Zitto ambaye ni kiongozi wa chama hicho alipata ajali Oktoba 6, 2020 mkoani humo wakati akielekea katika mkutano wa kampeni jimbo la Kigoma Kusini, akiwa na watu wengine wanne.
Baada ya kufika jijini Dar es Salaam, Zitto alipelekwa katika Hospitali ya Aga Khan na kufanyiwa upasuaji katika bega lake la kushoto.
Leo katika uwanja wa ndege mjini Kigoma wanachama na wafuasi wa chama hicho walifika eneo hilo kuanzia saa 3 asubuhi kwa lengo la kumlaki kiongozi wao huyo ambaye baada ya kushuka kwenye ndege alipokelewa na wanachama hao huku akiwashukuru kwa kumuombea.
0 comments:
Post a Comment