Thursday, 10 January 2019

SAKATA LA KUDHALILISHA BUNGE : NDUGAI AMPA BARUA YA WITO CAG..MAALIM SEIF NAYE AKOMAA

 Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema ofisi yake tayari imeshaandika barua ya wito kwenda ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ikimtaka kufika mbele ya Kamati ya Maadili, Kinga na Haki ya Bunge ili kuhojiwa.

Hatua hiyo imekuja siku tatu baada ya Spika Ndugai kumtaka CAG, Profesa Mussa Assad kufika mbele ya kamati hiyo kujieleza kuhusu kauli yake kuwa chombo hicho cha kutunga sheria hakitekelezi ipasavyo majukumu yake ya kuisimamia Serikali.

Profesa Assad, ambaye ametakiwa kufika mbele ya kamati hiyo Januari 21, alitoa kauli hiyo alipohojiwa na idhaa ya Kiswahili ya kituo cha televisheni cha Umoja wa Mataifa (UN), wakati alipokuwa jijini New York, Marekani kuhudhuria mkutano wa jopo la wakaguzi wa nje.

Mbali na CAG, mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee naye ameitwa mbele ya kamati hiyo Januari 22 kwa madai ya kutoa kauli iliyounga mkono kilichosemwa na Profesa Assad.

“Tayari tumeshamwandika barua yaani summons (hati ya wito), maana wito wetu unaenda kama wa kimahakama vile,” alisema Ndugai kwa njia ya simu jana, muda mfupi baada ya kuhudhuria hafla ya kuapishwa kwa mawaziri wawili na wateule wengine wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam.

Wakati Ndugai akisema hayo, katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharrif amemtaka Ndugai kumuomba radhi Profesa Assad akisema kilichofanywa na CAG ni kutimiza wajibu wake na si kulidhalilisha Bunge.


Na Bakari Kiango, Mwananchi 
Share:

LORI LAGONGA TRENI DODOMA

Na.Alex Sonna,Dodoma
Watu wawili wamenusurika kifo baada ya lori aina ya scania walilokuwa wakisafiria kutoka Dodoma kwenda Iringa kuigonga treni ya mizigo katika makutano ya reli na barabara eneo la hazina jijini Dodoma.


Tukio hilo lilitokea jana mchana mara baada ya lori hilo lenye namba za usajili T463 ADW likiwa na tela lenye usajili T483 BLP kuiigonga treni hiyo iliyokuwa ikitoka jijini Dar es salaam kuelekea mikoa ya kanda ya ziwa.


Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa ajali hiyo imechangiwa na mvua zilizokuwa zikinyesha na kumfanya dereva wa lori kutoona kizuizi cha treni mbele yake.


Mmoja wa mashuhuda hao Ramadhani Rashid Mkazi wa Majengo amesema kuwa ajali hiyo ilichangiwa na dereva wa lori kutaka kukatiza kwa mwendo mkali lakini alikuwa kacheleWa hali iliyosababisha kugongwa na treni hiyo ya
mizigo.


“Dereva wa lori alikuwa katika mwendo mkali wakati akikatiza kivuko cha reli hivyo alishindwa kusimama na treni likawa limekaribia na kumgonga tumetoa watu wawili wakiwa wamejeruhiwa vibaya mwingine mmoja utumbo ukiwa nje”alisema


Kaimu kamanda wa polisi mkoani Dodoma ACP William Mkonda, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema chanzo ni uzembe wa dereva wa lori ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi na majeruhi wamelazwa katika hosipitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma
Share:

TUME YA UCHAGUZI YAMTANGAZA TSHISEKEDI KUWA MSHINDI WA URAIS CONGO

Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Congo (Ceni) imetangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo yanayoonesha mgombea wa upinzani Felix Tshisekedi ameshinda kiti cha Urais katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Desemba 30 mwaka uliopita.

Tshisekedi amemshinda mgombea mwingine wa upinzani Martin Fayulu, pamoja na mgombea aliyekuwa anaungwa mkono na serikali ya Rais anayemaliza muda wake, Emmanuel Shadary.


Kwa mujibu wa Mkuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Ceni) Corneille Nangaa, mapema leo Alhamisi amesema kwamba kwamba Bw Tshisekedi amepata asilimia 38.57 ya kura zilizopigwa na kumtangaza rasmi kuwa Rais mteule wa nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini na mafuta.


Tshisekedi anatokea katika muungano wa kisiasa na aliyekuwa mgombea wa chama cha UNC (Union for the Congolese Nation), Vital Kamerhe ambaye atakuwa ni Waziri Mkuu wa serikali yao kwa mujibu wa makubaliano yao.


Ripoti zinaeleza kuwa mshindi wa kwanza (Felix Tshisekedi) amepata kura takriban milioni 7, huku mshindi wa pili (Martin Fayulu akipata kura takriban milioni 6.4 milioni na mgombea wa tatu ambaye anaungwa mkono na Rais Joseph Kabila (Emmanuel Ramazani Shadary) akipata takriban kura millioni 4.4.
Share:

Wednesday, 9 January 2019

AZAM FC YATINGA NUSU FAINALI MAPINDUZI..YAITWANGA MALINDI 2 - 1


Azam Fc imefanikiwa kutinga nusu fainali katika michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuichapa Malindi FC mabao 2-1.

Mechi hiyo imepigwa usiku huu kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar.

Kutokana na ushindi huo Azam FC inatinga nusu fainali na kuikwepa Simba SC.

Mabao ya Azam Fc yamefungwa na Agrey Morris pamoja na
Donald Ngoma huku bao la Malindi FC likifungwa Abdulswamad Kassim
Share:

SIMBA WAONESHA UBISHI

Simba wameonyesha kuwa wao ni wabishi kwenye soka kwa sasa baada ya jana kufanikiwa kuwachapa Mlandege bao 1-0 kwenye mchezo wa Kombe la Mapinduzi Kundi A, uliopigwa kwenye Dimba la Amaan.

Simba wamefanikiwa kushinda michezo yao yote ya kundi na hivyo wamemaliza kwa kukusanya pointi tisa kwenye kundi hilo.

Katika mchezo wa jana, Haruna Niyonzima ndiye alikuwa shujaa wa Simba baada ya kuifungia timu hiyo bao pekee kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 20 ya mchezo

Niyonzima alifunga bao hilo baada ya beki wa timu hiyo, Asante Kwasi kuangushwa kwenye eneo la hatari na mwamuzi kuamuru mkwaju wa penalti.

Hata hivyo, kipindi cha pili Mlandege walionekana kuwika zaidi kwenye eneo la kiungo lakini walishindwa kuipenya ngome ya Simba ambayo ilikuwa inaongozwa na Kwasi, Poul Bukaba na Hassan Mlipili ambao walionyesha kiwango cha hali ya juu.

Mbali na Simba timu nyingine ambayo imefuzu kwenda nusu fainali ni KMKM, huku Kundi B, Azam na Malindi nazo zikienda hatua hiyo.

Lakini kuna uwezekano mkubwa Simba ikakutana na kigingi kwenye hatua inayofuata kwa kuwa baada ya mchezo wa jana watabadilisha kikosi na wachezaji wengi wa kikosi cha kwanza watarejea Dar es Salaam kucheza mchezo wa hatua ya Makundi wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya JS Saoura kwenye Uwanja wa Taifa.

Moja ya timu ambayo Simba wanaomba wasipangwe nayo ni Azam ambayo iliwachapa wapinzani wao Yanga mabao 3-0 kwenye mchezo wa Kundi B.
Share:

YANGA YAMALIZA KOMBE LA MAPINDUZI KWA KUICHAPA JAMHURI 3 - 1

Yanga imemaliza mechi yao ya mwisho ya hatua ya makundi katika michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kuichapa Jamhuri kwa mabao 3-1.

Mechi hiyo imepigwa kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar, leo na timu zilicheza bila ya presha kubwa.

Yanga iliyoonyesha soka safi ilifanikiwa kushinda kwa mabao hayo ualiyofungwa na Faraji Kilaza, Gustafa Saimon.

Hadi mapumziko, tayari Yanga ilikuwa imepata mabao hayo matatu na Jamhuri moja, na kipindi cha pili kikawa hakina mabao.

Kipindi cha pili kilionekana kuwa cha tahadhari kwa kila timu. Licha ya Jamhuri kutaka kusawazisha mabao hayo mawili lakini ilionekana kujilinda kwa kiasi kikubwa.
Share:

BODI YA FIRAMU YAENDELEA KUMPIGA “PINI” WEMA SEPETU

NA KAROLI VINSENT Katibu mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fissoo amesema msanii wa filamu, Wema Sepetu hajafunguliwa kujihusisha na masuala ya uigizaji kama inavyovumishwa mitandaoni. Bi Fisso ameyasema hayo  leo Jumatano Januari 9 Jijini Dar es Salaam,wakati akizungumza na waandishi wa Habari katika ofisi za Bodi hiyo wakati wa kujadili Tasmini ya Tamasha la “KATAA MIHADARATI” lililofanyika katika viwanja vya Mburahati Barafu jijini Dar es Salaam.  Amesema endapo msanii huyo atafunguliwa Baraza hilo litaitisha mkutano na waandishi wa habari kwa ajili ya kulieleza jambo hilo na si kama inavyoelezwa…

Source

Share:

WILAYA YA KILOLO KUNG’ARISHWA KWA BARABARA ZA LAMI

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mh. Asia Abdallah amewataka wananchi wa Kilolo kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wakandarasi ili kufanikisha mradi wa ujenzi wa barabara za lami katika wilaya hiyo unaotokana na juhudi za mbunge wa jimbo la kilolo, Mh. Venance Mwamoto pamoja na serikali ya awamu ya tano utakaondoa changamoto ya usafiri kwa wakina mama wajawazito, wazee na watu wa Kilolo. “kwa hiyo watu watakapo kuja site tuwape ushirikiano wa asilimia 100 barabara itengenezwe na sisi tupate maendeleo kama wenzetu wa kule kaskazini walipofikia, sasa lami inakuja, Mh. Mbunge,…

Source

Share:

CALL FOR STUDENTS TO APPLY FOR HULT PRIZE CHALLENGE UNIVERSITY OF DODOMA 2018-2019

CALL FOR STUDENTS TO APPLY FOR HULT PRIZE CHALLENGE UNIVERSITY OF DODOMA 2018-2019

The University of Dodoma (UDOM) is selected among world’s top Universities to
host local edition of Hult Prize as students answer the United Nations Challenge and
go head-to-head for US$ 1M.

About HULT PRIZE UDOM Challenge
HULT PRIZE UDOM Challenge is a student lead (lead by the official appointed
HULT PRIZE Campus Director) event under the coordination of the UDOM
Innovation Spaces and Incubation Centre (UDOISIC). The HULT PRIZE UDOM
Challenge is a local edition of the world’s largest competition run by HultPrize in
partnership with United Nations, hosting College and University events around the
world in search of the next game changing start up.

About the HultPrize Foundation
Hult Prize is the world’s biggest engine for the launch of for-good, for-profit startups
emerging from University with over 2500 staff and volunteers around the world. In
nearly a decade, the movement has deployed more than $50M of capital into the
sector and mobilized more than one million young people to re-think the future of
business as it continues to breed disruptive innovation on college and University
campuses across 100 plus countries.

The Hult Prize Foundation been called the
“Nobel Prize for Students” and has been featured in a TIME Magazine Cover Story
highlighting the “Top 5 Ideas Changing the World.”
To learn more, visit www.hultprize.org

Objective of the HultPrize UDOM Challenge 2018/19
The Challenge aims at creating the best engine of social entrepreneurs worldwide by
inspiring and motivating youth to engage themselves in social entrepreneurship in
which they can turn social challenges to profitable ventures and be able to earn
income and create jobs for others.
Specifically, this year’s competition aims to have student “create a venture or a
business idea or an idea that can provide 10000 meaningful jobs to youth within
the next decade.
The winner of the intra – campus event will automatically advance to compete in
one of the fifteen regional finals. In our case, the winner will proceed to Nairobi in
April 19th – 20th
. The winning team will then proceed to summer business accelerator
in Ash ridge, United Kingdom in July 2019 for the whole one month and half where
the participants will receive free mentorship, advisory and strategic planning as they
create prototypes and set up to launch their new social business. A final round of
competition will be hosted in New York at United Nation’s headquarters in
September where the winner will be awarded $1,000,000 prize.
“The hultprize is a wonderful example of the creative cooperation needed to build a
world with shared opportunity, shared prosperity, and each year I look forward to
seeing many outstanding ideas the competition produces” (Former US President
Bill Clinton).

HultPrize is now recruiting teams who are interested in registering for the
competition.

Who is Eligible to Apply?
o Must be a team of 3 or 4 students.
o The team must have a name.
o Current student at University of Dodoma (Bachelor, Masters, and PhD).
o UDOM Alumni, Faculty or staff are NOT eligible.

How to Apply?
Applications will be done online by registering your team at
http://bit.ly/2Rf4arc

Application deadline
“It’s not every day that you have an opportunity to change the world. This is your
chance to show the world that you’re dedicated to impact.”
So, make sure you do not miss the application deadline, which is on 15
th January 2019!!!

For more information, contact:
Nominated HultPrize UDOM Campus Director,
Mr. Denice Benedict
+255745356808
+255657933934

For technical support, please contact:
College Innovation Space Coordinators UDOISIC Heads
CBSL: Mr. Mohamed Kaluse (+255717976 265)
E-mail: kaluseone@gmail.com
Dr. Alex F. Mongi
Head, UDOISIC
Technical Support
Phone: +255 755 498 126
E-mail: afmongi@gmail.com
CNMS: Mr. Benatus Mvile (+255 764 860 999)
E-mail: benimvile@yahoo.com
CHSS: Dr. Happyness Nnko (+255 754 816 634)
E-mail: happyjackson.nnko@gmail.com
CIVE: Dr. Mustafa H. Mohsin (+255 676016085)
E-Mail: muky4us@gmail.com
Dr. Lutengano Mwinuka
Head, UDOISIC
Business Support Services
Phone: +255 784 891 291
E-mail:
mwinuka.lutengano@gmail.com
CHS: Dr. David Munisi (+255 762 850 502)
E-mail: massugii@gmail.com
COED: Dr. Pambas Tandika (+255 758 198 170)
E-mail: tpambas@gmail.com
COES: Mr. Desmond Risso (+255 755 870 270)
E-mail: rissodesmond@yahoo.com

The post CALL FOR STUDENTS TO APPLY FOR HULT PRIZE CHALLENGE UNIVERSITY OF DODOMA 2018-2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

REB: Application for the result slip- Rwanda education board(REB)

REB: Application for the result slip- Rwanda education board(REB)

 

Responsibilities
• To contribute to determining education policy;

• To coordinate and fast track education programmes and activities aimed at providing to all categories of Rwandans a qualitative education;

• To design and distribute curricula, teaching materials, guides, methodologies and establish teaching methods for nursery, primary secondary, specialized schools and adult literacy education in accordance with the current educational development;

• To promote the use of information and communication technology in education;

• To coordinate programs and activities aimed at developing teachers, building their capacities and improving their management;

• To establish regulations determining how national examinations are conducted in various levels of education, except in vocational and technical training and in higher learning institutions;

• To cooperate and collaborate with other regional and international institutions having similar responsibilities

• To advise Government on all activities which can fast track education development in Rwanda.

 

APPLY FOR THE RESULT SLIP HERE

 

You may also Like

Rwanda Education Board-REB Results 2018-2019

The post REB: Application for the result slip- Rwanda education board(REB) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

The university of dodoma-UDOM humanities scholarship

The university of dodoma-UDOM humanities scholarship

THE UNIVERSITY OF DODOMA HUMANITIES SCHOLARSHIP

The University of Dodoma (UDOM) wishes to announce the University of Dodoma Humanities Scholarships for the undergraduate students admitted in the School of Humanities at UDOM in the 2018/2019 academic year.

1.0 INTRODUCTION

The University of Dodoma Humanities scholarship aims to support the needy students who have been selected to join degree programmes in the school of Humanities but who have not been able to secure sponsorship from the Higher Education Students Loan Board (HESLB or any other sponsors. The University of Dodoma will not require beneficiaries to repay the money at the end of the scholarship period.

2.0 TYPE OF SCHOLARSHIP

Students who are nominated for this scholarship will pay only 60% of the tuition fee and the remaining 40% will be paid by the University of Dodoma. Once a student secures the Humanities Scholarship, he/she will continue to be a beneficiary for the duration of three years of studies in the admitted degree programmes. Students failing to complete their studies within the three years shall cease to be beneficiaries of the scholarship.

3.0 ELIGIBILITY

1. Undergraduate (degree) students who are not beneficiaries of Higher Learning Students’ Loans Board (HESLB) or any other scholarship/grant.

2. Outstanding first year undergraduate students admitted to pursue BA in Literature, BA in Kiswahili Linguistics, BA in Kiswahili Literature, BA in Translation and interpretation, BA in English, BA in Theatre and Film, BA in Fine Arts and Designs, BA in History and BA in Cultural Heritage and Tourism in the School of Humanities of the University of Dodoma.

4.0 HOW TO APPLY

The application for the scholarship will open on 2nd January, 2019 and will close on 15th January, 2019. In order to apply, first-year students registered to the eligible programmes can click the button available in their UDOM SR account to lodge their applications.

MORE DETAILS—-PDF

Link

5.0 ENQUIRIES

For any enquiries please contact: Director of Undergraduate Studies: 0758968944 Dean, School of Humanities: 0767901870 Email:humanitiesscholarship@udom.ac.tz

The post The university of dodoma-UDOM humanities scholarship appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MC PILIPILI ATUHUMIWA KUCHUMBIA MPENZI WA KIDUME KINGINE


Mchekeshaji maarufu bongo, Emmanuel Mathias 'MC Pilipili' ambaye hivi karibuni amemvisha pete mchumba wake, amefunguka juu ya tuhuma zinazodaiwa kuwa ametumia pesa kumpata mwanamke huyo kutoka kwa mwanaume wake wa zamani.

Akizungumza na www.eatv.tv, MC Pilipili amesema kwamba anamuhurumia kijana huyo, lakini anaamini atapata mwanamke mwengine kwani wanawake ni wengi Tanzania.

“Aisee nampa pole, Tanzania inaonesha wanawake ni wengi kuliko wanaume, kwa hiyo sio rahisi kwa yeye kutembea na mwanaume mwingine, lakini ni rahisi kupata mwanamke, atapata mwanamke mwingine, kwani wanawake ni wengi Tanzania na duniani”, amesema Mc Pilipili.

Ikumbukwe kwamba mwishoni mwa wiki iliyopita, Mc Pilipili amechumbia msichana mmoja anayejulikana kwa jina la Philomena Thadey maarufu kama 'Cute Mena', na baada ya muda mfupi zikaibuka tuhuma mitandaoni kuwa alikuwa mchumba wa mwanaume mwingine hapo kabla.
Chanzo- EATV
Share:

SHILOLE AWACHANA 'WADANGAJI' WANAONYEMELEA NDOA YAKE


Shilole akiwa na mume wake, Uchebe.

Mwanamuziki Shilole amewataka wadada wa mjini 'wadangaji' kukoma kumfuatilia mume wake ' Uchebe' kwa madai kwamba anamtunza na kumpendezesha.

Shilole amesema hayo baada ya kugundua kwamba wapo manyamera wanaonyemelea penzi la mume wake ambapo akidai kwamba zamani wakati akiwa hana kitu hawakuonekana kumfuata.

"Niliridhika na hali yako tangu mwanzo mpaka sasa una'shine' ila wadangaji msivyo na haya mnaanza kumwambia mume wangu Uchebe 'amekuwa handsome'", amesema Shilole.

Shilole na Ashraf Uchebe walifunga ndoa Desemba 7, 2017 ambapo awali msanii huyo alipondwa kwa kukubali kufunga ndoa na Uchebe huku maneno yakiwa kwamba hawaendani kiuwezo.
Share:

KAMPUNI YA KICHINA YALALAMIKIWA KUWANYANYASA NA KUTOWALIPA WATUMISHI STAHIKI ZAO

Wafanyakazi wa kampuni ya Beijing New Building Material (BNBM) inayotengeneza vifaa vya ujenzi, wameilalamikia kampuni hiyo kwa kushindwa kuwalipa stahiki zao pale wanapoachishwa kazi. Wakizungumza na Darmpya wafanyakazi hao walisema kuwa kampuni hiyo imekuwa na tabia ya kuwaachisha kazi wafanyakazi wake bila kuwapa malipo yao wanayostahili hasa wale wanaoonekana kutetea haki zao. Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi katika kampuni hiyo Ramadhani Shukuru amesema “Wafanyakazi wengi wamefukuzwa kazi na wana mikataba lakini stahiki zao hawakuzipata, malalamiko haya tumeshayapeleka hadi ngazi ya wilaya wakasema watafuatilia lakini mpaka muda huu hatujawaona”. Ameongeza kwa…

Source

Share:

RAIS MAGUFULI : SITACHOKA KUFANYA MABADILIKO KWENYE SAFU YA UONGOZI

Rais Magufuli amesema hatochoka kufanya mabadiliko kwenye safu yake ya uongozi endapo ataona mambo hayaendi sawa kama anavyotaka.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumatano Januari 9, 2019 katika hafla fupi ya kuwaapisha viongozi aliowateua jana, akiwemo Waziri wa Madini, Dotto Biteko na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Angellah Kairuki.

Biteko amechukua nafasi ya Kairuki ambaye amedumu kwenye wizara hiyo kwa miezi 14 tangu ateuliwe Oktoba 2017.

Rais Magufuli amesema licha ya mabadiliko ambayo tayari ameyafanya kwenye Wizara ya Madini lakini sekta hiyo bado inaonekana kuwa na changamoto.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli changamoto hizo zinatokana na uongozi wa wizara hiyo kushindwa kuwajibika ipasavyo hali inayosababisha nchi kukosa fedha nyingi zinazotokana na madini.

“Sekta ya madini bado ina changamoto kubwa sana, ripoti inaonyesha nchi inayoongoza kwa kuuza dhahabu Afrika Mashariki si Tanzania wakati nchi yetu ndiyo inaongoza kuwa na dhahabu nyingi lazima tujiulize ni wapi tunakosea,” amesema Magufuli.

“Kuna udhaifu ambao Wizara ya Madini haiwezi kuukwepa. Kama tuna sheria nzuri, maeneo mengi ya kuchimba dhahabu, je tumeshawahi kujiuliza wanapochimba wanauza wapi na wanapouza tunapata mapato asilimia ngapi?

“Kwenye sheria kuna maelekezo ya kuanzishwa vituo vya madini je viko vingapi? Hivi vingesaidia kujua kiwango cha madini kinachopatikana na kinauzwa wapi?” Inauma unapoona kilo zaidi ya 300 zenye thamani ya zaidi ya bilioni 30 zinakamatwa zikisafirishwa. Wameshaiona Tanzania ni nchi ambayo unaweza kufanya lolote”,mesema Rais Magufuli na kusisitriza;

“Nitaendelea kufanya mabadiliko kila mahali nitakapoona sijaridhishwa mhusika ataondoka, hata Biteko nimekuteua nikiona mambo hayaendi ninavyotaka utaondoka.”
Share:

KIVUKO CHA MV MAGOGONI CHAPATA HITILAFU MAJINI,TEMESA YAOMBA RADHI

Leo tarehe 09/01/2019 mnamo saa 1:30 asubuhi kivuko cha MV. MAGOGONI kinachotoa huduma kati ya Magogoni na Kigamboni jijini Dar es Salaam kilipigwa na upepo mkali wakati kikikaribia upande wa Kigamboni. 

Hivyo, katika hali ya kupambana na upepo mitambo ya kuendeshea kivuko hicho iliingiliwa na takataka ambazo zilisababisha injini kupata moto na kupata hitilafu. 

Mafundi wetu wamefanikiwa kutatua hitilafu hiyo na huduma za kivuko hicho zimerejea katika hali ya kawaida mnamo saa 6:30 mchana. 

Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) unawaomba radhi abiria wote kwa usumbufu walioupata.

Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano
TEMESA
09/01/2019
Share:

POLISI WAPIGA MARUFUKU MAANDAMANO YA MBUNGE WA CHADEMA KUTETEA WASTAAFU

JESHI la Polisi wilayani Serengeti mkoani Mara imepiga marufuku maandamano yaliyopangwa kufanywa na Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha).

Maandamano hayo yalikuwa yafanyike leo Jumatano Januari 9, 2019 ili kumpongeza mbunge wa Bunda Mjini (Chadema), Ester Bulaya kwa jitihada zake za kuwatetea wastaafu kwenye suala la kikokotoo cha asilimia 25.

Barua ya kuzuia maandamano hayo imeandikwa na mkuu wa polisi wa wilaya hiyo, Mathew Mgema akisema suala la kusitisha kikokotoo cha asilimia 25 lilifanywa na Rais John Magufuli wakati alipozungumza na watumishi Desemba 28, 2018 na wala si Bulaya.

Polisi wamesema badala ya kufanya maandamano, wameshauri anaweza kuwasiliana na wananchi wake wa Bunda Mjini na kupanga namna ya kumpongeza Bulaya kwani ndio eneo lake la uwakilishi lakini si kufanya maandamano.

Mkuu huyo wa Polisi amesema hawatasita kuchukua hatua pale ambapo kuna ukiukwaji na dalili za uvunjifu wa amani.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger