kwa kasi. 

Hata hivyo, Rais huyo amesema Marekani haiwezi kuendelea kusitisha shughuli zake milele akiongeza kuwa itafika wakati ambao maamuzi magumu yatafanywa.

 Wakati visa vya maambukizi ya COVID-19 nchini Marekani vikithibitishwa kupindukia 300,000 kukiwa na zaidi ya vifo 8,300, kuna habari za kutia moyo nchini Italia na Uhispania ambako idadi ya imeanza kupungua. 

Sasa kuna visa milioni 1.17 vya maambukizi vilivyothibitishwa kote duniani na kumekuwa na vifo 63, 437 tangu mlipuko wa virusi hivyo ulipoanza nchini China mwaka jana. 

DW


Share:

Masanja Mkandamizaji Aitikia Wito wa DC Na Kuomba Msamaha

Baada ya kupewa masaa 72 awe ameripoti kwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi hatimaye jana mchekeshaji Emmanuel Mgaya ‘Masanja’aliitikia wito na kuomba radhi kwa watanzania kutokana video clip yake ya mahojiano na wananchi juu ya Corona.

DC Katambi alimpa Masanja siku tatu kuripoti ofisini kwake ili kuhojiwa na kueleza sababu ya yeye kurikodi kipindi chake akiwahoji wananchi wa Dodoma maana ya Covid19 jambo ambalo kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya lililenga kupotosha kwamba wananchi wake hawana uelewa na ugonjwa huo.

Kufuatia wito huo siku hiyo hiyo Masanja aliripoti ofisi ya DC na kuelekezwa kuja jana ambapo aliripoti na kuhojiwa na Kamati ya Usalama ya Wilaya hiyo aliomba msamaha na kuahidi kutumia nafasi yake kushirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo wa Corona.

Akizungumza na wandishi wa habari baada ya kumaliza mahojiano, Masanja amempongeza DC Katambi kwa kuwa mwepesi wa kugundua kuwa kulikua na shida kwenye kipindi chake alichorusha jambo linaonesha kweli yeye ni kijana na anaenda na spidi ya Rais Magufuli katika kuwatumikia watanzania.

" Niombe radhi kwa kueleweka vibaya lengo la kipindi chetu lilikua kuelimisha na siyo kuleta mzaha, namshukuru Mkuu kwa wito wake huu ambao umenisaidia pia kwa namna moja ama nyingine kujua wapi nilipoteleza.

Kama Taifa tunapita kwenye kipindi kigumu kutokana na maambukizi ya ugonjwa huu hivyo tuendelee kuchukua tahadhari zote kama tunavyoelekezwa na wataalamu wetu ili tuzidi kuwa salama," Alisema Masanja.

Mchekeshaji huyo ambaye pia ni Mchungaji amemuahidi DC Katambi kuwa atatumia kipawa chake cha kuhubiri pia kuhamasisha watanzania kutumia vitakasa mikono na kufuata masharti yote ambayo yanatolewa na viongozi.

Nae DC Katambi amesema hana tatizo binafsi na Masanja wala kituo cha DW ambacho muigizaji huyo anafanyia kazi bali walimuita kwa ajili ya kuwekana sawa.


Share:

Atiwa Mbaroni kwa Kufungua ukurasa wa Corona Facebook

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro limemtia mbaroni Awadhi Luguya (24), mkazi wa Mazimbu, Manispaa ya Morogoro kwa tuhuma za kufungua ukurasa katika mtandao wa kijamii wa Facebook na kuupatia jina la Coronavirus Tanzania.

Taarifa za Jeshi hilo zinaeleza kuwa, kupitia ukurasa huo, Awadhi alikuwa akisambaza taarifa zisizo rasmi ambazo zimejaa upotoshaji kuhusu ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona (COVID-19).

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa amesema mtuhumiwa alikamatwa Aprili 1, mwaka huu, majira ya saa 11 jioni katika eneo la Mazimbu.

Amesema polisi walipata taarifa kutoka kwa wananchi na kupitia mitandao ya kijamii kuwa kijana huyo amefungua ukurasa huo na anautumia kutoa taarifa ambazo sio rasmi, na zilizojaa upotoshaji mkubwa kwa watu kuhusu Corona.

“Tumemkamata na simu zake zote. Anaendelea kuhojiwa na atafikishwa mahakamani kwa makosa ya matumizi mabaya ya mtandao,” amesema Mutafungwa.


Share:

IKUNGI YATEMBEA NA FALSAFA YA RAIS JPM KWA ASILIMIA 100

 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Rehema Nchimbi mwenye miwani akiongea na akina mama wafanya biashara ya viazi lishe   wa Kitongoji cha Kideka kijiji cha Nkunikana kuhusu kuchukua tahadhari ya kujikinga na Corona-Covid 19 kulia Mkuu wa Wilaya ya Ikungi  Edward Mpogolo kushoto Mkurugenzi Mtendaji Justice Kijazi
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi(mwenye miwani) akitoa   maelekezo  ya namna bora ya kufanya kazi katika kikundi kwa  wakikundi   cha Jitume Vijana chenye vijana kumi katika kijiji Ikungi, ambacho pia kilichopata mkopo wa shilingi milioni 25 kwa ajili ya mradi wa kutengeneza matofali ya sementi kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi.. Mkopo huo ni Mkakati iliyojiwekea Halmashauri ya Ikungi wa kudhibiti na kupambana na ugonjwa wa Covid-19 kwa kutoa mikopo hiyo isiyo na riba kwa vijana ili waweze kujitenga na kujifungia na kuendelea na uzalishaji  mifuko hiyo.Nyuma yake Kulia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Justice Kijazi, pembeni  kulia (mwenye koti jeusi) ni Mkuu wa wilaya ya Ikungi Edward Mpogolo
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi(mwenye miwani) akipata maelekezo  kutoka kwa  katibu wa kikundi cha The New Bright Future - Petro Mwacha  jinsi mashine ya kutengenezea mifuko mbadala  ya kikundi cha The New Bright Future chenye vijana  10 waliopewa mkopo wa Milioni 25 na Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mara  baada ya kuzindua kiwanda hicho. Mkopo huo  ni Mkakati iliyojiwekea Halmashauri ya Ikungi wa kudhibiti na kupambana na ugonjwa wa Covid-19 kwa kutoa mikopo hiyo isiyo na riba kwa vijana ili waweze kujitenga na kujifungia na kuendelea na uzalishaji  mifuko hiyo.Nyuma yake Kulia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Justice Kijazi, Kulia (mwenye koti jeusi) ni Mkuu wa wilaya ya Ikungi Edward Mpogolo

Mkuu wa Mkoa wa  Singida(mwenye Miwani) akiuliza  maswali kwa  vijana wanaotengeneza mifuko mbadala  ya kikundi cha The New Bright Future(mwenye koti jeusi ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Edward Mpogolo, Nyuma ya Mkuu wa Mkoa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Justice Kijazi

Na John Mapepele, Singida


Falsafa ya Rais John Pombe Magufuli ya kutaka wananchi wake kuchukua tahadhari zote zinazotolewa na wataalam wa afya za kudhibiti na kujikinga na ugonjwa, wa Covid-19, kumwomba Mungu na kuendelea kuchapa kazi ili kunusuru kupoteza maisha na kushuka kwa uchumi wa nchi yao zimetekelezwa kwa vitendo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida.

Akitekeleza falsafa hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Rehema Nchimbi amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Ikungi na kuzindua kiwanda cha kutengeneza mifuko mbadala katika Kijiji cha Siuyu Wilaya ya Ikungi.

Kiwanda hicho kilichoanzishwa kikundi cha New Bright Future chenye vijana 10 waliopata mkopo usio na riba wa shilingi milioni 25 na Mradi wa kutengeneza matofali ya sementi wa Kikundi cha Jitume Vijana chenye vijana 10 kwenye Kijiji Ikungi ambacho pia kimepata milioni 25 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi.

Ikiwa ni mkakati maalum wa kupambana na gonjwa la Covid-19 kwa kuwatenga na kuwafungia vijana kwenye uzalishaji wa bidhaa badala ya kuzagaa katika mikusanyiko isiyo ya lazima inayoweza kusambaza ugonjwa huo kirahisi.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Justice Kijazi, hadi sasa tayari Halmashauri imeshatoa jumla ya milioni 127 kwa wanufaika 78 ambapo inatarajia kutoa hadi milioni 150 kwenye mwaka huu wa fedha endapo makusanyo yatakuwa kama yalivyokadiriwa



Dkt. Nchimbi amepongeza mikakati inayofanywa na Halmashauri ya Ikungi kwa ubunifu na uratibu mzuri wa kutoa na kuelekeza mikopo kwenye miradi ya viwanda vya uzalishaji bidhaa.

Ambapo amesema kwamba mkoa huo umeendelea kuweka mkakati wa kudumu wa kujitenga na kujifungia katika maeneo mbalimbali ya uzalishaji ikiwa ni pamoja na viwandani ili kuepukana na kuenea kwa ugonjwa wa Covid-19 na kuongeza uzalishaji unaoendana na falsafa ya Mhe. Rais Magufuli wa kuchapa kazi kwa bidii na kuendelea kuzingatia maelekezo ya wataalam katika kipindi hiki.

Ameitaka Halmashauri ya Ikungi kutatua changamoto zote zinazokikabili kikundi cha The New Bright Future ili kiweze kuzalisha kikamilifu na kisaidiwe kupata masoko ya uhakika wa bidhaa zake ili fedha ya Serikali iliyotolewa isipotee bali iwe na tija hatimaye iweze kurejeshwa na kuwanufaisha wakopaji wengine

Aidha amezielekeza Halmashauri zote katika Mkoa wa Singida kuiga mfano wa Halmashauri ya Ikungi katika utoaji wa mikopo inayoelekeza katika uzalishaji wa bidhaa na viwanda na kupiga marufuku kutoa mikopo ya fedha na kwamba mikopo lazima itolewe kwa kasi kama kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 ili wanavikundi hao wajitenge na kuendelea na uzalishaji

Akiwa kwenye Soko maarufu la viazi lishe kwenye Kitongoji cha Kideka katika Kijiji cha Nkunikana aliwapongeza wafanyabiashara hao kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 kwa kuandaa miundombinu ya maji ili kunawa mikono kwa sabuni katika maji yanayotiririka wakati wote.

Mkuu huyo wa mkoa pia aliwataka wakulima wa viazi lishe kuendelea kulima kwa bidii ili wananchi wapate lishe bora kutokana na viazi hivyo na majani yake ambapo alisisitiza kuwa katika kipindi hiki ni muhimu kusanitaizi mikono na kusanitaizi afya zao

“Naelekeza wakulima waache visingizio nao waendelee kwenda mashambani kujitenga na kulima kwa bidii katika kipindi hiki ili waweze kupata mazao mengi na wakati huo huo watekeleze matakwa ya Serikali ya kujitenga na mikusanyiko isiyo ya lazima ambayo ingeweza kusababishia maambukizi endapo mmoja ana maambukizi.”



Dkt. Nchimbi amesema ugonjwa Covid-19 uwe ni chachu ya kufanya kazi kwa bidii za uzalishaji na kwamba viwanda hivyo viwe darasa maalum ya kutolea mafunzo hayo bila malipo kwa vijana wengine ili kuwapa maarifa kwa vijana wengi zaidi

Katika uzinduzi huo mkoa huo ulitoa kiasi cha shilingi milioni moja huku Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ikitoa kiasi cha shilingi milioni tano na kufanya jumla ya shilingi milioni 6 zilizoombwa na kikundi cha The New Bright Future kwa ajili ya kununua malighafi kupatikana.

Katika hatua nyengine Mkuu wa Mkoa alielekeza Serikali ya Wilaya ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kutumia jengo jingine la Kijiji cha Isuna katika Wilaya ya Ikungi ambalo ni mali ya Serikali kwa vikundi vya uzalishaji ambalo kwa sasa halitumiki kwa shughuli yoyote ile.

Akisoma hotuba mbele ya Mkuu wa Mkoa Katibu wa kikundi cha The New Bright Future Petro Mwacha ameishukuru Serikali kwa kuwapa mkopo huo na kusisitiza kuwa mradi huu umelenga kuunga mkono juhudi na kauli mbiu za Rais, John Pombe Magufuli za kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka 2025.

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Edward Mpogolo alisema Serikali ya Wilaya tayari imejipanga vizuri kujikinga na ugonjwa huo ambapo hadi sasa elimu ya ugonjwa wa Covid-19 kwenye maeneo mbalimbali inaendelea kutolewa.

Amesema Wilaya ya Ikungi ni miongoni mwa Wilaya ambazo zipo katikati ya nchi ya Tanzania ambapo barabara kuu inayounganisha mikoa na nchi mbalimbali na kwamba mwingiliano wa watu ni mkubwa, hivyo njia bora ya kukabiliana na ugonjwa huu ni wakuwatenga watu kwa kutumia mkakati maalum wa kuwapa mikopo ambayo itawafanya wananchi wajifungie na waendelee na uzalishaji huku wakichukua tahadhari zote za kujikinga zinazotolewa na wataalam wa afya.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili April 5














Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili 05 April 2020













Share:

Saturday, 4 April 2020

ALIYEFUNGUA AKAUNTI FACEBOOK YENYE JINA 'CORONA VIRUS TANZANIA' AKAMATWA KWA UPOTOSHAJI


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro (SACP) Willbroad Mutafungwa akizungumza na waandishi wa habari. Mezani ni simu zilizokuwa zinatumiwa na mtuhumiwa Awadhi Lugoya kusambaza taarifa za upotoshaji kuhusu Corona.


Na Jackline Lolah Minja - Malunde 1 blog
Mkazi wa Mtaa wa Mazimbu Manispaa ya Morogoro Awadhi Lugoya anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani morogoro kwa tuhuma ya matumizi mabaya ya mitandao kwa kufungua akaunti kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook inayofahamika kwa jina CORONA VIRUS TANZANIA na kutoa taarifa za upotoshaji za ugonjwa wa Corona.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo aprili 4,2020  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro (SACP) Willbroad Mutafungwa amesema mtuhumiwa huyo baada ya kufungua akaunti hiyo amekuwa akitoa taarifa zisizo sahihi na zenye upotoshaji mkubwa kwenye jamii licha ya serikali kutoa onyo kuhusu utoaji wa taarifa za upotoshaji kuhusu ugonjwa huo. 

"Mnamo tarehe 1 mwezi aprili mwaka huu majira ya saa 11 jioni jeshi la polisi lilifanikiwa kumkamata kijana mmoja aitwaye Awadhi Lugoya kwa matumizi mabaya ya mtandao wa kijamii ( facebook) kutoa taarifa zisizo rasmi za upotoshaji kuhusu ugonjwa wa corona, mahojiano yanaendelea yakikamilika atafikishwa mahakamani",alisema Kamanda Mutafungwa.

Aidha Kamanda Mutafungwa ametoa tahadhari kwa wakazi wa Morogoro hasa wanaotumia mitandao ya kijamii kuwa makini kuhusu utoaji wa taarifa juu ya ugonjwa wa corona. 

Katika hatua nyingine jeshi la polisi limefanikiwa kumkamata mwanamke mmoja maeneo ya kata ya tungi kwa tuhuma za wizi wa bodaboda kwa kutumia nguvu akishirikiana na watu wengine. 

"Siku ya tarehe 3 mwezi wa nne mwaka huu majira ya saa tano usiku maeneo ya kata ya Tungi Udhuruni ndani ya manispaa ya Morogoro tulifanikiwa kumkamata bwana Geofrey (30-35)akiwa ameuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali na tulibaini alikuwa na mwanadada aitwaye Lightness John ambaye kwa sasa ni majeruhi amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Morogoro akiwa amevunjika mguu, hawa nia yao ilikuwa ni kuiba bodaboda ila wananchi waliwawahi dada huyo yuko chini ya ulinzi mkali upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani",amesema.
Share:

WAZIRI MBARAWA ASEMA WATATUMIA WATAALAMU WA NDANI KUFUNGA PAMPU ZA MAJI IWAPO UGONJWA WA CORONA UTAENDELEA KUWEPO

 WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa akizungumza leo wakati wa ziara yake wilayani Pangani kushoto ni Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo
 WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa akizungumza mara baada ya kuangalia mradi wa maji Kijiji cha Ubangaa
 MKURUGENZI wa Bonde la Maji la Mto Pangani Segule Segule akizungumza wakati wa ziara hiyo kulia ni Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Pangani
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Pangani Seif Ally akizungumza wakati wa ziara hiyo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah katikati aliyekaa ni WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa

 MKURUGENZI wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly akitolea ufafanuzi wakati wa ziara hiyo
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Pangani Seif Ally kushoto akimueleza jambo Waziri wa Maji Proffesa Makame Mbarawa wakati wa ziara hiyo katikati ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah
 WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa katika akivuka kwenye kivuko Mto Pangani mara baada ya kumaliza ziara yake wilayani humo
 MKURUGENZI wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly akivuka kivuko cha Mto Pangani leo wakati wa ziara hiyo
Mto Pangani kama unavyoonekana

WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa amesema miradi yote ya maji  ambayo pampu za kusukumia maji zimeletwa kutoka nje ya nchi lakini wataalamu wa kuzifunga wamekwama kutoka nchini Africa kusini kutokana na ugonjwa wa virusi vya Corona sasa watatumia wataalamu wa ndani kwa kibali.

Hatua hiyo inatajwa kwamba imekuwa ikikwamisha miradi mbalimbali ya maji kwa wananchi kutokana na wataalamu hao kushindwa kutoka kwenye nchi zao na kuja kuzifunga huku wananchi wakiendelea kukosa huduma hiyo muhimu.

Mbarawa aliyasema hayo leo wakati akihitimisha ziara yake kwenye wilaya za Pangani na Muheza ambapo alisema kwamba wakandarasi hao wataandikiwa barua huko ili watoe maelekezo na baadae watafutwe watu wengine wa kufanya kazi hiyo.

Alisema kwamba hawawezi kusema kwamba wanakaa kuwasubiri maana hawajui ugonjwa huo utaisha lini lakini lazima wawe na maamuzi mengine kwa kutumia wataalamu wa ndani kuweza kufunga pampu hizo ikiwemo makukabiliano kutoka kwa wataalamu hao.

Alisema kwamba hata kama wataalamu wangekuja wasingefunga pumpu hizo bali wangetoa maelekezo kwa wataalamu wa hapa nchini ndio wangeweaza kufanya kazi hiyo.

Aidha alisema wanachotaka kwa wakandarasi hao watoe kibali na maelekezo watu wafanye na hata ridhiki ya kazi wachukue ili kuweza kunusuru miradi isiendelee kukwama kutokana na uwepo wa ugonjwa huo.

“Naamini tukifanya hivyo miradi yote ya maji itakwenda na wananchi watapata huduma ya maji safi na salama kwa wakati na kuondokana na kero za kuifuata mbali”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Corona ni ugonjwa umekuja lakini na dawa mojawapo ni maji hivyo ni wakati muafaka wizara ya maji wajitoe wafanye kazi kwa bidii kama walikuwa wanafanya kazi kwa spidi 80 sasa wanapaswa kwenda spidi 160 kutokana na hduuma yao kuhitajika kupita kiasi.

Hata hivyo Waziri Mbarawa alisema kwamba kwa wataalamu wa manunuzi nchini wizara ya maji imebaini kuwepo kwa changamoto kwao kutokana na kuzembea kufanya jambo kwa haraka.

“Utakuta jambo ni la kufanya miezi miwili anachukia miezio sita mfano mzuri ni hapa fedha ilikuja Novemba mpaka leo Aprili mabomba hayajafika wakati kuna baadhi ya mikoa Mbeya, Iringa na meeneo mengine kazi zipo asilimia 70 matenki yapo nusu”Alisema Waziri huyo.

Alisema lakini mkoani Tanga mpaka leo hawajafanya chochote sasa hao watu wa namna hiyo ataendelea kuwahamisha na kupelekea mwengine na wakishindwa kujirekebisha wataondoilewa kabisa.

Awali akizungumza wakati akitoa taarifa ya mradi wa maji Kijiji cha Ubangaa na Mkwajuni Kaimu Meneja wa Wakala wa Maji Vijijini wilaya ya Pangani (Ruwasa) Mhandisi Sande Batakanwa alimueleza Waziri Mbarawa kwamba changamoto kubwa kwa kuanzia ilikuwa ni uhitaji wa pampu,moto na Transfoma iliyoondolewa na Tanesco baada ya mradi kusimama.

Alisema kwamba kwa uhitaji huo kama pampu,mota na transfoma iliyoondolewa na Tanesco vingepatikana na wananchi wangeanza kupata huduma kama awali .


Share:

VYAKULA UNAVYOPASWA KULA ILI KUIMARISHA KINGA YA MWILI WAKO


Virusi vya corona Covid-19 vimefanya uharibifu katika kila sekta ya maisha yetu duniani kuanzia China, Marekani bara Asia hadi Afrika.

Huku tukikabiliana na changamoto hii mpya, ni muhimu kutathmini na kutumia kila kifaa tulichonacho ili kupumguza maambukizi, vifo na mateso ya mlipuko huu.

Kutokaribiana, kuosha mikono na kujitenga kunaweza kupunguza maambukizi. Lakini je chakula na lishe bora kinaweza kuwa na jukumu gani katika mlipuko huu?



Tunaamini kwamba kuna njia tatu muhimu za utaratibu maalumu wa chakula ambazo zinaweza kukabiliana na tatizo hilo la kiafya.

Virutubishi


Kwanza, ulaji wa kiwango cha juu cha virutubishi fulani huimarisha mfumo wa kinga, huku ulaji wa kiwango cha chini ukidhoofisha kinga na kuvutia maradhi ya maambukizi.

Kinga imara mwilini inaweza kusaidia kukabiliana na virusi , na pia inaweza kuwasaidia baadhi ya wagonjwa kupona kwa haraka.

Virutubisho vinavyoweza kuimarisha kinga ya mwilini ni kama vile madini ya zinc, Selenium, iron na vitamin A,C,D,E , B-6 mbali na vyakula kama vile kama goji berry, broccoli, chai ya kijani, na manjano.

Mboga na matunda kama vile maembe, mananasi na tufaa ni muhimu katika kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa ya milipuko.

Baadhi ya madaktari wanasema kwamba matunda kama vile machungwa yana vitamin C nyingi ambayo ina uwezo wa kukabiliana na magonjwa.

Baadhi ya virutubishi hivi vinasaidia kuzuia uvimbe kupitia kiasi na uharibifu wa tishu unaosababishwa na virusi hivyo ambao unaweza kusababisha majeraha ya mapafu na hata kifo.
Ni mapema mno kujua ni mchanganyiko gani wa virutubisho ndio bora kukabiliana na covid-19.

Lakini tunajua kwamba baadhi ya virutubisho hivyo vimeonesha kukabiliana na homa ya kawaida na magonjwa mengine ya mapafu.

Huku mikahawa mingi ikiwa imefungwa, chukua fursa hii kula vyakula vyenye afya nyumbani kama vile machungwa, matunda, broccoli, mboga ya mchicha, uyoga, pilipili nyekundu, viazi vitamu, samaki, maharagwe, siagi, manjano na chai.

Vyakula hivi vinaweza kuwa muhimu kwa watu wazima ambao hula kiwango kidogo cha vyakula hivi na ambao wako hatarini zaidi kuambukizwa maradhi ya Covid-19.
Lishe duni

Pili uzoefu kutokana na milipuko mengine ya magonjwa ya maambukizi unaonesha wazi kwamba watu wanaokula lishe duni wako hatarini zaidi kuambukizwa virusi hivi.

Pia wanaweza kuwa wagonjwa kwa kipindi kirefu na hata kupoteza maisha yao. Katika mlipuko huu kuwalisha watu waliopo katika hatari kupata mambukizi haya ni muhimu zaidi.

Na hatimaye mbali na umri mkubwa, hatari ya maambukizi ya Covid-19 na vifo iko juu miongoni watu wanaougua magonjwa mengine kama vile yale ya moyo, na sukari.

Hali hii hudhoofisha uwezo wa moyo kukabiliana na shinikizo la mawazo huku kisukari kikidhoofisha mfumo wa kinga.
CHANZO - BBC
Share:

Masauni: Wapeni Dhamana Mahabusu Kuepusha Corona

Na Mwandishi Wetu,Dodoma
Serikali imewaagiza Makamanda wa Polisi na Wakuu wa Magereza mikoa yote nchini kuhakikisha inawapa dhamana mahabusu wote wanaokidhi vigezo vya dhamana na kuharakisha upelekwaji haraka wa kesi kwa watuhumiwa waliopo katika magereza mbalimbali nchini ili kuweza kuepusha na kupambana na ugonjwa wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona(Covid 19) usiweze kuingia katika mahabusu za polisi na magereza.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika Vituo mbalimbali vya Polisi mkoani Dodoma ambapo alibaini kuwepo msongamano wa mahabusu katika vituo vya polisi huku akifanikiwa kuzungumza na baadhi ya mahabusu ambao ilionekana kesi zao zinadhaminika huku wengine  wakiruhusiwa katika ziara hiyo.

“Maagizo ya Serikali na wataalamu wa afya ni kuepusha misongamano sasa nimetembelea kituo hiki cha kati nimekuta mahabusu wengine wamekaa siku kumi na nne,na wengine wanaingia wakiwa wametoka nje huko hali iliyopelekea msongamano mkubwa katika kituo hiki, na kuna mahabusu mmoja nimekuta wamemuweka siku tatu hapa kosa lake wamemkamata tu anapita nje ya bunge hii sio sawa huku hana kosa lolote.

“Sasa natoa maagizo kwa Makamanda wa Polisi nchi nzima katika kukabiliana na ugonjwa wa corona wahakikishe mahabusu wote ambao kesi zao zinadhaminika watolewe, agizo hili pia liende kwa wakuu wa magereza yote nchini kuhakikisha watuhumiwa wote kesi zao zinaharakishwa kupelekwa mahakamani hii yote ikiwa ni mkakati wa kupambana na gonjwa la Corona sasa watu wamerundikwa tu hakuna kinachoendelea hii si sawa” alisema Masauni

Pia alipata fursa ya kuzungumza na wananchi waliokusanyika nje ya vituo vya polisi wakija kuwaona ndugu zao huku akisisitiza washughulikiwe haraka kwani wamekusanyana wengi huku serikali ikiwa imepiga marufuku mkusanyiko wa watu na wataalamu wakishauri umbali kati ya mtu na mtu uwe mita moja.

“Wananchi wamekuja kuona ndugu zao waliopo mahabusu tunajua ni haki yao pamoja na kuwaletea chakula lakini muwahudumie haraka waondoke hii mikusanyiko ishakatazwa ni hatari sana” alisema Masauni.


Share:

Breaking : GARI YAUA WATU WANNE BAADA YA KUGONGA GEMA NA KUTUMBUKIA BWAWANI BARABARA YA OLD SHINYANGA



Gari yenye namba za usajili T.785 DBM Toyota IST ikitolewa bwawani na Trekta baada ya kugonga gema na kutumbukia katika bwawa hilo na kuua watu wanne  katika eneo la kitongoji cha Mwajinaganya kijiji cha Bubiki B, kata ya Bubiki, tarafa ya Mondo, wilaya ya Kishapu barabara ya Old Shinyanga kuelekea Bubiki - Mwanza . Picha zote na Malunde 1 blog

Sehemu ya bwawa hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba  akiwa katika eneo la kitongoji cha Mwajinaganya kijiji cha Bubiki B, kata ya Bubiki, tarafa ya Mondo, wilaya ya Kishapu barabara ya Old Shinyanga kuelekea Bubiki - Mwanza ambapo gari yenye namba za usajili T.785 DBM Toyota IST imegonga gema na kutumbukia bwawani.
Gari yenye namba za usajili T.785 DBM Toyota IST iliyokuwa ikiendeshwa na dereva aitwaye Gration Mlikozi iliyopoteza uelekeo na kugonga gema na kutumbukia katika bwawa la maji lilipo pembezoni mwa barabara ya vumbi ya Old Shinyanga na kuua watu wanne.


Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog 
Watu wanne wamefariki dunia baada ya gari waliyokuwa wanasafiria kugonga gema kisha kutumbukia katika bwawa lililopo pembezoni mwa barabara ya vumbi ya kutoka Old Shinyanga kuelekea Bubiki hadi Mwanza kwenye kijiji cha Bubiki B kata ya Bubiki wilaya ya Kishapu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema ajali hiyo ya gari kuacha njia na kugonga gema na kutumbukia katika bwawa la maji na kusababisha vifo imetokea leo Jumamosi Aprili 4,2020 majira ya saa saa tatu na dakika 20 katika eneo la kitongoji cha Mwajinaganya kijiji cha Bubiki B, kata ya Bubiki, tarafa ya Mondo, wilaya ya Kishapu. 

“Ajali hii imetokea katika barabara ya vumbi ya kutoka Old Shinyanga kuelekea Bubiki hadi Mwanza ambapo ,gari yenye namba za usajili T.785 DBM Toyota IST iliyokuwa ikiendeshwa na dereva aitwaye Gration Mlikozi, miaka haifahamiki, ilipoteza uelekeo na kugonga gema na kutumbukia katika bwawa la maji lililochimbwa kwa ajili ya kuchukulia udongo wa matengenezo ya barabara na kusababisha vifo kwa watu wanne”,ameeleza Kamanda Magiligimba. 

Amewataja waliofariki dunia katika ajali hiyo ni dereva wa gari hilo Gration Mlikozi pamoja na abiria watatu ambao ni Singu Isack Lazaro (57), Chrispin Ikate, miaka haijulikani, mwanaume, na Abdallah Mussa, mwanaume, miaka haifahamiki. 

“Chanzo cha ajali ni mwendokasi wa gari husika katika barabara ya vumbi kulikopelekea dereva gari kumshinda na kwenda kugonga gema na kutumbukia katika bwawa la maji na kusababisha vifo”,amesema. 


“Gari husika limeshatolewa katika maji na lipo katika kituo cha polisi Maganzo. Miili ya marehemu imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga. Natoa wito kwa madereva wote kutii sheria za usalama barabara na kuacha kuendesha vyombo vya moto kwa mwendo kasi”,amesema Kamanda Magiligimba.
Share:

TAHADHARI KWA WASAFIRI WOTE ILIYOTOLEWA NA WIZARA YA AFYA KUHUSU UGONJWA WA CORONA




Share:

UJERUMANI YAITUHUMU MAREKANI KUPORA MASKI ZAKE ZA KUKABILIANA NA CORONA


Ujerumani imeituhumu Marekani kuwa imetumia mbinu za uharamia katika kupora maski zake za kukabiliana na ugonjwa wa corona.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ujerumani Andreas Geisel amesema hatua ya Marekani kupora maski hizo za uso ni ‘uharamia wa kisasa’.

Vyombo vya habari vya Ujerumani vimeripoti kuwa maelfu ya maski ambazo zilikuwa zimenunuliwa kutoka shirika la 3M zimeelekezwa Marekani wakati zilipokuwa zikihamishwa baina ya ndege nchini Thailand zikitokea China.

Wakuu wa Ujerumani wamethibitisha kuwa maski 200,000 aina ya FFP2- ambazo zinashabihiana na zile za N95  zinazotumiwa Marekani, ziliibiwa katika uwanja wa ndege wa Bangkok na hivyo hazikufika Berlin. Ujerumani imesema tayari ilikuwa imeshalipia maski hizo ambazo zimeibiwa na maajenti wa Marekani nchini Thailand.



Akiwa ni mwenye hasiria, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani alisema siku ya Ijumaa kuwa, ‘Hii sio njia ya kuamiliana baina ya washirika wa Atlantiki.” Ameongeza kuwa hata kama kuna mgogoro wa kimataifa hakupaswi kutumiwa mbinu za magenge ya zamani ya Kimarekani. Waziri huyo amesema serikali ya Ujerumani itawasilisha malalamiko rasmi na kuitaka Marekani iheshimu sheria za kimataifa.

Ubalozi wa Marekani mjini Berlin, Ujerumani bado haujatoa taarifa kuhusu tukio hilo la uhalifu wa kimataifa.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger