Saturday 28 November 2020

Picha: MAONYESHO YA BIASHARA NA TEKNOLOJIA YA MADINI SHINYANGA YAZINDULIWA

...

 



Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel, (watatu kutoka kulia) akizindua maonyesho ya Biashara na Teknolojia ya madini mkoani Shinyanga, wa pili kulia ni mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, wakwanza kushoto ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Zainab Telack, akifuatiwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi.



Na Marco Maduhu -Shinyanga.

MKUU wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel, amezindua rasmi maonyesho ya biashara na Teknolojia ya madini mkoani Shinyanga, na kuwataka wawekezaji wa madini kwenda kuwekeza mkoani humo, ili kuunyanyua mkoa huo kichumi na kukua kimaendeleo.


Uzinduzi wa maonyesho hayo umefanyika leo katika eneo la Butulwa Kata ya Old Shinyanga manispaa ya Shinyanga, na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa madini, akiwemo na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi na Elias Kwandikwa wa Ushetu, ambayo yatakoma Desemba Mosi mwaka huu.

Akizungumza kwenye maonyesho hayo, mkuu wa mkoa wa Geita, aliupongeza mkoa wa Shinyanga kwa kuanzisha maonyesho hayo, ambayo yatakuwa ni chachu kubwa ya kukuza uchumi wa mkoa huo.

“Naupongeza sana mkoa wa Shinyanga kwa kuanzisha maonyesho haya ya Biashara na Teknolojia ya madini, ambayo ni muhimu sana katika kutangaza fursa za uwekezaji, pamoja na wawekezaji wadogo wa madini kujifunza namna ya kutumia Teknolojia za kisasa za kuchimba madini na kupata mali nyingi,” amesema Gabriel.

“Pia nawaomba wawekezaji wakubwa wa migodi mkoani Shinyanga, mtoe kipaumbele kwa wazawa katika ajira za migodini, ikiwamo na kusambaza bidhaa mbalimbali ndani ya migodi hiyo ili wapate kunufaika na rasilimali za nyumbani na siyo kutoa ajira kwa watu wanje,”ameongeza.

Katika hatua nyingine ameitaka migodi hiyo mikubwa kuwekeza miradi mikubwa ya kiuchumi mkoani Shinyanga, ambayo itaacha alama na kuleta maendeleo ili kuubadilisha mkoa huo kimaendeleo na kuendana na hadhi ya rasirimali ilizonazo, na siyo kuwaachia mashimo na umaskini mkubwa.

Naye mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, amesema wameanzisha maonyesho hayo ya biashara na Teknolojia ya madini, ili kutoa fursa kwa wawekezaji na wafanyabiashara kuwekeza mkoani humo kwa sababu ni mkoa ambao una madini mengi.

Amesema katika mauzo ya Almasi kuanzia Julai 2020 hadi Novemba, wameuza Almasi zaidi ya Shilingi Bilioni 42.5, hivyo haoni sababu ya mkoa huo kuendelea kuwa maskini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Geoffrey Mwangulumbi, amesema wazo hilo la kuanzisha maonyesho hayo lilianza mwaka 2017 hadi 2019, mara baada ya kufanya utafiti, na kuona Shinyanga imedumaa kimaendeleo kwa sababu ya kukosekana kwa mzunguko wa kifedha

Aidha amesema maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya madini yatakuwa yakifanyika kila mwaka mwezi Julai, ili kuongeza thamani ya mnyororo katika Sekta ya madini na kuuinua kiuchumi mkoa wa Shinyanga.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI.


Mgeni Rasmi mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel, akizungumza kwenye maonyesho ya Biashara na Teknolojia ya Madini mkoani Shinyanga.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, akisoma taarifa kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini.

Mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi, akisoma taarifa ya maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi, akizungumza kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini mkoani Shinyanga.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Abubakari Mkadam, akizungumza kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini.
Mwenyekiti wa Chemba ya wafanyabiashara na viwanda mkoani Shinyanga Meshack Kulwa, akitoa shukrani kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini.
Wananchi wakiwa kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini.

Wananchi wakiwa kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini.
Wananchi wakiwa kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini.

Wananchi wakiwa kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini, mwenye kofia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Shinyanga Hoja Mahiba.

Wananchi wakiwa kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini.

Wananchi wakiwa kwenye maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini.

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel, (watatu kutoka kulia) akizindua maonyesho ya Biashara na Teknolojia ya madini mkoani Shinyanga, wapili kulia ni mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, wa kwanza kushoto ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Zainab Telack, akifuatiwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi.

Zaoezi la ukaguzi wa mabanda kwenye maonyesho hayo likiendelea.
Mkuu wa mkoa wa Geita Robert Gabriel, kulia, akiwa kwenye Banda la Tume ya Madini, akiwa ameshika madini ya Almasi.

Zoezi la ukaguzi wa mabanda likiendelea kwenye maonyesho hayo ya Biashara ya Teknolojia ya Madini.

Zoezi la ukaguzi wa mabanda likiendelea kwenye maonyesho hayo ya Biashara ya Teknolojia ya Madini.

Zoezi la ukaguzi wa mabanda likiendelea kwenye maonyesho hayo ya Biashara ya Teknolojia ya Madini.

Zoezi la ukaguzi wa mabanda likiendelea kwenye maonyesho hayo ya Biashara ya Teknolojia ya Madini.

Zoezi la ukaguzi wa mabanda likiendelea kwenye maonyesho hayo ya Biashara ya Teknolojia ya Madini.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi, akiwa na Mbunge wa Jimbo la Ushetu Elias Kwandikwa, kwenye Banda la chama cha wachimbaji wadogo mkoani Shinyanya (SHIREMA).

Mbunge wa Jimbo la Ushetu Elias Kwandikwa, wakiwa kwenye Banda la Shirika la umeme Tanesco mkoani Shinyanga.

Awali mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, wapili kutoka kulia, akimpokea Mgeni Rasmi mkuu wa mkoa wa Geita Robert Gabriel, kuja kuzindua maonyesho hayo ya Biashara na Teknolojia ya Madini mkoani Shinyanga, wakwanza kulia ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko.

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel kushoto akisalimia na Mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini Partobas Katambi.

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandis Robert Gabriel, akisalimiana na Mstahiki Meya mteule wa manispaa ya Shinyanga David Nkulila.

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandis Robert Gabriel, akisalimiana na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Debora Magilingimba.

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandis Robert Gabriel, akisalimiana na Miss utalii Tanzania 2020.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, kushoto akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, kushoto, akiwa na mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi, katikati, wakiwa na Miss Utalii Tanzania 2020, wakiteta jambo.

Burudani zikitolewa kwenye maonyesho hayo, ambapo kwaya AICT Shinyanga ikitoa burudani na kusindikizwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko.

Kwaya ya AICT Shinyanga ikitoa burudani, na kusindikizwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi, Mbunge wa Ushetu Elias Kwandikwa, akifuatia katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela.

Awali mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, wapili kutoka kushoto, akikagua mazingira ya eneo hilo kabla ya mgeni Rasmi kufika na kukagua mabanda kwenye maonyesho hayo.

Eneo la maonyesho ya Biashara na Teknolojia ya Madini mkoani Shinyanga, lililopo eneo la Butulwa Kata ya Oldshinyanga.

Na Marco Maduhu- Shinyanga.














Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger