Friday, 17 September 2021

MREMBO ATEMBEA MTAANI DAR NA BANGO LA 'NATAFUTA MUME'

...

Picha ya Baby Nai akiwa na bango lake la kutafuta mume mtaani

Mrembo Baby Nai kutoka Buza Temeke amesema anatufuta mume wa maisha wa kumuoa mwenye miaka 20 hadi 70 na kigezo chake anataka awe mstaarabu na mcha Mungu.

Baby Nai ameongeza kusema hii ni siku ya tano kutembea na bango la kutafuta mume mtaani pia haoni shida ya kutembea na bango hilo kwa sababu havunji sheria za nchi.

Mwisho amemaliza kusema akikosa mume anayemtaka Dar es Salaam ataenda Arusha, Mwanza na Mbeya na akikosa hapo ataenda nchini Kenya na Uganda.

Chanzo - EATV
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger