Thursday 1 September 2022

KASINO NDANI YA MWANZA HOTEL YATEKETEA KWA MOTO

...

Kasino iliyopo Mwanza Hotel jijini Mwanza imeteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo huku chanzo cha moto huo kikiwa bado hakijafahamika

Inaelezwa kuwa hakuna mtu aliyedhurika na moto huo japo umesababisha hasara katika kasino hiyo kwa kuteketeza vitu vyote vilivyokuwa ndani

Jeshi la zimamoto na uokoaji lilifika kwa wakati na kuanza kuuzima moto huo ili usiendelee kuleta madhara kufuatia hoteli hiyo kuwa katikati ya jiji la Mwanza na kuzungukwa na majengo mengine.

Miongoni mwa waliofika katika tukio hilo ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza Adam Malima

Kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Kamila Labani amesema wamefanikiwa kuudhibiti moto huo usisambae katika hoteli hiyo huku bado wanaendelea kuchunguza chanzo cha moto huo.

Chanzo - EATV
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger