Monday, 27 January 2020

Business Development Officer Agency Banking (100 Job posts) at CRDB

Business Development Officer Agency Banking (100 Positions) CRDB Bank Plc seeks to recruit highly competent, self-motivated and professional individuals to fill 100 positions of Business​ Development Officer – Agency Banking  (1-year contract) in the following zones; Central Zone – 16, Eastern​      Zone – 28, Northern​   Zone – 17,​ Highland​   Zone – 9,​ Southern​     Zone – 8,… Read More »

The post Business Development Officer Agency Banking (100 Job posts) at CRDB appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tanzania Program Associate at One Acre Fund Morogoro, TZ

About One Acre Fund Founded in 2006, One Acre Fund supplies smallholder farmers with the agricultural services they need to make their farms vastly more productive. We provide quality farm supplies on credit, delivered within walking distance of farmers’ homes, and agricultural trainings to improve harvests. We measure our success by our ability to make farmers more prosperous:… Read More »

The post Tanzania Program Associate at One Acre Fund Morogoro, TZ appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Kesi ya Erick Kabendera Yapigwa Kalenda ad Februari 10

Upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi, inayomkabili, mwandishi wa Habari za uchunguzi Erick Kabendera, umeieleza Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu kuwa, mchakato wa makubaliano kati ya Kabendera na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) bado unaendelea.

Wakili wa Serikali Gloria Mwenda amedai hayo leo Januari 27,2020 Mbele ya Hakimu Mkazi, Jenet Mtega wakati kesi hiyo ilipokuja mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa.

Wakili Mwenda amedai upelelezi bado unaendelea na mchakato wa makubaliano kwa DPP pia unaendelea hivyo wanaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

 Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mtega ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 10 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Katika kesi hiyo, Kabendera anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka matatu likiwemo la utakatishaji wa Sh.Mil 173.



Kwa mara ya kwanza Kabendera alifikishwa mahakamani hapo Agosti 5, 2019 akikabiliwa na makosa hayo anayodaiwa kuyafanya kati ya Januari 2015 na Julai 2019, jijini Dar es Salaam.


Share:

Waziri mkuu wa Lesotho pamoja na Mkewe wakabiliwa na tuhuma za mauaji

Waziri Mkuu wa Lesotho Thomas Thabane pamoja na mkewe, Maesaiah Thabane wanatakiwa kuhojiwa kuhusiana na mauaji yaliyotokea mwaka 2017 ya Mke wa kwanza wa Thabane, Lipolelo Thabane (58)
 
Lipolelo alikuwa ametengana na mume wake na alikuwa akiishi peke yake tangu mwaka 2012 ambapo aliuawa siku 2 kabla ya Thabane kuapishwa kuwa Waziri Mkuu kwa kupigwa risasi sehemu mbalimbali za mwili wake

Ushahidi wa hivi karibuni uliowasilishwa Mahakamani na Kamishena wa Polisi umebaini kwamba kulikuwa na mawasiliano ya simu katika eneo la tukio kwa kutumia namba ya simu inayodhaniwa kuwa ni ya Thabane

Waranti ya kukamatwa kwa Maesaiah Thabane ilishatolewa lakini hajaonekana hadharani kwa wiki 2 sasa, hakuna anayejua alipo na Thabane amekataa kusema alipo mke wake


Share:

Ijue Sayansi ya Kusimama na Kusinyaa kwa Maumbile ya Kiume ( Sayansi ya Nguvu za Kiume)

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani.

Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ?
Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu


Hatua  mbili  Muhimu 
Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  maumbile yake ya kiume yapitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo :

Hatua  ya  kwanza, ni  lazima  yaweze  kusimama  barabara  na  kuwa  magumu  kama  msumari.

Na  hatua  ya  pili  ni  lazima, yaendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION

Endelea na Makala hii kwa <<Kubofya Hapa>.


Share:

Evariste Ndayishimiye Aidhinishwa Kuwa Mrithi Wa Rais Pierre Nkurunziza

Chama tawala cha Burundi CNDD-FDD, kimemteua katibu wake mkuu kuwa mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu wa Burundi utakaofanyika Mei 2020.

Jenerali Evariste Ndayishimiye ameidhinishwa na chama kama mrithi wa Nkurunziza wa Burundi.

Meja Jenerali Evariste Ndayishimiye ameteuliwa kama mgomba wa urais katika uchaguzi utakaofanyika Mei 2020 kumrithi Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza.

Jenerali Ndayishimiye ameteuliwa Jumapili kupeperusha bendera ya chama cha CNDD-FDD katika kikao kisicho cha kawaida kilichofanyika Gitega, mji mkuu wa kisiasa baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa saa tatu ya chama tawala cha CNDD-FDD.

Bwana Ndayishimiye ni miongoni mwa wanasiasa mashuhuri katika siasa za Burundi waliokaribu na Pierre Nkurunziza.

Pia ni miongoni mwa waliokuwa waasi wa CNDD-FDD aliyejiunga baada ya kunusurika katika mauaji ya kikabila ya wanafunzi wa Wahutu katika chuo kikuu cha Burundi mwaka 1995.

Jenerali Ndayishimiye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa chama cha CNDD-FDD tangu Agosti 2016.

Kabla ya kuteuliwa kwake, alikuwa Waziri wa mambo ya ndani na ulinzi wa umma.

-BBC


Share:

Business and Entrepreneurship Adviser – Remote VSO Mwanza Tanzania

Role Overview The Ideal person will train the Lake Zone Youth to improve market awareness and help them identify business opportunities. The candidate will work hand in hand with corporate volunteers who will be engaged in the similar position or Life Skills expert to engage marginalized youth on soft skills that will help them on how to employ… Read More »

The post Business and Entrepreneurship Adviser – Remote VSO Mwanza Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

FAO yasema tusipowadhibiti nzige wanaoikabilia Ethiopia, Kenya na Somalia watasambaa

Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO limeonya kwamba nzige walioivamia Ethiopia, Kenya na Somalia sasa ni wimbi kubwa kuwahi kushuhudiwa hivi karibuni na lisipodhibitiwa kuna uwezekano wa kusambaa katika nchi nyingine za Afrika Mashariki.

Wimbi kubwa la nzige walionekana kutamalaki angani na kughubika mashamba pembe ya Afrika, kwa mujibu wa FAO tayari limeshasababisha uharibifu mkubwa kwa kusambaratisha maelfu ya ekari za mazao hali ambayo inaathiri uhakika wa chakula katika nchi hizo ambazo zinakabiliwa na changamoto nyingine nyingi ikiwemo kutokuwa na uhakika wa chakula katika baadhi ya maeneo.

Rosanne Marchesich kiongozi wa timu ya dharura na mnepo ya FAO anasema mlipuko wa safari hii wa nzige ni mkubwa sana, “Tunachojua kuhusu uvamizi huu wa nzige wa jangwani ni kwamba ni mbaya zaidi kuwahi kushuhudia Ethiopia na Somalia katika kipindi cha miaka 25 na ni mbaya zaidi kushudiwa Kenya kwa zaidi ya miaka 70."

Hata hivyo amesema kiwango cha nzige hao kinatofautiana kutoka nchi moja hadi nyingine lakini kwa sasa nchi zilizoathirika zaidi ni Ethiopia , Kenya na Somalia na nzige wameshasababisha athari kubwa , na hofu ni kwamba wanavyoendelea kuvamia sehemu zingine za nchi hizo athari hasa katika uhakika wa chakula zitakuwa kubwa zaidi, lakini pia katika kilimo, na maisha kwa wakulima na wafugaji.

FAO imetoa wito wa kuwa na kampeni ya pamoja kukabiliana na janga hilo la nzige ikihofia kwamba janga linaweza kusambaa kwa nchi zingine za Afrika Mashariki.

“Kuna hatari ya kusambaa, nchi muhimu zaidi zinazoangaliwa hivi sasa ni Uganda na Sudan Kusini. Uganda haijawahi kukabiliana na wimbi la nzige tangu miaka ya 60, hivyo kuna wasiwasi kuhusu uwezo wa wataalam mashinani kuweza kukabiliana na janga hilo bila msaada toka nje. Na katika nchi kama Sudan Kusini tayari kuna asilimia 47 ya watu wasio na uhakika wa chakula.”

Ameongeza kuwa mbali ya zahma zingine zinazowakabili mabadiliko ya tabianchi yamekuwa kichocheo kikubwa cha nzige kuzaliana.

Pamoja na kufuatilia janga hili kwa karibu FAO inatoa msaada wa hatua za kuwadhibiti nzige hao kwa njia ya anga na ardhini lakini pia mbinu za kuweza kuwasaidia wakulima na wafugaji kuendesha maisha yao.

Pia imeonya kwamba mazingira ya kuruhusu kuzaliana bado yapo na ongezeko la nzige linaweza kuendelea hadi Juni mwaka huu 2020.

Umoja wa Mataifa waingilia kati
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya kibinadamu na msaada wa dharura OCHA imesema imetoa dola milioni 10 kutoka katika mfuko wake mkuu wa dharura CERF ili kuongeza nguvu katika kupambana na mlipuko wa nzige wa Jangwani ambao wamevamia maeneo kadhaa ya Afrika Mashariki. 

Akizungumza  na vyombo vya habari mjini Geneva Uswisi, Msemaji wa OCHA Jens Laerk amesema,“Ni mlipuko ambao uko Afrika Mashariki na pembe ya Afrika. Pia umebainika kusini magharibi mwa Asia na Bahari ya shamu, ni mlipuko mbaya wa aina yake katika miaka 25 kwa Ethiopia na Somalia na ni mbaya zaidi kwa Kenya kuwahi kuuona katika miaka 70. Madhara katika nchi hizo ni mabaya kwa kuwa malisho na mazao yanatoweka katika jamii ambazo tayari zilikuwa zinakabiliwa na upungufu wa chakula.”

Credit: Umoja wa Mataifa


Share:

Sekta ya mawasiliano ya simu inavyokuza ajira nchini

Mwanzoni mwa mwezi huu wa Januari 2020, Naibu Waziri katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye (Mb) alilitaka Shirika la Posta nchini (TPC)kujikita katika matumizi ya teknolojia na ubunifu katika utoaji wa huduma zake. 

Waziri Nditiye alienda mbali na kuelezea namna ambavyo mabadiliko ya kiteknolojia ya siku za karibuni yanavyosaidia kusukumu mbele ukuaji wa uchumi. 

Sekta ya mawasiliano ya simu ni moja ya sekta kubwa zaidi zinazosaidia kukua kwa uchumi wetu.Katika muongo mmoja uliopita sekta hiyo imewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye teknolojia na kuwezesha ongezeko kubwa la watumiaji wa simu mpaka sasa kwa mamilioni. 

Sekta hiyo pia imekua kwa kiasi kikubwa kabisa. Matokeo ya ukuaji huo ni sekta hiyo kuweza kuajiri Watanzania zaidi ya milioni moja na nusu (1,500,000)katika maeneo ya wahandisi wa programu za kompyuta, huduma kwa wateja, uuzaji na usajili wa laini za simu na huduma za kutoa na kupokea fedha. Sekta hiyo inapoendelea kupanuka mfano kwenda katika mfumo wa 4G unaotoa huduma bora zaidi inaamaanisha pia itatengeneza ajira zaidi.

Wakati huo huo, kampuni nyingi za mawasiliano ya simu zinaendesha huduma ya kutuma, kupokea fedha na kulipia bili mbalimbali pamoja na huduma nyinginezo ambazo zimesaidia watu wengi kuingia katika mifumo rasmi ya kifedha na kukuza uzalishaji na biashara. Mfano mmojawapo ni kampuni ya Tigo.

Mbali na huduma hizo Tigo pia imesaidia kukua kwa biashara ndogo na za kati kwa kukuza uwezo wao kufanya mambo kidijitali ikiwemo kuunganisha mtandao wa intaneti katika maeneo ya biashara na ofisini.

Ama kwa hakika sote hatuna budi kuishukuru na kufurahia ukuaji wa sekta hii. Muungano wa siku za karibuni wa Tigo na Zantel katika kutoa huduma nao ni jambo jema kwani utaruhusu kampuni hizo kutoa huduma bora zaidi za pande zote mbili lakini kukuza faida ambayo itawekezwa kuboresha huduma zaidi na zaidi. 


Muungano wa aina hii ni aina mojawapo ya namna sekta hii inaweza kujengewa mazingira bora ya kukua. Tunapouanza mwaka mpya, ni vyema kama Taifa tukaendelea kuiunga mkono sekta hii kuhakikisha inaendelea kukua na kufaidisha wateja na uchumi wetu.



Share:

Kasi ya maambukizo ya kirusi corona yaongezeka China

Serikali kuu ya China imesema  kwamba idadi ya waathirika wa virusi vibaya kabisa vya Corona imeongezeka na kufikia 2,774 kote nchini humo, huku kukiwa na visa vipya 769 vilivyogundulika. 

Hata hivyo ilisema hakukua na taarifa mpya za vifo iliyothibitishwa tofauti na jimbo la Hubei, ambako mapema liliarifu watu 24 waliokufa kutokana na maambukizi ya virusi hivyo wanafanya idadi ya waliokufa hadi sasa kufikia 80.

 Rais wa China Xi Jinping ameuita mripuko huo kuwa ni hali ya wasiwasi mkubwa na kusema serikali ilikuwa inafanya juhudi za kuzuia safari na mikusanyiko ya umma wakati ikiwapeleka wahudumu wa afya na vifaa kwenye mji ambao ni kitovu cha janga hilo wa Wuhan.


Share:

Masauni: ”Utaratibu wa kuzuia mikutano ya kisiasa isiyofuata sheria uko palepale”

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema, utaratibu wa kuzuia Mikutano ya Kisiasa isiyofuata Sheria na taratibu upo palepale

Amesema hayo akiwa Visiwani Zanzibar alipokuwa akizungumzia hali ya Usalama kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2019 visiwani humo

Amesema, muda wa Siasa ukifika Serikali itaruhusu mikutano hiyo yenye lengo la kutoa nafasi kwa Wanasiasa kuzungumza na Wananchi na kueleza kwa Wananchi walichokifanya kwa muda waliopewa baada ya kuchaguliwa na kuteuliwa katika nafasi mbalimbali

Kuhusu hali ya usalama kwa kipindi cha 2019, amesema matukio ya mauaji yamepungua kutoka 40 mwaka 2018 hadi 35 mwaka 2019 huku matukio ya udhalilishaji yakiongezeka kutoka matukio 15 mwaka 2018 mpaka matukio 35 mwaka 2019.


Amesema Serikali kupitia jeshi la polisi na mamlaka nyingine zinazohusika limeanza harakati za kudhibiti matukio  hayo  yanayosababishwa  na  mambo mbalimbali ikiwemo imani za kishirikina.



Share:

Vacancy: Field Supervisor-Adolescents Empowerment Project at The Organization for Community Development (OCODE)

Job Summary The Organization for Community Development (OCODE) is a grassroots national nongovernmental organization that works to improve lives of less privileged Tanzanians. It was established in 1999, registered in 2003 under the Society Ordinance Act of 1954 and complied with the NGO Act of 2002 in March 2011. The current OCODE’s focus is on supporting and facilitating… Read More »

The post Vacancy: Field Supervisor-Adolescents Empowerment Project at The Organization for Community Development (OCODE) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Ubalozi wa Marekani Nchini Iraq Washambuliwa Tena

Marekani imeitolea mwito Iraq kulinda majengo yake ya kidiplomasia baada ya ubalozi wake mjini Baghdad kushambuliwa kwa maroketi matatu. 

Msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani ametoa mwito kwenye taarifa yake kwa Iraq kutimiza wajibu wake wa kuyalinda majengo hayo. 

Jana Jumapili roketi moja lilishambulia eneo la kulia chakula kwenye ubalozi wa Marekani nyakati za chakula cha jioni, wakati maroketi mengine mawili yakiangukia karibu na eneo hilo, hii ikiwa ni kulingana na chanzo kilichozungumza na shirika la habari la AFP. 

Amesema tangu Septemba mwaka jana kumekuwepo na mashambulizi 14 yanayofanywa na wanamgambo wa Iran na wanaoungwa mkono na Iran dhidi ya watumishi wa Marekani waliopo Iraq. 

Amesema, hali ya usalama ni ya wasiwasi na makundi yenye silaha yanayoungwa mkono na Iran yanaendelea kusalia kitisho.


Share:

Consultant to Oversee HIV Data Collection at Palladium International – Health Policy Plus Tanzania

Job Summary Palladium is seeking a qualified Tanzanian consultant to manage data collection efforts related to an HP+ HIV activity-based costing and management exercise at facility, community, and above site-levels. The consultant will work closely with HP+ team members, MOHCDGEC, PEPFAR Tanzania, a Tanzania research institution contracted by HP+, public and private health facility staff, and other stakeholders.… Read More »

The post Consultant to Oversee HIV Data Collection at Palladium International – Health Policy Plus Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Financial Accountant at Michael page Africa, January 2020

Financial Accountant Financial Accountant Tanzania About Our Client Our client is the world’s largest provider of commercial explosives and innovative blasting systems to a variety of industries. They are over 140 years old, have more than 10,000 employees and are present on over 100 countries. Job Description The duties of the successful candidate will include: Month end processes… Read More »

The post Financial Accountant at Michael page Africa, January 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

CHIEF, PROCUREMENT OFFICER, P4 | UN – International Residual Mechanism for Criminal Tribunals

Job Opening Posting Title: CHIEF, PROCUREMENT OFFICER, P4 Job Code Title: PROCUREMENT OFFICER Department/Office: International Residual Mechanism for Criminal Tribunals Duty Station: ARUSHA Posting Period: 24 January 2020 – 22 February 2020 Job Opening Number: 20-Procurement-RMT-129296-R-Arusha (R) Staffing Exercise N/A   Org. Setting and Reporting This position is located in the Arusha branch of the Mechanism. The incumbent… Read More »

The post CHIEF, PROCUREMENT OFFICER, P4 | UN – International Residual Mechanism for Criminal Tribunals appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Operations Officer at World Bank

Job #: req5380 Organization: World Bank Sector: Operations Grade: GF Term Duration: 3 years 0 months Recruitment Type: Local Recruitment Location: Dar Es Salaam,Tanzania Required Language(s): English Preferred Language(s): English Closing Date: 2/2/2020 (MM/DD/YYYY) at 11:59pm UTC Description Established in 1944, the WBG is one of the world’s largest sources of funding and knowledge for development solutions. In… Read More »

The post Operations Officer at World Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger