Tuesday 28 July 2020

Kim Jong Un : Silaha za nyuklia zitazuia vita nyingine

...
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amesema hakutakuwa tena na vita kwa sababu silaha zake za nyuklia zitahakikisha ulinzi na hatma ya taifa hilo licha ya mbinyo na vitisho vya kijeshi kutoka nje. 

Kim ametoa matamshi hayo wakati wa sherehe za kuadhimisha miaka 67 tangu kumalizika kwa vita ya Korea ya mwaka 1950 hadi 1953 zililofanyika jana kwa halfa maalum iliyowajumuisha maveterani. 

Kiongozi huyo amesema hivi sasa Korea Kaskazini inao uwezo wa kujilinda dhidi ya vitisho vya kigeni na kwamba silaha za nyuklia zilizopo zitaweka kizingiti cha kuzuka mzozo mwingine wa kijeshi.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger