Thursday 9 July 2020

BENKI YA 1&M TANZANIA YATIA FORA SABASABA

...
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Huduma za Rejareja wa Benki ya I&M Tanzania, Lilian Mtali, Meneja Masoko na Mawasiliano, Anitha Pallangyo, Ofisa Mauzo, Beatrice Fusi, Meneja Mwandamizi (Madeni na Maendeleo ya Bidhaa), Deepali Ramaiya, Meneja wa Tawi la Nyerere, Said Gagu na Ofisa Masoko na Mawasiliano, Debora Mwakyoma wakiwa katika Maonyesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba, Dar es Salaam.
 
Na MWANDISHI WETU -DAR ES SALAAM

BENKI ya I&M Tanzania inashiriki kwa mara ya kwanza Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, lakini inang’ara kwa kutoa bidhaa na huduma za kipekee ambazo zinakidhi mahitaji yote ya mteja katika soko.

I&M Tanzania ilitambulisha akaunti mpya ya wanawake ya Tunaweza inayotoa suluhisho kwa wanawake wa ngazi zote kuanzia mmoja mmoja, wajasiriamali hadi kikundi au taasisi.

Akaunti hiyo inajitofautisha kwa kutoa huduma bila malipo yoyote, haina makato ya kila mwezi na viwango vyake vya riba vinavutia kwenye akiba.



Akizungumza leo jijini Dar es Salaa, katika maonyesho hayo, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo, alisema kuwa bidhaa hiyo mpya imeunganishwa kwenye mtandao wa benki wa kidijitali ili kuwapa wateja huduma bora na endelevu wakati wowote wanapohitaji.

Amesema I&M Tanzania ni sehemu ya I&M Holdings Kenya iliyoanzishwa mwaka 1974 kama kampuni ya huduma za kifedha kabla baadaye kubadilishwa kuwa benki ya biashara.

“Mwaka huu inasherehekea miaka kumi ya huduma zetu katika soko la Tanzania. Tunafurahi kuendelea kuhudumia wateja wetu na wateja wapya, pia tunashukuru wateja wetu na washikadau wote walioshiriki katikakuiletea benki mafanikio makubwa kwa kipindi chote cha miaka kumi kwenye soko.”

“Tunatoa huduma kadhaa za kifedha ikiwa ni pamoja na akaunti ya akiba, current akaunti kwa madhumuni ya biashara, mikopo ya biashara, huduma za kubadili fedha, uhamishaji fedha kitaifa na kimataifa, huduma za kidijitali ambazo hutoa fursa kwa mteja kupata huduma za benki kupitia simu za mkononi kwa kupiga namba *150*32# au kupitia iClick- huduma ya benki kwa njia ya mtandao inayopatikana bila kikomo kwa saa 24,” amesema Anitha

Meneja Masoko na Mawasiliano huyo wa benki hiyo, amesema kuwa pia benki yao wanatoa unafuu na urahisi wa kupata mikopo na huduma nyingine kadhaa ambazo ziliwafanya watu waliotembelea banda lake kwenye maonyesho ya Sabasaba lililopo ukumbi wa Karume, upande wa kulia wa lango la kuingilia kuhamasika na kutaka kujua zaidi kuhusu benki hiyo.

“I&M inafungua milango kwa Watanzania wote kwenda kujiunga na benki inayojali mahitaji yao, iliyo tayari kuwapa huduma za kipekee za kifedha kupitia wafanyakazi wake wenye uzoefu zaidi katika kutoa huduma bora kwa wateja.

“Mbali na kushiriki katika maonyesho ya Sabasaba, benki hiyo inatoa huduma zake bora kupitia mtandao wa matawi yake yaliyoko maeneo ya Maktaba, Indira Gandhi, Nyerere, Kariakoo, Oysterbay pamoja na mikoani ikiwa ni pamoja na Moshi, Arusha na Mwanza,” amesema


 Timu ya wafanyakazi wa mauzo na idara ya masoko wa benki hiyo kutoka matawi yake ya Dar es Salaam inayoongozwa na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo na Ofisa Masoko na Mawasiliano, Debora Mwakyoma wapo kwenye maonyesho hayo ili kuwapa wageni na wale ambao wanataka kuwekeza katika benki inayoaminika na salama ikiwa na huduma za ATM zinazopatikana kwa saa 24.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger