Wednesday, 16 October 2019

Nafasi 9 za kazi UDSM-Jobs at UDSM October 2019

VACANCIES AT UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM The University of Dar es Salaam invites applications from suitably qualified Tanzanians to be considered for immediate employment to fill the following vacant posts:  Job Title: Laboratory Scientist III (2 posts) in the following  University Units: College of Natural and Applied Sciences:  (a) Qualifications and Experience:  Laboratory Scientist III – Department… Read More »

The post Nafasi 9 za kazi UDSM-Jobs at UDSM October 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

UDSM: ERASMUS SCHOLARSHIP- Call for Application 2019

ERASMUS SCHOLARSHIP- Call for Application University of Dar es salaam in collaboration with other Universities are glad to announce a call for applications for an Erasmus+mobility  scholarship to Germany. You are a student? You want to gotoGermany for 4 months? APPLY NOW for an Erasmus+ scholarship!  CALL FOR APPLICATIONS 2020  Ardhi University, University of Dar es Salaam, University… Read More »

The post UDSM: ERASMUS SCHOLARSHIP- Call for Application 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

RAIS MAGUFULI ATAMANI MSANII HARMONIZE AKAGOMBEE UBUNGE TANDAHIMBA

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika ziara yake mkoani Lindi, Wilaya ya Ruangwa jana Oktoba 15, 2019 alisema anatamani msanii Rajabu Abduli maarufu kama Harmonize kugombea Ubunge Jimbo la Tandahimba.

Akitoa shukrani na pongezi kwa watu waliotoa burudani katika mkutano huo, Rais Magufuli alisema “La kumalizia nawapongeza sana waimbaji hawa wakina baba, lakini nampongeza sana Harmonize sijui anatoka jimbo gani?

“Anatoka jimbo gani huyu? Tandahimba? Mbunge wa kule ni nani?. Aaa ningetamani kweli Harmonize akagombee kule akawe mbunge wa Tandahimba” alisema
Share:

BITEKO AOMBA MABORESHO YA MIUNDOMBINU "KUVUTIA WAWEKEZAJI JIMBONI"

Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko (CCM) ameomba Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) pamoja na Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) kuongeza
kasi ya uboreshaji miundombinu ya barabara jimboni humo ili kuvutia wawekezaji zaidi.

Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini ametoa ombi hilo Oktoba 15, 2019 kwenye kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa Geita ambacho pamoja na mambo mengine kimejadili utekelezaji wa miradi mbalimbali ya barabara.

Amesema wakati Serikali inaendelea kuboresha mapori yaliyopo wilayani Bukombe kuwa na hadhi ya kuvutia watalii, ubora wa miundombinu ya barabara utavutia zaidi wawekezaji hivyo mamlaka hizo ni vyema zikatekeleza miundombinu iliyokwisha ingiza kwenye mpango.

Naye Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Mkuu wa Mkoa Geita, Mhandisi Robert Gabriel ameshauri mamlaka hizo ikiwemo TARURA kuzingatia vipaumbele vya wawakilishi wa
wananchi wakiwemo wabunge zinapokuwa zinatekeleza miradi ya barabara.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mbunge wa Bukombe, Doto Biteko (aliyesimama) ambaye pia ni Waziri wa Madini akizungumza kwenye kikao hicho. Waliokaa kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa Geita Alhaji Said Kalidushi, Mkuu wa Mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel, Mbunge wa Nyang'hwale Nassor Amar pamoja na Mbunge wa Busanda Lolensia Bukwimba.
 Mkuu wa Mkoa Geita, Mhandisi Robert Gabriel akizungumza kwenye kikao hicho.
 Diwani wa Kata ya Busonzo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Bukombe, Safari Mayala (CCM) akichangia hoja kwenye kikao hicho.
 Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Doto Biteko (kulia) ambaye pia ni Waziri wa Madini akikagua taarifa ya utekelezaji miradi mbalimbali ya barabara mkoani Geita. Kushoto ni Mbunge wa Nyang'hwale Nassor.
Tazama Video hapa chini


Share:

Malawi Yakanusha Kuwa Na Mgonjwa Wa Ebola

Malawi imekanusha ripoti zilizoenea kwamba mtu mmoja amegunduliwa kuwa na Ebola kwenye eneo la Karonga linalopakana na Tanzania.

Hofu hiyo ilitokea Jumapili wakati wafanyakazi wa afya kwenye eneo hilo waligundua mwanamume mwenye umri wa miaka 37 kuwa na dalili za Ebola.

Afisa wa afya katika eneo hilo,  Louis Tukula amesema mtu huyo alikuwa na maambukizi ya bakteria na si Ebola.

Amesema eneo hilo limekuwa katika hali ya tahadhari tokea ugonjwa wa Ebola uripotiwe katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.


Share:

Asilimilia 68 Wajiandikisha Kupiga Kura Uchaguzi Serikali za Mitaa

Watanzania 15,543,604 sawa na asilimia 68 wameshajiandikisha kwenye daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali unaotarajiwa kufanyika Novemba 24 mwaka huu.

Aidha, Mkoa wa Pwani umeongoza kwa kundikisha watu 473,639 sawa na asilimia 80, mkoa wa Dar es Salaam uliondikisha watu 2,064,820 sawa na asilimia 77 na Tanga ulioandikisha watu 823,194 sawa na asilimia 76.

Mikoa mingine ni Mtwara watu 530,523, Lindi watu 353,649 sawa na asilimia 75 na Iringa watu 381,134 sawa na asilimia 74.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo, ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam, wakati akielezea tathimini ya uandikishaji ulioanza Octoba 8 hadi 14.

"Tamisemi imejiwekea malengo ya kuandikisha wapiga kura watapatao milioni 22.916 wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu, baada ya hamasa iliyofanywa na wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya watendaji idadi ya waliojiandikisha imefika watu milioni 15.543 sawa na asilimia 68 ya lengo," Jafo amesema

Aidha, amesema mikoa ambayo ipo chini kiuandikishaji hadi juzi ni Kilimanjaro ambayo imeandikisha watu 446,954 sawa na asilimia 48, Kigoma watu 555,856 sawa na asilimia 53 na Arusha watu 551,614 sawa na asilimia 59.

Amesema pia zipo Halmashauri sita ambazo zimefanya vizuri zaidi kwa kuandikisha zaidi ya asilimia 95 na kuendelea ambazo ni Mpanda, Mlele, Kibiti, Ngorongoro, Songwe na Mbozi.

Jafo amezitaja pia Halmashauri ambazo zimeandikisha chini ya asilimia 50 ambazo Manispaa za Moshi kwa asilimia 31, Jiji la Arusha kwa asilimia 32, Msimbo asilimia 41, Kigoma asilimia 43, Jiji la Mbeya asilimia 46 na Musoma asilimia 49.


Share:

SUA: CALL FOR APPLICATIONS FOR MSc SCHOLARSHIPS IN GREEN RESOURCES INNOVATION FOR LIVELIHOOD IMPROVEMENT PROJECT

SUA: CALL FOR APPLICATIONS FOR MSc SCHOLARSHIPS IN GREEN RESOURCES INNOVATION FOR LIVELIHOOD IMPROVEMENT PROJECT Background Sokoine University of Agriculture (SUA) and other partner Universities and research institutions in Tanzania, in collaboration with the University of Copenhagen (UCPH) is implementing a collaborative research project titled “Green resources Innovations for Livelihood improvement (GRILI)”. The project is supported by the Danish Development… Read More »

The post SUA: CALL FOR APPLICATIONS FOR MSc SCHOLARSHIPS IN GREEN RESOURCES INNOVATION FOR LIVELIHOOD IMPROVEMENT PROJECT appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

SUA-CALL FOR PAPERS: 4TH CONFERENCE OF THE RANGELAND SOCIETY OF TANZANIA 23RD TO 24TH MARCH 2020, MOROGORO, TANZANIA

The Rangeland Society of Tanzania (RST) cordially invites abstracts for the 4th Scientific Conference to be held at EDEMA Hotel in Morogoro, Tanzania from 23rd to 24th March, 2020. FINAL DATE OF RECEIVING ABSTRACTS IS 31ST DECEMBER 2019 Authors of ACCEPTED ABSTRACTS will be notified by 20th January 2020 and will be requested to submit FULL PAPERS up to 20th February… Read More »

The post SUA-CALL FOR PAPERS: 4TH CONFERENCE OF THE RANGELAND SOCIETY OF TANZANIA 23RD TO 24TH MARCH 2020, MOROGORO, TANZANIA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano October 16























Share:

Tuesday, 15 October 2019

ORODHA YA WANAFUNZI 10 BORA WAVULANA MATOKEO DARASA LA SABA 2019

Baraza la Mitihani la Taifa la Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi ambako mikoa ya kanda ya ziwa imeonekana kuongoza kwa kushika nafasi zote 10 bora kwa wavulana.

Katika matokeo hayo yaliotangazwa leo Jumanne Oktoba 15, 2019 nafasi ya kwanza hadi ya 10 katika orodha ya wavulana waliofanya vizuri zimeshikwa na wanafunzi kutoka katika mikoa ya kanda ya ziwa.

Nafasi ya kwanza imekwenda kwa Francis Gwaji kutoka shule ya Paradise ya mkoa wa Geita, wakati nafasi ya pili hadi ya nne ilichukuliwa na wanafunzi wa shule ya Graiyaki ya Mara ambao ni Victor Godfrey, Aziz Yassin na Goldie Hihayuma.

Nafasi ya tano imeshikwa na Daniel Daniel wa shule ya Little ya Shinyanga huku nafasi ya sita ikichukuliwa na Hilary Nassor wa shule Peaceland ya Mwanza.

Bado mikoa ya kanda ya ziwa imeendelea kutesa katika nafasi ya saba ambayo imeshikiliwa na Mbelele Mbelele wa Kwema Modern iliyopo Shinyanga, nafasi ya nane ikishikwa na Derick Lema wa shule ya Musabe mkoani Mwanza.

Namba tisa imechukuliwa na Athanas Sekuro wa Paradise ya Geita na dimba la wavulana kumi bora likifungwa na Aron Mabuga kutoka shule ya Kwema Modern ya Shinyanga.
Share:

SHULE 10 BORA KITAIFA MATOKEO DARASA LA SABA 2019,WANAFUNZI BORA

Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya kumaliza elimu ya msingi mwaka 2019 ambapo asilimia 81.50 ya watahiniwa 933,369 wamefaulu mtihani huo huku watahiniwa 909 wakifutiwa matokeo kwa sababu ya udanganyifu.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumanne Oktoba 15, 2019 Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk Charles Msonde amesema kwa jumla yanaonyesha ufaulu umeongezeka kwa asililia 3.78 lakini ufaulu katika somo la Kiingereza bado ni mdogo likilinganishwa na masomo mengine.

"Ufaulu katika somo la Kiingereza unaendelea kuimarika mwaka hadi mwaka hivyo juhudi za makusudi zinahitajika kuendelea kufanyika ili kuinua kiwango cha ufaulu katika somo hili," amesema Dk Msonde.

Aidha katika matokeo hayo, Grace Imori Manga wa shule ya msingi Graiyaki ya mkoani Mara ametangazwa kuwa wa kwanza kitaifa akifuatiwa na Francis Gwani wa shule ya msingi Paradise ya mkoani Geita na namba tatu imeshikiliwa na Loi Kitundu wa Shule ya msingi Mbezi ya Dar es Salaam.

Wengine katika orodha ya 10 bora ni Victor Godfrey wa shule ya msingi Graiyaki, Azizi Yassin wa Graiyaki goldie Hhayuma wa Graiyaki, Daniel Daniel wa shule ya msingi Little Mkoani Shinyanga, Hilary Nassor wa Peaceland ya Mwanza, Mbelele Mbelele wa Kwema Modern ya Shinyanga na Nyanswi Richard wa Graiyaki ya Mara.

Shule 10 bora kitaifa ni Graiyaki ya Mara, Twibhoki ya Mara, Kemebos ya Kagera, Little Treasures ya Shinyanga, Musabe ya Mwanza, Tulele ya Mwanza, Kwema Morden ya Shinyanga, Peaceland ya Mwanza, Mugini ya Mwanza na Rocken Hill ya Shinyanga.

Kimkoa, Mkoa wa Dar es Salaam umeshika namba moja ukifuatiwa na Arusha, Iringa, Kagera, Katavi, Kilimanjaro, Mbeya, Simiyu, Njombe na Pwani.

Halmashauri 10 bora zimeongozwa na Arusha jiji, Ilemela, Kinondoni, Mwanza jiji, Ilala Manispaa, Moshi Manispaa, Bukoba Manispaa, Iringa Manispaa, Biharamulo na Arusha
Share:

Breking News : HAYA HAPA MATOKEO YA DARASA LA SABA 2019

Share:

NECTA yatangaza matokeo ya Darasa la Saba 2019. Ufaulu waongezeka kwa asilimia 3.78

Matokeo ya darasa la saba 2019, yametangazwa. NECTA imeeleza ufaulu umeongezeka kwa asilimia 3.78. Waliofaulu ni asilimia 81.50 ya watahiniwa 933,369. Pia Watahiniwa 909 wamefutiwa matokeo kwa sababu mbalimbali ikiwemo udanganyifu.

Dk. Msonde amesema mwanafunzi aliyeongoza Kitaifa ni Grace Manga kutoka Shule ya Msingi Graiyaki Mara, akifuatiwa na Francis Gwagi kutoka Shule ya Msingi Paradise ya Geita.

Amesema kuwa aliyeshika nafasi ya tatu ni Loi  Kitundu kutoka Shule ya Msingi Mbezi ya Dar  es Salaam, na Victor Godfrey kutoka Graiyaki ameshika nafasi ya nne.

"Katika ufaulu wa masomo, somo la Kiswahili, Kiingereza na Sayansi katika mtihani huo ufaulu wake umepanda na somo la Hisabati umeshuka,"


Share:

Advertising Key Accounts Manager (KAM) at Jumia

Advertising Key Accounts Manager (KAM)   We are currently looking for talented people with a passion for emerging markets and Africa to join our team and embark on our exciting journey. Jumia Services is the Logistics Marketplace company of Jumia. The mission of Jumia Services is to create a connected and integrated network of service providers, which addresses in… Read More »

The post Advertising Key Accounts Manager (KAM) at Jumia appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Madson Property Limited Inakuletea Mkopo Wa Viwanja Usio Na Riba Wala Dhamana

MADSON PROPERTY LIMITED
inakuletea Mkopo wa Viwanja usio na riba wala dhamana
✅Maeneo yapo GOBA, BOKO, BAGAMOYO, KIBAHA NA VIGWAZA.

📌Goba kinzudi- 35,000
📌Goba njia nne- 38,000
📌Goba mpakani- 32,000
📌Goba Kulangwa-30,000
✅ BOKO viwanja vipo karibu na St Joseph University- 32,000
✅KIBAHA- 11,000
✅BAGAMOYO-13,000
✅ Vigwaza-mashamba 2M kwa hekari moja.
 
NB: Bei hizo ni kwa sqm moja na Viwanja vyetu vimepimwa na Hati zipo tayari.
 
Karibuni ofisi zetu zipo Mwenge Tower Opposite na Mlimani city

Contact: 0718 65 71 89


Share:

Regional Inclusion Specialists at RTI International

Regional Inclusion Specialists at RTI International RTI is an independent, nonprofit institute that provides research, development, and technical services to government and commercial clients worldwide. RTI is recruiting candidates for the USAID-Funded Tanzania Arithmetic and Inclusion Education Project RTI International is accepting applications from qualified individuals for the recently awarded USAID/Arithmetic and Inclusive Education Activity (AIE). AIE is… Read More »

The post Regional Inclusion Specialists at RTI International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

CHADEMA watoa Kauli kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema hawatasusia uchaguzi wa Serikali za mitaa wa Novemba 24 mwaka huu na amewataka viongozi, wanachama na Watanzania kuhamasishana kujiandikisha.

Amesema hayo leo wakati akizungumza na waandishi ambapo ameeleza  uchaguzi huo ndio unawaleta viongozi wanaokwenda kutatua changamoto za wananchi hivyo kuacha serikali ifanye uamuzi ni kosa.

“Tunapaswa kuweka kando tofauti zetu, twendeni kwa wingi tukajiandikishe ili tushiriki kwenye uchaguzi huu muhimu,” amesema Mbowe

Ameendelea kwa kusema wananchi kusuasua kwenda kujiandikisha ni matokeo ya kile alichodai kuwa ni serikali  kuweka msisitizo katika kuwazuia watu wa upinzani kufanya mikutano ya kisiasa.

“Ni makosa makubwa na aibu kususia. Kwa muda wa siku tatu zilizoongozwa, viongozi wote wa kada zote, wahamasishane watoke kwa wingi kwenda kujiandikisha, hatuna sababu za kususia kwani tutakuwa tumesusia maisha yetu,” amesisitiza Mbowe

“Tunakwenda kushiriki uchaguzi huu na tutashinda, hatutakuwa woga na haya ni mapambano ya kisiasa, tutatumia nguvu za umma kuhakikisha tunashinda uchaguzi huu.”


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger