Wednesday 1 June 2022

MADEREVA WAKATAA KULIPIA TOZO WANAPOTUMIA BARABARA YA JUU

...

Nairobi Expressway

Katibu Mkuu wa Uchukuzi nchini Kenya, Paul Mwangi Maringa, amesema kwamba madereva nchini humo wamekuwa wakikataa kulipia tozo mara wanapotumia barabara ya juu (Nairobi Expressway) kwa madai ya kwamba hawana pesa za kutosha na wengine wakidai hawana kabisa.


Madereva hao wamekuwa wakikataa kufanya malipo hasa wanapofika mahali pa kutokea, na kusema ipo haja kwa wizara kutoa elimu juu ya matumizi ya barabara hiyo kwa wananchi wake.

Katibu Mkuu Maringa amesema, kuna aina tatu za ulipaji wa ushuru huo, ikiwemo kwa njia ya fedha taslimu ama kwa njia ya mtandao na kwa kutumia kadi ya malipo.

Ujenzi wa barabara hiyo ya juu nchini Kenya ulianza mwaka 2019 na ilifunguliwa wiki mbili zilizopita kwa ajili ya majaribio.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger