Wednesday, 17 August 2022
BARRICK NORTH MARA YAFANIKISHA UKARABATI WA BARABARA KOROFI TARIME
Tuesday, 16 August 2022
AJALI YAUA 19 , KUJERUHI 10 MBEYA

MTANDAO WA TELEGRAM SALAMA ZAIDI KULIKO WHATSAPP KWENYE UDUKUZI
RAILA ODINGA APINGA MATOKEO YA URAIS KENYA
JAMAA AKATA NYETI ZAKE AKIOTA ANACHINJA MBUZI
STENDI MPYA YA HIACE, BAJAJI SOKO KUU MJINI SHINYANGA YAZINDULIWA
Na Marco Maduhu, SHINYANGA
WAFANYABIASHARA wa usafirishaji katika Stendi ya Hiace, Bajaji na Bodaboda iliyopo Soko kuu Manispaa ya Shinyanga, wameipongeza Serikali kwa kuifanyia ukarabati Stendi hiyo, na kuwaboreshea mazingira mazuri ya kufanya biashara zao.
Mmoja wa Wafanyabiashara hao Paschal Mboje, amesema awali Stendi hiyo ilikuwa na vumbi na kipindi cha mvua tope linakuwa jingi na maji kutwama, lakini sasa hivi changamoto hizo hazipo tena na watafanyabiashara zao katika mazingira mazuri.
“Tunaipongeza Serikali kwa kuikarabati Stendi hii, na kutatua Changamoto ambazo tulikuwa tukikabiliana nazo za uchakavu wa miundombinu na tutafanya biashara zetu kwa raha mstarehe,”amesema Mboje.
Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko, amewataka wafanyabiashara hao waitunze miundombinu ya Stendi hiyo ili waendelee kufanyabiashara zao katika mazingira rafiki.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akizungumza mara baada ya kumaliza kuzindua Stendi ya Hiace, Bajaji na Bodaboda iliyopo Soku kuu Manispaa ya Shinyanga.
Mfanyabiashara wa usafirishaji Paschal Makoye akizungumza mara baada ya kumaliza kuzinduliwa Stendi hiyo.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko (katikati) akikata Utepe kuzindua Stendi ya Hiace, Bajaji na Bodaboda iliyopo Soko kuu Manispaa ya Shinyanga, (kulia) Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Getruda Gisema, (kushoto) Diwani wa Chibe John Kisandu.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko (katikati) akikata Utepe kuzindua Stendi ya Hiace, Bajaji na Bodaboda iliyopo Soko kuu Manispaa ya Shinyanga, (kulia) Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Getruda Gisema, (kushoto) Diwani wa Chibe John Kisandu.
Madereva wa Bodaboda wakiingia kwenye Stendi hiyo.
Madereva wa Bajaji wakiingia kwenye Stendi hiyo.
Hiace ikiingia ndani ya Stendi hiyo.
Hiace ikiingia ndani ya Stendi hiyo.
Hiace zikiwa ndani ya Stendi.
Bajaji zikiwa ndani ya Stendi.
BENKI YA EXIM YAADHIMISHA MIAKA 25 KWA KUPONGEZA NA KUTAMBUA JITIHADA ZA WAFANYAKAZI WAKE
RAIS SAMIA AMPONGEZA RUTO



























