Sunday, 11 October 2020

Bashiru Awaomba Watanzania Kutofanya Majaribio Ya Uongozi

...


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally, amewaomba watanzania kutofanya majaribio ya uongozi wa nchi kama baadhi ya vyama vinavyoendelea kuwalaghai kwa kuomba kujaribiwa.

Ameyasema hayo tarehe 10 Oktoba, 2020 katika mkutano wa kampeni jimbo la Ukonga.

“Hakuna Chama kingine mpaka leo tunapozungumza chenye uzoefu na uwezo wa kulinda umoja, upendo na mshikamano wa Taifa hili isipokuwa CCM.”

“Ndugu zangu, ninawaomba tusiwajaribu watu wasio na uzoefu, CCM inaouzoefu, inaweza kuwa na upungufu fulani kwa kuwa ni Chama cha watu sio cha malaika, lakini katika eneo la kulinda uhuru, Usalama, amani, umoja, mshikamano wa kitaifa na muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Hakuna Chama kingine cha kukupa uhakika katika hayo isipokuwa CCM.”


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger