Saturday 23 January 2021

RC SINGIDA AMVUA UONGOZI MWALIMU MKUU KWA TUHUMA ZA UBADHILIFU

...

 

Mkuu wa Mkoa wa Singida  Dkt. Rehema Nchimbi akizungumza na watendaji na wananchi ambapo alimuagiza Mkurugenzi wa Halmshauri ya Singida DC  Rashid Mwandoa  kumvua cheo  Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwachambia, Edward Ighonde pamoja na Mwalimu Mkuu Msaidizi Charles Mtiko kwa tuhuma ya wizi wa vifaa vya ujenzi wa nyumba ya walimu .

Mkuu wa Mkoa wa Singida  Dkt. Rehema Nchimbi akikagua ujenzi wa mradi huo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida  Dkt. Rehema Nchimbi akizungumza na wananchi na wanafunzi.

Na Mwandishi  Wetu, Singida

 MKUU wa Mkoa wa Singida  Dkt. Rehema Nchimbi amemwagiza Mkurugenzi wa Halmshauri ya Singida Dc Ndugu Rashid Mwandoa  kumvua cheo  Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwachambia, Edward Ighonde pamoja na Mwalimu Mkuu Msaidizi Charles Mtiko Kwa tuhuma ya wizi wa vifaa vya ujenzi wa nyumba ya walimu (Two in one).

Vifaa vinavyodaiwa kuibiwa ni mbao za kupauliwa, Saruji na nondo ambayo thamani yake bado haijafahamika.

Dkt. Nchimbi  ametoa agizo hilo baada ya kufanya ziara ya kushitukiza kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo ya ujenzi ambapo watuhumiwa wote wako Polisi.

Aidha ametoa maagizo kwa viongozi kuacha tabia ya kuwatetea watumishi wanao tuhumiwa kwa ubadhilifu na atakaye bainika atashughulikiwa vilivyo.

Nchimbi amewataka viongozi wa Serikali kusimamia miradi na kuwa waminifu katika fedha zinazoletwa na Serikali ya Rais Magufuli pia wananchi wa hakikishe wanalinda mali hizo kwani miradi hiyo ni kwa ajili ya maendeleo yao.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger