Tuesday, 29 November 2022

HATIMAYE WASHINDI WA SHINDANO LA KAMPENI YA TISHA NA TEMBOACARD WATINGA QATAR KUSHUHUDIA KOMBE LA DUNIA


Benki ya CRDB baada ya kuhitimisha awamu ya kwanza ya kampeni yake ya “Tisha na TemboCard” na kuwakabidhi tiketi za kushuhudia mashindano ya Kombe la Dunia wateja wake watatu walioibuka washindi wa jumla wa kampeni hiyo hatimae yawapeleka Qatar.

Wateja hao waliondoka tarehe 25 kupitia uwanja wa Julius Nyerere International Airport na kusindikizwa na baadhi ya wafanyakazi wa Benki hiyo.
Akizungumza kwaniamba ya washindi wenzake katika safari hiyo, Rajabu Dossa Mfinanga aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuwapa kipaumbele wateja wake kwani wanajihisi ni sehemu ya familia ya Benki hiyo, pia alitoa rai kwa watanzania kujijengea utamaduni wa kutumia kadi zao za benki hiyo kwa kuafanya manunuzi na malipo mbalimbali kama bili, usafiri na kadhalika si kwasababu ya kushinda zawadi;

“Niwape wito wateja wenzangu wa Benki ya CRDB na watanzania kwa ujumla tujenge utamaduni wa kutumia kadi kupata huduma mbalimbali badala ya kutumia fedha taslimu. Matumizi ya kadi ni rahisi na inakupa kujiamini zaidi kuliko ukibeba fedha taslimu, unakosa kujiamini kila uendapo unakuwa na wasiwasi kwa kuhofia kuibiwa, lakini ukiwa na Tembocard yako mambo ni burdani”. Aliongeza Mfinanga.

Kwakufahamu namna ambavyo Watanzania wanapenda michezo na hasa msimu huu wa Kombe la Dunia imeona ni vyema ikawa sehemu ya kutimiza shauku ya wateja wao ya kushiriki katika mashindano hayo makubwa duniani.

Katika safari hiyo Benki ya CRDB imewagharamia tiketi za ndege kuelekea Doha Qatar, malazi, pamoja na fedha za matumizi wakiwa huko.
Washindi walioibuka kidedea kwenye safari hiyo ya kushuhudia kombe la dunia ni pamoja na; Haji Athumani Msangi, Erick Boniface Kashangaki, Kelvin Jackson Twissa, na Rajabu Dossa Mfinanga wote wakazi wa Dar es Salaam.

Benki ya CRDB inatarajia kuendesha awamu ya pili ya kampeni hii na kuahidi kuleta mambo mazuri zaidi, hivyo imetoa rai kwa wateja wake kuendelea kutumia kadi zao za TemboCard kulipia manunuzi ili kupata punguzo la bei (discount) au kurudishiwa sehemu ya kiasi walichotumia (cashback) katika maduka mbalimbali.


--
Share:

WATOTO 521,025 KUPATIWA CHANJO YA POLIO SHINYANGA DESEMBA 1 - 4, 2022


Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Faustine Mulutyu akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Novemba 29,2022. 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Watoto walio chini ya umri wa miaka mitano wapatao 521,025 wanatarajia kupatiwa matone ya kuzuia ugonjwa wa Polio Mkoa wa Shinyanga kaya kwa kaya kuanzia Desemba 1 hadi 4,2022.


Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Novemba 29,2022 kuhusu maandalizi ya Kampeni ya utoaji wa matone ya chanjo ya Polio awamu ya nne, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Faustine Mulutyu amesema Mkoa wa Shinyanga umepokea jumla ya chanjo dozi 614,800 pamoja na vifaa vingine (marker pen, chaki, vipeperushhi, rejista) kwa ajili ya kufanikisha Kampeni hiyo.


"Mkoa wa Shinyanga ulitekeleza Kampeni ya Polio awamu ya tatu kwa mafanikio makubwa na kufikia kiwango cha utoaji kukiwa na ushiriki mkubwa wa wadau ambapo walengwa walikuwa 445,681 kuanzia Septemba 1 hadi 4,2022",amesema Mulyutu.


Mratibu wa Chanjo mkoani Shinyanga Timothy Sosoma, amesema Mkoa wa Shinyanga umeshapokea jumla ya dozi ya chanjo ya Polio 614,800 na walengwa wote watafikiwa na timu ya wataalam 1,021 lengo ni kufikia idadi ya watoto 521,025 ili kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa wa Polio.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Faustine Mulutyu akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Novemba 29,2022 kuhusu maandalizi ya Kampeni ya utoaji wa matone ya chanjo ya Polio awamu ya nne ikayofanyika kaya kwa kaya kuanzia Desemba 1 hadi 4,2022.
Mratibu wa Chanjo mkoani Shinyanga Timothy Sosoma akizungumza na waandishi wa habari juu ya kampeni ya utoaji Chanjo ya Polio awamu ya Nne kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.
Waandishi wa habari wakichukua taarifa juu ya kampeni ya utoaji Chanjo ya Polio kwa njia ya matone dhidi ya watoto waliochini ya umri wa miaka mitano.
Waandishi wa habari wakichukua taarifa juu ya kampeni ya utoaji Chanjo ya Polio kwa njia ya matone dhidi ya watoto waliochini ya umri wa miaka mitano.
Share:

MSANII HI SPEED KUTOKA NIGERIA AACHIA ZAWADI YA ALBUM KWA MASHABIKI


Precious Gift ni album mpya na ya kwanza kutoka kwa msanii wa muziki wa Afro Beat na Hiphop kutoka nchini Nigeria ambaye anafahamika zaidi kwa jina la Hi Speed.

Album ya Hi Speed ina nyimbo 13 ndani yake akiwa ameshirikiana na Mr Raw, Terry Akpala, Seriki, Halima Alao, Jumabee, Shatta Michy , Dj Baddoo, Jesse Jagz, Jay Teaser, Mf Honcho, Di’ja, Eche Ozoku, Dreez, Jahjah, Sharon Sonia, Yonique, Young J, Don Flash, Hajj, Itabreez na Zurezoo.
Lakini pia katika album hii iitwayo Precious Gift imeandaliwa na kuyarishwa na watayarishaji  mbalimbali kutoka nchini Nigeria ambao wamefanikiwa kufanya vizuri kazi mbali mbali akiwemo Mix Monster  pamoja na Don Adah.

Album hii inapatikana katika mitandao yote ya kusikiliza na kupakua muziki unaweza pia kumfuatilia kupitia ukurasa wake wa Instagram @hispeedmusic

Share:

BARAZA HURU LA USULUHISHI WA MALALAMIKO YA WANANCHI VIJIJI VINAVYOZUNGUKA MGODI WA MWADUI LAZINDULIWA


Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akikata utepe wakati akizindua Taratibu za Baraza la Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy kulia ni Simon Mutinda kutoka Kampuni ya Pricewaterhouse Coopers (PWC).

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui (Williamson Diamonds Limited) kwa njia ya maridhiano kuhusu madhira ,mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu limezinduliwa rasmi mkoani Shinyanga

Uzinduzi wa Baraza la Malalamiko ya Wananchi pamoja na Utaratibu wake katika Mgodi wa Mwadui umezinduliwa leo Jumanne Novemba 29,2022 na Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkude amesema matarajio kupitia baraza hilo ni kuona kutenda haki kwa wananchi waliopata madhara kupitia mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu.


“Tunahitaji haki itendeke lakini pia kwa kuzingatia mambo yote tuliyoelezekana ngazi mbalimbali, tuoneshe uhalisia wa haki hizo zinazotolewa na kuwe na tija kwa walengwa wenyewe”,amesema Mkude.


Amesema mara baada ya uzinduzi huo Baraza hilo litaanza kusikiliza malalamiko yaliyowasilishwa na wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa Mwadui.


“Utaratibu wa kuunda Baraza Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi ulivyoandaliwa vizuri ukisimamiwa na kufadhiliwa na Petra Diamonds Ltd. Utaratibu wote uliotumika mpaka kufikia leo umekuwa wa wazi na tumekuwa tukieleweshwa ngazi moja hadi nyingine kwa kushirikisha taasisi mbalimbali kuhusu baraza hili la malalamiko na namna likatavyokwenda kufanya kazi”, ameongeza Mkude.

“Lakini nitumie nafasi hii kupongeza imeonekana kwamba Baraza hili likianza kazi kwa ujumla malalamiko yaliyosajiliwa na wananchi yapo 5575 na wameongeza muda wa kuyasikiliza badala ya miaka mitatu imeenda zaidi, hili ni jambo jema, jambo la kiutu ambalo litasaidia kuangalia kwa undani zaidi haki za watu ambazo wamewasilisha malalamiko yao”,ameeleza.


Mkuu huyo wa wilaya amesema serikali itaendelea kushirikiana Baraza hilo wakati wote na pale ambapo panatokea tatizo au viashiria vya shida au tatizo basi jopo zima lisisite kuwasiliana na uongozi ngazi ya mkoa na wilaya ili kutatua mapema matatizo yanayoweza kujitokeza kabla ya kuleta athari kubwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy amesema wana imani Baraza la Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi litafanya kazi kwa weledi mkubwa ili haki iweze kupatikana.

“Petra Diamonds Ltd tukiwa ni wamiliki wa Mgodi wa Mwadui tunatambua changamoto zilizokuwepo, tulifanya mabadiliko mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kukidhi matakwa ya sheria za nchi na kimataifa”,amesema Duffy.

Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya Wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui, Dkt. Rugemeleza Nshala amesema tangu mwaka 2009 hadi 2021 jumla ya malalamiko 5575 yamesajiliwa na usikilizwaji wa hatua ya awali unaanza mara moja kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa.

“Kila mwananchi aliyesajili malalamiko yake na atayesajili malalamiko yake atafikiwa na Baraza hili kuhusu la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi”,amesema Dkt. Nshala.


Naye Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo kuzinduliwa kwa Baraza Huru la Usuluhusihi wa malalamiko ya wananchi yanayotokana nan a shughuli za uzalishaji wa madini katika mgodi wa Mwadui unafungua Ukurasa mpya wa ushirikiano baina ya wananchi na mgodi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Jijimya ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu kuruhusu kuundwa kwa Baraza hilo huku akilitaka Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya Wananchi kwenda kufanya kazi kwa weledi na kutenda haki.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akizungumza wakati akizindua Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu
kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema leo Jumanne Novemba 29,2022 Mjini Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akizungumza wakati akizindua Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui, Dkt. Rugemeleza Nshala akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui.

Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui,Dkt. Rugemeleza Nshala akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui.
Simon Mutinda kutoka Kampuni ya Pricewaterhouse Coopers (PWC) akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui ambapo amesema jopo la usuluhishi litaenda kufanya kazi kwa weledi ili jamii ipate suluhisho la malalamiko yao kwa ajili ya kuleta maendeleo katika taifa.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Jijimya akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui
Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui

Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude (kulia) akikata utepe kuzindua Baraza huru la kushughulikia malalamiko ya wananchi ambao wanazunguka Mgodi wa Almasi Mwadui, (kushoto) ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Petra Diamond Limited Richard Duffy
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude  akikata utepe wakati akizindua Taratibu za Baraza la Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akionesha Vitendea kazi vya Baraza Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akimkabidhi Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy (kushoto).
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy (kushoto) akimkabidhi Katibu Tawala wilaya ya Kishapu, Shadrack Kengese Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akimkabidhi Mbunge wa Jimbo la Kishapu, Boniphace Butondo, Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akimkabidhi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Jijimya  Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy (kushoto) wakikabidhi vitendea kazi kwa Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui, Dkt. Rugemeleza Nshala na Simon Mutinda kutoka Kampuni ya Pricewaterhouse Coopers (PWC).

Zoezi la makabidhiano ya Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui likiendelea
Zoezi la makabidhiano ya Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui likiendelea
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu

Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited wakipiga picha na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited wakipiga picha na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

UGANDA YAJA TANZANIA KUJIFUNZA USIMAMIZI WA HUDUMA ZA MAWASILIANO

Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Kundo Mathew (wa kwanza kushoto) akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt. Jabiri Bakari (wa pili kulia) walipomkaribisha Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA na Ulinzi-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey (katikati) kwenye Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma-TCRA Bi. Lucy Mbogoro. Picha na TCRA)

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt Jabiri Bakari (kushoto) akiwa sambamba na Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Mathew (wa pili katikati) wakimkaribisha Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA na Ulinzi-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey aliefika TCRA kwa ziara ya mafunzo akiambatana na Maafisa Waandamizi wa Tume ya Mawasiliano Uganda(UCC) (hawamo pichani). Wa kwanza kulia anaeshuhudia ni Msaidizi wa Waziri wa Uganda. PICHA NA TCRA Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Kundo Mathew (kulia) akiperuzi jambo kwenye kijitabu wakati alipomkaribisha Mgeni wake Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA na Ulinzi-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey (anaesaini kitabu cha wageni kushoto) Waziri huyo wa Uganda alioongozana ujumbe wa maafisa wa Tume ya Mawasiliano Uganda (UCC) waliokuja Tanzania kwa ziara ya mafunzo ya usimamizi wa sekta ya Mawasiliano kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ikiwa ni mkakati wa kuboresha Sheria ya Mawasiliano ya nchini kwao. Picha na TCRA)

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kundo Mathew (kushoto), akimweleza jambo Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA na Ulinzi-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey aliefika Tanzania kwa ziara ya mafunzo. Katika tukio hili anakaribishwa kujifunza kutoka TCRA namna Sheria za Mawasiliano zinavyowezesha usimamizi wa Sekta ya mawasiliano nchini. PICHA NA TCRA

**************************

Na Mwandishi Wetu

Tanzania imeihakikishia Uganda kuwa itaendelea kuipa ushirikiano katika kujenga uwezo wa usimamizi wa sekta ya Mawasiliano na TEHAMA, sambamba na kudumisha ushirikiano wa kitaalam katika usimamizi wa sekta hizo.

Akizungumza wakati alipoukaribisha ujumbe wa Tume ya Mawasiliano Uganda (UCC) ukiongozwa na Waziri wa Nchi anaeshughulikia Ulinzi na TEHAMA Mheshimiwa Kabbyanga Godfrey uliofika katika Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa ziara ya Mafunzo na kubadilishana ujuzi, Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrew Mathew alibainisha kuwa, Tanzania imefanikiwa kusimamia vilivyo sekta ya Mawasiliano kwa kuweka Sera Madhubuti za usimamizi wa huduma za Mawasiliano, huku akiwahakikishia wageni fursa tele ya kujifunza katika sekta ya Mawasiliano.

“Tanzania imepitisha sera zinazounga mkono ukuaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano - TEHAMA na mfumo wa kisheria na udhibiti unaounga mkono ukuzaji wa uchumi wa kidijiti,” alisisitiza Kundo na kuongeza kuwa “Ninakuhakikishia ujumbe wako kwamba utapata fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu ambao utakuwa muhimu katika marekebisho ya Sheria yenu ya Mawasiliano ya 2013,” alibainisha.

Kwa upande wake Waziri Kabbyanga akishukuru baada ya ukaribisho alimweleza Naibu Waziri Kundo, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Jabiri Bakari na Menejimenti ya TCRA lengo la ziara yao Tanzania kuwa ni kujifunza zaidi namna Tanzania inavyosimamia huduma za Mawasiliano ambao ziara yao mahususi katika ofisi za TCRA ililenga kujifunza namna Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali inavyowezesha usimamizi wa sekta ya Mawasiliano.

Akizungumza muda mfupi baada ya kuwasili kwenye ofisi za TCRA jijini Dar es salaam Waziri wa Nchi anaeshughulikia Ulinzi na TEHAMA Mheshimiwa Kabbyanga Godfrey alimweleza mgeni wake Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Mheshimiwa Kundo Mathew kwamba Uganda imeona vema kuja kujifunza Tanzania kwa kuzingatia ujirani na namna ambavyo Tanzania imefanikiwa katika kusimamia na kudhibiti sekta ya Mawasiliano.

“Tumeambiwa kwamba Tanzania mnazo Sheria Madhubuti za usimamizi wa sekta ya mawasiliano Tumekuja hapa kwa sababu mazingira yetu ni sawa na ya Tanzania hivyo tumeona hapa kwenu tutajifunza na kupata maarifa yenye uhalisia zaidi, tofauti na tungeamua kwenda kujifunza sehemu nyingine,” alisisitiza Kabbyanga.

Alieleza kwamba pia Uganda inanuia kuboresha huduma za Mawasiliano ya simu kwa raia wake hivyo imeamua kuja Tanzania kujifunza katika eneo linalohusu Mawasiliano ya simu.

Ziara ya Tume ya Mawasiliano Uganda kuzuru Tanzania, na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ni mwendelezo wa Mamlaka mbalimbali za Usimamizi wa Mawasiliano za Afrika kufika Tanzania kujifunza na kubadilishana ujuzi wa usimamizi wa huduma za Mawasiliano. Miongoni mwa nchi nyingine zilizozuru TCRA mwaka huu ni pamoja na Malawi, Zimbabwe, Burundi, Rwanda, Uganda, na Msumbiji.
Share:

Monday, 28 November 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 29,2022










Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger