Tuesday, 22 October 2019

Halmashauri Ya Wilaya Ya Msalala kinara ukusanyaji wa mapato ya ndani

HALMASHAURI ya Wilaya ya Msalala imekuwa ya kwanza Kitaifa katika ukusanyaji wa mapato kwa kukusanya asilimia hamsini na mbili (52%)  ya makisio ya mapato ya ndani kwa kipindi cha robo ya kwanza ya  mwaka wa fedha 2019/20 huku Halmashauri ya Kyerwa ikiwa ya mwisho kwa kukusanya asilimi tatu tu ya makisio yake.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo alipokuwa akitoa taarifa ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri kwa kipindi cha Julai – Septemba, 2019

Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Msalala imefanikiwa kukusanya mara mbili ya malengo  ya robo ya kwanza ambapo kila halmashauri inatakiwa kukusanya si chini ya asilimia 25 ya makisio ili kukamilisha asilimia 100 kwa robo nne za mwaka wa fedha.

Waziri Jafo alieleza kuwa Bajeti iliyoidhinishwa ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2019/20 ni shilingi Bilioni 765.48; Katika kipindi cha robo ya kwanza (Julai hadi Septemba, 2019) Halmashauri zimekusanya jumla ya shilingi bilioni 166.24 sawa na asilimia 22 ya makisio ya mwaka.

Alifafanua kuwa “Katika kipindi hiki Halmashauri zilipaswa kukusanya asilimia 25 ya makisio yake ya mwaka lakini halmashauri hamsini na nne tu (54) ndio zilizofanya vizuri kwa kukusanya zaidi ya asilimia 25 ya bajeti zao na halmashauri 121 hazikuweza kufikisha asilimia 25 ya mapato yake”.

Aidha, Mhe. Jafo alisema kuwa katika kuzipima Halmashauri zote kwa pamoja Halmashauri ya Jiji la Dododma imekusanya mapato mengi zaidi kuliko Halmashauri zote kwa kukusanya shilingi Bilioni 13.10 na Halmashauri ya Buhigwe imekuwa ya mwisho kwa kukusanya shilingi Milioni 35.15.

Pia Mhe Jafo aliongeza kuwa katika ngazi ya Mikoa, Mkoa wa Rukwa umeongoza kwa kukusanya wastani wa asilimia thethini na moja (31) ya makisio ya Halmashauri za Mkoa huo huku Mkoa wa Mwisho ukiwa ni Mtwara ambao Halmashauri zake zimekusanya wastani wa asilimi kumi na tatu (13) ya makisio yake.

Alisema Katika kipengele hicho cha Mikoa kwa kuzingatia wingi wa mapato Mkoa ambao unaongoza kwa kukusanya mapato ya ndani kwa wingi ni Mkoa wa Dar es salaam ambao umekusanya shilingi Bilioni 39.53 na Mkoa wa Mwisho katika wingi wa ukusanyaji wa mapato ni Mkoa wa Kigoma ambao umekusanya shilingi bilioni 2.12.

Akisoma mchanganuo wa ukusanyaji wa mapato kwa kuzingatia aina ya Halmashauri na vigezo mbalimbali Mhe. Jafo amesema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam imeongoza kundi la Halmashauri za Majiji kwa kukusanya mapato kwa asilimia 38 ya makisio yake ya mwaka huku halmashauri ya Jiji la Dodoma ikiwa ya mwisho katika kundi hili kwa kukusanya kwa asilimia kumi na nane (18%) ya makisio yake ya mwaka.

Mhe. Jafo alitaja Halmashauri za Majiji zilizokusanya mapato ya ndani kwa kigezo cha wingi (Ghafi) kuwa Jiji la Dodoma limeongoza kwa kukusanya shilingi bilioni 13.098 na Halmashauri ya Jiji la Mbeya imekuwa ya mwisho katika kundi hili kwa kukusanya shilingi bilioni 2.74 tu.

Halkadhalika Jafo alitaja Manispaa iliyoongoza kundi la Halmashauri za Manispaa kwa kigezo cha asilimia kuwa ni Manispaa ya Sumbawanga ambayo imekusanya kwa asilimia arobaini na mbili (42) na Manispaa ya mwisho katika kigezo hiki ni Manispaa ya Kigoma ambayo imekusanya kwa asilimia tisa tu ya makisio yake kwa mwaka.

“Katika kigezo cha wingi wa mapato kundi hili linaongozwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ambayo imekusanya shilingi bilioni 13.05 huku Manispaa ya Kigoma ikiwa ya mwisho tena kwa kukusanya kiasi kidogo cha fedha cha shilingi milioni 235.11 alisema Jafo”.

Akifafanua kipengele cha Halmashauri za Miji Jafo alisema kuwa Mji wa Tunduma umeongoza kwa kukusanya kwa asilimia thethini na tisa (39%) na Halmashauri ya Mji wa Nanyamba imekua ya mwisho kwa kukusanya asilimia nne (4%) ya makisio ya mapato yake ya ndani kwa mwaka.

Mhe. Jafo alisema kuwa Halmashauri ya Mji wa Geita imeendelea kuongoza kwa wingi wa mapato katika Halmashauri za Miji kwa kukusanya shilingi bilioni 2.34 na Halmashauri ya mwisho ni Mji wa Nanyamba ambayo imeksuanya shilingi milioni 74.72.

Wakati huo huo Jafo alizataja Halmashauri za Wilaya zilizofanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato kiasilimia kuwa ni Halmashauri ya Msalala ambayo imekusanya kwa asilimia hamisni na mbili (52%) na Halmashauri ya Kyerwa imekuwa ya mwisho kwa kukusanya asilimia tatu (3%) ya makisio ya mapato ya ndani kwa mwaka.

Upande wa wingi wa mapato Mhe. Jafo alitaja Halmashauri ya Wilaya iliyoongoza katika kundi hili kuwa ni Halmashauri ya Chalinze ambayo imekusanya shilingi bilioni 2.05 na ya mwisho ni Halmashauri ya Buhigwe iliyokusanya shilingi milioni thethini na tano (35) tu.

Jafo alisema kuwa katika matumizi ya mapato ya vyanzo vya ndani katika taarifa hii ya robo ya kwanza haionyeshi picha halisi ya uchangiaji wa mapato hayo katika shughuli za maendeleo kwenye sekta ya Elimu, Afya na Maji.

“Uchambuzi kamili wa uchangiaji wa kila halmashauri katika miradi ya maendeleo utafanyika katika robo ya pili na mwisho wa mwaka wa fedha 2019/20 lakini kila Halmashauri ifanye jitihada kuhakikisha inachangia mapato ya ndani kulingana na asilimia inayopaswa kuchangiwa kwa mujibu wa bajeti zake” Alifafanua Jafo.

Aidha, Mhe. Jafo alieleza kuwa katika kipindi cha Julai-Septemba,2019 Halmashauri zilitumia shilingi Bilioni 40.88 kati ya shilingi bilioni 340.68 zilizokasimiwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo swan a asilimia 12.

Mhe. Jafo alikumbushia matumizi sahihi ya mifumo ya kielektroniki ya ukusanyaji wa mapato na mashine za kukusanyia mapato (PoSs) na mifumo ya Kielektroniki ya kutolea taarifa.

Alimalizia  kuwataka viongozi kuweka mikakati madhubuti ya kukusanya mapato kutoka kwenye vyanzo vipya vinavyobuniwa na Halmashauri zao.

(mwisho)



Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya October 22




Share:

Monday, 21 October 2019

Documentation Specialist Jobs at PCI Tanzania

JOB DETAILS: PCI Tanzania implements development programs in different regions in Tanzania and we are increasing the documentation outputs. This Documentation Specialist will support the development of high-quality documents to be shared with externa stakeholders. She/he will work with the technical teams to fully understand the specific programming approach and will accompany the team in writing the documents.… Read More »

The post Documentation Specialist Jobs at PCI Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Project Officer – Gender Advocacy Jobs at World Vision

28-Oct-19 Purpose of the position: To coordinate the development of ENRICH project Gender and Advocacy strategy and oversee the implementation of the strategy. The gender specialist will be responsible for facilitating training on gender equality and Advocacy for staff and partners and for monitoring gender equality and advocacy results. Observe mission and core values of World Vision and… Read More »

The post Project Officer – Gender Advocacy Jobs at World Vision appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Project Administrator Jobs at Rufiji

Position : Project Administrator (1 Post) Reports to: Project Leader (PL)/Principal Investigator (PI) Work station: Rufiji and Kibiti Apply by: October 31, 2019 Institute overview Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. Driven by a core strategic mandate for research, training… Read More »

The post Project Administrator Jobs at Rufiji appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

38 Jobs at Morogoro Urban Water Supply and Sanitation Authority

OVERVIEW MORUWASA is an expanding autonomous Urban Water Supply and Sanitation Authority, which is responsible for supplying of clean, safe water as well as provision of wastewater disposal services for Morogoro Municipality. The general policies and guidelines to run Authority are provided by the Ministry of Water. EWURA and Board of Directors. The Authority is looking for competent,… Read More »

The post 38 Jobs at Morogoro Urban Water Supply and Sanitation Authority appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Marketing Specialist Job at Pralena Networking Ltd

Marketing Specialist Objectives of this Role Obtain a thorough understanding of our products, internal standards, and differentiators to develop strategies aimed at increasing effective communications and brand awareness Document process procedures and process flow, recommending any changes to make process more efficient Analyze qualitative and quantitative data, with special focus on psychographics and buying trend to understand how… Read More »

The post Marketing Specialist Job at Pralena Networking Ltd appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Technical Program Quality Advisor Jobs at Maryland Global Initiatives Tanzania (MGIT)

  Job Summary Maryland Global Initiatives Tanzania (MGIT) is looking for a qualified and dynamic Technical & Program Quality Advisor to work with local implementing partners and RHMTs to monitor quality improvement activities to improve health care services around HIV/AIDS by initiating QI interventions to address gaps within the REACH  project. Minimum Qualification: Bachelor Experience Level: Mid level… Read More »

The post Technical Program Quality Advisor Jobs at Maryland Global Initiatives Tanzania (MGIT) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Maintenance Worker Jobs at Kilombero Sugar Company

Kilombero Sugar Company Maintenance Worker   Kilombero Sugar Company Limited, the largest producer of sugar in the country operating cohesively with Extra Neutral Alcohol Distillery (IDTL) is seeking to recruit a dynamic and result oriented person to develop him/her through a Maintenance Worker in Training programmed to attain the necessary practical process engineering competences including monitoring and controlling plant… Read More »

The post Maintenance Worker Jobs at Kilombero Sugar Company appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Project Administrator Jobs at Ifakara Health Institute

  Ifakara Health Institute Job Summary Position : Project Administrator (1 Post) Reports to: Project Leader (PL)/Principal Investigator (PI) Work station: Rufiji and Kibiti Apply by:  October 31, 2019 Institute overview  Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. Driven by a… Read More »

The post Project Administrator Jobs at Ifakara Health Institute appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Field Workers Jobs at Ifakara Health Institute ( 70 Posts )

   Ifakara Health Institute Job Summary Position:  Field Workers (70 posts) Reports to:  Demographic Coordinator/ Project leader Work station:   Rufiji/Kibiti Apply by: October 31, 2019 Institute overview  Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. Driven by a core strategic mandate for… Read More »

The post Field Workers Jobs at Ifakara Health Institute ( 70 Posts ) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Mahakama yataka kesi ya aliyekuwa Mhasibu Mkuu Takukuru itendewe haki

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema haki itendeke katika kesi ya kumiliki mali ya zaidi ya Sh3.6 bilioni kinyume na kipato halali inayomkabili aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru),Godfrey GugaI na wenzake wawili kwa kuwa washtakiwa hao hawana dhamana.
 
Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba  ameeleza hayo leo Oktoba 21, 2019 wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kuendelea na ushahidi lakini upande wa mashtaka kupitia wakili wa Serikali Silivia Mitanto kudai kuwa kesi hiyo ilikuja kwa  ajili ya kuendelea na ushahidi lakini mawakili wanaosimamia kesi hiyo hawapo wapo mahakama ya mafisadi.

Baada ya maelezo hayo Hakimu Simba alisema hajafurahi kuona kesi hiyo inaahirishwa kwani lazima waitendee haki  kwa sababu mashtaka yanayowakabili washtakiwa hayana dhamana.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 28 mwaka huu kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.


Share:

Wanafunzi wavalishwa maboksi Kichwani ili Kuzuia Wasiangaliziane

Chuo cha The Bhagat Pre-University College, kilichopo nchini India kimeomba msamaha kufuatia kitendo cha kuwavalisha maboksi, Wanafunzi ili kuzuia kupiga chabo wakati wa majaribio ya zoezi hilo.

Taarifa za chuo hicho kufanya tukio hilo, zilisambaa baada ya kupostiwa katika mtandao wa kijamii wa Facebook na mmoja wa wafanyakazi katika chuo hicho ambazo zilionesha wanafunzi wamevaa maboksi, huku sehemu ya mbele la maboksi hayo yapo wazi.

Msamamizi mkuu wa chuo hicho, MB Satish, amesema walitumia njia hiyo kukabiliana na udanganyifu wa kupiga chabo kwa wanafunzi na walifanya hivyo kama jaribio la muda tu kisha waliwatoa maboksi hayo kichwani.

"Hakuna mwanafunzi aliyelazimishwa kuvalia boksi kichwani. Kama unavyoona katika picha hizi kuna baadhi ya wanafunzi ambao hawajazivalia, Waliokuwa wamevalia pia baadhi yao walivua baada ya dakika 15, wengine baada ya dakika 20 na hata sisi wenyewe tuliwambia wazivue baada ya saa moja" amesema MB Satish

"Kati ya wanafunzi 72 ni 56 ndiyo walivaa maboksi kama sehemu ya majaribio, walisema wanajisikia vizuri na jaribio hilo na chuo hakijamsumbua mwanafunzi yeyote kuhusu suala la kuvaa maboksi hayo" ameongeza.

Mamlaka ya usimamizi wa shule nchini India iliamuru chuo hicho kutoa ufafanuzi wa maelezo na kuomba  msamaha juu jaribio hilo.


Share:

Mkuu wa Shule ya Sekondari Mzindakaya Mkoani Rukwa ajisalimisha polisi kwa kubaka Wanafunzi Wawili na Kuwatia Mimba

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaagiza wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Rukwa kuhakikisha Mkuu wa Shule ya Sekondari Mzindakaya iliyopo kata ya Kaengesa, Wilayani Sumbawanga Dastan Mlelwa anafikishwa mahakamani haraka iwezekanavyo baada ya kuwabaka na kuwatia mimba wanafunzi wawili wa kidato cha pili na cha tatu katika shule hiyo.

Amesema kuwa anataarifa kuwa mwalimu huyo tayari amekwishajisalimisha katika mikono ya polisi na hivyo kumtaka kamanda wa polisi mkoa, Kamanda wa TAKUKURU mkoa pamoja na Mkuu wa Usalama wa mkoa kufuatilia jambo hilo ili mwalimu huyo asitoke kwenye mikono ya polisi bali apelekwe mahakamani.

“Hili jambo hatutalifumbia macho, Mkuu wa shule kuwatafuta wanafunzi kimapenzi na mpaka kuwatia mimba, yeye kama mzazi na mwalimu haikubaliki hata kidogo, huu ni ubakaji kwasababu wale wanafunzi wa kidato cha pili na cha tatu hawana umri wa miaka 18 ni chini ya hapo, ni ubakaji,” Alisisitiza.

Katika kusisitiza suala hilo pia ameitaka kamati hiyo kufuatilia kesi ya Mwalimu wa Shule ya Sekondari Mpui iliyoopo Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga aliyembaka na kumpa mimba mwanafunzi wa kidato cha pili na baadaye mwanafunzi huyo kuhamishwa katika shule ya Sekondari Mazwi iliyopo Manispaa ya Sumbawanga. 

Katika hatua nyingine Mh. Wangabo amewaagiza wajumbe hao wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa kufuatilia kesi ya wizi wa mifugo inayomhusisha Afisa mifugo wa mji mdogo wa laela, wilayani Sumbawanga Emanuel Tluwey baada ya kukamatwa akiwa anachinja ng’ombe wa wizi kesi ambayo ilifikishwa polisi na kuonya kuwa kesi hiyo isifinyangwe finyangwe ili mwizi huyo  asichukuliwe hatua.

“Lakini kuna Mazingira tata huenda kesi ikafinyangwa finyangwa na mwizi huyu asichukuliwe hatua, sasa narudisha kwa timu hii hapa, TAKUKURU yuko pale, jeshi la polisi na vyombo vingine vya usalama fuatilieni suala hili kule Laela huyu mwizi wa mifugo lazima achukuliwe hatua ya kisheria afikishwe mahakamani haraka iwezekanavyo,” Alisema.
 
Mh. Wangabo ameyasema hayo wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika kikao maalum kilichowajumuisha wajumbe wa kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na watumishi wa seksheni ya Elimu na watumishi wa seksheni ya uchumi na uzalishaji inayojumuisha watumishi wa  mifugo katika Mkoa.

Mh. Wangabo amesema kuwa nia ya kuyafanya hayo ni kupiga vita uhalifu ndani ya mkoa pamoja na ubakaji wa wanafunzi na kuonya kuwa itafika wakati kutakuwa na kura za maoni mashuleni kwa wanafunzi ili kumbaini anayewashawishi wanafunzi hao kujiingiza katika suala la mapenzi katika umri mdogo.

IMETOLEWA NA
OFISI YA MKUU WA MKOA WA RUKWA


Share:

Tanzania Yateuliwa Kuwa Mwenyeji Wa Mkutano Wa Mawaziri Sekta Za Mazingira, Maliasili Na Utalii SADC

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo amefungua mkutano wa Mawaziri wa Sekta za Mazingira, Maliasili na Utalii wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Arusha kaskazini mwa nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki, amesema kuwa, mkutano huo utajadili mwenendo wa hali ya mazingira, mabadiliko ya hali ya hewa na hali ya utalii na misitu katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Aidha amesema kuwa, mkutano huo utajadili utekelezaji wa mikakati ya hifadhi na usimamizi wa mazingira na kupitia mikakati na miongozo juu ya masuala hayo katika kutekeleza majukumu ya kila nchi ndani ya jumuiya hiyo ya SADC.

Wakati huo huo, Tanzania imekabidhiwa Uenyekiti wa Shirikisho la Mashauriano ya Kisheria la Asia na Afrika (Asian-African Legal Consultative Organization (AALCO) 58th Annual Session).

Mkutano huo umefunguliwa na mikutano ya Wataalamu wa Sekta ya Wanyamapori na mkutano wa Makatibu Wakuu wa Sekta za Mazingira, Maliasili na Utalii ulioanza leo Oktoba 21 hadi 24, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Mapema mwezi Agosti mwaka huu, nchi ya Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa 39 wa nchi wanachama wa Jumuiya ya maendelea ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Rais John Pombe Magufuli alikabidhiwa na kupokea rasmi jukumu la uenyekiti wa jumuiya hiyo.


Share:

Upelelezi kesi ya anayedaiwa kumuua mkewe kwa Kumchoma Moto Wakamilika

Hatimaye upelelezi wa kesi inayomkabili mfanyabiashara Khamis Said anayedaiwa kumuua na kisha kumchoma na moto wa magunia mawili ya mkaa mke wake, Naomi Marijani, na kisha mabaki ya mwili huo kwenda kuyafukia shambani kwake Mkuranga, umekamilika.

Wakili  wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon amedai hayo leo Jumatatu Oktoba 21, 2019 mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kuwa shauri lilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi umekamilika.

Simon amedai jalada la shauri hilo lipo kwenye hatua ya uchapaji kwa ajili ya maandalizi ili lipelekwe Mahakama Kuu ya Tanzania hivyo ameiomba mahakama hiyo ihairishe kesi hiyo.
 
Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mkuu wa Mahakama hiyo, Salumu Ally, aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 4, 2019.

Mshtakiwa huyo anadiwa kutenda kosa hilo Mei 15, 2019, nyumbani kwake maeneo ya Gezaulole Kigamboni.


Share:

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi ya Mbowe na Vigogo wengine CHADEMA

Viongozi 9 wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe wanatarajia kuanza kujitetea kwa siku tatu mfululizo kuanzia November 4, 5 na 8, 2019 katika kesi ya uchochezi inayowakabili Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Hatua ya viongozi hao wanaokabiliwa na Kesi ya jinai namba 112 ya 2018 inatokana na uamuzi mdogo uliotolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambapo katika uamuzi huo Viongozi wa CHADEMA wamewakilishwa na Wakili, Jeremiah Mtobesya na Hekima Mwasipu, huku upande wa Serikali ukiwakilishwa na Wakili Faraja Nchimbi, Wankyo Simon na Salim Msemo.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Simba amesema wiki tatu zilizoombwa na upande wa utetezi ni nyingi  hivyo amewapatia wiki mbili ili waweze kuwaanda washtakiwa waanze kujitetea kabla ya mashahidi wao na kusema mashahidi katika kesi hiyo mbali na washtakiwa ni wengi na wanafikia 200, hivyo upande wa utetezi wanahitaji kupewa muda wa maandalizi.

Pia Hakimu Simba amesema kuhusu kielelezo namba 5 ambacho ni video ya maandamano kilichoombwa na upande wa utetezi ili Wataalamu wao wakichunguze kwa sababu wana wasiwasi kimehaririwa, watakitumia kupitia vifaa vya mahakama kama vilivyotumiwa na upande wa mashtaka.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger