Friday 24 October 2014

NEWS:DIAMOND PLATINUMZ KUFUNGWA JELA MIAKA MITATU

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Kufuatia tukio la staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuonekana jukwaani na sare zinazoaminika kuwa za Jeshi la Wananchi (JWTZ) kisha kukamatwa kwa kundi lake la Wasafi Classic Baby (WCB) na meneja wake, Babu Tale, kuna uwezekano wa jamaa huyo kufungwa jela miaka miwili au mitatu.

Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akisubiri zamu yake kupanda jukwaani.
Kwa mujibu wa chanzo chetu ndani ya jeshi la polisi,…
Na Musa Mateja
Kufuatia tukio la staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuonekana jukwaani na sare zinazoaminika kuwa za Jeshi la Wananchi (JWTZ) kisha kukamatwa kwa kundi lake la Wasafi Classic Baby (WCB) na meneja wake, Babu Tale, kuna uwezekano wa jamaa huyo kufungwa jela miaka miwili au mitatu.
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akisubiri zamu yake kupanda jukwaani.
Kwa mujibu wa chanzo chetu ndani ya jeshi la polisi, baada ya jeshi kutoa tamko kuwa ni kinyume cha sheria, juzi Diamond alitakiwa kwenda kujisalimisha polisi lakini hakufanya hivyo jambo lililosababisha wenzake kukamatwa na kuwekwa nyuma ya nondo za mahabusu ya Oysterbay, Kinondoni jijini Dar.
Ilisemekana kwamba baada ya Wasafi (madensa wa Diamond) kukamatwa, Babu Tale naye alifikishwa katika kituo hicho ambapo maafisa kadhaa wa jeshi la polisi walionekana katika eneo hilo wakiweka ulinzi mkali.
Madensa wa ‘Diamond Platnumz’ wa kundi la Wasafi Classic Baby (WCB) wakisindikiza shoo yake.
Chanzo hicho kilieleza kwamba, siku ya tukio Oktoba 21, mwaka huu, uongozi wa Diamond ulipewa muda wa kujieleza kabla ya saa 2:00 asubuhi lakini haukufanya hivyo ndipo hatua hiyo ikachukuliwa.
Hata hivyo, baadhi ya watu walikuwa wakihoji kwa nini jeshi la polisi lilimshikilia Babu Tale peke yake bila Diamond lakini vyanzo vilieleza kuwa mwanamuziki huyo huenda alikuwa safarini.
Diamond akiendelea kutoa burudani jukwaani.
Ilielezwa kwamba wanaomsaka Diamond na waliowakamata Wasafi ni wanajeshi wa Military Police (MP) ambao waliwabwaga jamaa hao kituoni hapo kisha kuendelea na mambo yao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Dar, Camillus Wambura alisema bado hajawasiliana na kituo cha Oysterbay kuhusu suala hilo na hajapata taarifa kwa kuwa kesi hiyo inachunguzwa na iko chini ya Mkuu wa upelelezi wa Mkoa.
Akijibu kuhusu taarifa za uongozi wa Diamond na Diamond kupewa muda wa kujieleza, Kamanda Wambura alijibu:
Diamond Chege wakifanya yao.
“Uchunguzi unafanywa huko (Oysterbay). Kwa sasa hivi sina taarifa hiyo nina mambo mengi sana. Kwa hiyo kwa sasa hivi uchunguzi unafanywa chini ya Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa. Sijapata nafasi ya kujua wamefikia wapi katika uchunguzi wa suala hilo.”
Mapema wiki hii, Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) lilitoa taarifa kwa vyombo vya habari likipiga marufuku raia kuvaa sare za jeshi.
Kwa mujibu wa mwanajeshi wa JWTZ ambaye aliomba hifadhi ya jina kwa kuwa si msemaji wa jeshi hilo, taaluma yake ya sheria imemfanya kuchimba kwa undani suala hilo na kugundua kuwa endapo Diamond atapatikana na hatia atapigwa faini au kwenda jela miaka miwili au mitatu au vyote, yaani faini na kifungo.
Alisema kosa la Diamond ni kushindwa kutii wito kwani alitakiwa kuripoti mwenyewe polisi hivyo lazima atapanda mahakamani kujibu shitaka hilo na lile lenyewe la kutumia sare za jeshi hilo.Chanzo hicho kilidai kwamba si mara ya kwanza kwa jamaa huyo kuingia kwenye kashikashi kama hiyo kwani kuna kipindi alikwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambapo alionekana na sare hizo stejini na akapewa onyo lakini safari hii amejiongeza tena kuonesha kuwa ni kichwa ngumu.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger