Monday 20 June 2022

HAMIS AUAWA KWA KUPIGWA NA WANANCHI TUHUMA ZA KUIBA MAHINDI DEBE 2

...
NB- Picha haihusiani na Hamis wa kwenye hii habari chini

**
Mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Hamis Hassan, mkazi wa Kijiji cha Kambuzi, Kata ya Litapuga wilaya ya Mpanda mkoani Katavi, ameuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa na fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake kwa tuhuma za kuiba debe mbili za mahindi.

Inaelezwa kuwa kabla ya tukio hilo la mauaji, wananchi marehemu walimtuhumu kuiba debe mbili za mahindi mali ya Emmanuel Malela, na kiongozi wa mtaa huo aliwaagiza watu wanaomshikilia wamfikishe kituo cha polisi Kanoge ila wakajichukulia sheria mkononi.

Watu hao watano wanaotuhimwa kutekeleza mauaji ya Hamisi wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na kupitia kitengo cha upelelezi walibainika kukimbilia mkoani Tabora na kurudishwa Katavi kwa ajili ya kujibu mashtaka yanayowakabili.

Chanzo - EATV
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger