Wednesday 28 October 2020

Polisi Wamkamata na Kumwachia Halima Mdee

...

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni asubuhi ya leo Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 walimkata Mgombea Ubunge wa Kawe, Halima Mdee wa Chadema kufuatia sintofahamu iliyojitokeza katika zeozi la upigaji kura jimboni humo.

 Taarifa zinaeleza, Mdee alikamatwa katika Kituo cha Kawe kufuatia sintofahamu hiyo kutokea baada ya mgombea huyo kudai kuona masanduku ya kura yakiwa na kura zilizopigwa kinyume na utaratibu.

Akizungumzia sakata hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Edward Bukombe amesema, mgombea huyo alihojiwa baada ya kukamatwa kisha akaachiwa huru.

Kuhusu madai ya Mdee ya sanduku kukutwa na kura feki, Kamanda Bukombe amesema hawajapokea taarifa hizo.

.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger