Friday, 19 August 2022
MALIMA AKUBALI KUWA MLEZI WA MWANZA PRESS CLUB
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Adam Malima amekubali kuwa mlezi wa chama Cha Waandishi Wa Habari Mkoa Mwanza na kuahidi kushirikiana nao katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo.
Malima amekubali kuwa mlezi Klabu hiyo baada ya kuombwa na mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari kupokea kijiti hicho kutoka kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Robert Gabriel.
"Mimi nimevutiwa na utendaji wenu wa kazi na ndio maana mlivyoniita Leo nimekuja kuwasikiliza ila name Mimi nitawaita Ili niwaambie mambo yangu."alisema Malima
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mdahalo wa majadiliano juu ya umuhimu wa chanjo ya UVIKO 19 Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi Mkoa wa Mwanza Edwin Soko alimuomba Mkuu wa Mkoa kuwa mlezi wa Klabu hiyo ili pamoja na mambo mengine aweze kuwa mshauri Mkuu wa Klabu hiyo.
"Mhe. Mkuu wa Mkoa, huu umekuwa utamaduni wetu kila Mkuu wa Mkoa anayekuja Mwanza huwa tunamuomba kuwa mlezi wetu tukiamini kuwa ukaribu wetu unaweza kuwa na tija mwa Maendeleo ya Mkoa",amesema.
RC MALIMA : WAANDISHI WA HABARI MWANZA MKIANDIKA HABARI ZA KUCHOCHEA MAENDELEO MTAKUWA RAFIKI ZANGU
DIWANI AFARIKI KWENYE AJALI BASI LILILOUA WATU WATANO SINGIDA
Thursday, 18 August 2022
WIKI YA ASASI ZA KIRAIA 'AZAKI' YAZINDULIWA
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela (wa tatu kulia) akibonyeza kitufe kuashiria kufunguliwa rasmi kwa wiki ya AZAKI 2022 katika hafla iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela akizungumza katika uzinduzi wa Wiki ya Asasi za Kiraia (AZAKI) 2022 leo Agosti 18, Jijini Dar es Salaam ambapo alikuwa mgeni rasmi.
Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali kutoka Ofisi ya Rais (OR TAMISEMI) Linus Kahendagaza akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela (wa tatu kusho) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society (FCS) Francis Kiwanga (wa pili kushoto) pamoja na Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali kutoka Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Linus Kahendagaza (wa pili kulia) katika uzinduzi rasmi wa Wiki ya AZAKI uliofanyika leo Agosti 18,2022 Jijini Dar es Salaam. (wa kwanza kushoto) ni, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Lilian Liundi, na (wa kwanza kulia) ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la CBM Nesia Mahenge.
Mratibu wa Wiki ya Asasi za Kiraia (AZAKI) Justice Rutenge, akizungumza katika hafla hiyo kuelezea matukio mbalimbali yatakayofanyika katika Wiki AZAKI ya 2022 yatakayofanyika Jijini Arusha kuanzia Oktoba 24, 2022 mpaka Oktoba 28, 2022.




























