Wednesday 25 November 2020

IBRAHIM NGWADA AMECHAGULIWA KUWA MEYA WA MANISPAA YA IRINGA

...

 

Ibrahim Ngwada akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kushinda kuwa meya wa Manispaa ya Iringa

Na fredy Mgunda,Iringa.

Ibrahim Ngwada amechaguliwa Kuwa meya wa manispaa ya Iringa  kwa kupata kura 19 huku akifuatiwa na Jackson Chaula kwa kupata kura tano katika uchaguzi uliofanyika  ukumbi wa  chama cha mapinduzi (CCM) Manispaa ya Iringa.

Akitangaza matokeo hayo msimamizi wa uchaguzi huo wa kumtafuta meya na naibu meya wa Manispaa ya Iringa Toviki Kivike alisema kuwa uchaguzi wa meya umefanyika kwa amani,uwazi na haki na wagombea wote wameridhika mara baada ya matokeo hayo kutangazwa.


Aidha msimamizi huyo alisema kuwa uchaguzi wa naibu meya ulifanyika mara mbili kutokana na ushindani ulikuwepo hivyo kuamriwa kurudia ndio alipopatikana mashindi.


Baada ya kutangazwa kuwa meya wa Manispaa ya Iringa  Ibrahim Ngwada  alisema kuwa anazitambua changamoto za wananchi wa manispaa za Iringa hivyo atahakikisha anazitatua vilivyo ili wananchi wapate maendeleo.

Ngwada aliongeza kwa kusema kuwa miaka mitano iliyopita Manispaa hiyo ilikuwa chini ya CHADEMA na walifanya maendeleo hivyoatakikisha wanafanya kazi kubwa kuleta maendeleo zaidi ya yaliyofanywa na watangulizi wake kuwa sasa manispaa hiyo ipo chini ya CCM.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger