Saturday 11 July 2020

MAGUFULI AMCHAGUA SAMIA SULUHU KUWA MGOMBEA MWENZA URAIS TANZANIA

...

Samia Suluhu Hassan
Mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia CCM Dkt. John Pombe Magufuli amemchagua Mama Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM.

Magufuli amesema katika kipindi cha miaka mitano alichofanya kazi na Mama Samia kama makamu wa Rais amejifunza mengi na ameamua kuendelea naye katika awamu ya pili.

''Katika kipindi nilichofanya kazi na Mama Samia nimejifunza mambo mengi sana na kupitia yeye nawahikikishia nitakuwa mtetezi mzuri wa wanawake. Nimekuwa nikimtuma popote hakatai kama na nyie kina Mama mkitumwa hamkatai'', amesema.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger