Thursday 2 November 2023

PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI (AFDP) YASAIDIA WAKULIMA KUKABILIANA NA ATHARI ZITOKANAZO NA MABADILIKO YA TABIA NCHI.

...




Mtaalamu wa Masuala ya Ufuatilia na Tathmini Bw. Bernard Ulaya kutoka katika Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) akizungumza wakati Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa wa maendeleo ya Kilimo (IFAD) Ulipotembea Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Nchini Mkoani Arusha (TOSCI).
Mtaalamu wa masuala ya Lishe na Jinsia kutoka Mfuko wa Kimataifa wa maendeleo ya Kilimo (IFAD) Bi. Florence Munyiri akizungumza mbele ya wataalamu hawapo katika picha, mara Ujumbe huo kutoka IFAD ulipotembelea Taasisi ya Tafiti za Mbegu za Kilimo (TARI) Seriani Arusha.

Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD),na wataalamu wakiwa katika kikao na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Bw. Missaile Albano Musa, kabla ya Ujumbe huo kuanza ziara ya kutembelea baadhi ya Taasisi za Kilimo zinazotekeleza Programu ya kuelendela Kilimo na Uvuvi (AFDP) Mkoani humo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Bw. Missaile Albano Musa,na Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD),na wataalamu kabla ya Ujumbe huo kuanza ziara ya kutembelea baadhi ya Taasisi za Kilimo zinazotekeleza Programu ya kuelendela Kilimo na Uvuvi (AFDP) Mkoani humo.



NA; MWANDISHI WETU – ARUSHA


Imeelezwa kuwa, Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) imesaidia wakulima katika kufahamu na kutumia njia bora za kilimo cha kisasa zitakazowapelekea kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya Tabianchi.

Akizungumza wakati Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Kuendeleza Kilimo (IFAD)ulipotembelea kituoni hapo Novemba 1 mwaka huu , Mtafiti kutoka Taasisi ya Tafiti za Mbegu Nchini (TARI) tawi la Seriani Arusha Bw. Shida Nestory amesema, Wizara ya Kilimo kupitia Taasisi zake za Tafiti za Kilimo, (TARI) Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu (TOSCI) na Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA), Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Uchumi wa Buluu Zanzibar, umesaidia wakulima katika kufahamu na kutumia njia bora za kilimo cha kisasa.

TARI Seriani Mkoani Arusha inatekeleza kupitia zao la maharage na Mahindi ambapo kwa mazao yote mawili mradi umewasiaidia kuwafikia wakulima ambapo mabwana shamba wanapewa mafunzo ya namna ambavyo wakulima wawaweza kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi kupitia teknolojia mbalimbali ikiwa ni pamoja na matumizi bora ya aina za mbegu mbazo zinaweza kustahimili kwenye maeneo ya ukame.

“Tari inawaelimisha wakulima juu ya matumizi ya teknolojia ya kuvuna maji na kuwa na uhakika wa kulima katika misimu tofauti na matumizi ya mbegu bora ambazo zinaweza kukinzana na magonjwa.” Alisisitiza

Kwa Upande wake Mtaalamu wa masuala ya Ufuatiliaji na Tathmini kutoka katika Programu hiyo inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Bw. Bernard Ulaya alisema, Lengo la Timu hii ya IFAD kufanya ziara katika taasisi hizo ni kuangalia maendeleo ya program, mafanikio, changamoto zilizopo ili kama kuna maeneo yanayoweza kuboreshwa yaboreshwe.


“katika kituo cha Seriani program imeweza kuwasaidia kuwa na kitalu Nyumba mbacho kitaweza kuwasiaidia katika tafiti zao za kuweza kuzalisha mbegu mama na mbegu kwa matumizi ya wakulima.” Alifafanua


Wageni hao kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) pamoja na wataalam watatembelea maeneo hayo ya Kilimo katika Mikoa ya Arusha, Manyara Tabora, Morogoro na Dodoma kwa Upande waTanzania Bara Pamoja na Sekta ya Uvuvi na Uchumi wa Buluu katika baadhi ya mikoa ya Unguja na Pemba.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger