Wednesday 22 November 2023

TMA YATOA TAHADHARI YA MVUA KUBWA ZENYE HATARI YA MAFURIKO

...

Mvua

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imetoa tahadhari ya uwezekano wa kunyesha mvua kubwa kuanzia leo Jumatano Novemba 22 hadi Novemba 25 ambazo huenda zikasababisha mafuriko kwa maeneo machache ambayo yanaweza kusababisha vifo.

Mvua hizo zinatarajiwa kunyesha katika Mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Pwani, Lindi, Mtwara, Tanga na visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba.

Kupitia taarifa ya Mamlaka iliyotolewa jana Jumanne Novemba 21, 2023, imetaja athari zinazoweza kujitokeza ni pamoja na baadhi ya barabara kutopitika kutokana na mafuriko pamoja na vifo kwa siku hizo, hivyo wananchi wanapaswa kuchukua tahadhari.

Via EATV
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger