Tuesday 19 January 2021

JKT yasitisha mafunzo ya kujitolea mwaka 2020/2021

...


Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limesitisha kwa muda mafunzo ya kujitolea ya JKT kwa mwaka 2020/2021 yaliyokuwa yaanze hivi karibuni kwenye kambi mbalimbali nchini.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya JKT imeeleza kuwa mafunzo hayo yamesitishwa hadi hapo itakapotangazwa tena.

Kutokana na kusitishwa huko, JKT imewataka vijana wote ambao walichaguliwa na tayari wameripoti kwenye kambi walizopangwa, kurejea majumbani mwao.

Aidha, wale ambao walikuwa bado hawajaripoti kambini, wametakiwa kutoripoti.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger