Thursday, 5 November 2020

BARAZA LA MAWAZIRI KUKOMA SHUGHULI ZAKE LEO

...

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbas

Na Richard Mwaikenda,  Dodoma

BARAZA la Mawaziri limekoma leo kuendelea na shughuli za kikazi mara atakapoapishwa Rais Mteule, Dk. John Magufuli kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbas alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari jijini Dodoma jana, kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk Magufuli.

Dk Abbas alisema kuwa kisheria ni kwamba Baraza la Mawazili la 2015-2020 mwisho wake ni mara tu Rais Mteule atakapoapishwa kushika kipindi chake cha pili cha miaka mitano. Majukumu yote yatafanywa na makatibu wakuu wa wizara hadi atakapotangaza baraza jipya.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger