Wednesday 21 April 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 21,2021












Share:

Tuesday 20 April 2021

Naibu Waziri Masauni Awataka Vijana Kuchangamkia Fursa Za Uchumi Wa Blue Zanzibar


Na Benny Mwaipaja, Zanzibar
NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amewahimiza vijana Visiwani Zanzibar kuchangamkia fursa za uchumi wa blue unaotokana na shughuli za uvuvi na uchakataji wa samaki ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Masauni ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni-Zanzibar, ametoa rai hiyo wakati akizungumza na viongozi na baadhi ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi katika Jimbo la Kikwajuni akiwa katika ziara yake ya kikazi visiwani humo.

Amesema kuwa yeye binafsi na Mwakilishi wa Jimbo hilo katika Baraza la Wawakilishi Mhe. Nasor Ali Jazeerah pamoja na viongozi wengine wamejipanga kutoa vifaa vitakavyotumiwa na vijana kwa ajuili ya shughuli za uvuvi katika sekta hiyo ya uchumi wa blue ili waweze kujitegemea kwa kujipatia kipato cha uhakika.

“Tunataka tuangalie uwezekano wa kujenga mazingira mazuri ya kuwatafutia “ndoano” na siyo “samaki” na tumeandaa vitu vikubwa ambavyo sitaki niseme mapema hapa nitaondoa radha, mkawaambie vijana wa Kikwajuni kama hawatatoka kimaisha kipindi hiki hawatatoka maisha” alilisisitiza Mhe. Masauni.

Pamoja na kusisitiza masuala ya kiuchumi, Mhandisi Masauni alisema kuwa mipango mingine iliyowekwa na uongozi katika Jimbo la Kikwajuni ni kuendesha mashindano ya kusoma qoran kwa vijana na kuwataka wazazi kuwahimiza watoto wao kushiriki mashindano hayo.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Nasor Ali Jazeerah, aliwaahidi wakazi wa Jimbo la Kikwajuni-Zanzibar kwamba ahadi zote zilizoahidiwa wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita zitatekelezwa kikamilifu.

Alitoa wito kwa wakazi wa Jimbo hilo kushikamana, kupendana na kuacha majungu ili mipango ya maendeleo iliyopangwa iweze kutekelezwa kwa kasi zaidi.

Aliwashukuru wananchi kwa kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ili waendelee kuingoza nchi kwa umahili mkubwa.

Mwisho.


Share:

Dkt. Kalemani : Marufuku kuuza mafuta yasiyo na vinasaba


 Na Zuena Msuya Dodoma,
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amepiga marufu uuzaji wa mafuta ya Petroli, Dieseli, na Mafuta ya Taa yasiyo na vinasaba unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara nchini.

Dkt. Kalemani alitoa maagizo hayo Jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kushtukiza ya kukagua vinasaba kwenye mafuta yaliyopo katika vituo vya kuuzia mafuta mkoani humo, iliyofanyika Aprili 20, 2021.

Katika ziara hiyo aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Leonard Masanja, Naibu Katibu Mkuu, Kheri Mahimbali na Kamishna wa Petroli na Gesi, Adam Zuberi wa wizara hiyo, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka wa Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji nchini( EWURA),Mhandisi Godfrey Chibulunje.

Dkt. Kalemani Alisema kuwa vinasaba vinadhihirisha viwango na ubora wa mafuta nchini.

“Maelekezo yangu kwa wauzaji wa mafua nchini ni lazima muendelee kuuza mafuta yenye vinasaba kwa sasa ili kujiridhisha na kiwango na ubora wa mafuta nchini, na kama mafuta hayana vinasaba ni marufuku kuyachukuwa na kuuza, kuna minong’ono katika baadhi ya maeneo kuwa kuna mafuta yanayouzwa ya aina hiyo, tutakayembaini tutachukua hatua stahiki”, alisema Dkt. Kalemani.

Katika ziara hiyo, hakuna kituo hata kimoja kilichobaininika kuuza mafuta yasiyo na vinasaba.

Alieleza kuwa kwa sasa Shirika la Viwango nchini (TBS), ndiyo llililopewa kazi ya kupima na kuweka vinasaba katika mafuta yote yanayoingia nchini ili kudhibiti ubora na tayari kazi hiyo imeanza kufanyika.

Alisisitiza kuwa kuanzia sasa mafuta yote nchini yatakuwa yakipimwa na kuwekwa vinasaba na TBS na ikibainika kuna mafuta ambayo hana vinasaba hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watendaji husika.

“TBS ni chombo cha serikali, kinachofanya kazi ya kudhibiti ubora na viwango ikiwepo wa mafuta nchini hivyo kuanzia sasa ndiyo kifanya kazi ya kupima na kuweka vinasaba kwenye mafuta yote nchini, endapo atatokea mwingine mtaelekezwa na serikali”, alisisitiza Dkt. Kalemani.

Lengo la serikali kuipa TBS kazi ya kuweka vinasaba katika mafuta yote nchini ili kuokoa fedha za serikali zaidi ya shilingi bilioni tatu kwa mwezi ambazo awali alikuwa akilipwa aliyekuwa akifanya kazi hiyo.

Vilevile ni kuijengea uwezo taasisi hiyo na kuongeza ajira kwa watanzania.

Katika ziara hiyo, aliitoa maelekezo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Wizara ya Maji kuwachukulia hatua waafisa wawili katika idara ya manunuzi wa Mamlaka wa Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji nchini( EWURA), pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Manunuzi wa taasisi hiyo kwa kushindwa kutekeleza maelekezo ya serikali kwa wakati.

Dkt. Kalemani alisema kuwa watumishi hao, hawakutekeleza maagizo ya serikali yaliyotolewa tangu Februari 5, 2021, kwa sababu zao wenyewe, pia wachunguzwe kwa nini hawakutekeleza maagizo hayo, na kusababisha migogoro.


Share:

MGANGA ARUDISHA PESA BAADA YA NDUMBA ZAKE KUFELI KUNASA MCHEPUKO UNAOPAKUA ASALI YA JAMAA


Mganga kutoka Kathwana, Tharaka Nithi nchini Kenya aliyepokea kitita cha KSh 200,000 kutoka kwa jamaa flani ili amtengenezee dawa ya kumkomesha barobaro aliyezoea kuchepuka na mkewe amelazimika kuzirejesha pesa hizo baada ya dawa yake kutofanya kazi. 

Duru zinaarifu kwamba mzee alikuwa amechoka na tabia ya mkewe aliyempenda sana kugawa asali nje.

Kwa mujibu wa Taifa Leo, mzee huyo hakutaka kumkabili jamaa kwa kuwa alikuwa pandikizi la mtu ambaye angempokeza kichapo cha mbwa. 

Badala yake mzee aliamua kwenda kutafuta huduma za mganga ambapo alitoa donge nono la shilingi elfu mia mbili pesa taslimu.

 Inasemekana mganga alistaajabu kwani katika maisha yake ya huduma kwa wateja hajawahi pata kiasi kama hicho cha pesa.

“Mwanangu usiwe na shaka. Hapa ni maskani ya fundi. Hili suala litashughulikiwa kikamilifu. Halipo hata moja moja lilishawahi kunipiga chenga. Huyu lofa wako atakula nyasi. Wewe kamata hii dawa, uipake blanketi ambalo wawili hao hujifunika pindi wawapo kwenye gemu. Nakuhakikishia nyasi atazila,” mganga alijigamba.

 Mzee alirudi nyumbani akiwa mwingi wa matumaini kuwa dawa ya kutuliza mkewe aache kuruka ruka nje ya ndoa.

 Inaarifiwa kwamba pindi tu mama watoto alipoondoka, mzee alichukua dawa hiyo na kuinyunyiza kwenye blanketi na akasubiri kuona matokeo.

Hata hivyo siku iliyofuata nusra mzee azirai alipowafumania mke na mchepuko wake wakibarizi sebuleni baada ya kumaliza raundi tatu za mechi.

 Jamaa hakuingiwa na baridi kwani tayari alikuwa amezoea kupakua asali hata mzee wa nyumba akiwa karibu. 

Mzee aliingia kwenye gari lake moja kwa moja na kufululiza hadi kwa mganga huku akiwa na hasira.

 “Nipe hela zangu sasa. Zitoe hela zangu au nikutoe utumbo,” mzee alimuungurumia mganga. 

Mpiga ramli ambaye alikuwa na mipango ya kujenga nyumba hakuwa na lingine ila kuzitwaa hela hizo alizokuwa amezificha chini ya godoro akamrejeshea mzee.


Share:

WEKUNDU WA MSIMBAZI WAWASILI BUKOBA KUKABILIANA NA WAKATA MIWA KAGERA SUGAR


Na Abdullatif Yunus, Michuzi TV.

KLABU ya Simba tayari imewasili Mkoani Kagera mapema leo Aprili 20,2021 kusaka alama Tatu dhidi ya wenyeji wao Wakata miwa wa Kagera Sugar, ambapo Timu hiyo imewasili ikiwa na Kikosi chake kamili.

Wakiongea katika Mkutano na waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Coffee Tree Hotel Walimu wa Timu zote mbili wameonesha morali ya kupata ushindi kwa Timu zao, huku kila mmoja akionesha kuheshimu mwenzake kimchezo.

Akizungumza kwa Upande wake Kocha wa Kikosi Cha Wakata miwa wa Kagera Francis Baraza amesema Timu yake ipo sawa licha ya kuwa na majeruhi wachache huku akimwaga sifa kwa wapinzani wao kwa kile alichokisema kuwa Simba ni miongoni mwa Timu kubwa Afrika hivyo atapambana kupata ushindi.

Naye nahodha wa Timu ya Wekundu wa Msimbazi Mohammed Hussein amekiri kuwa Timu yao imekuwa Ikipata wakati mgumu hasa wanapokutana na Kagera Sugar katika Uwanja wa Nyumbani, Hali ambayo husababisha kupata Matokeo kwa tabu Sana.

Timu ya Simba itafanya mazoezi Jioni hii katika Uwanja wa Kaitaba tayari kwa kujiandaa na Mchezo wao wa Jumatano hii.





CHANZO - MICHUZI BLOG




Share:

SUPER – NHESHA: Dawa Bora Ya Kutibu Tatizo La Kisukari


SUPER – NHESHA
Ni dawa ya kutibu tatizo la sukari au jina la kitaalamu (Diabetes Mellitus) ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo Mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya Glucose katika mwili kutokana na mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza Insulin ya kutosha au seli za mwili wake kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote kwa pamoja na kupelekea mgonjwa wa sukari kupata haja ndogo mara kwa mara (Polyuria) uhisi kiu kila wakati (Polydipsia) Na (Polyphagia).


AINA YA KISUKARI
Kuna aina chache tofauti za ugonjwa wa kisukari (1) ni ugonjwa wa Auto hii aina mgonjwa wa Auto hushambulia mfumo wa kinga na kuharibu seli katika kongosho ambako insulin huzalishwa asilimia 10% ya watu wenye ungonjwa wa kisukari wanayo aina hii (Auto).


AINA YA PILI
Hii hutokea wakati mwili wako unakuwa sugu kwa insulin na sukari hujenga katika damu yako hii husababishwa na kuwa na sukari nyingi kwenye damu yako kuliko kawaida.


CHANZO CHA UGONJWA SUKARI
Viko vyanzo vingi mbalimbali vya sukari
1.     Shinikizo la damu (B.P)
2.     Viwango vya juu vya triglyceride (mafuta)
3.     Lishe yenye mafuta mengi na wanga
4.     Utumiaji mkubwa wa pombe kupita kiasi
5.     Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
6.     Mtindo wa maisha usiofaa kiafya
7.     Uzito na unene uliozidi
8.     Kutofanya mazoezi
9.     Umri
10.     Kurith


UNAJUAJE KUWA UNADALILI ZA KISUKARI
1.     Kusikia njaa mara kwa mara
2.     Kusikia kiu mara kwa mara
3.     Kupungua uzito
4.     Maono machafu
5.     Uchovu mara kwa mara
6.     Ukipata kidonda hakiponi
7.     Kushuka kwa kinga mwili


DALILI ZA KISUKARI KWA MWANAUME
Mbali na dalili za jumla za ugonjwa wa sukari wanaume wenye tatizo hilo wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa uume hushindwa kusimama misuri hulegea na kusinyaa, maumivu ya mgongo, kiuno, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kupata choo  kama cha mbuzi


DALILI ZA WANAWAKE
Wanawake wenye ugonjwa wa sukari wanaweza pia kuwa na dalili kama vile maambukizi kwa njia ya mkojo (U.T.I) maambukizi  ya gonzi kukakamaa


TIBA YA MAGONJWA YA SUKARI
Ugonjwa wa sukari unatibika bila kujali ni mda gani umepata hilo tatizo wengi wamekata tama na kuwa wabishi amini tatizo hili linatibika vizuri sana wengi wemepona.


Tumia dawa ya SUPER-NHESHAambayo ni dawa ya miti shamba yaani (asilia) ambayo humfanya mtu kupona na kuimalika kabisa.


Tutakuelekeza pia mfumo wa mtindo wa maisha utakao takiwa kutumia ili kutoluhusu tatizo hilo kurudi tena.


BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO/KANISANI NJIA PANDA YA KWENDA SINZA  SIMU: 0652 102 152/0788 330 105/ 0755 684 297 NYOTE MNAKARIBISHWA PIA TUNATUMA MIKOANI WHATAPPS NO 0652 102 152 



Share:

MAJALIWA: SERIKALI IKO IMARA, WATANZANIA ENDELEENI KUIAMINI


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ipo imara na miradi yote ya kimkakati inaendelea kujengwa, hivyo Watanzania waendelee kuwa na imani nayo.

Amesema Serikali inayoongozwa na Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ipo makini na inaendelea kuwatumikia Watanzania. ”Tuendelee kuchapa kazi”.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Aprili 20, 2021) baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota, Dar es Salaam.

”Siri ya kuwepo mafanikio na maendeleo nchini ni utulivu na amani. Tulianza vizuri tangu Serikali ya Awamu ya kwanza, tutaendelea kuimarisha amani na utulivu.”

Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kuwaasa Watanzania watumie muda mwingi kufanya shughuli za maendeleo kuliko mambo mengine yasiyo na tija.

Akizungumzia kuhusu mradi huo, Mheshimiwa Majaliwa amesema amefurahi kukuta majengo yamekamilika na kwamba ameridhika na maendeleo ya ujenzi wake.

Waziri Mkuu ameuagiza uongozi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wahakikishe wanakamilisha kazi iliyosalia haraka ili mwaka huu wananchi waanze kuishi hapo.

Naye, Mtendaji Mkuu wa TBA, Bw. Daud Kondoro amesema mradi huo una jumla ya block tano na ambazo zinauwezo wa kuchukua familia 656.

Amesema mbali na ujenzi wa nyumba hizo za makazi pia katika eneo hilo wanajenga maduka makubwa pamoja na vizimba kwa ajili ya wajasiriamali kufanya biashara.

Mradi ulianza kutekelezwa mwaka 2016 na unatarajiwa kukamilika Mei 2021. Hadi sasa umefikia asilimia 94 ya utekelezaji wake na gharama yake ni shilingi bilioni 50.

Baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za makazi za Magomeni Kota, Waziri Mkuu alikagua kituo cha Reli ya Kisasa cha Tanzanite jijini Dar es Salaam.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

RAIS SAMIA AKUTANA NA SPIKA NDUGAI IKULU DODOMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai leo tarehe 20 Aprili, 2021 Ikulu Jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiagana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai mara baada ya mazungumzo yao leo tarehe 20 Aprili, 2021, Ikulu Jijini Dodoma.
Share:

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AKUTANA NA KATIBU MKUU KIONGOZI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, akisalimiana kwa Ishara maalum na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Hessein Katanga walipokutana na kufanya mazungumzo Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Chamwino Jijini Dodoma leo April 20,2021.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Share:

WAZIRI UMMY AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI HALMASHAURI YA SENGEREMA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Ummy Mwalimu amemsimamisha Kazi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Magesa Boniphace kuanzia leo 20 Aprili, 2021 ili kupisha uchunguzi dhidi yake.

Amechukua hatua hiyo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Jimbo hilo, Hamis Tabasamu kuhusu tuhuma za ubadhirifu wa fedha za miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo.

Tuhuma hizo zinasema Mkurugenzi kwa kushirikiana na Wakuu wa Idara, wamekuwa wakifanya ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za Umma zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Share:

NAIBU WAZIRI KATAMBI: SERIKALI KUENDELEA KUWAPATIA VIJANA WA KITANZANIA MAFUNZO YA STADI ZA KAZI

Na: Mwandishi Wetu – Dodoma

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Patrobas Katambi amesema Serikali imeendelea kutambua umuhimu wa kuwapatia vijana ujuzi wa stadi za kazi na maarifa kama hatua mojawapo ya kuwawezesha vijana kumudu ushindani katika soko la ajira la ndani na nje.

Aliyasema hayo hii leo Aprili 20, 2021 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majiliwa (Mb) ambalo liliulizwa na Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Latifa Khamis Juakali, ambaye alitaka kujua ni lini vijana wa Tanzania watapewa stadi mbalimbali za kuwaongezea ujuzi wa maarifa kupitia mfuko wa uwekezaji wa wananchi kiuchumi.

Akijibu swali hilo Mheshimwa Katambi, alieleza kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu imeendelea kutekeleza Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi inayolenga kuwezesha nguvu kazi ya Taifa kupata ujuzi na stadi za kazi stahiki ili kumudu ushindani katika soko la ajira.

“Jumla ya vijana 5,538 wamepatiwa Mafunzo ya kukuza ujuzi kwa njia ya uanagenzi (Apprenticeship) katika fani za ufundi stadi katika nyanja mbalimbali kupitia Taasisi ya Don Bosco na Vyuo vilivyo chini ya VETA,” alieleza Katambi

Aliongeza kuwa, Serikali imeingia Mkataba na VETA wa kurasimisha ujuzi kwa vijana katika Mikoa yote nchini katika fani mbalimbali ikiwemo za Ufundi wa Magari, Useremala, Uashi, Upishi, Huduma za vyakula na vinywaji, Ufundi Umeme, Uchomeleaji vyuma, Ufundi bomba, Uchongaji Vipuri na Ushonaji wa Nguo.

“Katika mwaka wa fedha 2020/2021 kufikia Februari, 2021 jumla ya vijana 10,178 walikuwa wamerasimishwa na kati yao 28 ni Watu wenye Ulemavu,” alisema

Sambamba na hayo, alielezea Mafunzo ya Uzoefu Mahala pa Kazi ambayo yametoa fursa kwa Vijana wengi wanaohitimu elimu ya juu kuendelea kuwashikiza kwa Waajiri ili kupata uzoefu makazini.

“Kwa mwaka wa fedha 2020/21 hadi kufikia Februari 2021, jumla ya wahitimu 1,203 wa Vyuo vya Elimu ya Juu na Kati wamekamilisha mafunzo ya uzoefu kazini kupitia Viwanda, Taasisi na Kampuni mbalimbali za Sekta binafsi na Umma nchini na wahitimu 2,037 wanaendelea kupata ujuzi na uzoefu katika Taasisi binafsi na za umma na kati yao, wahitimu 92 ni Watu wenye Ulemavu,” alieleza Katambi

Aidha, Naibu Waziri Katambi alieleza vijana hao wanapomaliza mafunzo yao wamekuwa wakiwezeshwa kiuchumi kupitia mikopo yenye riba nafuu ikiwemo mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu kupitia halmashauri zilizopo nchini pamoja na Mfuko wa Maendeleo ambayo imekuwa chachu kwa vijana kuanzisha miradi mbalimbali.

Pia alibainisha kuwa serikali imekuwa ikitenga maeneo kwa ajili ya shughuli za vijana katika halmashauri zilizopo nchini ili kuwasaidia vijana kutumia fursa za kiuchumi zinazopatikana katika maeneo yanayowazunguka.

 

Share:

RAIS WA CHAD AUAWA KWA KUSHAMBULIWA NA WAASI


Jeshi la Chad limetangaza kuwa Rais wa nchi hiyo Idriss Deby amefariki baada ya kupata majeraha kwenye mapambano dhidi ya waasi.

Deby alienda mwishoni mwa wiki kuvitembelea vikosi vya nchi hiyo ambavyo vinapambana na waasi kaskazini mwa nchi hiyo. Waasi hao wamevuka mpaka wakitokea Libya.

Kifo chake kimetokea ikiwa ni saa chache tu tangu matokeo ya awali ya uchaguzi uliofanyika Aprili 11 kuonesha kuwa anaongoza kwa asilimia 80. Kwa ushindi huo, Deby angeiongoza nchi hiyo kwa awamu ya sita mfululizo.

Serikali na bunge vimevunjwa na sasa baraza la kijeshi ndilo litakaloiongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miezi 18 ijayo.



Share:

TBS YAFANYA UKAGUZI WA KUSHTUKIZA KANDA YA MAGHARIBI KWENYE MADUKA YA VYAKULA NA VIPODOZI

Wakaguzi wa TBS wakiendelea na ukaguzi na usajili wa majengo ya bidhaa za chakula na vipodozi Mkoani Pwani. TBS inawakumbusha wauzaji na waagizaji wa bidhaa hizo kuhakikisha wanasajili ili kuhakiki ubora na usalama wake ili kuepuka usumbufu usio wa lazima sambamba na kuzingatia taarifa muhimu kwenye bidhaa husika kama vile muda wa matumizi na orodha ya viambata.
Mkaguzi wa TBS, Bw. Elisha Meshack akimfanyia usajili mmiliki wa duka la chakula mara baada ya ukaguzi wa duka lake wilayani Kakonko. TBS inawakumbusha wenye majengo ya chakula na vipodozi kufanya usajili mara moja ili kuepuka usumbufu
 Mmiliki wa duka la chakula na vipodozi wilayani Kakonko akionesha vibali vyao vya majengo kwa wakaguzi wa TBS wakati wa ukaguzi wa kushtukiza sokoni na usajili wa majengo ya bidhaa za chakula na vipodozi. TBS inawakumbusha wenye majengo hayo kusajili ili kuepuka usumbufu
Mkaguzi wa TBS, Bw. Emmanuel Mushi akiendelea na ukaguzi wa kushtukiza wilayani Kakonko ili kuhakiki ubora na usalama wa bidhaa za chakula na vipodozi hususani muda wa mwisho wa matumizi.
Wakaguzi wa TBS wakiwa katika ukaguzi wa kawaida katika kiwanda cha kuzalisha maji ya kunywa wilayani Kibondo kijulikanacho kama " Malagarasi Mineral General Supply". TBS inawahimiza wazalishaji kuthibitisha ubora wa bidhaa zao ili kuepuka usumbufu.
Mkaguzi wa TBS, Bw. Elisha Meshack akiwa kwenye ukaguzi wa bidhaa za vilainishi Wilayani Uvinza ambapo sampuli zilichukuliwa kwa ajili ya kupimwa katika maabara ili kujiridhisha kama zimekidhi ubora wa kiwango husika.

**********************************

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa kushirikishana na mkoa na Halmashauri husika, limeendelea na mpango wa ukaguzi wa kushtukiza sokoni kwa wasambazaji na wauzaji wa bidhaa za vilainishi, vipuli vya magari, vifaa ya ujenzi, chakula na vipodozi uliofanyika Kanda ya Magharibi Mkoani Kigoma katika wilaya za Kakonko, Kibondo, Buhigwe, Kasulu, Uvinza na Kigoma.

Ukaguzi huo umelenga kuhakiki iwapo bidhaa zinazouzwa soko ni kama zimekidhi ubora wa kiwango husika kulingana na ukaguzi uliofanyika katika maeneo ya uzalishaji na wakati zikiingizwa kutoka nje ya nchi, ili kuhakikisha wanapunguza tatizo la uwepo wa bidhaa hafifu sokoni aidha zinazoingizwa kupitia njia zisizo rasmi au kuzalishwa kwa kutozingatia matakwa ya kiwango husika.

Ukaguzi huo ulienda sambamba na utoaji elimu kwa wauzaji na wanunuaji juu ya uhifadhi sahihi wa bidhaa na umuhimu wa kuzingatia na kusoma taarifa sahihi na muhimu katika vifungashio.

TBS imefanya ukaguzi huu sambamba na usajili wa majengo ya chakula na vipodozi ili kuhakikisha majengo husika yanazingatia ubora na usalama wa bidhaa za chakula na vipodozi vinavyohifadhiwa au vinavyouzwa ndani ya majengo hayo.

Kaimu Mkuu wa Kanda ya Magharibi (TBS),Bw. Rodney Alananga ametoa wito kwa waingizaji na wauzaji wa bidhaa zilizo katika viwango vya lazima kuzingatia sheria na taratibu za uingizaji na uuzaji bidhaa kwa kuuza na kuingiza bidhaa ambazo ni bora na salama ili kukuza biashara na kuepuka kupoteza masoko na kero ya kukutwa na bidhaa hafifu ambayo itawalazimu kuziteketeza kwa gharama zao.

Pia aliwashauri wasisite kuwasiliana na ofisi ya TBS mara kwa mara pale wanapohitaji msaada wa kitaalamu.

Kwa upande wake Afisa Usalama wa Chakula (TBS ), Bw. Elisha Meshack alisema ukaguzi huo ni iendelevu kwani ni moja ya majukumu ya Shirika na utahusisha bidhaa mbalimbali katika sekta zote kasoro dawa na unaendelea pia katika wilaya za Mpanda, Tanganyika, Mpimbwe, Sumbawanga, Kalambo na Nkasi kwa upande wa Kanda ya Magharibi.

"Huu ni mwendelezo tu wa shughuli zetu za kila siku, kwani Shirika linahakikisha ukaguzi kama huu unafanyika katika kila wilaya nchi nzima ili kuhakikisha tatizo la bidhaa hafifu linapungua kwa kiasi kikubwa kama sio kwisha kabisa " alisema.

Afisa udhibiti ubora (TBS), Bw. Emmanuel Mushi aliwasisitiza wafanyabiashara wa maduka ya chakula na vipodozi ambao wamefanyiwa ukaguzi na kupewa gharama za malipo na bado hawajalipia gharama za usajili kulipia mara moja ili wapate kibali cha kuuza bidhaa husika katika majengo hayo ili kuepuka usumbufu na wale ambao hawajasajili majengo yao kusajili mara moja.

Meneja wa kiwanda cha kuzalisha maji wilayani Kibondo kijulikanacho kama "Malagarasi Mineral General Supply",Bw. Samir Adam ameipongeza TBS kwa kusogeza huduma karibu na amekuwa akipata ushirikiano wa kutosha kutoka ofisi ya kanda ya magharibi- Kigoma.

" Hapo mwanzo tulipoanza tulikuwa na changamoto ya kupata cheti na kutembelewa kwa wakati ila kwa sasa nashukuru ofisi ya TBS kanda ya magharibi iko jirani na inanipa ushirikiano mkubwa sana" alisema.

Pamoja na ukaguzi huo TBS inatumia fursa hiyo ya kukutana na mfanyabiashara mmoja mmoja kuelezea majukumu ya Shirika ikiwa ni pamoja na yale yaliyokua yakifanywa na iliyokuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa ( TFDA).
Share:

Tanzia : MKURUGENZI WA SHUWASA FLAVIANA KIFIZI AFARIKI DUNIA




Flaviana Kifizi enzi za uhai wake
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA),Flaviana Kifizi amefariki dunia leo alfajiri Jumanne Aprili 20,2021wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam baada ya kuugua muda mrefu.

 R.I.P Flaviana Kifizi




Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRILI 20,2021















 


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger