Monday, 14 January 2019

AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMPA MIMBA DADA YAKE



Picha haihusiani na habari hapa chini

Gabriel Nyantori (25) amefikishwa mbele ya mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wilaya ya Serengeti mkoani Mara akituhumiwa kwa makosa ya kuzini na dada yake na kumpa mimba.

Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Ismael Ngaile, mwendesha mashitaka, Faru Mayengela leo Jumatatu Januari 14, 2019 amesema mshitakiwa anakabiliwa na makosa mawili.

Amesema kosa la kwanza ni kuzini na dada yake mwenye umri wa miaka (16) mwanafunzi wa darasa la saba Shule ya Msingi Kibeyo na kosa la pili ni kumpa mimba dada yake, makosa ambayo aliyatenda Aprili 30, 2018 nyumbani kwao, Kibeyo.


Na Anthony Mayunga, Mwananchi
Share:

POLISI WATOA SABABU ZA TRAFIKI KUMTEMBEZEA KICHAPO DEREVA WA LORI


Jeshi la Polisi mkoani Songwe limeeleza sababu ya askari wa usalama barabarani kumshambulia dereva kwa kumpiga kuwa alitumia lugha ya matusi na kutotii amri ya kumtaka atoe ushirikiano kwa wanausalama hao ambao walikuwa wakifanya kazi kwa kushirikiana na maofisa toka Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchikavu (Sumatra).


Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa Yusuph Sarungi amewaambia waandishi wa habari leo Jumatatu Januari 14, 2019 kuwa tukio hilo lilitokea juzi Jumamosi Januari 12, 2019 saa 2:30 asubuhi katika eneo la Transforma, halmashauri ya mji wa Tunduma wilayani Momba wakati askari hao wakishirikiana na maofisa toka Sumatra wakiwa kwenye ukaguzi wa magari mbalimbali.

Amesema dereva huyo Mawazo Jairos (29) mkazi wa Mbeya aliyekuwa akiendesha gari aina ya Mistubishi Fuso lenye namba za usajili T842 AAC, baada ya kusimamishwa alianza kutoa lugha za kashifa na matusi kwa askari na maofisa wa Sumatra.

Kamanda huyo amesema Jairos aliliondoa gari bila ya kuruhusiwa kwa kupitia barabara ya vumbi hali iliyolazimu askari hao kumfuatilia na kumkamata tena katika eneo la Makambini ambapo walimzuia tena.

Sarungi amesema dereva huyo aliteremka kwenye gari kwa jazba huku akiendelea kutoa matusi na kumshambulia askari...... 
Na Stephano Simbeye, Mwananchi
Share:

MAKOCHA WAPYA WA SINGIDA UNITED WAANZA KUCHAPA KAZI


Kikosi cha Singida United

Klabu ya soka ya Singida United imethibitisha kuwa makocha wao wapya wamewasili jijini Mwanza na kuungana na timu tayari kuanza kazi ya kusaka alama tatu dhidi ya Mbao FC.

Mkurugenzi wa Singida United Festo Sanga ameiambia www.eatv.tv kuwa benchi lao hilo jipya la ufundi limechukua majukumu tayari kutoka kwa makocha waliokuwa na timu.

''Makocha wetu wameshaungana na timu Mwanza, tayari kwa mchezo dhidi ya Mbao FC siku ya Jumatano, makocha hao ni kocha mkuu Dragan Popadic, kocha msaidizi Dusan Kondic na wataendelea na kocha wa makipa Mirambo'', amesema Sanga.

Makocha wapya wa Singida United.

Aliyekuwa kocha mkuu wa Singida United, Hemed Morocco amepewa majukumu katika timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys. Makocha wengine Jabir Mahamoud na Shadrack Sanjigwa wataendelea na kikosi B cha timu hiyo.

Singida United ambayo msimu uliopita ilimaliza katika nafasi ya tano, kwasasa ipo katika nafasi ya 10 wakiwa na alama 24 katika mechi 20 walizocheza.
Via>> EATV
Share:

MWANAFUNZI AIBURUZA SHULE MAHAKAMANI KISA NDEVU



Mwanafunzi wa chuo cha St. John nchini Zimbabwe ameupeleka uongozi wa chuo hicho mahakamani, baada ya kuzuiwa kuingia chuoni kwa kosa la kufuga ndevu.

Baba wa mtoto huyo Bw. Mohammed Ismail, amefungua shtaka rasmi kwa niaba ya mtoto wake kwenye Mahakama Kuu ya nchi hiyo, akidai kwamba kitendo hicho ni kuvunja katiba ya nchi na unyanyasaji.

Akiendelea kuelezea tukio hilo, Bw. Mohamed amesema kwamba mtoto wake huyo amekuwa akirudishwa mara kwa mara na uongozi wa chuo, ili anyoe nywele wakidai kuwa anakiuka sheria za chuo.

Baba huyo amesema kwamba suala hilo linaruhusiwa kwa mujibu wa dini yao ya Kiislam na kwamba mtoto wake alikuwa anasoma ili aje kuwa 'Imam', lakini uongozi wa chuo hauruhusu suala hilo, jambo ambalo limekuwa likimpa shida mwanafunzi huyo kwa kurudishwa nyumbani mara kwa mara.

Hata hivyo Mahakama ya nchi hiyo bado haijataja tarehe ya kusikiliza kesi hiyo.
Share:

MBOWE,MATIKO WAITWA MAHAKAMA YA RUFAA


Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko wakiwa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam

KESI ya kupinga kurejeshewa dhamana iliyofunguliwa na serikali dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasim na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na Mwekahazina wa Baraza la Wanawake la chama hicho (BAWACHA), Esther Matiko, itasikilizwa Mahakama ya Rufaa jijini Dar es Salaam, tarehe 18 Februari mwaka huu. 

Serikali iliwasilisha Mahakama ya Rufaa, maombi ya kuwazuia Mbowe na Matiko kurejeshewa dhamana zao. Ni baada ya Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, kutupilia mbali mapingamizi ya serikali yaliyotaka mahakama hiyo kutosikiliza shauri lililofunguliwa na Mbowe na Matiko.

Kwa mujibu wa vyanzo via taarifa kutoka Mahakama ya Rufaa na ambazo zimethibitishwa na Prof. Abdallah Safari, ambaye anaongoza jopo la mawakili katika kesi hiyo, ni kwamba “Mbowe na Matiko, watafika mbele ya majaji wa mahakama ya rufaa, Jumatatu ya tarehe 18 Februari.”

Mbowe ambaye pia ni mbunge wa Hai, mkoani Kilimanjaro na Kiongozi wa Kambi rasmi ya upinzani bungeni, alifutiwa dhamana na mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa madai ya kukiuka masharti ya dhamana aliyopewa.

Katika uamuzi wake, mahakama ilisema, maelezo yaliyotolewa na Mbowe, mdhamini wake na wakili wake, yalilenga kuidanganya mahakama.

Naye Matiko ambaye pia ni mbunge wa Tarime Mjini, alifutiwa dhamana na mahakama baada ya kushindwa kufika mahakamani kwa mara mobile mfululizo kwa maelezo kuwa alikuwa nje ya nchi kwa shughuli za Bunge.

Chanzo- Mwanahalisionline
Share:

WATAWA,WANAKIJIJI WATAKIWA KUTUMIA BUSARA KUMALIZA MGOGORO WA ARDHI .

Na.Amiri kilagalila. Wakazi wa Kijiji cha MADOBOLE Kata ya LUPONDE Wilayani NJOMBE pamoja na Shirika la Watawa wa Kanisa Katoliki wa Jimbo la Njombe Wametakiwa kutumia busara kumaliza mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya Miaka Kumi na Tatu Sasa. Kauli Hiyo Imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka mara baada ya kutembelea eneo lenye mgogoro na kusikiliza pande hizo mbili zinazogombewa eneo lililopo ndani ya eneo linalodaiwa kumilikiwa kisheria na watawa hao. “Tutawatuma wataalamu hapa wachukue ramani ya shamba hilo lote namba 535 waje wapitie mipaka…

Source

Share:

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA ZITTO NA WENZAKE KUPINGA MUSWADA

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeifuta kesi iliyofunguliwa na Kiongozi wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe na wenzake wa vyama vya upinzani waliyokuwa wakiitaka mahakama hiyo kuzuia kusomwa kwa Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa wakidai kuwa uko kinyume na katiba ya nchi. Mahakama imetoa uamuzi huo leo Jumatatu, Januari 14, 2018 ambapo walalamikaji, Zitto na wenzake wamekubali maamuzi hayo na kusema sasa nguvu yao ni kwenda kuupinga muswada huo kwenye kamati za bunge. Jaji Benhajo Masoud amesema Mahakama imeliondoa shauri hilo baada ya waombaji kuchanganya…

Source

Share:

MAMA ALIYEMFANYIA MTOTO UKATILI AFIKISHWA MAHAKAMANI.

Na,Naomi Milton Serengeti. Mwanamke mmoja aitwaye Penina Petro(20) mkazi wa Kijiji cha Nyamakendo wilayani hapa amefikishwa mbele ya mahakama ya wilaya ya Serengeti kwa kosa la kumfanyia ukatili mtoto mwenye umri wa miaka 6(jina limehifadhiwa). Mwendesha mashtaka wa Jamhuri Faru Mayengela mbele ya Hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya Ismael Ngaile alisema katika shauri la Jinai namba 5/2019 mshitakiwa anakabiliwa na kosa moja la utesaji wa mtoto kinyume na kifungu namba 169 A cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002. Mshitakiwa alitenda kosa hilo Januari 12…

Source

Share:

BIBI ANUSURIKA KUFA AKIPAMBANA NA MAMBA AKIOGA ZIWA VICTORIA

Mkazi wa kitongoji cha Mwibale wilayani Serengeti, Chibona Matoyo (64) akihojiwa na Mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Daniel Makaka (kushoto) baada ya bibi huyo kunusurika kifo kufuatia kushambuliwa na mamba alipokuwa akioga ndani ya Ziwa Victoria, wilayani humo.


 Chibona Matoyo (64), mkazi wa Kijiji cha Kanyala Wilaya ya Sengerema, Mara amenusurika kifo baada ya kujeruhiwa na mamba wakati akioga katika Ziwa Victoria.

Katika tukio hilo lilitokea Alhamisi iliyopita, Chibona alivunjika mikono na kujeruhiwa paji la uso na sasa anapatiwa matibabu kwenye Kituo cha Afya Mwangika, Buchosa wilayani humo.

Akizungumza na Mwananchi jana, mama huyo mwenye watoto watano na wajukuu tisa, alisema wavuvi ndio waliookoa maisha yake baada ya kupiga kelele akiomba msaada.

“Walipoona napiga kelele walifika eneo la tukio na kunikuta napambana na mamba, walinisaidia kujinasua, walifanikiwa,” alisema.

Baada ya kupata taarifa za tukio hilo, mume wa Chibona, Ernest Majula (81) aliangua kilioakisema mkewe amepata kilema na kuiomba Serikali kuchukua hatua kuwadhibiti wanyama hao.

Mtoto wa mama huyo, Agnes Majula alisema wamekuwa na mazoea ya kwenda kuoga ziwani wakiamini kuwa kufanya hivyo ni vizuri zaidi kuliko majumbani mwao.

Daniel Makaka - Mwananchi
Share:

MSTAAFU ADAIWA KUUAWA KWA KUCHOMWA MKASI NA 'HOUSE BOY' WAKE


Tunsume Sakajinga (60), mkazi wa wilayani Temeke jijini Dar es Salaam ameuawa baada kupigwa na kitu kizito kichwani kisha kuchomwa na mkasi shingoni na mtu anayedaiwa kuwa kijana wake wa kazi za nyumbani.

Msemaji wa familia ambaye ni kaka wa marehemu, Kisa Mwankusye amelieleza Mwananchi kuwa mauaji hayo yametokea juzi Januari 12, 2019 saa tano asubuhi na kwamba marehemu alikutwa amechomwa mkasi shingoni na kupigwa na kitu kizito kichwani.

“Tulipata taarifa hizo saa tano asubuhi, jambo hili linaumiza sana kwa sababu lipo chini ya mikono ya polisi tunawaachia wao,” amesema Mwankusye.

Amesema dada yake alistaafu Desemba 31, 2018 na kwamba nyumbani alikuwa akiishi na kijana huyo.
Na Tumaini Msowoya, Mwananchi 
Share:

ALIYEZINI NA DADA YAKE AKANA MAELEZO YA AWALI MWINGINE ASOMEWA SHTAKA LA MAUAJI.

Na,Naomi Milton Serengeti. Gabriel Nyantori(25) mkazi wa Kijiji cha Kibeyo wilayani hapa ambaye ni mshtakiwa katika shauri la jinai namba 138/2018 amekana maelezo ya awali mara baada ya kusomewa maelezo yake katika mahakama ya wilaya ya Serengeti. Mbele ya Hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya Ismael Ngaile mwendesha mashtaka wa Jamhuri Faru Mayengela kabla ya kusoma maelezo ya awali alimkumbusha mshitakiwa makosa yake . Mwendesha mashtaka alisema katika shauri hilo mshtakiwa anashitakiwa kwa makosa mawili kosa la kwanza ni Kuzini kinyume na kifungu 158(1)(a) cha kanuni ya adhabu sura ya 16…

Source

Share:

MAHAKAMA KUU YATUPILIA MBALI KESI YA ZITTO KABWE NA WENZAKE

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeifuta kesi iliyofunguliwa na Kiongozi wa ACT Wazalendo na wenzake wa vyama vya upinzani waliyokuwa wakiitaka mahakama hiyo kuzuia kusomwa kwa Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa wakidai kuwa uko kinyume na katiba ya nchi.

Mahakama imetoa uamuzi huo leo Jumatatu, Januari 14, 2018 ambapo walalamikaji, Zitto na wenzake wamekubali maamuzi hayo na kusema sasa nguvu yao ni kwenda kuupinga muswada huo kwenye kamati za bunge.

Jaji Benhajo Masoud amesema Mahakama imeliondoa shauri hilo baada ya waombaji kuchanganya mashataka mawili kwa pamoja.

“Mahakama imeondoa shauri letu dhidi ya serikali kupinga muswada wa sheria ya vyama vya siasa na kifungu cha 8(3) cha sheria ya Haki na Wajibu ( BRADEA ) kwa sababu ya maombi hayo mawili kuunganishwa. Kufuatia uamuzi huo wa mahakama tumeagiza mawakili leo wafungue kesi mpya ya BRADEA.

“Tunaheshimu maamuzi ya mahakama na tunaamini mahakama imetenda haki. Hivyo tumeamua kurudi mahakamani kwa ombi moja la kupinga kifungu cha 8(3) cha sheria ya Haki na Wajibu. Kifungu hiki kinakiuka katiba kwa kuzuia mashauri ya kupinga miswada ya sheria. Mahakama ni chombo cha haki.

“Tutaendelea kuupinga muswada wa sheria ya kurekebisha sheria ya vyama vya siasa mbele ya kamati za bunge na ndani ya bunge. Muswada ukipita kuwa sheria kama ulivyo au kuwa mbaya zaidi, tutaupinga mahakamani tena. Hatutakata tamaa katika kudai haki,” amesema Zitto.

Share:

Picha : CHUO KIKUU MZUMBE CHAANZISHA SAFARI YA MABADILIKO WEZESHI KATIKA SEKTA YA AJIRA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof.Lughano Kusiluka,akizungumza na Wahadhiri wa Chuo Kikuu Mzumbe waliohudhuria warsha ya mabadiliko katika Sekta ya ajira kwa manufaa ya Jamii Afrika Mashariki (TESCEA) inayoendelea Morogoro.
Mwezeshaji wa warsha hiyo kutoka nchini Kenya Prof. Charles Kingsburry akifafanua kuhusu mradi huo kwa Waandishi wa Habari.
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe (Taaluma) Prof. Ganka Nyamsogoro akiwasisitiza washiriki umuhimu wa warsha hiyo katika kubadili mbinu za ufundishaji.
Baadhi ya washiriki wakiwa katika majadiliano. 
Mratibu wa mradi wa TESCEA Dkt. Albogast Musabila akifafanua kuhusu mradi huo kwa Waandishi wa Habari.
Mwezeshaji toka Chuo Kikuu, Afrika Nazarene cha nchini Kenya Dkt. Kendi Muchungi akieleza umuhimu wa mpango huo na jinsi unavyoweza kunufaisha wasomi na Jamii zao.
Mratibu Msaidizi wa mradi wa TESCEA wa Chuo Kikuu Mzumbe Dkt. Jennifer Sesabo akitambulisha mpango wa mradi huo kwa Washiriki.
Washiriki wakifuatilia maelekezo yanayotolewa katika warsha hiyo inayoendelea Hoteli ya Morogoro.
Washiriki wa warsha ya TESCEA katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi rasmi.
 ***
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia mradi wake mpya wa ‘TESCEA’ kimeendesha warsha ya kuwajengea uwezo wahadhiri katika mbinu bora za ufundishaji zinazosaidia wanafunzi kuweza kujiajirika pindi wanapohitimu masomo yao ya elimu ya juu.

Akizungumza katika uzinduzi wa warsha hiyo inayoendelea katika hoteli ya Morogoro, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof.Lughano Kusiluka amesema Chuo Kikuu Mzumbe ni mahiri katika kufundisha masomo ya biashara na menejimenti na sasa kinakwenda hatua ya mbele zaidi kwakuwaandaa wahitimu wa ndani na hata nchi nyingine kutengeneza ajira kabla ya kuhitimu masomo yao. 

Prof.Kusiluka ameeleza kuwa kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa waajiri dhidi ya wahitimu wa vyuo vikuu nchini na kuonekana kutokuwa na ujuzi wa kutosha na umahiri katika fani walizosomea pindi wanapotaka kuajiriwa.

 Hivyo, Chuo Kikuu Mzumbe kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dodoma na vyuo vikuu viwili kutoka Uganda (Uganda Martys na Gulu), pamoja na asasi za AFELT, LIWA, ASHOKA kutoka Kenya na INASP kutoka Uingereza, wameanza kwa kuwajengea wahadhiri ili kubadili mbinu za ufundishaji zitakazowawezesha wahitimu kuwa na maarifa, ubunifu na ujuzi zaidi kutambua na kutumia fursa zilizopo ili kutengeneza ajira au kuajiriwa. 

Kwa upande wake mwezeshaji wa warsha wa asasi ya umoja wa Vyuo vikuu vinavyofundisha mbinu zinazohitajika katika kuboresha ufundishaji Afrika Mashariki (AFELT) na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Daystar cha Kenya Prof.
 Charles Kingsburry, amesema ni muhimu sasa kubadili mfumo wa ufundishaji unaowafanya wahitimu kujua vitu kulingana na elimu wanayofundishwa darasani pekee na kwa kutegemea mitandao ya intaneti na badala yake mbinu mpya za ufundishaji ziwajenge katika ubunifu ,maarifa,mbinu na stadi halisia zitakazowawezesha kujiajiri wao na kuweza kuajiri watu wengine. 

Hii ina lengo si tu la kuwafanya wahitimu kujua vitu tofauti bali kuwajenga kuwa watu tofauti wanaoleta mabadiliko chanya kwa jamii nzima na kujinufaisha wao na jamii zinawazunguka kupitia elimu waliyopata. 

Naye mwezeshaji mwingine kutoka Asasi ya AFELT na mhadhiri wa Chuo Kikuu, Afrika Nazarene cha nchini Kenya Dkt. Kendi Muchungi amesema wahitimu wa Vyuo Vikuu vyote vya Afrika Mashariki hawatofautiani na wamekuwa wakikosa uwezo wa kujiajiri na kuajiriwa na hivyo kushindwa kuisaidia jamii katika suala la ajira kupitia elimu waliyopata,badala yake wamekuwa wakitegemea kuajiriwa. Hivyo ni imani yake kuwa mpango huo utaleta mabadiliko kwa wahadhiri wa vyuo vikuu katika ufundishaji na kunufaisha jamii nzima ya Afrika Mashariki kupitia wasomi wachache. 

Wakati huo huo mratibu wa Mradi wa ‘TESCEA’ kutoka Chuo Kikuu Mzumbe,Dkt.Albogast Musabila amesema pamoja na lengo kuu la mpango wa mradi huo la kuwajengea wahitimu uwezo wa kujiajiri na kuajiri,Chuo Kikuu Mzumbe kwa ushirikiano na wadau wa Sekta ya ajira, wahadhiri na wanafunzi kimeanza mchakato wa kukusanya maoni ya wadau kwa ajili ya kuandaa mapendekezo yatakayozingatiwa wakati wa kuboresha mitaala na kuanzisha mitaala mipya.
Share:

PAKA ATUMWA KAMA KIFURUSHI POSTA..ALIYETUMA ALIMWA FAINI

Bwana mmoja nchini Taiwan amepigwa faini baada ya kumsafirisha paka wake kama kifurushi kwa njia ya mawasiliano ya posta.

Kwa mujibu wa mtandao wa habari wa habari wa UDN bwana huyo mwenye miaka 33 aliyetambulika kwa jina lake la ukoo la Yang amepigwa faini ya dola za Taiwan NT$60,000 ( sawa na dola za Marekani 1,952) kwa kuvunja sheria ya Ulinzi wa Wanyama ya Taiwan.

Tukio hilo lilitokea wiki iliyopita ambapo bw Yang alimfungasha kwenye kifurushi paka wake aina ya Scottish fold kwenda kwenye kituo kimoja cha kuhifadhi wanyama nchini humo katika wilaya ya Banciao. Yang amedai kuwa hakuwana mahitaji tena ya kuendelea kumfuga paka huyo.

Kutokana na kosa hilo, alilipishwa faini ya ziada ya NT$30,000 kwa kuvunja sheria ya kuzuia na kupambana na magonjwa ya kuambukiza ya wanyama sababu wafanyakazi wa kituo cha wanyama alipopokela paka huyo waligundua kuwa hakupewa chanjo ya kichaa na kuzuia hasira kali.

Maafisa wa ulinzi wa wanyama wa mjini Taipei walifanikiwa kumnasa mtuma kifurushi hicho kupitia kampuni ya posta na mkanda wa kamera za ulinzi za polisi.Mamlaka ya ulinzi wa wanyama inasema paka huyo ana afya njema na baada ya uchunguzi zaidi anaweza kuchukuliwa na mmiliki mpya.

Baada ya kufanya uchunguzi wao, wakamtia mikononi mwao bw Yang ambaye alijitetea kuwa alijaribu kumgawa paka huyo bila ya mafanikio. Yang pia alidai hakuwa na muda wa kutosha wa kumuangalia mnyama huyo na kumtunza. Paka huyo pia ana matatizo ya kutembea baada ya kujeruhiwa, na licha ya kupatiwa matibabu kadhaa, yakiwemo ya kimila bado hali yake haijatengemaa.

Mkurugenzi wa mamlaka ya wanyama, Chen Yuan-chuan, amelaani vikali mkasa huo akisema: "Mnyama anaweza kupatwa na hali mbaya kwa kukosa hewa ndani ya kifurushi na kupandwa na ghadhabu pia hakukuwa na maji safi na salama."

Bw Yuan-chuan amewataka watu kufuata taratibu halali za kisheria pale wanapoona hawawezi tena kuendelea kuwatunza wanyama wao wa nyumbani.
Chanzo- BBC
Share:

KESI YA 'UCHOCHEZI' INAYOMKABILI ZITTO YAOTA MBAWA

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (mwenye nguo nyeusi) akiwa na viongozi wengine kutoka vyama vya upinzani leo katika Mahakama ya Kisutu.


Kesi ya 'uchochezi' inayomkabiili Mbunge wa Kigoma Mjini, Zito Zuberi Kabwe imeahirishwa mpaka Januari 29, itakapoitwa kwa ajili ya kwenda kusikilizwa.

Kesi hiyo ya Jinai namba 327 ya Mwaka 2018 inayomkabili Kiongozi huyo leo tarehe 14 Januari 2019 katika Mahakama ya Kisutu, Jijini Dar es salaam ilifika kwa ajili ya kutajwa na kutolewa maamuzi ambayo yalitolewa na Hakimu Mkazi, Janeth Mtega baaada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili .

Upande wa Mashtaka ukiwakilishwa na Wakili wa Serikali, Adolf Kissima ulidai kwamba kesi hiyo leo ilikwenda kwa ajili ya kutajwa lakini upande wa mashtaka hawakuwa na jalada halisi la kesi hiyo.

Upande wa utetezi ukiongozwa na Wakili wa Zitto, Steven Mwakibolwa uliikumbusha mahakama kuwa shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kutajwa na mahakama hiyo kupitia Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama, Huruma Shaidi na ilishapanga tarehe ya kuanza kusikilizwa, ambayo ni Januari 29, 2019.

Inadaiwa kuwa Oktoba 28,2018 katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi za makao makuu ya chama cha ACT Wazalendo, kiongozi huyo alitumia maneno yenye kuleta kuleta chuki miongoni mwa wananchi wa Tanzania dhidi ya Jeshi la Polisi.

Mbunge huyo alifikishwa Mahakama ya Kisutu kwa mara ya kwanza, Novemba 2, 2018, bado anaendelea na dhamana.

Chanzo:Bbc
Share:

SERIKALI YAPIGA 'STOP' BOMOA BOMOA KWENYE MAKAZI YASIYO RASMI

Rais, John Pombe Magufuli.

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli ametoa fursa kwa wananchi waliojenga bila ya kufuata mipango miji na hawana hatimiliki za ardhi kufanyiwa urasimishaji wa makazi na kuelekeza kuwa wasibomolewe nyumba zao tena kwakuwa hayakuwa makosa yao kujenga maeneo hayo.

Hayo yamesema na Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo na Makazi, William Lukuvi, wilayani Simanjiro mkoani Manyara alipofanya ziara ya kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi kwa wakazi wa mji huo, ambapo amewataka wananchi wote wachangamkie fursa hiyo iliyotolewa na Rais.

Amesema kwamba Serikali ya awamu ya tano kuanzia sasa haitabomoa tena nyumba za wananchi waliojenga maeneo ya makazi yasiyo rasmi badala yake itarasimisha makazi holela.

“Serikali ya awamu ya tano inajali sana wananchi wake kwakuwa zamani wananchi ambao hawakujenga kwa kufuata mipango miji wangebomolewa nyumba zao, lakini kwa sasa imeanzisha mpango kurasimisha makazi holela na kuwapatia hati wananchi wote waishio mijini ili waishi katika makazi rasmi”, amesema Lukuvi.

Pamoja na hayo Lukuvi amewataka wananchi wote waishio mijini kuwa wazalendo kwa kurasimisha maeneo yao waweze kujipatia hati na ili walipe kodi ya pango la ardhi jambo ambalo litaiongezea Serikali mapato.

Chanzo:Eatv
Share:

TATIZO SUGU LA SIMBA NA YANGA LAITAFUNA AFRIKA


Klabu ya soka ya Simba inawakilisha nchi kwenye michuano ya kimataifa na tayari ipo katika hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Afrika ikiwa inaongoza kundi D, baada ya kushinda 3-0 dhidi ya JS Saoura.


Pamoja na kuwakilisha nchi lakini, Simba inaacha manyanyaso kwa vilabu vingine vinavyoshiriki ligi kuu ya soka Tanzania bara ambavyo havijui lini vitacheza mechi zake dhidi ya klabu hiyo ambayo tangu ianze kucheza mechi za kimataifa imejikusanyia viporo takribani 6.

Wiki hii ambapo baadhi ya timu zitakuwa zinacheza mzunguko wa 21, Simba wao hawatakuwa sehemu ya ratiba hiyo ya ligi kuu kwani watakuwa wanajiandaa kwaajili ya mchezo wa pili wa hatua ya makundi dhidi ya AS Vita Club, utakaopigwa Januari 19 huko DR Congo.

Vinara wa ligi kuu msimu huu, klabu ya Yanga huenda wakawa hawafurahishwi na Simba kuwa na viporo vingi lakini msimu uliopita Yanga walifika hatua ya makundi ya Kombe la shirikisho Afrika na walikuwa na viporo kama ilivyo kwa Simba msimu huu.

AFRIKA
Kwa upande wa timu ziliopo kundi moja na Simba, Al Ahly nao wamecheza mechi 14 tu kati ya 17 ambazo timu nyingine zimecheza huku pia ikiwa haipo kwenye ratiba ya ligi wiki hii ambapo itasafiri kuifuata JS Soura ambayo imecheza mechi 16 kati ya 17 za ligi.

Kwa upande wa DR Congo, AS Vita Club wao wamecheza mechi 14 kati ya 15 za ligi. Nchini Afrika Kusini Mamelodi Sondowns ambao wapo kundi A klabu bingwa Afrika wamecheza mechi 13 pekee kati ya 17 ambazo tayari timu nyingine zimecheza.

Chanzo:Eatv
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger