Thursday, 18 September 2025

SERIKALI IMETOA BILIONI 17 KUKABILIANA NA UHABA WA LITA MILIONI 2.7 ZA MAJI CHAMWINO



Na Dotto Kwilasa, Dodoma

Serikali imetoa Shilingi Bilioni 17 kutekeleza Mradi wa Maji wa Miji 28 katika wilaya ya Chamwino, mkoani Dodoma, hali itakayosaidia kuondoa upungufu wa zaidi ya lita milioni 2.7 za maji unaojitokeza kila siku Wilayani hapo.

Kwa mujibu wa Meneja wa DUWASA Wilaya ya chamwino Gray Mbalikila
ameeleza kuwa kwa sasa mahitaji ya maji katika mji huo ni wastani wa lita milioni 7.5 kwa siku, huku uzalishaji ukiwa lita milioni 4.8, hivyo kusababisha upungufu mkubwa kwa wananchi.

Akizungumza mapema leo Sept 15,2025 Mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule kutembelea Mradi huo,Meneja huyo amesema mradi huo unalenga kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama, kuchochea shughuli za kijamii na kiuchumi, na kupunguza magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji yasiyo salama.

Amesema Mkataba wa mradi huo ulisainiwa tarehe 6 Juni 2022 na utekelezaji ulianza rasmi mwaka 2023 na kwamba Utekelezaji huo unatarajiwa kukamilika ifikapo 10 Desemba 2025, ambapo hadi sasa mradi umefikia asilimia 45.

Amefafanua kuwa kazi zinazotekelezwa ni pamoja na uchimbaji wa visima virefu, ujenzi wa tenki la maji lenye ujazo wa lita 500,000 Chamwino, tenki la lita 200,000 Msanga na tenki kubwa la lita milioni 2.5 Buigiri. 

Vilevile, mradi unahusisha ulazaji wa mabomba umbali wa kilomita 47, ikiwemo km 31 za mabomba makuu na km 16 ya kusafirisha maji kuelekea Msanga na Buigiri.

Amesema Mradi huo utakapokamilika, zaidi ya wananchi 59,000 katika kata 4, vijiji 7 na vitongoji 48 watanufaika na huduma hiyo.

"Upatikanaji wa maji safi utaongezeka kutoka asilimia 91 ya sasa hadi kufikia asilimia 100, huku uzalishaji ukiongezeka hadi wastani wa lita milioni 12.32 kwa saa 22 za uzalishaji, " ameeleza

Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amesisitiza kuwa serikali imejipanga kuhakikisha wananchi wanapata maji bora na salama kwa wakati, na kuwataka wakandarasi kukamilisha kazi kwa viwango na muda uliopangwa.

“Tunataka wananchi wa Chamwino wapate maji safi na salama yenye ubora unaohitajika, ni lazima mkandarasi ajipange ili kuhakikisha kazi inakamilika kwa wakati,” amesema Senyamule.

Ameongeza kuwa wakandarasi wanapaswa kuongeza idadi ya mafundi na kuondoa visingizio visivyo na msingi, huku akiwataka vijana wazawa wanaoshiriki kwenye ujenzi wa mradi huo kuwa walinzi wa ubora wa kazi inayoendelea.

Kutokana na hayo baadhi ya Wananchi wa Chamwino wameeleza matumaini yao kwa mradi huo ambapo Juma Shabani wa Buigiri amesema mgao wa maji ulikuwa kero kubwa, lakini sasa hali inabadilika.

Kwa upande wake Theresia Paulo wa Msanga ameeleza kuwa watoto walikuwa wanapoteza muda wa masomo kwa kufuata maji mbali, hali ambayo sasa itabaki historia.

Naye Richard Mawela wa Chamwino mjini amesema mradi huo utaleta mabadiliko makubwa na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa juhudi za kumtua mama ndoo kichwani.


Share:

Wednesday, 17 September 2025

CEMEX VENTURES LIMITED YATARADIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MAFUTA YA KUPIKIA HADI TANI 100 KWA SIKU




Na Mwandishi Wetu, Dodoma


Kiwanda cha Cemex Ventures Limited kinatarajia kuongeza uzalishaji wa mafuta ya kupikia kutoka tani 50 hadi kufikia tani 100 kwa siku ndani ya miezi miwili ijayo.
Akizungumza wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Meneja Mkuu wa Kiwanda hicho, Frank Goyai, alisema kuwa kampuni imewekeza zaidi ya Sh. bilioni 10 na kutoa ajira kwa zaidi ya wafanyakazi 110.

Goyai alisema teknolojia mpya ya mitambo imewekwa na inafanya kazi masaa 24 kwa siku. 

“Hapa kiwandani mashine hatuzimi, zinafanya kazi muda wote,” aliongeza. Alibainisha kuwa Cemex Ventures Limited, kampuni ya Kitanzania inayomilikiwa kwa asilimia 100 chini ya Mac Group, ilianzishwa mwaka 2023 baada ya kununua kiwanda cha Pyxus kilichokuwa kimesimama kwa muda mrefu.

Kiwanda hicho kimepatiwa ekari 30 katika Eneo la Viwanda la Nala, na kinatarajia kuwekeza zaidi ya Sh. bilioni 100 kujenga kiwanda kipya cha kisasa kitakachozalisha: mafuta ya kupikia ya alizeti, sabuni za kuogea na kufulia, sabuni za unga, glycerine, malighafi za vipodozi, pamoja na mashudu kwa ajili ya chakula cha mifugo. Kupitia chapa yake kuu ya Zeti Sunflower Oil na chapa mpya ya kimataifa Golden Harvest, Cemex inatoa mafuta salama, yasiyo na cholesterol, yaliyoimarishwa kwa vitamini na yenye uthibitisho wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Goyai aliongeza kuwa zaidi ya tani 8,000 za mbegu za alizeti zimenunuliwa, huku uwekezaji huo ukilenga kutoa ajira zaidi ya 110. Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, alisema amefurahi kuona uwekezaji mkubwa kama huo katika uzalishaji wa mafuta ya kupikia na kusisitiza kuwa alizeti ni zao la kimkakati.


 Alisema matarajio ya serikali ni kujitegemea kwa mafuta kwani sehemu kubwa ya mafuta yamekuwa yakiagizwa nje ya nchi.

Sen. Senyamule aliweka wazi kuwa serikali ina wajibu wa kutatua changamoto zinazokwamisha wawekezaji. “Nimeambiwa kuna changamoto ya upatikanaji wa alizeti; hii ni fursa kubwa kwa wakulima kuongeza uzalishaji kwani fursa za masoko ni nzuri,” alisema.

 Alisisitiza kuwa wadau wanatakiwa kukaa pamoja ili kuongeza uzalishaji wa alizeti na kwamba mashamba ya umwagiliaji yametengezwa kwa ajili ya kuhakikisha uzalishaji unafanyika ipasavyo.

Aliwataka wakuu wa wilaya za Bahi, Chamwino na Dodoma, maeneo yenye miradi mikubwa ya umwagiliaji, kushirikiana kuona namna zao hilo litaendelezwa. 

“Dhamira yetu ni kuendeleza mkoa wa Dodoma kwa kuvutia wawekezaji,” alisema. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri, alisema kiwanda hicho ni miongoni mwa wadau wakubwa katika uzalishaji wa alizeti. “Kuzalisha tani 50 za mafuta kila siku sio uwekezaji mdogo; kwa mwaka wanazalisha tani 18,650. Tunapaswa kushirikiana nao kwani wananunua alizeti za wakulima na pia kutoa ajira,” alimalizia.








Share:

WAFANYABIASHARA DODOMA WAIPONGEZA SERIKALI KWA KUTATUA KERO ZA KODI KWA 85% HALI INAYOSABABISHA BIASHARA KUNG’ARA



Na Dotto Kwilasa,Dodoma


Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) kwa Mkoa wa Dodoma imesema,
Makusanyo ya kodi katika Mkoa huu yameongezeka kwa kasi kubwa, kufikia zaidi ya shilingi bilioni 204 ikilinganishwa na lengo la awali la shilingi bilioni 88 hali iliyotajwa kuwa ni ushahidi wa mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Hayo yameelezwa mapema leo September 17,2025 Jijini Dodoma na Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo(JWT)Alexander Mallya kwenye mahojiano maalumu na Waandishi wa habari ambapo amefafanua kuwa ongezeko hilo ni kielelezo cha uboreshaji wa mazingira ya biashara na uaminifu wa wafanyabiashara kulipa kodi.

Katibu huyo amesema kero za kodi na ushuru ambazo kwa muda mrefu zilikuwa kikwazo zimepungua kutoka kero 119 hadi kubaki 18 pekee, huku 36 zikiwa kwenye hatua za mwisho za kutatuliwa na kueleza kuwa ni jambo la kuishikuru Serikali kwa Uongozi thabiti na hatua za kimkakati katika Sekta ya biashara na uchumi.

“Hii ni hatua kubwa na inatupa matumaini ya kufanya biashara kwa uhuru na kuendelea kuchangia mapato ya taifa,” amesema Mallya.

Ameeleza kuwa wafanyabiashara wanataka kuona kilimo kikipewa msukumo mkubwa ili kuvutia miradi mikubwa, kuongeza viwanda vitakavyotoa ajira kwa vijana, pamoja na kuimarishwa kwa sekta ya madini.

Aidha amewashauri wafanyabiashara wa Dodoma kutumia fursa ya SGR kama kitovu cha biashara kwa kujibidiisha kufanya kazi kwa bidii.

Mallya amesema maendeleo makubwa yameonekana kupitia miradi mikubwa ya kimkakati ukiwemo ujenzi wa Magufuli City na SGR inayopunguza safari za Dodoma–Dar kutoka saa 8 hadi saa 3, na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato unaotarajiwa kuhudumia safari za kimataifa.

"Tunaamini serikali inaendelea kuboresha mtandao wa barabara ili kurahisisha usafirishaji wa bidhaa,kazi kubwa imebaki kwetu wafanyabiashara na Watanzania wote kulipa kodi kwa hiari,naamini kwa sasa hakuna mfanyabiashara anayetozwa kodi kubwa kupita uwezo wake, "amesema na kuongeza;

“Kila mfanyabiashara analipa kodi kulingana na ukubwa wa biashara yake, Serikali haiwezi kumtoza kodi kubwa bila kuzingatia uhalisia wa biashara, Kodi ndizo zinazojenga shule, hospitali na miundombinu ya kijamii tunayojivunia leo,” amesema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Dodoma, Gilbert Chuwa, amesema Serikali imeondoa urasimu na chuki kati ya wafanyabiashara na TRA, jambo lililowezesha biashara kufanyika kwa amani.

Ametumia nafasi hiyo kuwataka Watanzania waendelee kulipa kodi na kuiunga mkono Serikali ya Rais Samia ili kudumisha amani na maendeleo yaliyopatikana.

“Tunapolipa kodi, tunajenga taifa letu, Tunataka kodi zote ziwekwe kwenye kapu moja ili kupunguza utitiri wa kodi na kuongeza ufanisi,tunaamini haya yote yatafanikiwa endapo Rais Samia ataendelea kuongoza taifa hili,” amesema

Naye mfanyabiashara Sylivano James Chami amesema tofauti na zamani ambapo maduka yalifungwa kutokana na madeni na urasimu wa kodi, sasa mazingira ya biashara ni salama na rafiki.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 17,2025

Share:

Tuesday, 16 September 2025

84 CHURCHES IN ETHIOPIA CHANGE THEIR CHURCH SIGNBOARDS TO SHINCHEONJI CHURCH OF JESUS, THE TEMPLE OF THE TABERNACLE OF THE TESTIMONY MASS ENROLLMENTS DEMONSTRATE THE IMPACT OF THE “REVEALED WORD” 181 NEW PASTORS VOLUNTARILY JOIN THE EDUCATIONAL PROGRAM



On the 10th, representative pastors from 84 churches in Ethiopia posed for a commemorative photo at the “Shincheonji Church of Jesus, the Temple of the Tabernacle of the Testimony, Peter Tribe, Ethiopia Signboard Changing Ceremony. [Photo Credit: Shincheonji Church of Jesus]
On the 10th, during the “Shincheonji Church of Jesus, the Temple of the Tabernacle of the Testimony, Peter Tribe, Ethiopia 84 Churches Signboard Changing Ceremony,” representative pastors from all 84 churches conducted a pledge ceremony.

 ***
A total of 84 churches across 10 cities in Ethiopia have officially changed their church signboard names to Shincheonji Church of Jesus, the Temple of the Tabernacle of the Testimony (Chairman: Lee Man-hee, hereinafter "Shincheonji Church of Jesus").

On the 10th, the Peter Tribe of Shincheonji held the "Ethiopia 84 Churches Signboard Changing Ceremony." During the event, 84 church pastors declared that they had become members of Shincheonji Church of Jesus, committed to preaching the Word of the New Covenant Revelation, and resolved to become one through the "revealed Word."

This development stems from the participation of Pastor Asefa Angeto (President of the Misgana Denomination Association) in the "2nd Global Invitation Revelation Seminar" held last November at Shincheonji Cheongju Church. After returning to his home country, Ethiopia, Pastor Asefa continued to lead local seminars based on the Word he had learned.

Pastor Asefa had traveled to over 100 churches in 10 cities, conducting seminars and testifying to the revealed Word he learned from Shincheonji.

This signboard replacement is being regarded as more than a simple change of signage—it is seen as a major breakthrough in spreading a Word-centered transformation across the Ethiopian Christian community.


At the commemorative ceremony, the 84 representative pastors declared, “We have become members of Shincheonji Church of Jesus, having mastered the Word of the New Covenant Revelation. We resolve to preach this Word throughout Ethiopia, so that both pastors and believers alike may follow only the truth and devote themselves more fervently to the ministry of the Word.”

A representative of the Peter Tribe of Shincheonji stated, “Currently, 181 pastors in Ethiopia are learning the revealed Word from Shincheonji Church of Jesus. We will continue to make known the fact that the prophecies of Revelation have been fulfilled today, and we will do our utmost so that churches around the world may become united through the Word.”
Share:

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025 ,MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI AVIFUNDA VYAMA VYA SIASA HANDENI







Na; Mwandishi Wetu - Handeni

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imevitaka vyama vyote vya siasa katika Wilaya ya Handeni kuhakikisha vinazingatia kanuni, taratibu na sheria zilizowekwa wakati wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani, uwazi na kwa mujibu wa sheria.

Akizungumza katika kikao kazi na wawakilishi wa vyama vya siasa katika Wilaya ya Handeni, Bi. Edna Assey kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa alisema kuwa jukumu la vyama vya siasa ni kuhakikisha vinashiriki uchaguzi kwa kuzingatia misingi ya kidemokrasia na kuepuka vitendo vinavyoweza kuhatarisha uhalali wa mchakato mzima.


"Vyama vya siasa haviruhusiwi kujihusisha na vitendo vya rushwa kama kutoa fedha, mikopo, zawadi au hata ahadi za vyeo kwa lengo la kushawishi wapiga kura. Kitendo hicho ni kinyume cha sheria na kinaweza kupelekea hatua kali za kisheria kuchukuliwa,” alisema Bi. Edna


Aidha, aliwakumbusha viongozi wa vyama kuzingatia haki na wajibu wao wakati wa kampeni, ikiwemo kuendesha kampeni za kistaarabu, kuheshimiana na kuepuka kutumia lugha za matusi, kejeli, uchochezi au vitisho dhidi ya vyama vingine.

Ofisi ya Msajili imeeleza kuwa uchaguzi ni zoezi la kitaifa linalohusu mustakabali wa taifa lote, hivyo vyama vyote vinapaswa kushiriki kwa kuonyesha mfano bora wa uongozi unaojali maslahi mapana ya wananchi na taifa.


Bi. Edna Assey alisisitiza kuwa kuzingatia taratibu na sheria zilizowekwa kutasaidia kujenga mshikamano wa kitaifa, kuimarisha demokrasia na kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumu kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu.


Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa pia imewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi kwa kutumia haki ya kupiga kura na kufanya maamuzi kwa uhuru bila kushawishiwa kwa rushwa au vitisho. Wananchi wamehimizwa kutanguliza amani na mshikamano na wa kitaifa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger