Saturday, 7 December 2019

WAZEE 2271 WAPATIWA KADI ZA CHF KAHAMA


Na Salvatory Ntandu - Kahama 
Wazee 2271 katika Halamshauri ya Mji wa Kahama mkoani Shinyanga wamepatiwa kadi za bima ya afya iliyoboreshwa (CHF) ambazo zitawasaidia kupata matibabu bure kwa mwaka mzima na kuondokana kwenda kwa waganga wa kienyeji kutafuta tiba.

Wazee wasiojiweza waliosajiliwa na baraza la wazee la Halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga ni 6247 na waliopatiwa kadi za CHF ni 2271.

Hayo yalibainishwa jana Mwenyekiti wa Baraza la wazee wa Halmshauri ya Mji kahama, Willfred Bilago wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini kahama alisema hapo awali wazee walikuwa wanahangaika kupata matibabu kutokana na kukosa kadi za CHF iliyoboreshwa.

“Wazee tulikuwa tunaona ni bora kwenda kwa waganga wa kienyeji kutafuta tiba mbadala kuliko kwenda katika hospitali ambapo tulikuwa hatuthamini na wengi wetu walipoteza maisha kutokana huduma hizo zisizokuwa za kitaalamu”alisema Bilago.

Alisema kadi za CHF zimesaidia wazee wasiojiweza kupata huduma za matibabu ambapo kwa unafuu na haraka kwani katika hospitali ya Halmashauri ya Mji wa kahama kunadirisha la kuhudumia wazee na madaktari maalum kwa ajili wao.

“Tunawaomba wadau,wafanyabiashara,viongozi wadini kusaidia upatikanaji wa kadi za CHF kwa wazee wasiokuwa na waangalizi ili waweze kupata matibabu bure kwani suala hili tukiiachia serikali pekee kwani nasi tunawajibu wa kuwatuza wazee wetu” alisema Bilago.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Abel Shija alisema kuwapatia kadi za CHF wazee katika halmashauri hiyo ni takwa la kisheria hivyo hawana budi kulitekeleza agizo hilo.

Kwa mujibu wa sera ya taifa ya wazee ya mwaka 2003 inazielekeza halmashauri kuhakikisha haki za wazee waliofikia miaka 60 zinalindwa pamoja na kuwapatia huduma bure za matibabu.
Share:

Picha : BODI YA WAKURUGENZI AGPAHI YATUA SIMIYU...RC MTAKA AWAPONGEZA KUSAIDIA WANANCHI...'KAZI ZENU SIYO ZA KUMULIKA KWA TOCHI'


Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ameipongeza Asasi ya kitaifa isiyo ya kiserikali ya Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) kwa kutekeleza kikamilifu miradi ya UKIMWI na kuwagusa wananchi moja kwa moja. 

Mhe. Mtaka ametoa pongezi hizo Desemba 6,2019 kwenye kikao cha Bodi ya Wakurugenzi wa AGPAHI na wadau wa UKIMWI mkoani Simiyu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu. 

Mtaka alisema AGPAHI ni taasisi maarufu mkoani Simiyu kutokana na kwamba imekuwa ikifanya vitu vinavyoonekana katik sekta ya afya mkoani humo kwa kusaidia wananchi. 

“Nawapongeza sana AGPAHI kazi yenu inaonekana,kazi yenu haihitaji tochi ili kuona mnachofanya. Huwezi kuzungumzia mafanikio ya mkoa wa Simiyu kwenye sekta ya afya bila kuwataja AGPAHI”,alisema Mhe. Mtaka. 

“Tunazo taasisi 14 zinazojishughulisha na masuala ya afya mkoani Simiyu. Hawa wadau 13 wangefanya walau robo tu ya kilichofanywa na AGPAHI,tungekuwa na maendeleo makubwa sana katika mkoa wetu na nchi kwa ujumla”,aliongeza Mtaka. 

Mkuu huyo wa mkoa aliipongeza Bodi ya Wakurugenzi wa AGPAHI inayoongozwa na Watanzania kwa kutekeleza miradi inayogusa maisha ya wananchi huku akizitaka taasisi zingine kuiga mfano wa AGPAHI. 

“Wajumbe wa bodi ya AGPAHI mna ujasiri wa kutembelea miradi yenu kwenye mikoa kwa sababu miradi ipo.Nyinyi mna vitu,magari yenu pia yamekuwa yakitusaidia sana.Kuna baadhi ya taasisi hazina ujasiri wa kutembelea miradi kwa sababu hawana miradi,wengine kazi yao ni kugonga semina tu mwaka mzima.Hebu tufanye kazi zinazogusa wananchi tubadilishe mkoa huu”,alieleza Mtaka. 

Katika hatua nyingine Mtaka alisema serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote wa maendeleo mkoani humo ili katika kuwaletea maendeleo wananchi. 

Mtaka alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wananchi kutumia kondomu ili kupunguza maambukizi ya VVU huku akibainisha kuwa kuwa upo umuhimu wa kuvunja ukimya,vijana waelezwe ukweli kuhusu UKIMWI kwamba upo na unaua hivyo wachukue tahadhari. 

Kwa upande wake,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu alisema AGPAHI inatekeleza miradi yake ya UKIMWI kwa kushirikiana na serikali lengo likiwa ni kuhakikisha fedha zinazotolewa na wafadhili zinawanufaisha watanzania. 

“Tunaushukuru mkoa wa Simiyu kwa ushirikiano mnaotupatia,tunajitahidi kufanya kazi kuwafikia wananchi,AGPAHI tunataka mtoto asizaliwe na maambukizi ya VVU,hivyo tutaendelea kushirikiana na serikali katika kutoa huduma za VVU na UKIMWI kwa wananchi”,alisema Dkt. Ngirwamungu. 

Alisema AGPAHI inaendelea kuongeza ubora na upatikanaji wa huduma za matunzo na tiba za VVU kwa watoto wachanga,vijana na watu wazima katika mikoa ya Simiyu,Mwanza,Mara na Shinyanga. 

Meneja Miradi AGPAHI mkoa wa Simiyu Dkt. Julius Sipemba alisema AGPAHI inatoa huduma za VVU na UKIMWI kwa mkoa mzima wa Simiyu ambapo Mkoa wa simiyu una vituo 233 vya kutolea huduma za afya na 73 kati ya hivyo hupata usimamizi wa moja kwa moja kutoka AGPAHI.

Alisema wagonjwa wanaopata huduma kwenye vituo 73 ni sawa na 95% ya wagonjwa wote walioko kwenye vituo 233.

"AGPAHI inaboresha miundombinu kwa kujenga na kukarabati majengo, huduma za maabara kwa kununua madawa na vifaa 'iliwezesha maabara za wilaya kutoka nyota moja mpaka tatu', imetoa magari mapya kwa halmashauri 4 kati ya 6, imetoa pikipiki, msaada wa kuchunguza kifua kikuu, Saratani ya mlango wa kizazi",alieleza Dkt. Sipemba.

Aliongeza kuwa AGPAHI pia inaajiri watoa huduma wa afya kwenye maeneo yenye uhitaji na inatoa mafunzo kwa watoa huduma kulingana na miongozo ya wizara ya afya.

Wakiwa mkoani Simiyu,Wajumbe wa bodi ya AGPAHI wametembelea Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi,kukutana na Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu na Mkuu wa mkoa wa Simiyu pamoja na wadau wa VVU na UKIMWI mkoani Simiyu.

 ANGALIA PICHA ZA MATUKIO HAPA CHINI
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akizungumza katika kikao cha Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa AGPAHI na wadau wa afya mkoani Simiyu Desemba 6,2019. Kushoto ni Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa,kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akiipongeza AGPAHI kwa huduma za VVU na UKIMWI inazotoa mkoani Simiyu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akielezea namna serikali inavyoshirikiana na wadau kuwaletea maendeleo wananchi.
Katibu Tawala mkoa wa Simiyu mhe. Jumanne Sagini akiipongeza AGPAHI kwa kutekeleza miradi inayogusa wananchi mkoani Simiyu.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu akizungumza katika kikao cha wadau wa afya mkoa wa Simiyu. Alisema lengo la AGPAHI ni kuhakikisha hakuna mtoto anazaliwa na maambukizi ya VVU.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu akizungumza katika kikao cha wadau wa afya na kueleza kuwa AGPAHI itaendelea kushirikiana na serikali katika kutoa huduma za VVU na UKIMWI.
Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa akielezea shughuli zinazofanywa na AGPAHI mkoani Simiyu.
Awali Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa akiwashukuru viongozi wa mkoa wa Simiyu kwa kuendelea kushirikiana na AGPAHI katika kutekeleza miradi ya VVU na UKIMWI. Kulia ni Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Simiyu Dkt. Gamitwe Mahazo.
Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Simiyu Dkt. Gamitwe Mahazo akizungumza katika kikao hicho.
Meneja Miradi AGPAHI mkoa wa Simiyu Dkt. Julius Sipemba  akiwasilisha mada kuhusu shughuli zinazofanywa na asasi ya AGPAHI mkoani Simiyu.
Meneja Miradi AGPAHI mkoa wa Simiyu Dkt. Julius Sipemba akielezea maeneo ambayo AGPAHI inahudumia mkoani Simiyu.
Mkuu wa wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kaswaga akichangia hoja wakati wa kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange akichangia hoja wakati wa kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Mganga Mkuu Halmashauri ya wilaya ya Busega Dkt. Godfrey Mbagali akichangia hoja wakati wa kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Kikao kinaendelea.
Mnufaika wa miradi inayotekelezwa na AGPAHI mkoa wa Simiyu Pendo Gidion akielezea namna huduma ya baba,mama na mtoto ilivyomsaidia ambapo aliwataka wanawake wajawazito kujitokeza kupima VVU ili kuepuka kuzaa watoto wenye maambukizi ya VVU.
Kijana James Leonard akielezea jinsi alivyonufaika na Klabu za watoto na vijana zinazohudumiwa na AGPAHI. Aliwataka vijana wajitokeze kupima afya zao na pale wanapobainika kuwa na maambukizi ya VVU basi watumie dawa za kufubaza makali ya VVU kwani kuwa na maambukizi ya VVU siyo mwisho wa maisha.
Kijana Duhye Masunga akiwashauri wazazi kuwa wawazi kwa watoto wao kama wamezaliwa na maambukizi ya VVU
Minza Manyama akiwahamasisha wazazi na walezi kuwa wawazi kwa watoto waliozaliwa na maambukizi ya VVU. Alitumia fursa hiyo kuipongeza AGPAHI kwa huduma za VVU na UKIMWI inazoendelea kutoa kwa wananchi.
Kikao cha wadau wa afya kikiendelea.
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa kwenye kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa kwenye kikao cha wadau wa afya mkoani Simiyu.
Kikao kinaendelea.
Awali Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu (kulia) akimwelezea Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka huduma zinazotolewa na AGPAHI katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI wakati wajumbe wa bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI ilipotembelea ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akielezea namna mkoa wa Simiyu unavyonufaika na huduma zinazotolewa na AGPAHI mkoani Simiyu. Kushoto ni Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa,kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akiwapongeza wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI kwa kusimamia vizuri asasi ya AGPAHI ambapo asasi hiyo imekuwa maarufu sana mkoani Simiyu kutokana na kugusa maisha ya wananchi.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akiipongeza AGPAHI kwa kutekeleza miradi inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja ..alisema 'Tunahitaji local contents zaidi kutoka kwa wadau wanaotekeleza miradi katika mkoa wa Simiyu.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange akiwashukuru AGPAHI kwa kusaidia sekta ya afya mkoani Simiyu.
Awali Mkurugenzi wa AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa akitambulisha wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI baada ya kuwasili katika ofisi ya Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange (wa kwanza kulia),katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange akiwakaribisha wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu akielezea lengo ziara ya wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI mkoani Simiyu. 
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange akiwakaribisha wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI mkoani Simiyu. 
Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Festo Dugange  akiteta jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu wakati wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI wakielekea katika kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi ili kuangalia namna huduma zinavyotolewa.
Kushoto ni Meneja Miradi AGPAHI mkoa wa Simiyu Dkt. Julius Sipemba  akielezea huduma zinazotolewa na AGPAHI katika Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI, Dkt. Edith Ngirwamungu (katikati) akiuliza jambo katika Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi.

Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa katika chumba cha kutunzia mafaili ya wateja katika Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi. Wa kwanza kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Bariadi,Dkt. Mwanaidi Churu akitoa maelezo kwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Bariadi,Dkt. Mwanaidi Churu akionesha kitabu cha kumbukumbu za wateja katika Kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi. 
Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa kwenye chumba cha dawa katika kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi. 
Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya AGPAHI wakiwa nje ya kituo cha Tiba na Matunzo cha Hospitali ya wilaya ya Bariadi. 
Picha ya pamoja uongozi wa mkoa wa Simiyu,AGPAHI na wadau wa afya mkoani Simiyu.
Picha ya pamoja uongozi wa mkoa wa Simiyu,AGPAHI na  wanufaika wa miradi inayotekelezwa na AGPAHI mkoani Simiyu.
Picha ya pamoja uongozi wa mkoa wa Simiyu na AGPAHI.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Form One Selection 2020 Mwanza

Form One Selection 2020 Mwanza Region The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://Mwanza.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020/2021 The following students have been selected to join form one for Mwanza Secondary schools for the… Read More »

The post Form One Selection 2020 Mwanza appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba Mwanza Form one selection 2020

Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba Mwanza Form one selection 2020 The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office Form one selection for the academic year 2020  The following students have been selected to join form one for Mwanza Secondary schools for the… Read More »

The post Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba Mwanza Form one selection 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form One Selection 2020 Mkoa wa Morogoro

Form One Selection 2020 – Waliochaguliwa kidato cha kwanza 2020 Morogoro Region for 2020/2021 Morogoro The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://Morogoro.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020  The following students have been selected to… Read More »

The post Form One Selection 2020 Mkoa wa Morogoro appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Form one selection 2020

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Form one selection 2020 The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office Form one selection for the academic year 2020  The following students have been selected to join form one for Singida Secondary schools for the academic… Read More »

The post Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Form one selection 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form One Selection Singida Region for 2020/2021

Form One Selection 2020 Singida The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office Form one selection for the academic year 2020  The following students have been selected to join form one for Singida Secondary schools for the academic year 2020 Form one… Read More »

The post Form One Selection Singida Region for 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza 2020 Mkoa wa SONGWE

Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametangaza wanafunzi waliochaguliwa kujiunga  na Kidato cha Kwanza  mwaka 2020  kuwa ni  701,038 sawa na asilimia 92.27 ya wanafunzi 759,000 waliofaulu.

Bonyeza Hapo Chini Kuona Majina ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mkoa wa Songwe   Na Mikoa Mingine



Share:

Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Singida- Form one selection 2020

Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Singida- Form one selection 2020 The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://singida.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020  The following students have been selected to join form one for Singida… Read More »

The post Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Singida- Form one selection 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Ikungi Singida Form One Selection 2020

Ikungi Singida Form One Selection 2020 The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://singida.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020  The following students have been selected to join form one for Singida Secondary schools for the… Read More »

The post Ikungi Singida Form One Selection 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

LIVE: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Wa Daraja La Kigongo Busisi Jijini Mwanza

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anaweka jiwe la msingi Ujenzi wa Daraja la Kigongo - Busisi lenye urefu wa 3.2 kilometa katika Ziwa Vitoria  litakalounganisha Mkoa wa Mwanza na Geita.


Share:

Form One Selection 2020 Njombe Region

Form One Selection 2020 – Waliochaguliwa kidato cha kwanza 2020 Njombe Region for 2020 Njombe The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://Njombe.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020  The following students have been selected to… Read More »

The post Form One Selection 2020 Njombe Region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form One Selection 2020 Songwe Region

Form One Selection 2020 – Waliochaguliwa kidato cha kwanza 2020 Songwe Region The List of Selected Candidates is available for each Ward Education Coordinator, Each Board’s Advertising Boards and the Office of the Regional Head Office, Check it here http://songwe.go.tz/ Form one selection for the academic year 2020  The following students have been selected to join form one… Read More »

The post Form One Selection 2020 Songwe Region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Mkuchika Atoa ONYO Kwa Watumishi Wa Umma Wanaokaa Na Barua Za Watu Bila Kuwafikishia Wahusika

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma
Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Menejimenti, Utumishi wa Umma na Utawala bora Kepteni Mstaafu George Mkuchika amewakemea viongozi wa umma wanaokaa na barua za uhamisho wa watumishi bila kuwafikishia wahusika.

Mkuchika ameyasema hayo jijini Dodoma Disemba 6,2019 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandhimisho ya siku ya maadili na haki za binadamu yatakayofanyika Disemba 11,2019 Jijini hapa.

Amesema kuna watu baadhi ya viongozi wanachukua nafasi ya Katibu Mkuu Utumishi kwa kukaa na barua za wafanyakazi wao kinyume cha sheria za utumishi wa umma.

Amesema ili kukabiliana na changamoto hiyo wanapanga kufanya semina kwa viongozi na watumishi wa umma Kuhusu utawala bora na misingi ya maadili.

Mkurugenzi wa idara ya ukuzaji maadili katika Wizara ya Utumishi Fabiani Pokela amesema Serikali inataka taasisi wote ziweke mfumo wa ushughulikiaji wa malalamio ambayo yanatokea kwa wateja mbalimbali yanasababishwa na watumishi wa umma.

Siku ya maadili mwaka huu itafanyika Jijini Dodoma Disemba 11, 2019 ikiwa na kauli mbiu isemayo ‘kuwa maadili katika utumishi wa umma ni nguzo muhimu katika kuimarisha utawala bora na haki za binadamu’.

Mwisho.


Share:

Bodi ya Pamba Tanzania (TCB) yatekeleza agizo la Naibu waziri wa kilimo Hussein Bashe.

SALVATORY NTANDU
Siku chache baada ya Naibu waziri wa kilimo, Husein Bashe kuiagiza bodi ya Pamba Tanzania (TCB) kugawa mbegu za pamba kwa mkopo kwa pamba kwa wakulima wote nchini, hatimaye agizo hilo limeanza kutekelezwa katika wilaya ya mbogwe mkoani Geita.

Mahitaji ya mbegu kwa wilaya ya Mbogwe  ni tani 200 na mbegu ziliyopokelewa ni tani 126.5 kwa AMCOS ambazo zitakopeshwa kwa vyama vya msingi (AMCOS) 35 kwaajili ya msimu wa mwaka 2020.

Akipokea mbegu hizo kwa niaba ya wakulima katika wilaya ya Mbogwe mkoani Geita jana, mkuu wa wilaya ya Mbogwe, Matha Mkupas alisema mbegu hizo zimeletwa kwa wakati muafaka na zitasaidia kuongeza uzalishaji  kwa msimu huu.

“Wakulima walikuwa wamekata tamaa ya kulima zao la pamba kutokana kuuziwa mbegu na kampuni za ununuzi wa pamba lakini baada ya serikali kuagiza zikopeshwe kwa wakulima mwitikio wa ukopaji umekuwa ni mkubwa zaidi”alisema Mkupas.

Mkupas aliwataka viongozi wa vyama vya msingi kuhakikisha mbegu hizo zinawafikia wakulima wote kwa haraka ili kwenda sambamba na msimu wa kilimo ambao umeshaanza sambamba na kudhibiti wakulima kulisha mifugo mbegu hizo kwa msimu uliopita.

Kwa upande wake Mkaguzi wa Pamba wa wilaya ya Mbogwe, Atupele James alisema morali ya wakulima wa pamba kulima zao hilo kwa mwaka huu ilikuwa chini kutokana na kulazimika kununua mbegu kwa sababu baadhi yao bado hawajalipwa fedha.

“Wapo wakulima ambao mpaka sasa bado hawajalipwa fedha zao baada ya kuuza pamba katika msimu uliopita na kampuni zilizonunua mazao yao na kusababisha kushindwa kuendelea na kilimo ila kupatikana kwa mbegu hizi zitawahamasisha kulima”alisema James.

Simon Mtagwa ni mmoja wa wakulima wa pamba katika wilaya ya Mbogwe alisema kucheleweshwa kwa malipo yao baada ya kuuza pamba kumesababisha kushindwa kufanya maandalizi ya msimu mpya wa kilimo kutokana na kushindwa kunua mbegu.

Novemba 29 mwaka huu Naibu waziri wa kilimo Hussein Bashe kwenye kikao cha wadao wa pamba  aliiagiza wakulima  nchini wakopeshwe mbegu ili kwenda sambamba na msimu wa kilimo wa mwaka 2020.

Mwisho.


Share:

Waratibu Elimu Wazembe Kuchukuliwa Hatua Kali Mkoani Songwe

Waratibu Elimu kata na Wasimamizi wa Sekta ya Elimu Mkoa wa Songwe waliobainishwa katika ripoti ya uchunguzi wa hali ya sekta ya Elimu kuwa ni wazembe katika kusimamia maendeleo ya elimu watachukuliwa hatua kali za kinidhamu.

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila amesema hayo jana wakati wa kikao na Waratibu Elimu Kata na Maafisa Elimu ili kutathmini maendeleo ya Sekta ya Elimu kwa mwaka 2019 na kupanga mikakati ya kuboresha elimu kwa mwaka 2020.

“Tuliwapa kazi wadhibiti ubora ya kufanya uchunguzi kwanini Mkoa wetu haufanyi vizuri kielimu na ripoti yao imebainisha uwepo wa uzembe wa waratibu elimu Kata katika usimamizi, sasa nitachukua hatua kali kwa waratibu elimu wote wazembe.”, amesema Kafulila.

Kafulila amesema Waratibu Elimu kata wote walisaini Mkataba ambao uliwataka kusimamia Sekta ya elimu na kuhakikisha kiwango cha elimu kinapanda lakini pia serikali imewawezesha posho na usafiri lakini wapo baadhi yao ambao wameshindwa kutekeleza majukumu yao.

“Serikali imewapa posho na Waratibu Elimu Kata lakini baadhi yao wamebainishwa katika ripoti kuwa wanafanya kazi kwa kuogopana na kuendekeza urafiki, hawawachukulii hatua walimu na wakuu wa shule ambao hawatimizi majukumu yao, hao hatuwezi kuwavumilia.”, amesisitiza Kafulila.

Naye Mwenyekiti wa Wadhibiti Ubora wa Elimu Mkoa wa Songwe Mwalimu Jackson Lwafu amesema walitathmini kwanini baadhi ya shule katika Mkoa wa Songwe zimeshuka kielimu na walibaini kuwa usimamizi dhaifu umechangia kwa kiasi kikubwa.

Lwafu amesema endapo wasimamizi wa Elimu Mkoa wa Songwe watatambua majukumu yao na kuyasimamia, maendeleo ya sekta ya Elimu Mkoa wa Songwe yatakuwa mazuri.

Mratibu Elimu Kata ya Mkukwe Wilayani Songwe Mwalimu Judith Mwasoke amesema taarifa ya wathibiti ubora inasikitisha kwakuwa ili kuwe na mafanikio lazima taratibu zifuatwe hivyo suala la kuoneana aibu na kuogopana halifai na waratibu Elimu Kata wenye tabia hiyo waache.

Afisa Elimu wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma Mtafya Wilson amesema kwa mwaka 2020 watahakikisha walimu wanafundisha vipindi vyote pamoja na kuwasimamia Waratibu Elimu Kata wanatimiza wajibu wao.

Afisa Elimu Mkoa wa Songwe Juma Japhet Kaponda amesema Matokeo ya darasa la saba mwaka 2019 hali haikuwa nzuri kwakuwa Mkoa ulipanda ufaulu kwa asilimia 1.65 kwa kuwa na ufaulu wa asilimia 75 na Mkoa ukishika nafasi ya 21 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2018 wa asilimia 73 na nafasi ya Mkoa wa Songwe ilikuwa 17.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger