Thursday 9 July 2020

SERIKALI YAKUTANA NA WADAU KUTATUA CHANGAMOTO KATIKA KILIMO CHA MKONGE

...
strong>
Naibu Waziri Kilimo Mhe. Omari Mgumba,akizungumza na wadau wa Tasnia ya mkonge katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Royal Village Jijini Dodoma

Mwenyekiti wa Bodi ya Mkonge Bi Mariamu Mkumbi wakati akihutubia wadau wa Tasnia ya mkonge katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Royal Village Jijini Dodoma
Wakuu wa Mikoa mbalimbali wakisikiliza mawasilisho mbalimbali katika mkutano wa wadau wa tasnia ya mkonge uliofanyika leo Jijini Dodoma.

Naibu Waziri Kilimo Mhe. Omari Mgumba (kushoto) akiwa na Katibu Mkuu Kilimo Bw. Gerald Kusaya wakifuatilia mjadala wakati wa mkutano wa wadau wa tasnia ya mkonge uliofanyika leo Jijini Dodoma.


Na.Alex Sonna, Dodoma

Serikali yakutana na wadau wa Mkonge nchini ili kujadili na kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazoikabili tasnia ya hiyo ili kuongeza tija katika uzalishaji, ajira na kukuza sekta ya viwanda, pato la mkulima na Taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo imebainishwa leo jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary wakati wa kufungua mkutano wa wadau wa mkonge nchini.

Aidha Mhe. Mgumba amesema kuwa serikali imeanda mikakati katika zao la mkonge ili kuongeza tija na uzalishaji kwa kuanzisha vitalu vya mbegu ya mkonge katika Halmashauri zote amabako zao la mkonge linastawi.

Mhe. Mgumba amesema kuwa kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo TARI Mlingano uzalishaji wa mbegu bora umeanza ili ziweze kuzalishwa kwa wingi.

Mhe. Mguma ameeleza kuwa serikali inafanya uhakiki wa mashamba ya Mkonge yaliyobinafsishwa ili yaweze kuzalisha mkonge kama ilivyokubaliwa kwenye mikataba.

Pia amesema kuwa selikari imejipanga Kutoa elimu kwa maafisa ugani katika vijiji na kata kwenye maeeo yanayolima mkonge ili kuwajengea uwezo wa kuwahudumia wanachi katika kulima zao la mkonge.

“serikali itaongeza Bajeti nakuwezesha Kituo cha Utafiti Mlingano kufanya utafiti wa aina mbalimbali za mbegu ya mkonge na kuzisambaza kwa wakulima bila kusahau Kulinda ardhi ya kilimo ili isibadilishwe matumizi ambapo Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imeshaanza kufanya maboresho katika Sera na Sheria zake”, ameweka wazi Mhe. Mgumba.

Mhe. Mgumba ameongeza kuwa watahakikisha wanahimiza na kushawishi wawekezaji kuwekeza mnyororo wa thamani wa Tasnia ya Mkonge hususan kwenye viwanda na teknolojia bora za uzalishaji wa bidhaa za mkonge ikiwemo magunia, mazuria, matofali, mapambo, n.k ili kupanua soko la ndani na nje.

Hata hivyo Mhe. Mgumba amesema kuwa watanzania kwa kushirikiana na serikali wanatakiwa kulinda viwanda vya ndani kwa kuongeza tozo na kodi kwa bidhaa mbadala wa mkonge zinazoingizwa hapa nchini kutoka nje ya nchi.

Naye Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Evarist Ndikilo ametoa wito kwa wadau wa mkonge kuwa wawazi katika mkutano huo ili baada ya kikao hicho basi wakatekeleze yale yatakayo kuwa yameamuliwa katika mkutano huo ili kufufua kilimo cha mkonge nchini na shabaha kubwa ikiwa ni kurudisha taswira ya zao hilo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mkonge Tanzania, Bi. Mariam Mkumbi amesema kuwa kutokana na zao la mkonge kuwa moja kati ya mazao saba ya kimkakati hapa nchini Pamoja na maelekezo ya serikali ya kuongeza uzalishaji wa zao la mkonge kutoka tani 36,000 mwaka 2019 na kufikia tani 120,000 mwaka 2025.

“Bodi ya Mkonge Tanzania imeandaamkakati wa kurudisha hadhi ya zao la mkonge kama ilivyo kuwa katika miaka ya 1960 ambapo Tanzania ilikuwa inaongoza kwa uzalishaji na ubora wa mkonge duniani”, ameeleza Bi. Mkumbi.

Bi. Mkumbi ameongeza kuwa uzalishaji huo unalenga kuhusisha takribani tani 62,331 kutoka kwa wazalishaji waliopo katika mashamba makubwa na tani 60,256.9 na zaidi ya hapo kutoka kwa wakulima wadogo katika mikoa 16 ndani ya kanda sita zilizoainishwa katika mpango huo wa ndani ya Tanzania Bara ambao watahamasishwa kpitia mpango huo.

Itakumbukwa kuwa zao la mkonge lina historia ndefu nchini kwani mwaka 1964 Tanzania iliweza kuzalisha jumla ya Tani 230,000 na kuongoza Duniani kwa uzalishaji wa zao la mkonge. Kipindi hicho mkonge ulikuwa unachangia asilimia 65% ya fedha za kigeni nchini.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger