Sunday 20 November 2016

MAJALIWA :SERIKALI IMEONDOA URASIMU WAWEKEZAJI WATOE HOFU

...

reli
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli nchini TRL, Masanja Kadogosa (kulia) kuhusu ujenzi  wa reli  inayounganisha  reli ya kati na  kiwanda cha Kiluwa Still Group cha Mlandizi Pwani Novemba 19, 2016  . Kulia kwake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa.(Picha na Ofisi ya Waziri  Mkuu)
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
WAZIRI mkuu Kassim Majaliwa amesema serikali imefanikiwa kuondoa urasimu katika baadhi ya halmashauri nchini na idara husika katika kutoa hati miliki kwenye maeneo ya uwekezaji ili kukuza sekta ya uwekezaji.
Aidha Majaliwa amefarijika kukuta njia ya reli yenye urefu wa km 4.3 kutoka reli ya kati kuelekea kiwanda cha kutengeneza nondo cha kilua kilichopo Kibaha Vijijini mkoani Pwani imekamilika kwa asilimia 100.
Sambamba na hayo amezisihi halmashauri nchini kutoa Ushirikiano kwa wawekezaji ili kuongeza ari ya kushawishika kuongeza viwanda.
Majaliwa aliyasema hayo katika ziara yake ya kutembelea maendeleo ya kiwanda cha Kilua cha Mlandizi na kiwanda cha kuunganisha magari na zimamoto cha Equator suma jkt Ruvu.
Alisema ameridhishwa na hatua zinazoendelea katika kukamilisha ujenzi wa viwanda hivyo.
Majaliwa alitoa wiki mbili kwa mkandarasi wa umeme katika kiwanda cha kilua kuhakikisha anakamilisha kufikisha umeme wa uhakika kiwandani humo.
Alieleza kuwa viwanda hivyo vimefikia kwenye hatua nzuri kwani vimekamilika kwa asilimia 80 na vyote vinatarajiwa kuanza kazi mapema mwaka 2017.
Hata hivyo alisema licha ya serikali kuondoa urasimu ulipokuwa ukilalamikiwa sasa halmashauri ziendelee kutenga maeneo, kupima maeneo ili kufungua milango ya uwekezaji.
Majaliwa alisema serikali imedhamiria kujenga viwanda na kufufua ambavyo vilikufa .
Aliiupongeza uongozi wa mkoa wa Pwani kwa kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano chini ya rais John Magufuli kujenga viwanda na kuvuta wawekezaji.
“Kiwanda hicho ni mradi mkubwa wenye thamani ya zaidi ya bil 200 mara utakapo kamilika utazalisha tani 2,000 na kuajili ya watu 300-800’
“Awamu ya kwanza ya kiwanda hiki kimegharimu dola za kimarekani mil. 45 sawa na sh. bil. 90 za kitanzania, na awamu ya pili kitagharimu zaidi ya dola milioni 100 sawa na zaidi ya bil 200, mitambo imefungwa na kipo vizuri,hivyo alimpongeza mwekezaji mzawa Mohammed Kilua”alielezea.
Waziri mkuu alisema mradi huo utakapoanza kazi utaliingizia mapato taifa kwa kiasi kikubwa ,kuwezesha ajira kwa wazawa na kuwaingizia kipato wajasiliamali.
Alisema mkoa wa Pwani unaangaliwa kupeleka viwanda na anashukuru uongozi wa mkoa na kupokea wawekezaji.
Kuhusu kiwanda cha kuunganisha magari na zimamoto Majaliwa alisema ni kiwanda mkombozi nchini.
Majaliwa alisema kwa kuunganisha matrekta na zimamoto kutarahisisha kupata kwa gharama nafuu vyombo hivyo vya moto nchini.
Nae waziri wa uchukuzi, pro. Makame Mbalawa aliomba reli hiyo itumike kwa matumizi lengwa.
Pro. Mbalawa alielezea viwanda vinavyohitajika njia za reli zinaboreshwa na kujengwa lakini pia ni jukumu la wawekezaji hao kuzitunza na kuzitumia vyema.
Mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ,alisema serikali mkoani hapo imedhamiria kuongeza wawekezaji na ongezeko la viwanda ili kuongeza ajira hususan kwa kundi la vijana.
Alisema wapo baadhi ya wananchi waliotakiwa kupisha reli hiyo ambao wanadai fidia ya sh. mil 95.726 na halmashauri inadai sh. mil 307.206.
Mhandisi Ndikilo alisema mkoa wanayotaarifa na wanaendelea na mazungumzo ili haki yao walipwe kwa wakati.
Alisema wananafasi kubwa ya kufanikisha nchi kuwa ya viwanda kwa kushirikiana na wamiliki wa viwanda.
Mhandisi Ndikilo alisema kuwa kwa sasa mkoa wa Pwani ajenda yake ni kuhakikisha unakuwa mkoa wa viwanda na hilo linawezekana kwa kuwa na viwanda vingi vya kuzalisha bidhaa mbalimbali.
Kwa upande wake mkurugenzi wa shirika la reli nchini, Masanja Kadogosa, alisema waziri mkuu alitoa agizo wakamilishe reli hiyo na sasa wamemalizia.
Alisema ujenzi huo umetumia sh. Mil 863 kwa kutumia mafundi wa ndani gharama ambayo ni ndogo.
Kadogosa alielezea kwamba wangetumia mafundi wa nje gharama ingekuwa kubwa.
Alisema licha ya kumaliza reli hiyo lakini kiwanda hicho cha kilua kimeomba tena kuongezewa reli nne za ziada.
Mkurugenzi wa kiwanda hicho Mohamed Kilua alisema wanatarajia kujenga kwenye eneo hilo viwanda vingine vinne.
Alitaja viwanda vinavyotarajiwa kujengwa kuwa ni kiwanda cha kutengeneza pikipiki, gemsum, tissues na nguzo za umeme.
Kilua alisema kukamilika kwa kiwanda hicho kinaliingizia pato taifa bil.25 kwa mwaka na  kuzalisha nondo tani 2,000 kwa siku
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger