Tuesday 20 April 2021

WAZIRI UMMY AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI HALMASHAURI YA SENGEREMA

...

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Ummy Mwalimu amemsimamisha Kazi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Magesa Boniphace kuanzia leo 20 Aprili, 2021 ili kupisha uchunguzi dhidi yake.

Amechukua hatua hiyo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Jimbo hilo, Hamis Tabasamu kuhusu tuhuma za ubadhirifu wa fedha za miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo.

Tuhuma hizo zinasema Mkurugenzi kwa kushirikiana na Wakuu wa Idara, wamekuwa wakifanya ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za Umma zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger